Tigo na Airtel acheni usumbufu kwenye kusajili laini

masare

JF-Expert Member
Oct 12, 2010
1,231
1,365
Haya makampuni ya Simu ya Tigo na Airtel yanafanya zoezi la usajili wa laini kuwa gumu kutokana na utaratibu wao wa kipekee waliojiwekea.

Ukienda kusajili laini Vodacom unatakiwa uoneshe kitambulisho chako cha NIDA pekee alafu unawatajia namba zako za Vodacom unazotaka kusajili (hata kama ni tano zote unawatajia palepale moja baada ya nyingine).

Lakini kwa upande wa Tigo na Airtel wao wanataka namba zote unazowatajia laini zake ziwe kwenye simu wakati huohuo. Sasa unakuta mteja ana laini nyingi za mtandao huohuo na moja tu ndio inakua active kwenye simu kwa mudahuo. jibu wanalokupa ni kwamba hawawezi kuzisajili hizo laini.

Nimewauliza kwanini utaratibu wao ni tofauti na Vodacom wakati mchakato wa kusajili laini ni zoezi la pamoja la kitaifa hawakunipa jibu linaloeleweka.

Walichoniambia ni kuwa ukimaliza kusajili laini yako iliyopo kwenye simu ujumbe unakuja wenye namba ambazo huyo wakala wa usajili anatakiwa ajaze.

Lakini kwa Voda ukishamaliza kuwatajia namba zako inakuja confirmation message/ meseji ya uthibitisho wa kukamilika kwa usajili basi na sio kingine.

Kwa maoni yangu naona Tigo na Airtel mnaleta usumbufu kwa wateja na kufanya zoezi la usajili hasa kwa mitandao yenu kusuasua huku wenzenu Voda wakiendelea kufanya vizuri kwa sababu wanafanya mambo kuwa rahisi yaani unaenda na kitambulisho chako cha utaifa au namba ya NiDA,unawatajia namba zako zote za mtandao husika kazi inakua imeisha.

Leo pia nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa hadi sasa laini zaidi ya milioni 30 nyingi kutokea makampuni haya hazijasajiliwa huku zikibakia wiki 13 pekee kabla zoezi halijaisha.

Karibuni tujadili
 
Ila huo ujumbe wa namba unaokuja ktk simu yako na wakala anatakiwa ajaze ktk simu inasaidia kurekebisha laini ambazo hazina majina yako au kama yalikosewa ambayo kwa voda awana hivyo
 
Halotel pia wana utaratibu huo,ni mzuri maana waoinakuja sms ya code unampa msajili anakamilisha usajili wako
 
Ila huo ujumbe wa namba unaokuja ktk simu yako na wakala anatakiwa ajaze ktk simu inasaidia kurekebisha laini ambazo hazina majina yako au kama yalikosewa ambayo kwa voda awana hivyo
Hapana...majina ya mwanzo kwenye ule usajili wa zamani yote yapo kwenye database.
Nadhani huo utaratibu wa mawakala kujaza tena namba za meseji unayotumiwa ni kwaajili ya malipo yao ya commission ndiomana wanapita hadi mitaani wakigombania kusajili watu.
 
Sababu ni Hizi hapa soma
1. Mtandao wa vodacom umeweka security kwamba huwezi kamilisha usajrili wa simcard isiyo na majina yako. Ni lazima iwe na majina yako hasa jina lwa kwanza lazima liendanane na jina la kwanza kwenye national id. Otherwise lazima ukaape mahakamani ili ukabadilishe jina ndio usajili.

2. TIGO NA AIRTEL hawana hiyo security, hata ukichukua simcard ya jirani yako haina majina yako unaisajili kwa alama za vidole inakubali.
SABABU YA KUTAKA SIMCARD IWE HEWANI NI ILI KUJIRIDHISHA/ KUHAKIKISHA HIYO SIMCARD NI YAKO KWELI NDIO MAANA UNATUMIWA *ONE TIME PASSWORD *

MY TAKE: utaratibu wa Tigo, airtel na halotel ni mzuri kuliko Vodacom
Haya makampuni ya Simu ya Tigo na Airtel yanafanya zoezi la usajili wa laini kuwa gumu kutokana na utaratibu wao wa kipekee waliojiwekea.

Ukienda kusajili laini Vodacom unatakiwa uoneshe kitambulisho chako cha NIDA pekee alafu unawatajia namba zako za Vodacom unazotaka kusajili (hata kama ni tano zote unawatajia palepale moja baada ya nyingine).

Lakini kwa upande wa Tigo na Airtel wao wanataka namba zote unazowatajia laini zake ziwe kwenye simu wakati huohuo. Sasa unakuta mteja ana laini nyingi za mtandao huohuo na moja tu ndio inakua active kwenye simu kwa mudahuo. jibu wanalokupa ni kwamba hawawezi kuzisajili hizo laini.

Nimewauliza kwanini utaratibu wao ni tofauti na Vodacom wakati mchakato wa kusajili laini ni zoezi la pamoja la kitaifa hawakunipa jibu linaloeleweka.

Walichoniambia ni kuwa ukimaliza kusajili laini yako iliyopo kwenye simu ujumbe unakuja wenye namba ambazo huyo wakala wa usajili anatakiwa ajaze.

Lakini kwa Voda ukishamaliza kuwatajia namba zako inakuja confirmation message/ meseji ya uthibitisho wa kukamilika kwa usajili basi na sio kingine.

Kwa maoni yangu naona Tigo na Airtel mnaleta usumbufu kwa wateja na kufanya zoezi la usajili hasa kwa mitandao yenu kusuasua huku wenzenu Voda wakiendelea kufanya vizuri kwa sababu wanafanya mambo kuwa rahisi yaani unaenda na kitambulisho chako cha utaifa au namba ya NiDA,unawatajia namba zako zote za mtandao husika kazi inakua imeisha.

Leo pia nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa hadi sasa laini zaidi ya milioni 30 nyingi kutokea makampuni haya hazijasajiliwa huku zikibakia wiki 13 pekee kabla zoezi halijaisha.

Karibuni tujadili
 
Huu sio ukweli. Nenda na simcard isiyo na majina yako vodacom utajua tofauti yake
Hapana...majina ya mwanzo kwenye ule usajili wa zamani yote yapo kwenye database.
Nadhani huo utaratibu wa mawakala kujaza tena namba za meseji unayotumiwa ni kwaajili ya malipo yao ya commission ndiomana wanapita hadi mitaani wakigombania kusajili watu.
 
Back
Top Bottom