Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,582
- 113,795
Wanabodi,
Leo ni kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha mtangazaji huyu mwanamke wa RTD baadaye TBC, Halima Mchuka, aliyefariki siku kama ya leo, miaka 10 iliyopita.
Huyu ndiye Mtangazaji mwanamke wa kwanza wa RTD kutangaza mpira redioni , enzi hizo RTD sasa TBC, na mpaka leo ni miaka 10 baada ya kifo chake, bado ameacha legacy inayoishi hadi leo, kwani mpaka leo, bado Tanzania, hatuna mtangazaji mwingine yoyote wa kike wa mpira wa miguu yaani kabumbu redioni. (correct me if I'm wrong maana redio sasa ni nyingi).
Hebu tujikumbushe kidogo kwa kibwagizo hiki cha video hii, ya sauti ya Halima Mchuka, kwa hisani ya Mtangazaji mwenzake, Aboubakar Liongo
Halima Mchuka, aliacha mume na watoto watatu, Amina, Yekini na Prince Naseem, jee vipi majaaliwa ya familia yake na watoto wake aliyewaacha huku nyuma?. Sisi ambao ni wafanyakazi wenzake, marafiki zake na watu wake wa karibu, jee tulimjali, hata tuu kuwajulia hali?.
Kisomo Cha Halima Mchuka.
Kwa mujibu wa dada mkubwa wa Halima Mchuka, Mwajuma Mchuka, aliyekuwa ATC, kwa jina maarufu la Da Mwajuma,
Wale wenye mapenzi mema na Halima Mchuka, tukutane leo, 29/12/2021 Saa 10: 00 Jioni pale Nyumbani kwa Mwajuma Mchuka, Msasani Mwisho/ Masaki Dar es Salaam, to pay our tribute to this lovely Lady, Halima Mchuka kwa kuhudhuria kisomo hicho.
Kwa wale mtakaokuwa na nafasi kujumuika nasi, wasisiana na Da Mwajuma 0784737253
Na mwisho tujikumbushe kile kilichotokea miaka 10 iliyopita, wakati wa msiba wa Halima Mchuka
Halima Mchuka, Tutakukumbuka Daima.
RIP HALIMA MCHUKA.
Paskali.
Leo ni kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha mtangazaji huyu mwanamke wa RTD baadaye TBC, Halima Mchuka, aliyefariki siku kama ya leo, miaka 10 iliyopita.
Huyu ndiye Mtangazaji mwanamke wa kwanza wa RTD kutangaza mpira redioni , enzi hizo RTD sasa TBC, na mpaka leo ni miaka 10 baada ya kifo chake, bado ameacha legacy inayoishi hadi leo, kwani mpaka leo, bado Tanzania, hatuna mtangazaji mwingine yoyote wa kike wa mpira wa miguu yaani kabumbu redioni. (correct me if I'm wrong maana redio sasa ni nyingi).
Hebu tujikumbushe kidogo kwa kibwagizo hiki cha video hii, ya sauti ya Halima Mchuka, kwa hisani ya Mtangazaji mwenzake, Aboubakar Liongo
Halima Mchuka, aliacha mume na watoto watatu, Amina, Yekini na Prince Naseem, jee vipi majaaliwa ya familia yake na watoto wake aliyewaacha huku nyuma?. Sisi ambao ni wafanyakazi wenzake, marafiki zake na watu wake wa karibu, jee tulimjali, hata tuu kuwajulia hali?.
Kisomo Cha Halima Mchuka.
Kwa mujibu wa dada mkubwa wa Halima Mchuka, Mwajuma Mchuka, aliyekuwa ATC, kwa jina maarufu la Da Mwajuma,
Wale wenye mapenzi mema na Halima Mchuka, tukutane leo, 29/12/2021 Saa 10: 00 Jioni pale Nyumbani kwa Mwajuma Mchuka, Msasani Mwisho/ Masaki Dar es Salaam, to pay our tribute to this lovely Lady, Halima Mchuka kwa kuhudhuria kisomo hicho.
Kwa wale mtakaokuwa na nafasi kujumuika nasi, wasisiana na Da Mwajuma 0784737253
Na mwisho tujikumbushe kile kilichotokea miaka 10 iliyopita, wakati wa msiba wa Halima Mchuka
Tribute to Halima Mchuka: Alikuwa Mtu wa Watu!
Wanabodi Leo saa 11:30 alfajiri nimepokea simu ya Da Mwajuma Mchuka kunijulisha kuhusu huu msiba!. Hii ni thread ya Tribute kuhusu nilivyomfahamu marehemu, Halima Mchuka. Kwanza jikumbushe sauti yake Video kwa hisani ya Aboubakar Liongo. Pia Baadhi ya Tasirwa mbalimbali za Halima Mchuka...
www.jamiiforums.com
RIP HALIMA MCHUKA.
Paskali.