'The Economist' Takes Gloves off on Kikwete...

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
DEAR MZEE MATONYA WA UKWERENI....​


Damn, Damn, Damn! Florida Evans would have cursed!

Damn, Damn, Damn, Mchungaji Kishoka is cursing!

Walahi huu Umatonya umetukaa fiti kama vile kushoneshewa suti kwa fundi pale Gerezani. Yaani bado tunalilia misaada na tunadai eti tunataka kujitegemea?

Nitataja kwa kifupi kwa nini Tanzania inashindwa kujitegemea na inategemea misaada na hivyo kauli za Viongozi siku zote ni kuomba omba na kung'ang'ania kuwa misaada ni muhimu na si kuimarisha uzalishaji wa mali na matumizi mazuri ya rasilimali zetu ndani ya nchi.

1. Serikali yetu ni kubwa mno, na haina ufanisi wala uwiano chanya kati ya ukubwa wake na matunda ya kazi zake.
2. Serikali, inapenda kutumia pesa kupita uwezo wake. Hakuna utamaduni wa kupunguza au kubana matumizi.
3. Serikali na Taifa zina mfumo mbovu wa fedha ambao unatoa mianya ya matumizi mabaya ya fedha, kukosekana kwa nyaraka, stakabadhi na mtiririko sahihi wa kihasibu na mahesabu katika matumizi ya fedha.
4. Viongozi wa Tanzania ni wavunjaji wa kanuni za sheria na mahesabu kwa kutumia nguvu za madaraka yao. Waziri au mtendaji, hutoa amri ya matumizi au kutumia fedha bila kuwa na fungu katika bajeti au kupangiwa, hivyo kujichotea kutoka fungu lolote kukidhi kauli na mahitaji ya mkubwa na si kuendana na bajeti.
5. Ulimbukeni wa ukarimu wa kijima, unatupunguzia mapato kwa kisingizio cha vivutio vya uwekezaji. Misamaha ya kodi na ushuru ni mikubwa sana na haiendani hata kidogo na ama kinachovunwa na mwekezaji au uwezo wa mwekezaji.
6. Udhaifu wa mipango na mikataba, ni moja ya mambo ambayo yanasababisha Taifa kupoteza mapato na kuishia kutumia fedha nyingi na kuombaomba badala ya kuwa makini na kujiongezea mapato na kuhakiki mipango kwa kutoa kipaumbele kwa mipango na matumizi ya lazima na yenye manufaa.
7. Hujuma. Iwe ni ufisadi, uvivu, uzembe, wizi au kukosekana kwa mwamko, Watanzania tunajihujumu wenyewe na hata kama leo tutadai Rostam, Somaiya, Manji, Mengi na Patel ni mafisadi, bado sisi wenyewe kama wananchi tunachangia kwa sehemu kubwa sana kuimarika kwa ufisadi.

Ukisoma habari hii hapa chini, inabidi ujiulize, je ni lini tutaamka na kubadilisha mwenendo wetu?

Rais Kikwete katembelea dunia na nchi tajiri wahisani kwa asilimia 40 ya muda wake aliokuwa madarakani, je tumefanikiwa kiasi gani kujiimarisha kiuchumi kwa kutumia nyenzo zetu wenyewe?

Je Tanzania tuko umbali gani kabla ya tumaini ka kujitegemea kuonekana hata kupata imani kutopka kwa wawekezaji na wafadhili kuwa tumeanza kwenda kwenye njia nyoofu?

Hii kauli aliyoisema Mzee Matonya wa Ukwere kuwa tunajitahidi tujitegemee, na tunafurahia misaada ni kauli iliyonidhoofisha na kuniambia kuwa ni wazi Serikali ya Tanzania, CCM au Watanzania bado hatujaamka na kuanza kuitutumua kwa vitendo na si maneno kuwa tunataka kkujenga Taifa linalojitegemea.

Hiki kipande kinatoka gazeti la Economist.

