Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,131
- 35,168
Kwanza, ninapenda kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, washikaji na wanaJF walioguswa na kifo cha William Malecella. Mungu awape faraja katika kipindi hichi kigumu cha majonzi.
Sasa, twende moja kwa moia kwenye mada, kupitia mada hii, bila kuficha wala kumumunya maneno, William Malecela (Le mutuz) alijulikana na kufahamika zaidi kama mtu wa ovyo kwa sifa hizi (sifa ambazo alikuwa akijivunia nazo hadharani mitandaoni na mitaani);
1. Mpenda sifa popote.
2. Mpenda pombe.
3. Mpenda umalaya.
4. Mpenda maisha ya kujirusha na kuponda raha.
5. Mpenda kujipendekeza kwa watu maarufu (chawa)
Le Mutuz japokuwa alikuwa na umri wa zaidi ya miaka 50, akijaliwa kuwa na watoto, akipambana kwa namna mbalimbali kutafuta kipato, huku akitokea kwenye familia ya mzee Malecela yenye heshima kubwa sana kisiasa na kijamii ndani na nje ya Tanzania, lakini mienendo na tabia za Le mutuz zilikuwa zenye kutia aibu na kinyaa, akiishi kama kijana aliyepevuka juzi, aliyekosa malezi yoyote ya kijamii na kidini.
Japokuwa hayo yalikuwa ni maisha yake binafsi (sio busara sana kuyahukumu) lakini ni vyema kusema ukweli na kuweka angalizo muhimu kwa vijana ambao ndio wamejaa mtandaoni kuwa makini na kukwepa kuiga au kujifunza kupitia maisha binafsi ya Le mutuz ambayo yalijaa anasa na uchafu mwingi.
UKWELI USEMWE KIKAMILIFU.
Sasa, twende moja kwa moia kwenye mada, kupitia mada hii, bila kuficha wala kumumunya maneno, William Malecela (Le mutuz) alijulikana na kufahamika zaidi kama mtu wa ovyo kwa sifa hizi (sifa ambazo alikuwa akijivunia nazo hadharani mitandaoni na mitaani);
1. Mpenda sifa popote.
2. Mpenda pombe.
3. Mpenda umalaya.
4. Mpenda maisha ya kujirusha na kuponda raha.
5. Mpenda kujipendekeza kwa watu maarufu (chawa)
Le Mutuz japokuwa alikuwa na umri wa zaidi ya miaka 50, akijaliwa kuwa na watoto, akipambana kwa namna mbalimbali kutafuta kipato, huku akitokea kwenye familia ya mzee Malecela yenye heshima kubwa sana kisiasa na kijamii ndani na nje ya Tanzania, lakini mienendo na tabia za Le mutuz zilikuwa zenye kutia aibu na kinyaa, akiishi kama kijana aliyepevuka juzi, aliyekosa malezi yoyote ya kijamii na kidini.
Japokuwa hayo yalikuwa ni maisha yake binafsi (sio busara sana kuyahukumu) lakini ni vyema kusema ukweli na kuweka angalizo muhimu kwa vijana ambao ndio wamejaa mtandaoni kuwa makini na kukwepa kuiga au kujifunza kupitia maisha binafsi ya Le mutuz ambayo yalijaa anasa na uchafu mwingi.
UKWELI USEMWE KIKAMILIFU.