Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Magari ya kifahari ya viongozi wa serikali bado yananunuliwa licha ya Pinda kusema kuwa hayatonunuliwa tena
 
Jeshi la polis halifanyi kazi kwa kufuata sheria za nchi na za Jeshi la Polisi ila linafanya kwa muongozo wa bei, una bei gani ndiyo wakupatie huduma.

Sasa hapa ndipo hata wasiokuwa na hatia hupata makosa ya kutengenezewa.
 
Kuna jipu lipo Monduli
Mkuu wa shule ya Sekondari Irkisongo, kuna michango ya wazazi ya kuendesha shule, kuna fedha toka Serikalini, kuna wafadhili toka nje ya nchi kama Uholanzi. n.k

Hizo fedha zimekuwa zikipigwa kwa miaka kadhaa.

Pale panahitaji CAG aende mwenyewe na team yake. Hao wakaguzi wanaotumwa pale ni njaa tu, wanapoozwa na hela hizohizo.
 
WAKUU, yeyote aliyewahi kupanda mlima Kilimanjaro lazima ajue kituo kimoja kinachoitwa HARO. Kipo juu zaidi.

Sehemu hiyo kuna jiwe kubwa ukijaribu kulizunguka jiwe hilo utaona kuna jembe ukiangalia zaidi utaona FUVU la binadamu hapo na mifupa ya binaadamu inaonesha uyo mtu alikufa kipindi kirefu sana uwenda ikawa ni zaidi ya miaka 25+ iliyopita.

Sasa basi wausika na mlima huo wajaribu kuangalia hilo ili wageni wasijeona ikawaongopesha.
 
UBALOZI WA TANZANIA LONDON, UNITED KINGDOM pt 1

Madereva wa watumishi wa ubalozi.

Ukitazama structure ya Jiji la London na ukiwa unafanya Kazi kwenye City, hakuna ulazima zima wa kuwa Na Gari let alone kuwa Na Dereva wa kukuendesha.

Jiji ambalo meya wake anatembea kwa baiskeli, Waziri mkuu na Chancellor of exchequer mara kwa mara wanasafiri kwa Train.

Tufanye Hesabu kidogo:

Mshahara wa dereva wastani ni £9 kwa saa. Congestion charge(gari kuingia kati kati ya jiji) £11 kwa siku. Mafuta £15 kwa siku.
£9 x 7.5 masaa ya kazi kwa siku =£67.5 kwa siku x 5 siku za kazi kwa wiki= £335 kwa wiki.
£11x 5 siku=£55 kwa wiki
£15x5 siku= £75 kwa wiki
Jumla £465 kwa wiki x 52 wiki kwa mwaka= £24180x 3200 change ya pound kwa shilings= 77,376,000 shillings kwa mwaka.

Nawafahamu wafanyakazi wanne ambao wana Madereva.

77,376,000 x 4 watumishi= 309,504,000 tsh kwa mwaka gharama za kuendeshwa na gari kwa watumishi wa 4 wa ubalozi.

Nyumba wanazoishi:
B
aadhi ya watumishi wa Ubalozi wanaishi maeneo ya Hendon, Finchley na Golders Green, ukiingia kwenye website ya http://www.rightmove.co.uk ukiangalia rent ya nyumba ya vyumba vi 3 maeneo hayo ni kati £2,000 hadi £3,000.

Council tax(kodi ya serikali za mitaa) Maeneo hayo ya Hendon ni Band B ambapo wanatakiwa kulipa £857 kwa mwaka.

Ikiwa kama serikali ndio inawalipia kodi watumishi wake hesabu ina kuwa hivi.

£2000 x 12= £24,000 + £857 Council Tax=£24,857.

Ikiwa kama watalipiwa umeme na gesi, umeme na gesi wastani ni £30 kwa wiki x 52=£1560 kwa mwaka.

