Tuhuma dhidi ya Zitto hazina msingi

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
610
1,540
CHAMA CHA ACT WAZALENDO
---------------------------------------------

KAMATI YA BUNGE NA SERIKALI ZA MITAA
TAARIFA MUHIMU KWA UMMA.
Ndugu wanahabari na watanzania kwa ujumla.

Mtakumbuka kwamba jana tarehe 13,04.2016 mmoja wa vijana wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) bwana Augustine Matefu alizungumza na waandishi wa habari na kuzungumzia masuala kadhaa huku akirusha tuhuma kwa wabunge na wafanya biashara mbali mbali mbunge na kiongozi wa chama chetu cha ACT-WAZALENDO ndugu Zitto Ruyagwa Kabwe.

Tuhuma zake zisizo na msingi bwana Matefu zinaweza zikatafsiriwa katika makundi makuu matatu kama ifuatavyo

i. Hofu ya rais wa Chama chake kushindwa kuongoza na hivyo kuandaa mazingira ya kuogopa kupingwa na kwamba kila atakayemkosoa basi atakuwa ametumwa.

ii. Kujipendekeza kwa viongozi wa chama chake kama wanavyofanya vijana wenzake wa CCM kipindi hiki wanachojiegemeza na viongozi wa Serikali kusubiria uteuzi wa Ukuu wa wilaya (U-DC) na hivyo kujitia upofu hata kwa vitu vilivyo wazi na kuonekana kabisa.

iii.Kujitwisha utetezi wa tuhuma za ubadhilifu zinazomkabili Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Bwana Charles Kitwanga za zaidi ya Shilingi Bilioni 34 kupitia kampuni yake ya Infosys iliyoshirikiana na Kampuni ya Lugumi katika mkataba wa Kifisadi walioshindwa kuutekeleza kama ilivyoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni.

Kwa msingi huo basi, kwa niaba ya Kamati ya Vijana ya Chama cha ACT-WAZALENDO. Tunamtaka ndugu Matefu na vijana wengine wote wa UVCCM na vyama vingine, ambao wameamua kujitwisha usemaji na utetezi wa wanasiasa,wafanyabiashara na taasisi mbalimbali kwa kuanzisha majina na ama majukwaa ama viji taasisi vya uongo na kweli ili kujipatia pesa na fursa (kama matefu alivyofanya) . waache mara moja kumuhusisha Kiongozi wa chama chetu na tuhuma zote zinazoendana na misingi ya chama chao (Chama cha mapinduzi).

Sio hulka wala mwenendo wa kiongozi wa Chama cha ACT-WAZALENDO kujihusiah na vitendo vyovyote vya matumizi mabaya ya ofisi, kuomba ama kupokea rushwa, na mengine yanayofanana na hayo. Na tabia hii kwa miongo kadhaa sasa imekuwa ikifanywa na viongozi na wanachama wa chama cha mapinduzi CCM (mifano ipo wazi).

Pamoja na mambo mengine. Tunahitaji kuona ifuatavyo

i. Rais John Magufuli, aache kuogopa kivuli chake kwa kuhisi kuna watu wana mpango wa kumuhujumu, mbunge wa chama chetu hatujamtuma kwenda bungeni kumuhujumu Magufuli, tumemtuma kwenda kuwasimamia na kuwapigania watanzania kwa kufuata misingi na itikadi ya ACT-WAZALENDO. Hivyo hatutarajii wala yeye hatarajii kuwa mtetezi wa Rais. Magufuli hata kama serikali yake itapeleka bungeni mapendekezo ya Hovyo.

ii. CCM na Serikali yake itambue kuwa Zitto Ruyagwa Kabwe ni Kiongozi wa chama cha siasa cha Upinzani kilichojipa wajibu wa kuwatetea watanzania, hivyo kamwe hatakuja kuwa mtetezi wa madudu yoyote yatakayofanywa na Magufuli na Serikali yake. Ni wajibu wa Zitto Ruyagwa Kabwe kuhakikisha CCM na Serikali yao inatoka Madarakani sio kuwatetea. Hivyo waache hofu.

