Hii ni kwa kizazi cha cha mapenzi ya barua na zawadi za maua

NUHWAHI

JF-Expert Member
Jan 23, 2014
304
464
Hii ni kwa kizazi cha cha mapenzi ya barua na zawadi za maua

LEO nimemkumbuka neema kupitia uzi fulani wa ..kimasihara zilizofeli,,,,
Popote alipo neema mwambieni mungu atalipa tu alonitendea mimi
Picha lilianza pale darasa la 5 na neema ni la6..neema matiti yameshajiumba, mazuri, yanaonesha weupe hapa kifuani yalipojagawa..nami ndo wakati wa balehe umekuja..

Wacha nijletelete kwake.muda wote nipo nae, kuni, matete, fagio kidumu cha maji vyote nambebea..kiunga chake cha maua namwagi ila kumwambia nampenda ni gumu.Kila nkitaka kujaribu kijasho kinanitoka na kitu kinakaba kooni neno halitoki

Nikaongeza mbinu..baba alikuwa wakala wa kununua kahawa,nikawa naiba sh.200 ile za noti, nachomoa ya katikati ya fungu nikijua mzee hatogundua..nikija shule ni mwendo mdundo kwa neema.. NEEMA otea,, nimebeba hela sio hela,,,,,, sh mia mbili sio miambili..... Nadhani hata wewe unaweza kisia majibu ya neema...akishapokea hela hiyo najipa moyo leo jioni atakubali nikimueleza,,kufika jioni domo zito,,,
Nikakwazana na wanafunzi wenzangu wengi..nikiona yeyote kamkwaza neema ugomvi mimi na yeye ni mkubwa..siku moja nikajichanganya kumchimba mkwara JOHN,, mbabe wa darasa la saba kwa kumuhisi anatoka na neema, Kichapo alichonipa mpaka shati la shule likawa rangi ya jezi za SIMBA
NEEMA, , usidhani alikuwa akiish mbali mtaani na kwetu...!

Inamaana neema hukujua kama nakupenda!?

Tuma vibarua kibao, vyenye ujumbe wa kumpenda kama mchuzi wa jogoo, kumuona kwenye glass, kujitahidi mimi kuchora makopa,, rembesha maua kwenye kingo za barua,,,, lakini tukiwa ana kwa ana hooillaaa..neni halitoki

Siku ya siku nikajitosa kumwambia...,, oyyaa neema badae nitakuja kwenu,, .. Si akajibu .. , karibu....Kilichonikuta,, sikuamini kama ni nema wewe

Mara saa za 4 ya usiku hiyyoo mama baba wamelala nikasema hapa ndo penyewe wacha ninyate kutoka.. nikafanikiwa .. pita mashamba kadhaa ya kahawa mpaka kwa akina neema, moja kwa moja dirishani kwake. Ngo,ngo,ngo,ngo neema,..neema .kwa sauti ya chin.. nikasikia ( ne mbwito.. mie sitaki),, nikajikausha dak 2 nikagonga tena,, mara akamuita mama yake..MAMAAA MAMA,, nje kuna mtu.. nikadhani mama mtu hajasikia, dak 4 nyingi nilipigwa kibao cha kisogoni.. kuja kutahamaki Kofi zito,, akili ikanijia ni baba mtu huyo, chap uume ukasinyaa utadhani sijawahi kua nao....Mbio nilizofyatuka pale hata mbwa stadi wa kuwinda swala asingenipata,,, Kuja nyumbani kumbe dingi alishaamka na kukuta mlango wazi..

ile naruka kaukuta fulani niingie nipo mikononi mwake dingi.. kichapo alichonipa,, mbalamwezi nikaita jua...nikabuni fasta hapa ili dingi aniachie nilie kwa sauti majirani waje, hii mbinu nayo ikachana mkeka, si akaja na baba neema...

.....TAFUTA KILICHOFUATA PALE....
eti neema toka siku hiyo hata shobo nami hakutaka tena

KARIBUNI KWA VISA VYENUVYA ENZI ZA UDOMO ZEGE .. TUFURAHI
 
Huyu aliitwa shukuru Binti toka Kijiji jirani. Alikua na kaka yake darasa la SITA na wakati huo Mimi darasa la Tano mwaka 2005 Hiyo. Alikua white flani mpaka nilimpenda ila kumuambia ikawa shida. Nikaja na mbinu ya kutengeneza ukaribu na kaka mtu. Nilipambana mpaka nikafanikiwa ingawa ilikua ngumu. Jamaa tukawa marafiki mpaka kwao nikawa naenda na kurudi. Siku Moja nilipanga nimuambie na nivunje name amri ya muumba, hivyo nikajipa moyo usiku itakua poa.

Nikaenda Kwa jamaa nikabaki mpaka usiku, Binti akaachiwa kupika huku mama yake na baba yake wameenda kilabuni kurudi saa nne. Jamaa akasema anaenda kuangalia video (miaka ya VHS na machogo). Tukabaki wawili tu lakini akili na mdomo vilipishana.

Wakati ubongo unawaza kumwaga sera na kuibandua mdomo ulichokua unakisema ni vice versa. Yaani maneno yaliyokuwa yakitoka ni kuhusu masomo, wanafunzi wezi darasani, mwalimu mkali, wanafunzi wababe na Kama amefanya zoezi la hesabu yaani pumba tupu. Jamaa alifika tukaingia kulala mpaka asubuhi nikarudi home kinyonge.

Now anawatoto watatu nimetafuta namba nimepata na nawasiliana nae nikazie maarifa.
 
Huyu aliitwa shukuru Binti toka Kijiji jirani. Alikua na kaka yake darasa la SITA na wakati huo Mimi darasa la Tano mwaka 2005 Hiyo. Alikua white flani mpaka nilimpenda ila kumuambia ikawa shida. Nikaja na mbinu ya kutengeneza ukaribu na kaka mtu. Nilipambana mpaka nikafanikiwa ingawa ilikua ngumu. Jamaa tukawa marafiki mpaka kwao nikawa naenda na kurudi. Siku Moja nilipanga nimuambie na nivunje name amri ya muumba, hivyo nikajipa moyo usiku itakua poa.

Nikaenda Kwa jamaa nikabaki mpaka usiku, Binti akaachiwa kupika huku mama yake na baba yake wameenda kilabuni kurudi saa nne. Jamaa akasema anaenda kuangalia video (miaka ya VHS na machogo). Tukabaki wawili tu lakini akili na mdomo vilipishana.

Wakati ubongo unawaza kumwaga sera na kuibandua mdomo ulichokua unakisema ni vice versa. Yaani maneno yaliyokuwa yakitoka ni kuhusu masomo, wanafunzi wezi darasani, mwalimu mkali, wanafunzi wababe na Kama amefanya zoezi la hesabu yaani pumba tupu. Jamaa alifika tukaingia kulala mpaka asubuhi nikarudi home kinyonge.

Now anawatoto watatu nimetafuta namba nimepata na nawasiliana nae nikazie maarifa.
Hahahaahahahahahaaaa.. ngoja nami nisake namba nikazie hayo maarifa...ile zama si mchezo
 
Back
Top Bottom