£24,857 x 3200 pound kwa shilling = 79,542,400 shilling kodi ya nyumba 1.

£1560 x 3200 pound kwa shilling = 4,992,000 shilling gharama za umeme na gesi.

Watu 4 for sure watakuwa wanalipiwa kodi na serikali.

79,542,400 x 4 (balozi, naibu, admin na mwambata) =318,169,600 kwa mwaka.

Kama wanalipiwa gas na umeme 4,992,000 x 4 = 19,968,000 kwa mwaka.

Hitimisho:

Nyumba na gari watumishi wa 4 jumla ni 627,673,600 shilling kwa mwaka.

Tuanze na hivi kwanza halafu tutaendelea na pt 2.
 
Jipu hili hapa:

Kuna meli huleta malighafi za viwanda vya Saruji nafikiri malighafi hiyo juitwa "crinca" material hayo huwa na uzito mkubwa, mwenye tenda ya kuyatoa badarini akisema afuate sheria kama wanavyotaka TANROADS haiwezi kupata faida kwani atalazimika kukodi magari mengi au magari aliyonayo yatalazimika kurudia mara nyingi.

Ili kuepuka hilo, mwenye tenda hutoa kama 20mln kwa msimamizi wa vijana Wa mzani hasa ule unaotembea na baada ya hapo wale wafanyakazi wanapatrol usiku na mchana huagizwa wasionekane katika barabara ambako mzigo huo utapita, baada ya mwenye tenda kuwa amemaliza mzigo wake bandarini humpigia mhusika sim basi mzani hurejea kazini kama kawaida. Hapo watanyanyasa watu mchanga, kokoto, matofali, vifusi, mawe nk.

Hilo ndo jipu linalotakiwa kutumbuliwa ili kuokoa Barbara zetu na kuongeza mapato
Mkuu eleza barabara husika ili wanusika walifanyie kazi
 
Tanzania Police Force.....

Fanya uende kituo cha Police ama upate road accident kisha wao wawe ni msaada kwako kufanikisha suluhu ya tatizo lako...

Hilo lipo wazi... utaona mwenyewe kwamba hawa tuwa group wapi...

No grudges officers
 
Jipu kubwa zaidi lipo kwa uhamiaji kuna wahamiaji haramu wanaofanya kazi bila vibali na hawana vibali vya kuishi nchini pia. Tumetoa sana ripoti kwa maafisa wa uhamiaji lakini tukageuziwa kibao tukaitwa na boss tueleze kwa nini tunataka kuua kampuni yake yeye hana pesa ya kulipia wageni maana wapo zaid ya 50 so serikali hapa imekosa zaidi ya million 100. Huyo afisa aliyetuchoma anaitwa John M jina la pili tumemstai kwa sasa tu natafuta namna ya kuakikisha tunafikisha hizi taarifa kwa Magufuli maana huyo Waziri Kitwanga nae ni mzigo tu hatumuamini.

Huu ni ujipu wa hali ya juu sisi tunatoa sapoti kwa taifa wao wanaenda kuchukua rushwa alafu wanatuchoma. Uhamiaji ni jipu jipu kubwa sana.
Toa direction vizuri mkuu tukuoneshe kazi inavyofanywa?
 
Wafanyakazi wa kitengo cha mipango miji Halmashauri ya Kinondoni wanatakiwa watumbiliwe haraka iwezekanavyo.

Hawa wafanyakazi hasa cartographers ambao wengi wao ni wakina mama wa makamo wakiongozwa na mama mmoja wa kipare wanakalia kazi walizoambiwa warekebishe na wizara ili kuwawezesha wananchi wapewe hati zao.

Hati nyingi hazijakamilika kule wizarani kwasasababu "VIZIDUO" vilivyoambatanishwa toka wizarani havijafanyiwa kazi na wahusika wanaomba rushwa mpaka ya shs.700,000 mpaka shs 800,000 ili wawakamilishie wahusika vizuduo vyao na kuvipeleka wizarani!!

