Tuache unafiki, sasa ndio nchi inagawanyika!

voicer

JF-Expert Member
Jul 13, 2020
5,553
11,885
Sasa tunao walamba asali, walamba shubiri, walala hoi na pia mafisadi papa na machawa wao! Mnajitoa akili sababu ya shibe haramu, mnasifia mlipostahili kukemea! Wabunge mmegeuka "wabonge". Mbunge mwenye akili timamu, anasimama na kuomba bei ya mafuta iongezwe (ulaaniwe Jerry Slaa). Bila hata aibu, wakati anaomba hivyo... Bei huko mitaani ziko hivi:
  • Sukari @kg 3,200/=
  • Mchele @kg 3,200/=
  • Sembe @kg 1,700/=
  • Nyama @kg 7,500/= mpaka 8,500/=
  • Mkaa gunia @ 70,000/=
  • Maharage @kg 4,000/=
Sasa bado hatujaongelea tozo kwenye miamala! Bei za vifaa tiba bei juu! Madawa bei juu, huku hata upatikanaji wake ukiwa ni 30% huko kwenye hospitali za umma. Kiwango cha elimu shule za umma iko hoi!

Malipo ya wafanyakazi wanaostaafu au kuachishwa kazi kwenye mifuko ya pensheni yamegeuka sababu kuu ya vifo kwa wastaafu hao, kisa hayatolewi kwa wakati stahiki.

Lakini wafanyakazi na maafisa wa mashirika hayo, wanazitumia pesa za wastaafu kwa kujikopesha kiasi kwamba, mikopo yao inaelekea kulingana na pato zima la mifuko hiyo!

Rushwa mitaani na kwenye ofisi za umma imerejea kwa kasi ya kutisha!

Ubadhirifu kuanzia miradi ya kimkakati hadi Tamisemi ni wa kutisha, na pengine ni haijawahi kutokea katika historia ya nchi hii.

Ripoti ya CAG inatisha kuisoma, halafu Spika wa bunge, anawazuia wabunge kuhoji bungeni... eti mpaka baada ya miezi saba kuanzia sasa.

Huku wajinga fulani, waandishi habari wasakatonge, wanajiundia cartel pamoja na mafisadi wa Tanesco, mafisadi wa mashirika ya mawasiliano, mafisadi wa hazina ya taifa, mafisadi wa miundombinu ya nchi hii.

Eti wanaandika kitabu kuhusu miradi ya wilayani Chato, kwamba ni kielelezo cha udikteta wa Magufuli.

Ila wanashindwa kutuandikia kama kuna tofauti gani kati ya miradi ya Chato na hii mingine ambayo yote aliiasisi Magufuli kama vile:
  • Mahospitali na vituo vya afya zaidi ya 360 nchi nzima.
  • Mitambo mipya ya vipimo kwenye hospitali zote za rufaa nchi nzima.
  • Miradi ya ujenzi wa masoko mapya ya kisasa mikoani.
  • Bwawa la umeme la JNHP.
  • Reli mpya ya kisasa ya SGR, ambayo sasa wanaifisadi kwa kwenda mbele.
  • Ujenzi wa meli mpya ziwa Victoria na Ziwa Nyasa, pamoja na ukarabati mkubwa wa MV Victoria.
  • Ujenzi wa daraja la Sallender, ambalo wao wamekuja kulipa jina jipya la Tanzanite.
  • Ujenzi wa daraja jipya la Mto Wami.
  • Ujenzi wa daraja jipya la Kigongo - Busisi la kipekee na la kwanza kwa urefu Afrika Mashariki.
  • Ununuzi wa Rada mpya nne, uliopelekea nchi kuingiza mapesa ya kigeni, kutokana na huduma tunayoitoa kwa nchi jirani za Kenya, Rwanda, Burundi na DRC.
  • Ufufuaji wa viwanda vya viatu na samani, pamoja na kilimo vinavyomilikiwa na majeshi yetu ya Magereza, JKT na hata JWTZ.
  • Ununuzi wa madawati kwa shule zote za umma nchi nzima.
  • Kukomesha tatizo la ukatikaji wa umeme, iko chini ya shirika la Tanesco nchini.
  • Kuwakamata bila uoga mafisadi, pamoja na vibaraka wao na kuwasweka lupango bila uoga.
  • Kuondoa vyeti feki kwenye ajira rasmi za umma.
  • Kukomesha mishahara hewa na kutumbua wazembe na wabadhirifu bila haya.
  • Ujenzi na ukamilishwaji wa Nyumba za Maghorofa ya Magomeni Quarters!
  • Ujenzi wa hosteli za Chuo Kikuu UDSM na kuondoa kero iliyokuwepo.
  • Ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami kote jijini Dar es Salaam.
  • Kuihamishia serikali makao makuu Dodoma na ujenzi wa Ikulu mpya ya Chamwino!
Mambo ni mengi huwezi kuyataja humu yote.....
Magufuli hachafuki, kadri mnavyotaka kumchafua ndivyo mnavyochafuka nyinyi vibaraka wa mafisadi mpaka siku zenu zitakapotimia.
 