Waiting for that great leap forward

[SIZE=-2][FONT=verdana,geneva,arial,sans serif]May 7th 2009 | DAR ES SALAAM [/FONT][/SIZE]
[SIZE=-2][FONT=verdana,geneva,arial,sans serif]From The Economist print edition[/FONT][/SIZE]


Worries about one of east Africa’s steadier economies

THE country already gets 40% of its government budget in aid, but now it wants even more foreign cash to help it through the economic downturn. How much is enough? Tanzania’s president, Jakaya Kikwete, smiles grimly. “We’re trying to bring down our dependency, but we’re grateful for what we receive.”

With 44m people, Tanzania has often been given the benefit of the doubt simply for being the gentler twin of harsher Kenya, which has 40m. What it lacks in dynamism it makes up for in placidity and a common national identity. It is unlikely to fall apart at elections or any other time.

Its founding party of independence, Chama Cha Mapinduzi (CCM, the Party of the Revolution), formerly the Tanzanian African National Union, known as TANU, still suffocates the country’s ragtag opposition parties with its size and ponderous propaganda. Mr Kikwete is a CCM man; his breakthrough job was as the youthful head of political indoctrination for Tanzania’s armed forces. He will almost certainly be returned to office with a big majority in elections next year. He still charms would-be investors with his sales patter.

Yet those who set up shop in the country are often disappointed. Tanzania, many complain, is a “slow” or even “terrible” place to do business—and “ungrateful” for foreign aid or investment. Even its boosters admit it is wrapped in red tape and lacks skilled workers. Almost everyone says Mr Kikwete is spending too much time burnishing Tanzania’s image abroad and not enough fixing problems at home. Last year he chaired the African Union.

In any event, he hopes that aid will keep Tanzania afloat long enough for its economy eventually to make a great leap forward. Shiny new buildings even in provincial towns, along with new roads and water projects, signal optimism. Politics are stable. A rowdy separatist movement in the island of Zanzibar is quiet for now.

By Tanzanian standards there is a new sense of urgency. The energy ministry says it wants tenders “immediately” for a power station to cover a paralysing shortfall in electricity. Mr Kikwete turns up unannounced at state-owned outfits such as the port and the railways to demand efficiency and rail against corruption. He has also lambasted the country’s “Wabenzi” (those who drive a Mercedes-Benz).

But Mr Kikwete turns mournful when he spells out the effects of the global recession: missed government revenue targets; a cancelled sovereign-bond issue; projects for a nickel plant and a vast aluminium smelter put on hold; revenue from coffee down; cotton hit even harder; tourism suffering as well. An exception is gold, with new finds still to be exploited and the price holding up fairly well.

Tanzania may already, in some respects, be falling behind. A recent Chinese state visit failed to bring much investment. The government in Beijing thinks Kenya, not Tanzania, is the gateway to the mineral wealth of Congo. Tanzania’s two main railways are rickety. The port of Dar es Salaam failed to pinch business from Kenya’s port, Mombasa, when Kenya was in turmoil a year ago. No one seems to know how Tanzania’s main port will hit its target of a tenfold increase in goods traffic by 2030. Tanzania is not even spending all the aid it is given. Last year, $2.4 billion of pledged funds were not disbursed.

Tanzania must also decide whether to integrate more closely into the East African Community (EAC), which includes neighbouring Burundi, Kenya, Rwanda and Uganda. It has dragged its feet over opening its borders and moving towards a common currency, though it recently insisted that a common market would get going next year. It suspects Kenya of using the EAC as a way of grabbing arable Tanzanian land on the cheap. And the country’s tiny middle class fears being swamped in a common market by better-qualified Kenyans and Ugandans. Moreover, the world crisis may bolster old socialists in the CCM who want a return to ujamaa, a failed model of rural collectivisation propounded by Tanzania’s founding president, Julius Nyerere. That would set it back even further.

Tanzania waits for a leap forward | Waiting for that great leap forward | The Economist
 
Last edited by a moderator:
The Economist wamemaliza kila kitu. Matatizo yanayotutatiza yanajulikana, njia za kuyatatua zipo, kwa nini hayatatuliwi ? Hili gazeti ni very reliable on economic issues.Jirani zetu wakiandikwa possitively on economic issues inabidi tushtuke. What is wrong with Tanzania?
 
What a breathe of fresh air on the Forum, thank you mkuu, you always are a calm hand in the midst of calamity.