iii. Tunamtaka Waziri wa mambo ya Ndani CHARLES KITWANGA aache kujificha kwenye koti la Rais MAGUFULI hasa kwenye hizi Tuhuma zinazomkabili za Kampuni ya INFOSYS kampuni yake binafsi yeye na Rafiki yake Mkurugenzi Mkuu wa NIDA la kuitia hasara serikali zaidi ya Bilioni 34 baada kushirikiana na kampuni ya LUGUMI na kushindwa kukamilisha zabuni waliyopewa. Na Badala yake ajitokeze hadhani na atoe ufafanuzi wa kwanini asipandishwe mahakamani kama wahujumu uchumi wengine walivyofanya.

iv. Tunamtaka Rais. John Magufuli, amchukulie hatua za kinidhamu haraka iwezekanavyo Waziri huyu anayediriki kutumia madaraka yake kusimamia kampuni zake binafsi za kibiuashara na kuitia hasara serikali huku ukizingatia inatumika pesa za walipa kodi masikini. Mpaka sasa Kitwanga anafanya mchezo huu.



Imetolewa leo

14.04.2016 na:-

Wiston A. Mogha

Kaimu Msaidizi wa Katibu Kamati ya Bunge na Serikali za Mitaa
ACT – WAZALENDO
 
Kila jambo huwa linamwisho wake, sijui kwanini watu wengine hawapendi kukubali? Kujinafkisha ili ufikiriwe kwenye nafasi ya uteuzi katika zama hizi hakupotena. Tumeambiwa "HAPA KAZI" Jamani Tufanye KAZI.
 
Kaimu msaidizi wa katibu mkuu.. Duuu hiki cheo balaa. Umekaimu kusaidia ukikaimu kabisa?
 
Kitwanga sio Anna kiasi cha kukubari kudhaliliswa watu wapate kick usitegemee atawajibishwa .
 
Mimi nasema kitu pekee kisichokuwa na ubishi ni muda, maadamu tupo tuombe uzima itafika kipindi chepe tutaliita chepe na siyo kijiko kikubwa
 
Kitwanga sio Anna kiasi cha kukubari kudhaliliswa watu wapate kick usitegemee atawajibishwa .
Ana kipi cha maana mpaka watu wamfuatilie yeye tu.kama kahusika atawajibika tu.hakuna shortcut.otherwise mtuambie rais ana watu wake na wasio wake.
 
Lugumi.... Kweli tz balaa. kila siku sinema mpya,kuiongoza inabidi ujitie uchizi.. maana kuchekacheka na kuwa kauzu sana vyote ni uchizi. kazi kwako rais jpm,the choice is yours!!!!!!
 
Ndoa ya ACT na CCM hatihati kuvunjika. Wameanza kutetana. Magufuli sio JK. Makubaliano kati ya ACT na CCM kwa sasa yamepuuzwa. Zitto anaingilia maslahi ya wakubwa ndani ya CCM. Lazima waanze kumshughulikia. Ni wakati sasa wa ACT kuacha unafiki. Ni lazima waungane na vya vingine vya upinzani badala ya kujinasibisha na CCM. Wasithubutu tena kupambana na CHADEMA/UKAWA kwani malengo yao yanafanana (kuing'oa CCM madarakani)....ACT huu ndo wakati wa kurudi kundini.
 
Mnamdhalilisha zitto kwa kutomtaja kwa cheo chake act, mtajeni kwa cheo chake, kiongozi mkuu wa act wazalendo
 
Pumba at work. Zitto ni mnafiki na mzandiki na mla rushwa mkubwa. Ndiyo maana hata CDM walimfukuza, pamoja na kwenda mahakamani alifukuzwa. Zitto ni moja ya vijana wasioaminika ktk siasa za Tanzania. Alianzisha chama akiwa bado chadema, huyo nadhani siyo mtanzania halisi, anaweza akaivuruga Tanzania then akajiandaa kwenda nje ya nchi (kama alivyofanya chadema-kuanzisha chama wakati ni mwanachama wa chadema).





Itikadi za kisiasa ni moja ya majanga yanayotishia kudidimiza na kuua uwezo wa kifikra wa Watanzania wengi hususan vijana.Ni jambo la kutisha kukiruhusu kiwiliwili kiongozwe na itikadi badala ya utashi,utu na uzalendo.Tukiruhusu mihemko ya kisiasa na matamanio ya kupata vyeo kuwa msingi wa kujenga hoja,tutaishia kulitumbukiza Taifa letu katika misuguano isiyo ya lazima.

