Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
John Tendwa, msajili wa vyama vya siasa nchini
MSAJILI wa Vyama Vya Siasa, John Tendwa amesema kwamba ofisi yake inafikiria kuwezakubadilisha mifumo ya uchaguzi kwa kufikiria nafasi na haki za msingi za mpigakura dhidi ya chama kinapomfukuza uanachama mbunge. Kauli hiyo ilitolewa leo na Tendwa wakati akizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dares Salaam mara baada ya kuapishwa kwa viongozi wapya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) ambapo alisema suala la kufukunzwa uanachama mbunge si geni lilishatokea hata katika mfumo wa chama kimoja.
Tendwa alitoa kauli hiyo mara baada ya kuulizwa swali la waandishi wa habari kuhusiana na kitendo cha Mbunge wa Jimbo la Wawi, Hamad Rashid kufukuzwa uanachama na Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF) hali ilimfanya kupoteza nyadhifa zake. Ambapo Tendwa aliongeza kuwa katika mfumo wa demokrasia ya vyama vingi inapotokea hali ya namna hiyo , alihoji kuwa mpigakura anafikiriwaje na chama juu ya sifa na haki za msingi dhidi ya chama.