Badala ya kupoteza muda kwa kushabikia katika threads zingine naomba nichangie hapa:
Economist ni wanafiki sana, nadhani ukipiga search mwaka 2006 waliandika article ambapo walimsifia JK ya kuwa ni John F Kennedy of Africa!!!! I am not joking! That does not mean that I dsmiss this article out of hand in fact I have continued to read the Economist ever since. However we have to be cautious and say haijashushwa kutoka Mungu, so we should always weigh what and why they write it.

Mimi naamini ya kuwa Western world has ended its love affair with the 'young and dynamic' leader of Tanzania and they finally see him for what he is - an ineffective leader. But this is not about him, we have to look at some of the very important points raised in particular the competetiveness of Tanzania within the region.

Another alarming issue is that Aid or donor money was not disbursed! Why and what happened. Mi naamini kuwa hata hao donors inabidi tuwabane na kuwalazimisha wachapishe katika magazeti wametoa misaada kiasi gani kwa nchi yetu ili tuweze kufuatilia pesa zetu maana any aid is given to the people of Tanzania na siyo serikali na watendaji wake.

I also think it is high time for donors to consider not giving money to the govenrment. They should disperse funds with the private sector, na hizi NGOs pia haifai, inatakiwa iwe Foundations that are audited na zipite some form of test that qualifies them to handle money on behalf of the Tanzanian people.

All in all I think that the analysis is fair although it is still trying to paint a rosy picture somewhat lakini at least there is acknowledgment that there is trouble and even bigger problems ahead.
 
Nchi ya 'shamba la bibi'. Waliochukuliwa kama 'manabii' wa Nyerere ndo wamegeuka mchwa na kuanza kushambulia Uchumi. Mkulo juzi kaaidiwa kupewa pesa na IMF za mkopo.
 
1. Serikali yetu

2. Serikali, inapenda

3. Serikali na

5. ... Misamaha ya kodi

6. Udhaifu wa mipango na mikataba,

7. Hujuma. Iwe ni ufisadi, uvivu, uzembe, wizi au kukosekana kwa mwamko, Watanzania tunajihujumu wenyewe na hata kama leo tutadai Rostam, Somaiya, Manji, Mengi na Patel ni mafisadi, bado sisi wenyewe kama wananchi tunachangia kwa sehemu kubwa sana kuimarika kwa ufisadi.

... ni wazi Serikali ya Tanzania, CCM au Watanzania bado hatujaamka na kuanza kuitutumua kwa vitendo na si maneno kuwa tunataka kkujenga Taifa linalojitegemea.

Rais Kikwete katembelea dunia ...

Hiyo sababu ya saba, Watanzania, ndio kiini cha tatizo. Si CCM, si Kikwete, si serikali.

ECONOMIST wametutandika fimbo wote, kwamba Watanzania ni watu slow, tusio na mwendo wa kwenda mbele, hatuna "dynamism." Hatuna ujuzi, tumezidiwa na Wakenya na Waganda, tunawaogopa. Tuko slow wanasema mpaka tumeshindwa hata kutumia hela tulizoomba, $ 2.4bil. Ukweli si kejeli, ashakum si matusi.

Kikwete sio dawa, sio ugonjwa. Miundombinu yetu ya reli na bandari imechoka mbaya, "rickety," wanasema. Reli, bandari, ndege, barabara, magari ya usafirishaji yalianza kuchoka toka enzi Nuhu anaibuka kutoka kwenye Gharika ya Kwanza ya Dunia. Kikwete kakikuta hiki kifafa cha miundombinu, na hana dawa.

Wananchi wa Tanzania, sio Kikwete, wote tumejaa uvivu, uchovu, ukilaza, uzembe wa mawazo na kazi. Jumatatu unaingia saa sita, jana ulilala msibani ukihani marehemu Mzee Dau, baba wa shangazi yake mke mdogo wa jirani yako. Jummanne inabidi uombe udhuru kumpeleka Pili hospitali. Jumatano unaenda kwenye mazishi, haupo kazini nusu siku. Alhamisi unaondoka mapema kuwahi lifti ya Mama Tarimo maana ukiikosa hii basi usafiri jioni udhia mtupu, isitoshe yabidi uwahi kwenye send off. Ijumaa unatakiwa harusini, ulitoa mchango. Wiki ijayo huna udhuru, utajitahidi kutulia kazini unasoma "Acha Umbea" na "Alasiri," ukichoka unachomoka kidogo kutafuta supu ya utumbo, ukirudi ni kusogoa na kunywa chai na maandazi. Nusu ya maisha yako ya kazi ni livu, na mshahara utapata wote. Sio wewe tu utapata mshahara mzima, na marehemu Mzee Dau nae atalipwa.