Uzuri yote hayo yanafanywa na chama chako
Acha upumbavu,ifike wakati muelewe kwamba kuwa CCM sio hoja ya kuwahusisha wote na huo upumbavu unaoendelea!

Sio kila mwana CCM anafurahia kinachoendelea kwa sasa!
Ndio maana hata upinzani wa kweli uko huko huko ndani ya CCM na sio huku kwa walambishwa asali.

Ndio sababu unaona huyo mama haishi panguapangua kwa hifu aliyonayo sababu anaujua ukweli.

Watanzania wengi mmelemazwa na huu upumbavu wa kuona kila mwanachama anashiriki ujinga wote wa chama chake ilhali sivyo inavyokuwa.
 
Umeongea sana Mkuu Binafsi viongozi wa aina hii nimemuachia Mungu atajua cha kuwafanya kama si wao basi hata vizazi vyao nimechoka kabisa na kukata tamaa ya maisha.
 
Sasa tunao walamba asali, walamba shubiri, walala hoi na pia mafisadi papa na machawa wao! Mnajitoa akili sababu ya shibe haramu, mnasifia mlipostahili kukemea! Wabunge mmegeuka "wabonge". Mbunge mwenye akili timamu, anasimama na kuomba bei ya mafuta iongezwe (ulaaniwe Jerry Slaa). Bila hata aibu, wakati anaomba hivyo... Bei huko mitaani ziko hivi:
  • Sukari @kg 3,200/=
  • Mchele @kg 3,200/=
  • Sembe @kg 1,700/=
  • Nyama @kg 7,500/= mpaka 8,500/=
  • Mkaa gunia @ 70,000/=
  • Maharage @kg 4,000/=
Sasa bado hatujaongelea tozo kwenye miamala! Bei za vifaa tiba bei juu! Madawa bei juu, huku hata upatikanaji wake ukiwa ni 30% huko kwenye hospitali za umma. Kiwango cha elimu shule za umma iko hoi!

Malipo ya wafanyakazi wanaostaafu au kuachishwa kazi kwenye mifuko ya pensheni yamegeuka sababu kuu ya vifo kwa wastaafu hao, kisa hayatolewi kwa wakati stahiki.

Lakini wafanyakazi na maafisa wa mashirika hayo, wanazitumia pesa za wastaafu kwa kujikopesha kiasi kwamba, mikopo yao inaelekea kulingana na pato zima la mifuko hiyo!

Rushwa mitaani na kwenye ofisi za umma imerejea kwa kasi ya kutisha!

Ubadhirifu kuanzia miradi ya kimkakati hadi Tamisemi ni wa kutisha, na pengine ni haijawahi kutokea katika historia ya nchi hii.

Ripoti ya CAG inatisha kuisoma, halafu Spika wa bunge, anawazuia wabunge kuhoji bungeni... eti mpaka baada ya miezi saba kuanzia sasa.

Huku wajinga fulani, waandishi habari wasakatonge, wanajiundia cartel pamoja na mafisadi wa Tanesco, mafisadi wa mashirika ya mawasiliano, mafisadi wa hazina ya taifa, mafisadi wa miundombinu ya nchi hii.

Eti wanaandika kitabu kuhusu miradi ya wilayani Chato, kwamba ni kielelezo cha udikteta wa Magufuli.