Hakuna mahali popote ambapo Mh.Zitto alituhumiwa kuanzisha chama cha siasa akiwa CHADEMA,sababu zilizomuondoa Zitto CHADEMA zipo wazi na zilishajadiliwa hapa vyakutosha.Kumuhusisha Zitto kabwe na uchafu wa wateule wa serikali ya chama cha majipu (CCM) ni jaribio la mwisho la kutaka kuuficha Ukweli uliodhahiri wa ubadhirifu unaofanywa na wateule hao.

Hivi kwa nakisi ya ufahamu uliyonayo unadhani unaweza kuuhamisha mjadala huu wa ufisadi kwa hoja nyepesi zisizo na mashiko yoyote?Au unadhani watu wote ni wavivu wa kufikiri kiasi cha kushindwa kung'amua namna mnavyojaribu kututoa kwenye hoja za msingi?

Kujaribu kuuaminisha umma kuwa kila atakayeupinga utawala wa Magufuli na serikali yake aonekane amenunuliwa na ni msaliti wa serikali ya CCM ni upumbavu uliovuka viwango vya upumbavu wenyewe.Tumeona na kushuhudia namna serikali inavyoshughulikia kile inachoita majipu kwa mwelekeo tofauti,imekuwa haraka mno kutoa maamuzi juu ya wale ambao vitendo vyao vya ubadhilifu hata vikiwekwa kwenye Mizani,havina madhara ya moja kwa moja na mustakabali wetu kama Taifa,lakini katika yale yenye kuathiri ustawi wa Taifa letu,serikali inapata kigugimizi katika kuchukua hatua.

Unaposema Mh.Zitto alianzisha chama akiwa ndani ya chama huku ukijifanya kuwasahau mawaziri waandamizi wa serikali ya CCM walioasisi CCJ huku wakiwa wanachama na viongozi wa Umma ni kiashiria cha mwisho cha upumbavu ulionao.Umewasahau Sitta,Mwakyembe,Mpendazoe,Napelape na wenzao walioasisi CCJ?

CCM Na serikali yake haipaswi kuyafanyia siasa mambo ya msingi,inapaswa iwawajibishe mara moja wale wote waliojigeuza wajasiliamali na kufungua vikampuni uchwara ili wapige hela za Umma kupitia miradi hewa.Hatutokubali ghiliba za kuwafunga midomo watetezi wa wanyonge kwa kuwasingizia tuhuma uchwara.Tunataka haki itendeke kwa kuhakikisha michoro yote ya kifisadi ambayo mingi iliratibiwa Ikulu,wahusika wanawajibishwa badala ya kusaidiwa kutoroka nchini.

Tunataka mshororo huu: LUGUMI - MTOTO WA IJP - RIZ 1 - IGP - MKWERE -MAWE MANNE na mishororo mingi ya aina hiyo ambayo iliundwa ili kupiga hela za Umma inadhibitiwa bila kigugumizi.

Hekaya za utumbuaji majipu huku mtumbuaji akikwepa majipu ya dhahili yaliyoota usoni mwake na kujifanya hayaoni hauwezi kuvumilika kwa viwango vyovyote vile.
 
kitwanga anatetewa nini na wanaccm. wananchi tunaomuamini mugufuli tunamtaka kitwanga atoke adharani na ajieleze kuhusu tuhuma za kampuni yake kuitia serekali hasara katika mkataba tete wa lugumi.

Mzee wa majibu Rais mpendwa wa tanzania tuonaomba utumbue hili jipu lililokaa pabaya.
 
Pumba at work. Zitto ni mnafiki na mzandiki na mla rushwa mkubwa. Ndiyo maana hata CDM walimfukuza, pamoja na kwenda mahakamani alifukuzwa. Zitto ni moja ya vijana wasioaminika ktk siasa za Tanzania. Alianzisha chama akiwa bado chadema, huyo nadhani siyo mtanzania halisi, anaweza akaivuruga Tanzania then akajiandaa kwenda nje ya nchi (kama alivyofanya chadema-kuanzisha chama wakati ni mwanachama wa chadema).
Naanza kuelewa kwanin mnaitwa manyumbu
 
CHAMA CHA ACT WAZALENDO
---------------------------------------------

KAMATI YA BUNGE NA SERIKALI ZA MITAA
TAARIFA MUHIMU KWA UMMA.
Ndugu wanahabari na watanzania kwa ujumla.

