HIMARS
JF-Expert Member
- Jan 23, 2012
- 69,373
- 94,566
Taarifa
View attachment 2520526
GST inapenda kuutangazia umma kwamba kumekuwa na matukio ya matetemeko ya ardhi katika maeneo ya wilaya ya Manyoni kwenye mpaka kati ya Mkoa wa Singida na Dodoma yakiwa na ukubwa wa 4.3 na 4.9 katika kipimo cha Richter kama yalivyoainishwa kwenye jedwali hapa chini:
Matukio hayo yalisikika katika maeneo ya mkoa wa Dodoma na Singida. Hata hivyo, pamoja na matetemeko hayo kusababsha taharuki kubwa kwa wakazi wa Jiji la Dodoma na maeneo ya jirani, GST haijapata taarifa zozote za kutokea kwa madhara kutokana na matetemeko hayo.
Ikumbukwe kwamba mikoa ya Dodoma na Singida imepitiwa na ukanda wa bonde la ufa la Afrika Mashariki mkondo wa mashariki. Mikoa mingine katika mkondo wa mashariki ni Manyara, Arusha, Mara, Iringa na Njombe ambapo mkondo wa magharibi una mikoa ya Kagera, Kigoma, Katavi Rukwa, Songwe, Mbeya na Ruvuma. Maeneo ya ukanda wa bonde la ufa kwa kawaida ni maeneo tete ya mabadilko ya kijiolojia ambayo hukumbwa na matetemeko ya ardhi na milipuko ya volkano.
Mateteneko ya adhi hutokana na nguvu za asili ambazo husababisha rngandamizo katika ya miamba. Hadi hivi sasa hakujagunduliwa teknolojia ya kuweza kutabiri kutokea kwa tetemeko la ardhi, hivyo GST inatoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari muda Wote kama ambavyo imekuwa ikishauri ili kuepuka madhara Yanayoweza kusababishwa na majanga asili ya Jiolojia ikiwemo matetemeko ya ardhi. Mojawapo ya hatua za tahadhari dhidi ya tetemeko la ardhi ni kama zifuatazo:
Kabla ya tukio; Kujenga nyumba bora na imara kwa kuzingatia viwango halisi vya ujenzi, kupata ushauri wa kitaalamu wa aina ya majengo yanayofaa kujengwa kulingana na jiolojla ya eneo husika, kuepuka ujenzi wa nyumba katika miinuko yenye kuambatana na mawe/miamba na mipasuko ya miamba.
Wakati wa tukio; Kama uko nje ya Jengo unashauriwa kubaki nje. simama mahali pa wazi mbali na majengo marefu, mti mirefu, nguzo na nyaya za na ujikinge kichwani kadri inavyowezekana; endapo litatokea ukiwa ndani ya nyumba unashauriwa kubaki ndani na ukae sehemu salama kama vile chini ya uvungu wa meza imara, kitanda, ama simama kwenye makutano ya na makabati ya vitabu, vyombo au fenicha ili kuepuka kuangukiwa na vitu hivyo; usitangetange muda mrefu kutafuta mahali salama kwa sababu tetemeko la ardhi hutokea ghafla na huchukua muda mfupi Sana; jihadhari na moto kwakuwa tetemeko la ardhi linaweza kusababisha matukio ya moto kwa kutokea hitilafu ya umeme au kupasuka kwa rnabomba ya gesi; usiendeshe chombo cha moto wakati wa tukio tetemeko; toa taarifa kwa uongozi wa husika au kwa vyombo vya uokoaji ili kupata msaada zaidi;
Baada ya tukio: kagua ili kuhakikisha kama hayakupata madhara na kama ikilazimu unashauriwa kuwaita wataalamu wa kufanya ukaguzi kuona kanu ni salama wa majengo hayo kuendelea kutumika.
View attachment 2520526
GST inapenda kuutangazia umma kwamba kumekuwa na matukio ya matetemeko ya ardhi katika maeneo ya wilaya ya Manyoni kwenye mpaka kati ya Mkoa wa Singida na Dodoma yakiwa na ukubwa wa 4.3 na 4.9 katika kipimo cha Richter kama yalivyoainishwa kwenye jedwali hapa chini:
Tarehe ya tukio | Muda wa tukio | ukubwa | Mahali lilipotokea | ||
Latitudo | Longitudo | Eneo | |||
16/2/2023 | 12:13 Jioni | 4.9 | -50 25' 47" | 340 57' 35" | Makuru |
17/2/2023 | 1:45 Asubuhi | 4.3 | -50 27' 35" | 340 57' 35" | Makuru |
17/2/2023 | 6:26 Mchana | 4.9 | -50 37 7.4" | 350 13' 156" | Zuboru |
Ikumbukwe kwamba mikoa ya Dodoma na Singida imepitiwa na ukanda wa bonde la ufa la Afrika Mashariki mkondo wa mashariki. Mikoa mingine katika mkondo wa mashariki ni Manyara, Arusha, Mara, Iringa na Njombe ambapo mkondo wa magharibi una mikoa ya Kagera, Kigoma, Katavi Rukwa, Songwe, Mbeya na Ruvuma. Maeneo ya ukanda wa bonde la ufa kwa kawaida ni maeneo tete ya mabadilko ya kijiolojia ambayo hukumbwa na matetemeko ya ardhi na milipuko ya volkano.
Mateteneko ya adhi hutokana na nguvu za asili ambazo husababisha rngandamizo katika ya miamba. Hadi hivi sasa hakujagunduliwa teknolojia ya kuweza kutabiri kutokea kwa tetemeko la ardhi, hivyo GST inatoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari muda Wote kama ambavyo imekuwa ikishauri ili kuepuka madhara Yanayoweza kusababishwa na majanga asili ya Jiolojia ikiwemo matetemeko ya ardhi. Mojawapo ya hatua za tahadhari dhidi ya tetemeko la ardhi ni kama zifuatazo:
Kabla ya tukio; Kujenga nyumba bora na imara kwa kuzingatia viwango halisi vya ujenzi, kupata ushauri wa kitaalamu wa aina ya majengo yanayofaa kujengwa kulingana na jiolojla ya eneo husika, kuepuka ujenzi wa nyumba katika miinuko yenye kuambatana na mawe/miamba na mipasuko ya miamba.
Wakati wa tukio; Kama uko nje ya Jengo unashauriwa kubaki nje. simama mahali pa wazi mbali na majengo marefu, mti mirefu, nguzo na nyaya za na ujikinge kichwani kadri inavyowezekana; endapo litatokea ukiwa ndani ya nyumba unashauriwa kubaki ndani na ukae sehemu salama kama vile chini ya uvungu wa meza imara, kitanda, ama simama kwenye makutano ya na makabati ya vitabu, vyombo au fenicha ili kuepuka kuangukiwa na vitu hivyo; usitangetange muda mrefu kutafuta mahali salama kwa sababu tetemeko la ardhi hutokea ghafla na huchukua muda mfupi Sana; jihadhari na moto kwakuwa tetemeko la ardhi linaweza kusababisha matukio ya moto kwa kutokea hitilafu ya umeme au kupasuka kwa rnabomba ya gesi; usiendeshe chombo cha moto wakati wa tukio tetemeko; toa taarifa kwa uongozi wa husika au kwa vyombo vya uokoaji ili kupata msaada zaidi;
Baada ya tukio: kagua ili kuhakikisha kama hayakupata madhara na kama ikilazimu unashauriwa kuwaita wataalamu wa kufanya ukaguzi kuona kanu ni salama wa majengo hayo kuendelea kutumika.