The Hunter
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 1,049
- 305
Kimsingi narejea hali halisi ambayo nchi yetu imekumbana nayo toka tulipopata uhuru
Vijana wengi wenye moyo walisahauliwa katika nafasi za kiuongozi na kimamlaka huku wakipoozwa na maneno ya vijana taifa la kesho,
Sisi wote ni mashuhuda nafasi nyingi toka ukuu wa wilaya mpaka ukatibu mkuu wa wizara, uwaziri na ukurugenzi hata uraisi umekuwa ni maalumu kwa wazee na wastaafu wa majeshi ama wateule wachache, kundi dogo la vijana lililopata kuambulia nafasi hizo either ni lile lenye undugu na ubini na watawala or nyumba ndogo za watawala.
Tukikumbuka matukio kama ya Bulyankulu ni wazee hawa hawa waliuza na kuruhusu wazawa kufukiwa kwenye mgodi ule.
Pale shinyanga pamebaki mashimo na mahandaki, vumbi na mabaki ya kemikali hii nikutokana na maamuzi ama ruhusa toka kwa wazee hawa, kama mtakumbuka uncle Benny alipozawadiwa ndama wa dhahabu nini kilitokea.
Kitalu C, na vingine vingi pale mererani vilipomilikishwa kwa wageni kipindi cha bwana Lyatonga akiwa waziri kilipelekea yote tunayoyaona Arusha leo, hakuna kazi vijana wamechoka, wamebaki kubeba mizigo ya watalii kama punda, na kuuza maziwa mjini.
Tukubali sasa yatosha, vijana wapewe nafasi ya kufanya maamuzi na kuongoza, tumeshaona mifano ya vijana ambao wamefanya ama wanafanya mambo makubwa kwenye majimbo yao mfano Ndugu Mnyika,ndugu Filikunjombe, ndugu Kabwe, ndugu Lema, ndugu Joseph Mbilinyi, ndugu Mdee Halima.
NB
Wazee wetu wachache kama kina Silaa, Mbowe, Lipumba, Marando, ambao wamejitahidi kuielimisha jamii na kuwapa nafasi vijana nyie ni nguzo yetu, tutawakumbuka na historia itawaenzi
Vijana wengi wenye moyo walisahauliwa katika nafasi za kiuongozi na kimamlaka huku wakipoozwa na maneno ya vijana taifa la kesho,
Sisi wote ni mashuhuda nafasi nyingi toka ukuu wa wilaya mpaka ukatibu mkuu wa wizara, uwaziri na ukurugenzi hata uraisi umekuwa ni maalumu kwa wazee na wastaafu wa majeshi ama wateule wachache, kundi dogo la vijana lililopata kuambulia nafasi hizo either ni lile lenye undugu na ubini na watawala or nyumba ndogo za watawala.
Tukikumbuka matukio kama ya Bulyankulu ni wazee hawa hawa waliuza na kuruhusu wazawa kufukiwa kwenye mgodi ule.
Pale shinyanga pamebaki mashimo na mahandaki, vumbi na mabaki ya kemikali hii nikutokana na maamuzi ama ruhusa toka kwa wazee hawa, kama mtakumbuka uncle Benny alipozawadiwa ndama wa dhahabu nini kilitokea.
Kitalu C, na vingine vingi pale mererani vilipomilikishwa kwa wageni kipindi cha bwana Lyatonga akiwa waziri kilipelekea yote tunayoyaona Arusha leo, hakuna kazi vijana wamechoka, wamebaki kubeba mizigo ya watalii kama punda, na kuuza maziwa mjini.
Tukubali sasa yatosha, vijana wapewe nafasi ya kufanya maamuzi na kuongoza, tumeshaona mifano ya vijana ambao wamefanya ama wanafanya mambo makubwa kwenye majimbo yao mfano Ndugu Mnyika,ndugu Filikunjombe, ndugu Kabwe, ndugu Lema, ndugu Joseph Mbilinyi, ndugu Mdee Halima.
NB
Wazee wetu wachache kama kina Silaa, Mbowe, Lipumba, Marando, ambao wamejitahidi kuielimisha jamii na kuwapa nafasi vijana nyie ni nguzo yetu, tutawakumbuka na historia itawaenzi