Ila wanashindwa kutuandikia kama kuna tofauti gani kati ya miradi ya Chato na hii mingine ambayo yote aliiasisi Magufuli kama vile:
  • Mahospitali na vituo vya afya zaidi ya 360 nchi nzima.
  • Mitambo mipya ya vipimo kwenye hospitali zote za rufaa nchi nzima.
  • Miradi ya ujenzi wa masoko mapya ya kisasa mikoani.
  • Bwawa la umeme la JNHP.
  • Reli mpya ya kisasa ya SGR, ambayo sasa wanaifisadi kwa kwenda mbele.
  • Ujenzi wa meli mpya ziwa Victoria na Ziwa Nyasa, pamoja na ukarabati mkubwa wa MV Victoria.
  • Ujenzi wa daraja la Sallender, ambalo wao wamekuja kulipa jina jipya la Tanzanite.
  • Ujenzi wa daraja jipya la Mto Wami.
  • Ujenzi wa daraja jipya la Kigongo - Busisi la kipekee na la kwanza kwa urefu Afrika Mashariki.
  • Ununuzi wa Rada mpya nne, uliopelekea nchi kuingiza mapesa ya kigeni, kutokana na huduma tunayoitoa kwa nchi jirani za Kenya, Rwanda, Burundi na DRC.
  • Ufufuaji wa viwanda vya viatu na samani, pamoja na kilimo vinavyomilikiwa na majeshi yetu ya Magereza, JKT na hata JWTZ.
  • Ununuzi wa madawati kwa shule zote za umma nchi nzima.
  • Kukomesha tatizo la ukatikaji wa umeme, iko chini ya shirika la Tanesco nchini.
  • Kuwakamata bila uoga mafisadi, pamoja na vibaraka wao na kuwasweka lupango bila uoga.
  • Kuondoa vyeti feki kwenye ajira rasmi za umma.
  • Kukomesha mishahara hewa na kutumbua wazembe na wabadhirifu bila haya.
  • Ujenzi na ukamilishwaji wa Nyumba za Maghorofa ya Magomeni Quarters!
  • Ujenzi wa hosteli za Chuo Kikuu UDSM na kuondoa kero iliyokuwepo.
  • Ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami kote jijini Dar es Salaam.
  • Kuihamishia serikali makao makuu Dodoma na ujenzi wa Ikulu mpya ya Chamwino!
Mambo ni mengi huwezi kuyataja humu yote.....
Magufuli hachafuki, kadri mnavyotaka kumchafua ndivyo mnavyochafuka nyinyi vibaraka wa mafisadi mpaka siku zenu zitakapotimia.

Ni hivi, dhalimu ni dhalimu hata ungekesha hapa jukwaani kumtetea. Unadhani hatujui tofauti ya dhalimu na hayo uliyolist hapo juu? Na kwa yako taarifa haitakaa itokee nchi hii kutawaliwa tena na mshamba wa style ile.
 
Kuna bei za vitu hutakiwi kuziweka hapa kwa maana bei hutokana na mazingira halisi. Mfano KYELA mchele huwezi nunua kwa 3200 huo ni Uongo, au Maharage Mbeya huwezi nunua kwa 3000.

Hali kama hiyo ipo kwenye NYAMA, huwezi nunua Shinyanga nyama 8500 lkn ukienda Mtwara utanunua 9000
Hali kadharika ukienda Mtwara Korosho utanunua kwa kilo 15000 lkn ukienda Arusha si chini ya 30000.

Unapotoa hoja zingatia mazingira, wewe uko Singida huko basi unadhani Tanzania nzima bei iko hivyo.
 
Hizo takataka zenu mnazohubiri hapa kila siku kwa kutokubaliana na ukweli kwamba mungu wenu hayupo ndo zinagawa watu sasa!
Hata Hitler alijenga barabara na viwanda lakini alikufa na taifa likaendelea sembuse nyie wanyea kwenye mashimo?
Kwamba kwasababu fulani amefariki basi matatizo yameongezeka huo ni unafiki mkubwa ambao mm naukataa
Mtu ambae hakuajiri watu miaka 6 na kupandisha mishahara anaonekanaje kwamba Ali solve matatizo?
Mtu ambaye alidanganua taifa kwamba anajenga viwanda kumbe uongo hili mbona hamsemi?
Ni mpumbavu mmoja kama wewe tu!
Ni mbinafsi mmoja tu kama wewe!
Ni mjingamjinga mmoja tu kama wewe!
Ambaye wajati tunaangalia yaliyoko mbele yetu,wewe bado umeshikilia koleo pembeni ya kaburi la mfu aliyeondoka Duniani miaka miwili iliyopita!