Kuna umuhimu wa kuwamulika vizuri hawa cartographers ambao ni watu wazima na heshima zao lakini wanawasumbua wananchi kwa kutotimiza wajibu wao na kuomba rushwa.

Mimi ni muhanga wa tatizo hili na natarajia kwenda kumuona mkurugenzi wa halmashauri nione nae atalishuhulikia vipi kwani ninafuatilia hati yangu toka mwaka 2010 NA SIKO TAYARI KUHONGA!!!

Hawa cartographers hawajui kuwa kwa ufisadi wao huo wanaikosesha serikali mapato kutokana na land rent ambayo hailipwi kwani wananchi hawajapewa hati zao!!
 
Hili jambo hata mimi limenikuta.ila suluhisho la hawa watu aidha ni kuwakazia wakuandikie risit halali au kuwaweka hadharani kwa smartphone,wanakwepa sana kodi.
Watanzania tunalalamika mno mpaka inakera ebo! hivi wewe na akiri yako unatoa laki unaandikiwa elfu ishirini unakubalije kuondoka na kuja kulalamika kwenye mitandao, wewe mwenyewe ni jipu kwani umeshiriki kuiibia serikali.
 
Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu sana hapa JF kuhusu trafiki na RTO wao mkoani Arusha, hili mbona TAKUKURU wamelikalia kimya?

Kwamba Arusha hakuna TAKUKURU au ni hadi Mh Rais aanze kufuatilia ndipo na wao waamke kuitisha mafaili waonekane wako busy???

Kuna kipindi nilisema Mh Rais ana lengo zuri sana na utawala wa nchi hii ila kumteua aliyewahi kuwa Polisi kuongoza TAKUKURU au TISS atazorotesha uchunguzi na utumbuaji ndani ya jeshi la polisi kwa maana wote wanajuana.

Naamini ingekuwa ni taasisi nyingine inalalamikiwa tayari TAKUKURU wangesha ingilia kati.
 
Asilimia kubwa ya maafisa wa jeshi la polisi, magereza na JWTZ ( maafisi kuanzia nyoto moja) watumia Magari binafsi hayana vibali vya kuwa barabarani na kodi:
- Road licences
- Car Insurance
Etc etc

Hii ni kutokana Na kwamba wakisimamishwa wanaitana afande afande afande Ndio imetoka hiyo, au kuvaa sare zao Za kijeshi.

Maafisa wakuu wa majeshi wakague Magari ya watumishi wao inatia aibu polisi kuongoza kwa kuvunja sheria, majeshi yote yaanzishe ukaguzi wa magari yanayoingia kwenye maeneo yao ili kulinda nidhamu majeshini.

Lazima kuwe Na utaratibu wa hawa watu kukaguliwa kitofauti, au wakuu wa majeshi watangaze zawadi Kwa watakao waumbua hawa watu. Kama askari anavunja sheria hivi ndogo ndogo basi ni mwanzo wa kuwa askari mchafu
 
Jipu kubwa liko Chuo kikuu cha kilimo cha sokoine, SUA. Hapa kuna matatizo mawili makubwa mawili:

1. Wizi na ufisadi
2. Ukabila ktk uongozi

Kuna wizi wa muda mrefu hapa sua na sehemu kubwa ya wizi unafanyika kupitia miradi ya ujenzi wa majengo. Kila jengo liliojengwa kwa miaka 8 ilyopita hadi sasa halina kiwango. Majengo yote yameonta nyufa mengine baada ya miaka mitatu tu.

Viongozi wa chuo tayari wameshamdaka naibu katibu mkuu anayejihusisha na vyuo vikuu na amekwisha watembelea. Badala ya kukagua majengo aliyotajiwa kwamba ni mabovu, yeye amejitia upofu na kuamua ni mazuri na ni baada ya kutembelea majengo mengine kabisa! Naona ni ushirikiano maana naye naibu katibu mkuu alitokea kwenye Taasisi za Elimu.