Mtakumbuka kwamba jana tarehe 13,04.2016 mmoja wa vijana wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) bwana Augustine Matefu alizungumza na waandishi wa habari na kuzungumzia masuala kadhaa huku akirusha tuhuma kwa wabunge na wafanya biashara mbali mbali mbunge na kiongozi wa chama chetu cha ACT-WAZALENDO ndugu Zitto Ruyagwa Kabwe.

Tuhuma zake zisizo na msingi bwana Matefu zinaweza zikatafsiriwa katika makundi makuu matatu kama ifuatavyo

i. Hofu ya rais wa Chama chake kushindwa kuongoza na hivyo kuandaa mazingira ya kuogopa kupingwa na kwamba kila atakayemkosoa basi atakuwa ametumwa.

ii. Kujipendekeza kwa viongozi wa chama chake kama wanavyofanya vijana wenzake wa CCM kipindi hiki wanachojiegemeza na viongozi wa Serikali kusubiria uteuzi wa Ukuu wa wilaya (U-DC) na hivyo kujitia upofu hata kwa vitu vilivyo wazi na kuonekana kabisa.

iii.Kujitwisha utetezi wa tuhuma za ubadhilifu zinazomkabili Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Bwana Charles Kitwanga za zaidi ya Shilingi Bilioni 34 kupitia kampuni yake ya Infosys iliyoshirikiana na Kampuni ya Lugumi katika mkataba wa Kifisadi walioshindwa kuutekeleza kama ilivyoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni.

Kwa msingi huo basi, kwa niaba ya Kamati ya Vijana ya Chama cha ACT-WAZALENDO. Tunamtaka ndugu Matefu na vijana wengine wote wa UVCCM na vyama vingine, ambao wameamua kujitwisha usemaji na utetezi wa wanasiasa,wafanyabiashara na taasisi mbalimbali kwa kuanzisha majina na ama majukwaa ama viji taasisi vya uongo na kweli ili kujipatia pesa na fursa (kama matefu alivyofanya) . waache mara moja kumuhusisha Kiongozi wa chama chetu na tuhuma zote zinazoendana na misingi ya chama chao (Chama cha mapinduzi).

Sio hulka wala mwenendo wa kiongozi wa Chama cha ACT-WAZALENDO kujihusiah na vitendo vyovyote vya matumizi mabaya ya ofisi, kuomba ama kupokea rushwa, na mengine yanayofanana na hayo. Na tabia hii kwa miongo kadhaa sasa imekuwa ikifanywa na viongozi na wanachama wa chama cha mapinduzi CCM (mifano ipo wazi).

Pamoja na mambo mengine. Tunahitaji kuona ifuatavyo

i. Rais John Magufuli, aache kuogopa kivuli chake kwa kuhisi kuna watu wana mpango wa kumuhujumu, mbunge wa chama chetu hatujamtuma kwenda bungeni kumuhujumu Magufuli, tumemtuma kwenda kuwasimamia na kuwapigania watanzania kwa kufuata misingi na itikadi ya ACT-WAZALENDO. Hivyo hatutarajii wala yeye hatarajii kuwa mtetezi wa Rais. Magufuli hata kama serikali yake itapeleka bungeni mapendekezo ya Hovyo.

ii. CCM na Serikali yake itambue kuwa Zitto Ruyagwa Kabwe ni Kiongozi wa chama cha siasa cha Upinzani kilichojipa wajibu wa kuwatetea watanzania, hivyo kamwe hatakuja kuwa mtetezi wa madudu yoyote yatakayofanywa na Magufuli na Serikali yake. Ni wajibu wa Zitto Ruyagwa Kabwe kuhakikisha CCM na Serikali yao inatoka Madarakani sio kuwatetea. Hivyo waache hofu.

iii. Tunamtaka Waziri wa mambo ya Ndani CHARLES KITWANGA aache kujificha kwenye koti la Rais MAGUFULI hasa kwenye hizi Tuhuma zinazomkabili za Kampuni ya INFOSYS kampuni yake binafsi yeye na Rafiki yake Mkurugenzi Mkuu wa NIDA la kuitia hasara serikali zaidi ya Bilioni 34 baada kushirikiana na kampuni ya LUGUMI na kushindwa kukamilisha zabuni waliyopewa. Na Badala yake ajitokeze hadhani na atoe ufafanuzi wa kwanini asipandishwe mahakamani kama wahujumu uchumi wengine walivyofanya.

iv. Tunamtaka Rais. John Magufuli, amchukulie hatua za kinidhamu haraka iwezekanavyo Waziri huyu anayediriki kutumia madaraka yake kusimamia kampuni zake binafsi za kibiuashara na kuitia hasara serikali huku ukizingatia inatumika pesa za walipa kodi masikini. Mpaka sasa Kitwanga anafanya mchezo huu.