Ambae wewe Kinoamiguu mjinga ambae hata ripoti ya CAG bado unataka ukasome na Marehemu Magufuli!

Tatizo lako ni msongo wa mawazo uliopitiliza,....

Ninas8kitika kuchangia uraia na wapuuzi kama wewe usiyejitambua hata kujua ulikuja Duniani kufanya nini?
 
Acha upumbavu,ifike wakati muelewe kwamba kuwa CCM sio hoja ya kuwahusisha wote na huo upumbavu unaoendelea!

Sio kila mwana CCM anafurahia kinachoendelea kwa sasa!
Ndio maana hata upinzani wa kweli uko huko huko ndani ya CCM na sio huku kwa walambishwa asali.

Ndio sababu unaona huyo mama haishi panguapangua kwa hifu aliyonayo sababu anaujua ukweli.

Watanzania wengi mmelemazwa na huu upumbavu wa kuona kila mwanachama anashiriki ujinga wote wa chama chake ilhali sivyo inavyokuwa.
Umelima ekari ngapi za mahindi, maharage na mpunga!?
 
Umeongea sana Mkuu Binafsi viongozi wa aina hii nimemuachia Mungu atajua cha kuwafanya kama si wao basi hata vizazi vyao nimechoka kabisa na kukata tamaa ya maisha.
Asante kaka tuko pamoja,Tanzania ni tatizo kubwa ukiiongezea viongozi wa aina tulio nao!
 
Uko sahihi,tatizo ni kwamba sasa hivi hakuna upinzani makini nchi hii.
Angalia jana ACT wamezuiwa maandamano yao,lakini wakachukulia poa as if hakukuwa na hoja makini.
Ulitegemea upinzani imara utoke wapi kwa mungu? Ulipozuiliwa kufanya shughuli zake kihalali wewe si ulikuwepo na ulishangilia kwamba ni sawa tu kwakuwa tunajenga madaraja? Ulitegeme upinzani utoe wapi huo uimara sasa?
Wabunge wa upinzani walipo nunuliwa kwa kilichoitwa kuunga mkono juhudi wewe ulikuwepo na ulishangilia kwakuwa tunajenga viwanja vya ndege vijijini kwetu huo upinzani uimara wautoe wapi sasa
Viongozi wa upinzani wamepigwa risasi hadharani kama wezi, wameswekwa ndani kwa kesi za kuogofya kabisa nyie mlikuwa mnashangilia leo unataka CHADEMA , ACT na wengine wawe imara kwakuwa mungu kawapoka mate?
Wewe na wenzio wa legacy hamna lolote jema kwa TANZANIA ni mkate tu kuponyoka
MNATAKA UPINZANI IMARA LEO?
 
Ni mpumbavu mmoja kama wewe tu!
Ni mbinafsi mmoja tu kama wewe!
Ni mjingamjinga mmoja tu kama wewe!
Ambaye wajati tunaangalia yaliyoko mbele yetu,wewe bado umeshikilia koleo pembeni ya kaburi la mfu aliyeondoka Duniani miaka miwili iliyopita!

Ambae wewe Kinoamiguu mjinga ambae hata ripoti ya CAG bado unataka ukasome na Marehemu Magufuli!

Tatizo lako ni msongo wa mawazo uliopitiliza,....

Ninas8kitika kuchangia uraia na wapuuzi kama wewe usiyejitambua hata kujua ulikuja Duniani kufanya nini?
Lakini,ni wewe ndiye unaonekana haujaanua matanga.Bado una sonona na ni sadist!Watu hawakuyapenda yale maisha ya kupelekeshwa,kufunguliana kesi za uongo,kupigwa bila kosa,kudhulumiwa mali na hata wengine kupotezwa na kuuwawa.Ni bora ujinyonge tu kama bei za bidhaa zinakushinda.KUMBUKA kutumia kamba ya bei rahisi na ujichimbie mwenyewe shimo la kukufukia.
 
Back
Top Bottom