Elizabeth Dominic
Platinum Member
- Dec 7, 2007
- 4,555
- 3,649
Niliwahi kusema na nitaendelea kusema Mheshimiwa Lema anahitaji msaada mkubwa wa wanaCDM wenye akili na wanaojua thamani na dhamana ya uongozi.Kitendo cha Mheshimiwa Lema kukaa juu ya gari ni uvunjifu mkubwa wa sheria za usalama barabarani na ni hatarishi kwa maisha yake na mashabiki wake.
Hii si mara ya kwanza Mheshimiwa Lema kuvunja sheria za usalama barabarani,mwaka jana sikumbuki mwezi alinin'ginia kwenye gari lililokuwa linakwenda mwendo kasi,likiwa limewasha taa na kupiga honi bila sababu za msingi nilipouliza kulikoni nikaambiwa ametoka kwenye mkutano Kijenge wa kuwamaliza madiwani wake waliofukuzwa na uongozi wa CDM.Tulikuwa tumesimama eneo la Metropole watu wazima walibaki na mshangao huku vijana na wapiga debe wakishangilia kana kwamba kitendo cha Lema kilikuwa cha maana sana.
Wengi hapa jamvini wanajua msimamo wangu linapokuja suala la Lema wengi walinipinga wengi walidhani nina chuki binafsi lakini leo wengi wanakubaliana na hoja zangu kwamba Lema anahitaji msaada hasa wa viongozi wa chama chake bahati mbaya viongozi wa chama chake badala ya kumsaidia wamebaki kumsifia hata katika masuala ya kijinga.
Ninachekaje! Kwani we unavyohona kina Malima, Mwigulu, Nape, Chenge, Lowassa...mh! the list is endless hawaitaji ushauri kutoka kwa viongozi wao oops! nimesahau kumbe viongozi nao wako kwenye list.