Imetolewa leo

14.04.2016 na:-

Wiston A. Mogha

Kaimu Msaidizi wa Katibu Kamati ya Bunge na Serikali za Mitaa
ACT – WAZALENDO
Sasa nawe unawazuia vijana kujitwisha mzigo wa kuwatetea viongozi, wakati huo huo nawe unajitwisha mzigo wa kumtetea Zitto. Zitto katajwa kwa jina lake na hakuna ACT-wazalendo ilipotajwa. Kwa nini umtetee Zitto. Ajitokeze mwenyewe aseme anachokijua.

Miaka hii 5 lazima njaa ituume wotee! Tupate neema wotee!
 
CHAMA CHA ACT WAZALENDO
---------------------------------------------

KAMATI YA BUNGE NA SERIKALI ZA MITAA
TAARIFA MUHIMU KWA UMMA.
Ndugu wanahabari na watanzania kwa ujumla.

Mtakumbuka kwamba jana tarehe 13,04.2016 mmoja wa vijana wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) bwana Augustine Matefu alizungumza na waandishi wa habari na kuzungumzia masuala kadhaa huku akirusha tuhuma kwa wabunge na wafanya biashara mbali mbali mbunge na kiongozi wa chama chetu cha ACT-WAZALENDO ndugu Zitto Ruyagwa Kabwe.

Tuhuma zake zisizo na msingi bwana Matefu zinaweza zikatafsiriwa katika makundi makuu matatu kama ifuatavyo

i. Hofu ya rais wa Chama chake kushindwa kuongoza na hivyo kuandaa mazingira ya kuogopa kupingwa na kwamba kila atakayemkosoa basi atakuwa ametumwa.

ii. Kujipendekeza kwa viongozi wa chama chake kama wanavyofanya vijana wenzake wa CCM kipindi hiki wanachojiegemeza na viongozi wa Serikali kusubiria uteuzi wa Ukuu wa wilaya (U-DC) na hivyo kujitia upofu hata kwa vitu vilivyo wazi na kuonekana kabisa.

iii.Kujitwisha utetezi wa tuhuma za ubadhilifu zinazomkabili Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Bwana Charles Kitwanga za zaidi ya Shilingi Bilioni 34 kupitia kampuni yake ya Infosys iliyoshirikiana na Kampuni ya Lugumi katika mkataba wa Kifisadi walioshindwa kuutekeleza kama ilivyoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni.

Kwa msingi huo basi, kwa niaba ya Kamati ya Vijana ya Chama cha ACT-WAZALENDO. Tunamtaka ndugu Matefu na vijana wengine wote wa UVCCM na vyama vingine, ambao wameamua kujitwisha usemaji na utetezi wa wanasiasa,wafanyabiashara na taasisi mbalimbali kwa kuanzisha majina na ama majukwaa ama viji taasisi vya uongo na kweli ili kujipatia pesa na fursa (kama matefu alivyofanya) . waache mara moja kumuhusisha Kiongozi wa chama chetu na tuhuma zote zinazoendana na misingi ya chama chao (Chama cha mapinduzi).

Sio hulka wala mwenendo wa kiongozi wa Chama cha ACT-WAZALENDO kujihusiah na vitendo vyovyote vya matumizi mabaya ya ofisi, kuomba ama kupokea rushwa, na mengine yanayofanana na hayo. Na tabia hii kwa miongo kadhaa sasa imekuwa ikifanywa na viongozi na wanachama wa chama cha mapinduzi CCM (mifano ipo wazi).

