the Football, au Nuclear Football

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,525
14,395
THe FOOTBaLL

Kuanzia mwaka 1960 hadi Leo hii, Marais wote wa Marekani wamekuwa wakiambatana na mlinzi ('boardguard') maalum ambaye huwa anabeba mkoba, yaani ('briefcase')
Briefcase hii ni shurti iwe karibu na rais popote pale anapokuwa, hivyo ni wajibu wa mlinzi huyu kuwa sambamba na Rais popote pale anapoenda.

Briefcase hii imepewa jina la 'the football'

Sasa Ili kufahamu 'the football' inabeba nini, na ni kwa ajili ya nini, naomba ufuatane nami katika makala haya.

☆☆☆☆☆☆

Katika kile kinachojulikana kama uhasama kati ya mataifa ya kikomunisti na mataifa ya kibepari al maarufu kama "vita baridi" Dunia imekua ikishuhudia ugomvi wa kisiasa, kiuchumi, na kijeshi baina ya pande hizo mbili huku kila upande ukijidhatiti kujilinda dhidi ya mwingine.

Marekani ikiwa ndio kinara kwa upande wa mataifa ya kibeberu huku muungano wa usovieti kwa upande wa Mataifa ya kikomunisti (capitalist vs socialist blocks)

Katika kipindi chote cha vita baridi, muungano wa nchi za kisovieti, (USSR) walikua wanawaunga mkono nchi ya Cuba, na hivyo mwaka 1962 waliamua kutega makombora ya nyuklia ya masafa ya kati, nchini humo (cuba), hali iliyozusha mvutano mkubwa na kuisogeza dunia karibu kabisa na kulipuka kwa vita vya kinyuklia.

Mara tu Baada ya Marekani kubaini uwepo wa makomboa hayo, Rais wa marekani kwa wakati huo John F. Kennedy akapatwa na wasiwasi kwamba huenda siku yeyote na muda wowote USSR wanaweza kufanya shambulio la nuclear dhidi ya ya nchi yake, na ukizingatia makombora hayo yametegwa nchini Cuba jirani kabisa na Marekani.

Hivyo katika kujilinda na kujihami dhidi ya shambulio hilo, Kennedy akatoa maagizo kwenda kwa idara ya ulinzi ya marekani 'Pentagon', kuuandaa mfumo unaomuwezesha rais anapokuwa mahala popote kufanya shambulio la nyuklia kwa nchi maadui na ndani ya sekunde moja tuu.

Ndipo jeshi likatengeneza kitu ambacho kilimuwezesha rais kufanya shambulio tuu kwa 'kubonyeza kitufe'. (only by just pressing the button).

Na kitu hiko kilijulikana kama "The football" au wengine huita majina mbalimbali kama vile the nuclear button; 'Nuclear football'; 'the button'; 'presidential emergency button'; au 'emergency satchel'; n.k

Ifahamike kwamba leo hii, Marekani ikitaka kufanya shambulizi la silaha za nyuklia ni shurti Amri itoke kwa Rais.. yaani Rais ndiye mtu pekee wa kuidhinisha shambulizi hilo, na si mtu mwingine.

Hapa Nitaeleza ni kwanini ipo hivyo.����

wazo la kumfanya rais kuwa ndiye mtu wa pekeee wa kutoa amri kuhusu kufanya shambulizi la kinyuklia, lilikuja kufuatia nchi ya Marekani kudondosha mabomu ya nyuklia huko Hiroshima na Nagasaki nchini Japan, mabomu ambayo kwa hakika ndiyo yalizima Vita ya pili ya dunia mnano mwaka 1945

Katika shambulizi hilo, Rais yaliyekuwa madarakani Harry Truman aliitaka marekani itatumia silaha za nyuklia katika vita ya pili ya dunia ila hakutaja 'specifically' ni siku ipi au muda upi na mahala gani mabomu hayo yatumike, lakini badala yake maamuzi hayo yalifanywa na jeshi, na kisha yeye akaoneshwa tuu mpango mkakati. Yaan kwa maneno mengine niseme kuwa Rais hakuwa na maamuzi ya mwisho kuhusu Shambulizu hilo la Hiroshima na Nagasaki, Japan

Siku mojà baàda ya kumalizika kwa mashambulizi ya nagasaki na Hiroshima, rais, Truman aliamuru kuwa kuanzia siku hiyo ili jeshi litekeleze shambulio, ni lazima Amri itoke moja kwa moja kwa rais.Yàani rais atakuwa ndio Mwenye maamuzi wa mwisho.