Sasa kama hapo tatizo ni Kikwete basi waandishi wa makala hiyo wametutusi wote maana wamesema Mrisho atachaguliwa tena, wameongea kwa ukomo wa uhakika, atachaguliwa tena, na itakuwa ni kwa kishindo cha mmomonyoko wa ardhi ya uchaguzi, landslide. Kwa nini, kwa sababu Chama cha Mapinduzi kimewachota watu akili, wanasema kimetukuka katika longolongo dufu, "ponderous propaganda."

Na wametuasa kusikiliza wenyenchi ndani ya chama kutaka kuwapeleka tena wananchi kwenye Ujamaa kwa kigezo cha mporomoko wa ubepari duniani. Wachambuzi wa The Econonimist wanasema genda ulole.
 
Hiyo sababu ya saba, Watanzania, ndio kiini cha tatizo. Si CCM, si Kikwete, si serikali.

Wananchi wa Tanzania, sio Kikwete, wote tumejaa uvivu, uchovu, ukilaza, uzembe wa mawazo na kazi.

CCM iliacha lini kuwa ya Watanzania na Kikwete aliacha lini kuwa Mtanzania. Nikikumbuka hesab za seti, Watanzania ndiyo seti kuu.. lakini hiyo haiondoi uwezekano wa seti ndogondogo.. ila inaonekana wewe umeondoa CCM, Kikwete na serikali kwenye seti kuu. Kwa misingi gani? Na wewe ndiye mkosoaji wetu mkuu humu una overlook vitu kama hizi internal contradictions.
 
The Economist, like many others, made a flawed assessment of JK at first. They were taken in by the man’s charm and affable demeanor. But they have now judged him correctly by using the results of his work. Some of us did that from the beginning; we looked at his dismal performance as Minister of Foreign Affairs and pronounced him unqualified to vie for the Presidency. But the CC and NEC have never been able to look further than facial maneuvers, handshakes and jobs for the boys!

It is true that Kenyans and Ugandans are perceived as being more skillful workers than us. It is our fault. Only education can help us catch up. Schools like St. Francis (Mbeya) Marian (Bagamoyo) and the seminaries (the real ones, not the ones that simply copied that name), will produce a new crop of Tanzanians who compete on the global market. We owe our educational backwardness to the nationalization of schools by Mwalimu, and to the many years that we wasted while pursuing Socialism.

We must solve our problems by attacking their root cause. That is CCM. It is true that we have one fundamental problem in Tanzania. It is called CCM. This den of vipers is the axis of evil that is spewing corruption, mismanagement and general underdevelopment in our country.

Next year, Tanzanians will get an opportunity to make a real choice. They can choose to continue with the current statusquo by re-electing CCM, or they can opt to give themselves a new beginning by replacing the CCM government by some broad based coalition of opposition leaders. I would place Wilbroad Slaa at the head of such a new crop of leaders. It can be done; it has been done in Zambia and Kenya, and the results speak for themselves. Why not in Tanzania too?
 
Last edited:
Mimi nikisikia jina la kikwete naugua kabisa nibora kagame mara mia hivi huyu RAIS wetu alitoka kwenye familia gani ?.Hata mama yake hakumfundisha kwamba mwanangu kuombaomba ni kubaya, ni shida kwelikweli je hata hakuwahi kujua kwamba kutembea sana kama mtalii wakati hujazalisha na kuwa na hakiba ni hasara badala yake utaweka inchi kwenye mikono ya mapapa.
Huyu RAISI wetu au kabadilishwa kuwa dondocha ebu jamani mtuangalizie huko wajuzi kwani mimi naona kama Tangu EL ajiuzuri huyu jamaa kawa mtambo kwelikweli.
 