Pamoja na mambo mengine. Tunahitaji kuona ifuatavyo

i. Rais John Magufuli, aache kuogopa kivuli chake kwa kuhisi kuna watu wana mpango wa kumuhujumu, mbunge wa chama chetu hatujamtuma kwenda bungeni kumuhujumu Magufuli, tumemtuma kwenda kuwasimamia na kuwapigania watanzania kwa kufuata misingi na itikadi ya ACT-WAZALENDO. Hivyo hatutarajii wala yeye hatarajii kuwa mtetezi wa Rais. Magufuli hata kama serikali yake itapeleka bungeni mapendekezo ya Hovyo.

ii. CCM na Serikali yake itambue kuwa Zitto Ruyagwa Kabwe ni Kiongozi wa chama cha siasa cha Upinzani kilichojipa wajibu wa kuwatetea watanzania, hivyo kamwe hatakuja kuwa mtetezi wa madudu yoyote yatakayofanywa na Magufuli na Serikali yake. Ni wajibu wa Zitto Ruyagwa Kabwe kuhakikisha CCM na Serikali yao inatoka Madarakani sio kuwatetea. Hivyo waache hofu.

iii. Tunamtaka Waziri wa mambo ya Ndani CHARLES KITWANGA aache kujificha kwenye koti la Rais MAGUFULI hasa kwenye hizi Tuhuma zinazomkabili za Kampuni ya INFOSYS kampuni yake binafsi yeye na Rafiki yake Mkurugenzi Mkuu wa NIDA la kuitia hasara serikali zaidi ya Bilioni 34 baada kushirikiana na kampuni ya LUGUMI na kushindwa kukamilisha zabuni waliyopewa. Na Badala yake ajitokeze hadhani na atoe ufafanuzi wa kwanini asipandishwe mahakamani kama wahujumu uchumi wengine walivyofanya.

iv. Tunamtaka Rais. John Magufuli, amchukulie hatua za kinidhamu haraka iwezekanavyo Waziri huyu anayediriki kutumia madaraka yake kusimamia kampuni zake binafsi za kibiuashara na kuitia hasara serikali huku ukizingatia inatumika pesa za walipa kodi masikini. Mpaka sasa Kitwanga anafanya mchezo huu.



Imetolewa leo

14.04.2016 na:-

Wiston A. Mogha

Kaimu Msaidizi wa Katibu Kamati ya Bunge na Serikali za Mitaa
ACT – WAZALENDO

Zzk ni mpambe wa dau na mmojawapo wa wafilisi wa nssf
 
kitwanga anatetewa nini na wanaccm. wananchi tunaomuamini mugufuli tunamtaka kitwanga atoke adharani na ajieleze kuhusu tuhuma za kampuni yake kuitia serekali hasara katika mkataba tete wa lugumi.

Mzee wa majibu Rais mpendwa wa tanzania tuonaomba utumbue hili jipu lililokaa pabaya.

Sasa kitwanga si akipewa kazi na lugumi yeye anahusika vipi,zzk anadhani ananasuka ktk ishu ya Nssf maana akipiga sana akiwa mwenyekiti wa PAC, ndo maana gazeti lake linajitahidi kumsafisha dau
 
Kwa mujibu wa taarifa za kibenki ambazo
Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu
imezipata, mnamo tarehe 10 Desemba, 2012,
Hifadhi ya Taifa ya Saadani ilihamisha jumla ya
shilingi 12,200,000 kwenda kwenye akaunti na.
0150357447800 iliyoko CRDB Bank tawi la
Pugu Road, Dar es Salaam, inayomilikiwa na
Leka Dutigite Ltd. Hifadhi ya Taifa ya Saadani
inamilikiwa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa
(TANAPA), ambayo ni shirika la umma. Siku
moja baadae, fedha hizo zilitolewa kwa pesa
taslimu kutoka kwenye akaunti hiyo.
Baada ya hapo, kati ya tarehe 14 Januari na 7
Februari, 2013, akaunti ya Leka Dutigite Ltd.
iliingiziwa jumla ya shilingi 28,600,000. Fedha
hizi zote ziliingizwa kama fedha taslimu na mtu
aitwaye Mchange (shilingi 3,600,000 tarehe 14
Januari, 2013) na Leka Dutigite (shilingi
25,000,000 tarehe 23 Januari na 7 Februari,
2013). Kufikia tarehe 7 Februari, 2013, fedha
hizo zote zilikwishatolewa benki.
Mheshimiwa Spika, Tarehe 28 Februari, 2013,
akaunti ya Leka Dutigite Ltd. iliingiziwa shilingi
32,367,000 na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya
Jamii (NSSF). Kwa mujibu wa taarifa za
kibenki, siku hiyo hiyo, fedha hizo zilitolewa
kwenye akaunti hiyo. Siku nne baadae, yaani
tarehe 4 Machi, 2013, NSSF ilifanya malipo
mengine kwenye akaunti ya Leka Dutigite Ltd.,
kwa mikupuo miwili, ya jumla ya shilingi
46,663,000. Siku hiyo hiyo, fedha hizo nazo
zilitolewa kutoka kwenye akaunti hiyo kwa
mikupuo miwili. Kwa hiyo, katika kipindi cha
miezi mitatu katika ya tarehe 10 Desemba,
2012 na 4 Machi, 2013, Leka Dutigite Ltd.
ililipwa shilingi 119,930,000 kwa utaratibu huo
huo wa ingiza na toa fasta. Kati ya fedha hizo,
shilingi 12,200,000 zililipwa na TANAPA na
shilingi 79,027,000 zililipwa na NSSF.
 
