tujifunze matumizi ya "L" na "R" wana JF!!

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Kama hapa ni nyumbani kwa wazamivu waliobobea katika kufikiri (Great thinkers) basi na matumizi ya lugha nayo yazingatiwe. Ingawa dunia nzima inajulikana kwamba lugha za asili huathiri lugha za pili, lakini hiyo hutokea zaidi kwenye utamkaji wa maneno na si kwenye uandishi wake.

Sisi tujitahidi kuwa mfano wa matumizi bora ya herufi hizi mbili za "L" na "R". Tusiandike "Lafiki" badala ya "Rafiki" au "Jilani" badala ya "Jirani"
 
Mimi hili jambo linaniudhi kweli kweli...imefikia mahali nikikuta mchangiaji kachanganya hizo herufi, basi post nzima inakosa ladha na huyo mchangiaji namweka kwenye "ignore list", that's how serious I view the whole issue.
 
Mimi kuna mijitu inanikera sana kwa kutumia neno "udhibitisho" badala ya neno "uthibitisho"
 
Mkuu, wengine mtawaua tu. Hivi kweli umwamvie mkurya atumie 'L' badala ya 'R' utamweza kweli? Au ukimwambia msukuma atumie 'R' badala ya 'L' si ni kumtafuta lawama tu? Hizo herufi hazimo kwenye lugha zao za asili, sasa waje wazipatie huku ukubwani, wataweza kweli? Tutapiga, tuue, mpaka tugalagaze, lakini sidhani Kama tutaweza kuwabadilisha.
 
Back
Top Bottom