Ukabila ni mkubwa kiasi kwamba sasa lazima uwe unatokea miko a ya kusini ili uweze kupewa madaraka. Uongozi wa chuo sasa unalazimisha hata promosheni za wafanyakazi toka mikoa ya kusini na hasa Iringa ili tu waweze kupewa madaraka.

Tunaomba Serikali iingilie kati michakato ya kuwapata viongozi maana pia inasimamiwa kwa miaka mingi na viongozi toka mikoa ya kusini kwa makusudi kabisa!!
 
Jumanne tuliambiwa eti mabasi ya mwendokasi Yataanza kufanya kazi kesho Yake Yaani Jumatano.

Cha kushangaza mpaka sasa hivi hamna kinachoendelea.

Hilo si jipu Jamani!
 
ARDHI- MIPANGO MJI ARUSHA NI JIBU KUBWA, WAKATI RAIS AKIHIMIZA MAENDELEO NA WATENDAJI KATIKA MAOFISI YA SERIKALI KWENDA NA KASI YA RAIS KIUTENDAJI OFISI NILIYOITAJA IMEONEKANA KWAMBA NI TOFAUTI KABISA.

KUNA WATU WAMEOMBA VIBALI VYA UJENZI TANGU MWEZI WA KUMI NA MBILI MWAKA JANA 2015 NA HADI LEO HII HAWAJAPEWA PAMOJA NA KWAMBA WAMEKAMILISHA TARATIBU ZOTE ZINAZOTAKIWA KISHERIA IKIWA NI PAMOJA NA KUPELEKA MICHORO NA VIBALI KUTOKA NEMC NA SOIL LAKINI CHA AJABU NI KWAMBA WAHUSIKA KTK OFISI TAJWA WAMEKUWA WAKIZUNGUSHA KTK SWALA LA KUTOA VIBALI KWA WAHUSIKA NA HAPA HAWATAMKI AMA KUTOA MAELEKEZO KWA WAHUSIKA ZAIDI YA KWAMBA SUBIRI.

HAWAJALI IKIWA KAMA WAOMBA VIBALI WAMECHUKUA MIKOPO KWA AJILI YA KUENDELEZA AMA KUFANYA UJENZI HUSIKA NINAONGEA HIVI KWA MAANA NINAYE RAFIKI YANGU WA KARIBU AMBAYE AMECHUKUA MKOPO BANK CRDB KWA AJILI YA UJENZI LAKINI AMEKUWA AKIZUNGUSHWA HIVYO TANGU MWAKA JANA HADI LEO KIASI KWAMBA MKOPO ALIOCHUKUA BANK UNAKUWA KWA MAANA YA KWAMBA RIBA INAONGEZEKA SIKU BAADA YA SIKU KWANI ALITEGEMEA KUFANYA UJENZI TANGU MWEZI WA 12 MWAKA JANA NA SASA NI MWEZI WA NNE HAMNA KILICHOFANYIKA

AMEKWAMISHWA NA MIPANGO MIJI ARDHI ARUSHA KWA KUTOKUMPATIA KIBALI.

PAMOJA NA KWAMBA AMEANZA KUOMBA KIBALI TANGU MWEZI WA 11 MWAKA JANA .

TUNAMWOMBA RAIS AMA WAZIRI HUSIKA PIA AANGALIE UPANDE HUU ATUMBUE HAYA MAJIBU MAANA INAVYOONEKANA HAWA HAWAPO KWA AJILI YA WANANCHI NA MAENDELEO BALI WAPO KWA MANUFAA YAO BINAFSI NDIYO MAANA WANAZUNGUSHA ILI WAAMBIWE AMA KUTAMKIWA RUSHWA KWA SABABU WALIZOEA TANGU AWALI KWENYE SERKALI ZA AWAMU ZILIZOTANGULIA .