Kwa kufanya hivyo, ilisaidia kupunguza mamlaka ya jeshi juu ya silaha za nyuklia katika kipindi cha utawala wa Rais Harry Truman

Baada ya utawala wa Truman kumalika, ulifuatia utawala wa Rais Dwight Eisenhower na kisha Rais John F Kennedy akafata.

Ndipo tunaona katika utawala wake, kunazinduliwa kitu kinachoitwa 'The football', ni briefcase linalobeba kifaa kilichowekewa mfumo wa ki tehama ambao utamfanya rais kutekeleza shambulizi la silaha za nyuklia popote pale atakapokuwa.


Miezi michache ilopita mwaka 2018, katika mtandao wa kijamii wa 'Twitter' tuliona Rais wa wakati ule wa marekani, Donald Trump akimjibu rais wa Korea Kaskazini Kim Jon Un na aliandika hivi;.

North Korean Leader Kim Jong Un just stated that the “Nuclear Button is on his desk at all times.”... Please inform him that I too have a Nuclear Butt but it is a much bigger & more powerful than his, and my Button works!..

Akiwa na maaana kwamba " Kim jong Un anasema ana kitufe cha Nyuklia wakati wote..sasa mpeni taarifa kuwa hata Mimi ninacho kitufe cha nyuklia, na ni kikubwa na chenye nguvu kuliko chake..."..

☆☆☆☆☆☆

Lakini Tofauti na fikra za Watu wengi, Hiyo 'the Football' ki uhalisia haina Kitufe chochote kama inavosemwa, ila ni 'lugha' tuu inayotumika kuashiria kwamba shambulizi la Nyuklia linaweza kufanywa ndani ya sekunde chache tuu, ambapo ni kama kubonyeza kitufe.

Kiuhalisia, the football, au nuclear football, ni briefcase ambalo ndani yake kuna mtambo unaotumia mfumo wa tehama( teknolojia, habari, mawasiliano) ambao unamuwezesha Rais kuwasiliana ili Kutoa Amri kwa jeshi(pentagon) kufanya Shambulio. Na mawasiliano haya hufanyika ndani ya sekunde chache Tu.

Kwakuwa ili jeshi liweze kufanya shambulizi la nyuklia dhidi ya nchi maadui ni sharti lipokee amri/agizo kutoka moja kwa moja kwa rais.. Hivyo Rais Kennedy alijiuliza baadhi ya maswali, na moja ya maswali hayo alijiuliza hivi:
“How would the person who received my instructions verify them?”


Kutokana na swali hilo ndipo jeshi likabuni mfumo ambao utathibitisha pasi na shaka yeyote kuwa Rais ndiye aliyetoa amri.

Na hapo ndio ukawa mwanzo wa The Football, briefcase jeusi lenye uzito wa kilo ishirini linalobebwa na moja ya ma boardguard wa Rais, ambalo ndani yake kuna...pale duniani.

Katika kitabu kilichoitwa Breaking Cover, kilichoandikwa na aliyekuwa mkurugenzi wa ofisi ya jeshi ya ikulu, bwana Bill Gulley kinaeleza kwamba..

Ndani ya 'the football' kulikuwa na vitu vinne vikuu.
Kwanza kulikuwa na kitabu kilichojulikana kama Black Book, ambacho kuliandikwa orodha ya nchi zote zinazotengeneza silaha za Nyuklia ambazo Marekani waliziita 'target Areas'.

Pa kulikua na mtambo wa redio ya satelaiti ambayo inawezesha kusafirisha mawasiliano kwenda idara ya ulinzi (pentagon), ambao wao ndio hurusha makombora kwenda nchi husika.

Kuna kitabu kingine Kinachoelezea namna ya kutumia mfumo wa dharula yaani Emergency Alert System. Huu ni mfumo wezeshi unaomfanya Rais aweze kuzungumza na wasaidizi wake, au Kutoa taarifa kwa umma, wakati wa tukio la dharula.

Pia kuna kadi inayojulikana kama 'biscuit',mithili ya kadi za Benki..ambayo ina code maalum zinazoitwa Gold Codes ambazo ndio hubeba utambulisho wa rais (Identification). Hii inawesaidia pentagon kuthibitisha kuwa pasi na shaka kuwa anayetumia the Football kwa mda huo ni Rais..Kadi hii Rais anaweza kutembea nayo mfukoni ama ampe msaidizi wake amshikie.


Naaam..!!
Hiyo ndio the Football, au Nuclear Football inayotumiwa na marais wa Marekani. Yote ikiwa ni katika ulimwengu wa Vita vya Nyuklia.
 

Attachments

  • images (15).jpeg
    images (15).jpeg
    39.7 KB · Views: 2
Back
Top Bottom