Hawa sio akina George Washington na wenzake wakati wanatia sahihi Declaration of Independence katika miaka ya Karne ya 18? Lakini pengine siyo kwani pale maeneo ya katikati kuna watu kama Mao se Dong, Abraham Lincoln, Charles Darwin, Joseph Stalin, Albert Einstein, Mahatma Gandhi, William Shakespeare, n.k.
Hawa ni watu wa kale na watu wa sasa mchanganyiko lakini ni mashuhuri.Namwona mchezaji bora Pele,na watu kama Tyson,Bill Clinton,Hitler,Sadam Hussein,Koffi Annan,Mahatma Gandhi etc..hapa sijamuona Mwalimu Nyerere,Nelson Mandela,George Bush...
Hii picha inaonyesha kama ina-predict siku za mwisho!!! kutakuwa na kusanyiko kubwa sana... Wengine niliowaona hapo ni MICHAEL JORDAN,CHARLIE CHAPLIN,MIKE TYSON,BRUCE LEE... Etc...
Download and zoom, utawaona vizuri. kuna Arafat yuko karibu na Bush na Koff Anan n.k. sasa kwa haraka haraka picha hii inaonyesha watu maarufu mbalimbali walioko hai na ambao walishafariki. kwa hiyo hii inaonyesha kuwa kuna siku watu wote waliowahi kuwa hapa dunia watakuta bila kujali nani alimfanyia nini mwenzake.
Nashindwa kuelewa ni kwa nini Bin Laden anaondoka na kundi kubwa la waumini wakielekea kwenye ma-pyramidi. Ila naomba kuuliza swali kwa nini Mwalimu Nyerere haja-qualify kuwa kwenye hii picha????????
Mi naona mambo ya Yesu vile enzi zile watu walikuwa wakikusanyana wao na mbuzi, kondoo, paka, mbwa na kila kitu.....that is what i see. Otherwise hiyo camera ni kiboko.
Naona hii ni paint.
Nilioweza kuwafahamu ni: Albert Einstain amekalia vitabu mbele, Mao, Yaser Arafati, Ariel Sharon, Saddam Hussein, Mike Tyson na Putin wako pamoja, Lincoln, Bill Clinton, Hillary Clinton, Fidelis Castro, Bush na Anan wenye tarumbeta, Hitla aliye karibu na mwanasoko mbrazili, Bruce lee.
Ni picha ambayo imebuniwa kwa mkusanyiko wa watu mbalimbali mashuhuri duniani katika nyanja mbali mbali kama siasa na michezo mpaka mwaka jana.
Kwa haraka haraka nimewatambua Che guevara,Fidel Castro,Arafat, Prince Charles, Charlie Chaplin, Tyson, Abraham Lincon,Elvis Presley,Mahatma Gandhi,Margaret Hatcher, Malkia Elizabeth II na Adolf Hitler na nembo yake ya Nazi.
Pia kuna mchezaji wa Brazil jezi no.10 huyo ni Pele.Huyo mtoto mdogo anaitwa Shirley Temple.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.