Wakuu,

Askofu Kishoka na mwandishi wa 'ze uchumi' nimewapata. Ninachokiona hapa ni cynisism,kwamba hatuwezi hiki hatuwezi kile,ya kweli hayo? Nakataa, we can.

Mambo ya msingi ya kufanya yapo na tukiamua tunaweza. Kwa mfano badala ya kung'ang'na eti mpaka tupate bilioni mia moja ndo tuanze mradi wa kujenga kilomita 100 za barabara kwa nini tusikusanye bilioni kumi tukajenga kilomita 10 na kila mwaka tukaendelea hivyo hivyo kidogo kidogo? Baada ya miaka kumi hiyo barabara si itakuwa imetoka Mwanza na kufika Shinyanga na huku tunafanya matengenezo kwa kutumia vifaa vyetu wenyewe?

Jamani waswahili si ndivyo tunavyojenga nyumba zetu? vivyo hivyo kwa madarasa,zahanati,miundo mbinu ya maji n.k.We are not that poor,ni mipango tu.Kwa nini kwa mfano tusiseme enough is enough hatutaki kuagiza mchele tena toka nje hivyo tuamue kulivaa bonde la mtoto Rufiji kwa tukajenga dams na irrigation system na kulikata bonde katika blocks kisha watu waka lease na kulima mpunga?Yote yanawezekana ni mipango tu,lakini above all tujenge positivity na tuache kuwa watu wa kulalamika tuuuuuu!

Sincerely speaking change comes from the people,tusiwategemee sana wanasiasa (itikadi zao notwithstanding), tujibidiishe wenyewe,tutafute,tutapata na nchi itaendelea.Kamwe tusijione wanyonge ambao hatuwezi , kumbuka pamoja na ulaini wake maji hupasua miamba!
 
duh..hii makala imenifanya nishindwe kula.. what on earth is going on!?

What always went on, Mkuu! Hamna kipya. Wote tunajua lakini labda wakisema wenzetu ndiyo tutaamka!

Unamkumbuka Nero Claudius Caesar Augustus Germanicus (15 December AD 37 – 9 June AD 68) na kuungua kwa Roma?

Amandla...........
 
Hivi lini tumewahi kukalishwa kama taifa na kuambiwa ukweli wa hali yetu? Hivi ni lini, hao tuliowachagua wamewahi kukaa na kutueleza wanakotaka tufike na NAMNA tutakavyoweza kufika huko? In detail na si kwa majibu mepesi tuliyozoea! Tunahitaji tough love sasa hivi lakini sioni wa kutupa.

Amandla......
 
Dont know what to say....inasikitisha sana..inafika sehemu ukiulizwa wewe wa nchi unafukiria kujibu.
 
Hivi lini tumewahi kukalishwa kama taifa na kuambiwa ukweli wa hali yetu? Hivi ni lini, hao tuliowachagua wamewahi kukaa na kutueleza wanakotaka tufike na NAMNA tutakavyoweza kufika huko? In detail na si kwa majibu mepesi tuliyozoea! Tunahitaji tough love sasa hivi lakini sioni wa kutupa.

Amandla......

Umeisahau hotuba ya Kikastro ya masaa takriban 4 aliyoitoa Mheshimiwa Rais kwa Taifa kupitia Bunge Tukufu mnamo Agosti 2008?
 
Jamani tunaokoelekea kumeainishwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM! Tumeambiwa wapi tunakoelekea-labda kama tumesahau.
 
Jamani tunaokoelekea kumeainishwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM! Tumeambiwa wapi tunakoelekea-labda kama tumesahau.

Na namna tutakavyoweza kufika huko? Tumewahi kuongelea hali ya shule zetu na namna tutakavyoweza kupandisha uwezo wa wanafunzi wetu? Tumeongelea namna gani tutakavyoweza kupunguza vifo vya wakina mama wanaokufa wakiwa wanajifungua? Tumeweka statistics za kila wilaya na kupambanua nini matatizo yao na namna gani wanaweza kujikwamua? Na baada ya kufanya hivi, je tumeuwekea umma uweze kuchangia na kuchambua tulichowaeleza?