WAPO KAMA MIUNGU WATU
 
Kwa ufupi kabisa, ofsi ya ardhi iliyo chini ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro ni JIPU KUBWA MNO....

Kuna watendaji bado wanaendelezea tabia zile zile walizokuwa wakizifanya kipindi cha utawala wa JK...

Mfano, baadhi ya watendeja kwa makosa ya kuuza viwanja mara mbili alafu watu hao hadi mabosi wao wanawajua lakini hawawagusi kwa kuwa wao wanamuda mrefu hapo kazini so ni "mataita" a.k.a watoto wa Mjii....pia unakuta mtumishi mmoja ana viwanja 20-28 anamiliki...jamani hii ni haki kweli?? Mradi wa upimaji viwanja ukianzishwa wanahakikisha kila mtu anaviwanja visivyopungua 5..

Naomba waondolewe wote waliokaa hapo muda mrefu wapelekwa mikoa mingine yaani ifanyike exchange afu afisa misitu hafanyi kazi zake ipasavyo kazi ni pombe tuu anakuja ofsini amelewa akipelekewa taarifa za uchomaji moto na uchanaji mbao mazingira ya mlima Uluguru na watu waliofanya hivyo hakuna hatua zinazochukuliwa...

Utendaji wa kuogopana bado upo, ukomeshwe mara moja.
 
Institute of accountancy Arusha (I.A.A) taasisi ya serikali ya kufunza wahasibu:

Rais wetu siku ukija tena Arusha njoo utumbue hapa, Monyo mkuu wa chuo ashaiba mamilioni ya fedha na bado yupo.

Mpaka leo, chuo hiki wanabandikiwa matokeo badala ya kuwekewa kwenye internet.

Kiufupi hii taasisi ifanyiwe uchunguzi
 
Jipu:

Kilombero sugar na Unitransi Kilombero wanauza mafuta ya Diesel na Petrol yenye msamaha wa kodi kwa kampuni sisizo na sifa ya kupata msamaha huo ya Kk Security, MML & Buffet
 
Polisi Wanamaji,

Uvuvi wa Kutumia Mabomu ni kero Bahari ya Hindi hasa Kigamboni. Chukueni hatua!
 
Kama kweli Rais Magufuli amekusudia kupambana kwa dhati vita ya ufisadi basi anatakiwa afumbe macho na kuziba masikio ili aweze kupambana kikamilifu.

Ukianza kushughulikia tatizo hili la ufisadi kwa uhalisia utagundua kuwa takribani viongozi wote waandamizi wa chama na serikali ya awamu ya nne wana mkono katika ufisadi mkubwa nchi.

Hili la polisi linaonyesha wazi kwamba nchi imeshafilisiwa muda mrefu kama vyombo vya dola vimediriki kushiriki kwenye ufisadi basi mzizi ni mrefu sana.

Hakuna namna yoyote ya kumtenga Kikwete na ufisadi mkubwa ambao umetokea nchini. Huwezi kumtenga Kinana na ufisadi pamoja na viongozi wengine wengi...kama kweli unataka kushughulikia ufisadi basi amua kutoa maisha yako sadaka na watakao kuwa wahusika wakubwa ni hao waliokuwa kwenye madaraka kwenye chama na serikali ya awamu ya nne...Kikwete ameiuza nchi kwa wafanyabiashara wezi waliokuwa wanajifanya kuunga mkono ccm. ndio maana kumekuwa na vigugumizi sana kunapotokea kashfa za ufisadi maana zinawakumba viongozi wakuu.

Ili kuweza kushughulikia ufisadi nchini lazima Rais afumbe macho na kuziba masikio awakamate viongozi waandamizi wa jeshi la polisi kama mambo hayatakuwa hadharani kesho...Rizi 1 hatakwepa na wenzake
 
Back
Top Bottom