Kitwanga sio Anna kiasi cha kukubari kudhaliliswa watu wapate kick usitegemee atawajibishwa .
Zile pesa alizoficha Sasa kaamua kuzitumia kujisafisha katoa Rushwa kubwa Kwa kamati ya Bunge na wale wote waliotumwa kumchunguza , Lugumi kakimbia kinachofuata ni kubebeshwa Zigo lolote kisha Kitwanga aonekane hana Hatia , Hii ndiyo Tanzania kila jambo linawezekana kabsa.
 
Kwa mujibu wa taarifa za kibenki ambazo
Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu
imezipata, mnamo tarehe 10 Desemba, 2012,
Hifadhi ya Taifa ya Saadani ilihamisha jumla ya
shilingi 12,200,000 kwenda kwenye akaunti na.
0150357447800 iliyoko CRDB Bank tawi la
Pugu Road, Dar es Salaam, inayomilikiwa na
Leka Dutigite Ltd. Hifadhi ya Taifa ya Saadani
inamilikiwa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa
(TANAPA), ambayo ni shirika la umma. Siku
moja baadae, fedha hizo zilitolewa kwa pesa
taslimu kutoka kwenye akaunti hiyo.
Baada ya hapo, kati ya tarehe 14 Januari na 7
Februari, 2013, akaunti ya Leka Dutigite Ltd.
iliingiziwa jumla ya shilingi 28,600,000. Fedha
hizi zote ziliingizwa kama fedha taslimu na mtu
aitwaye Mchange (shilingi 3,600,000 tarehe 14
Januari, 2013) na Leka Dutigite (shilingi
25,000,000 tarehe 23 Januari na 7 Februari,
2013). Kufikia tarehe 7 Februari, 2013, fedha
hizo zote zilikwishatolewa benki.
Mheshimiwa Spika, Tarehe 28 Februari, 2013,
akaunti ya Leka Dutigite Ltd. iliingiziwa shilingi
32,367,000 na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya
Jamii (NSSF). Kwa mujibu wa taarifa za
kibenki, siku hiyo hiyo, fedha hizo zilitolewa
kwenye akaunti hiyo. Siku nne baadae, yaani
tarehe 4 Machi, 2013, NSSF ilifanya malipo
mengine kwenye akaunti ya Leka Dutigite Ltd.,
kwa mikupuo miwili, ya jumla ya shilingi
46,663,000. Siku hiyo hiyo, fedha hizo nazo
zilitolewa kutoka kwenye akaunti hiyo kwa
mikupuo miwili. Kwa hiyo, katika kipindi cha
miezi mitatu katika ya tarehe 10 Desemba,
2012 na 4 Machi, 2013, Leka Dutigite Ltd.
ililipwa shilingi 119,930,000 kwa utaratibu huo
huo wa ingiza na toa fasta. Kati ya fedha hizo,
shilingi 12,200,000 zililipwa na TANAPA na
shilingi 79,027,000 zililipwa na NSSF.
Tanzania ni Nchi Tajiri lakini kuna wajanja wengi pesa nyingi inapotelea kwenye matumbo ya wajanja wachache.
 
Back
Top Bottom