Nashindwa hata kusema "Amandla....."
 
Fundi Mchundo kila kitu kimeelezwa kwa kina. Takwimu zimetolewa. Mwelekeo upo. Tatizo ni je huo mwelekeo ni wa kwenda wapi - Egalite au Eliteville?
 
Hiyo sababu ya saba, Watanzania, ndio kiini cha tatizo. Si CCM, si Kikwete, si serikali.

ECONOMIST wametutandika fimbo wote, kwamba Watanzania ni watu slow, tusio na mwendo wa kwenda mbele, hatuna "dynamism." Hatuna ujuzi, tumezidiwa na Wakenya na Waganda, tunawaogopa. Tuko slow wanasema mpaka tumeshindwa hata kutumia hela tulizoomba, $ 2.4bil. Ukweli si kejeli, ashakum si matusi.

Kikwete sio dawa, sio ugonjwa. Miundombinu yetu ya reli na bandari imechoka mbaya, "rickety," wanasema. Reli, bandari, ndege, barabara, magari ya usafirishaji yalianza kuchoka toka enzi Nuhu anaibuka kutoka kwenye Gharika ya Kwanza ya Dunia. Kikwete kakikuta hiki kifafa cha miundombinu, na hana dawa.

Wananchi wa Tanzania, sio Kikwete, wote tumejaa uvivu, uchovu, ukilaza, uzembe wa mawazo na kazi. Jumatatu unaingia saa sita, jana ulilala msibani ukihani marehemu Mzee Dau, baba wa shangazi yake mke mdogo wa jirani yako. Jummanne inabidi uombe udhuru kumpeleka Pili hospitali. Jumatano unaenda kwenye mazishi, haupo kazini nusu siku. Alhamisi unaondoka mapema kuwahi lifti ya Mama Tarimo maana ukiikosa hii basi usafiri jioni udhia mtupu, isitoshe yabidi uwahi kwenye send off. Ijumaa unatakiwa harusini, ulitoa mchango. Wiki ijayo huna udhuru, utajitahidi kutulia kazini unasoma "Acha Umbea" na "Alasiri," ukichoka unachomoka kidogo kutafuta supu ya utumbo, ukirudi ni kusogoa na kunywa chai na maandazi. Nusu ya maisha yako ya kazi ni livu, na mshahara utapata wote. Sio wewe tu utapata mshahara mzima, na marehemu Mzee Dau nae atalipwa.

Sasa kama hapo tatizo ni Kikwete basi waandishi wa makala hiyo wametutusi wote maana wamesema Mrisho atachaguliwa tena, wameongea kwa ukomo wa uhakika, atachaguliwa tena, na itakuwa ni kwa kishindo cha mmomonyoko wa ardhi ya uchaguzi, landslide. Kwa nini, kwa sababu Chama cha Mapinduzi kimewachota watu akili, wanasema kimetukuka katika longolongo dufu, "ponderous propaganda."

Na wametuasa kusikiliza wenyenchi ndani ya chama kutaka kuwapeleka tena wananchi kwenye Ujamaa kwa kigezo cha mporomoko wa ubepari duniani. Wachambuzi wa The Econonimist wanasema genda ulole.

Raisi, CCM na serikali yake ndio kiini cha matatizo yote maana wao ndio tumewakabidhi jukumu la kutuongozea njia. Hilo halipingiki na mtu yeyote. Watanzania as whole tunawajibika only kwa sababu tuliwachagua kwa hiari yetu (we can debate this), nothing else. Uzembe kazini, uwajibikaji, attitude etc, hayo yote yanaweza kushepiwa na uongozi. Ukiwa na uongozi wa wezi, huwezi kuwadhibit wezi. Ukiwa na uongozi ulio makini na wenye mwelekeo, watu wake watakuwa shaped accordingly.

The Economist is spot on. Time for change is now. Wengi tulidanganyika na tabasamu pale mwanzoni, sasa hali halisi tunaiona hata bila kuambiwa na The Economist. Kumbe kinachohitajika ni uchapa kazi na sio mizaha na kucheckacheka kila wakati.
 
Back
Top Bottom