Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 302
Viongozi wa vyama vya siasa wamepinga vikali Kamati ya Kuangalia Uchaguzi Tanzania (Temco) kuruhusiwa kuwa mwangalizi wa ndani wakati wa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 31 na kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuiondoa kwenye orodha, kwa kile walichodai hawana imani na chombo hicho.
Wamesema hawana imani na watendaji wa Bodi ya Wakurugenzi ya Temco, kwa madai kuwa wanaonekana kuwa mashabiki wa chama tawala.
Mratibu wa Temco, Dk. Benson Banna, yumo ndani ya Redet sasa kweli hapa haki itatendeka, hata kama wataona matokeo halisi hawawezi kusema ukweli wa mambo tunajua ndani ya Temco kuna mashabiki wa CCM, walisema
Wakurugenzi wa Temco ndio wamo pia kwenye Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (REDET) na kwamba walishatoa utafiti kuonesha wagombea urais, ubunge na udiwani wa CCM ndio wanaoongoza na hivyo inawapa shaka kama Temco inaweza kusema uhalisia wa hali ya uchaguzi ulivyokwenda.
Wamesema hawana imani na watendaji wa Bodi ya Wakurugenzi ya Temco, kwa madai kuwa wanaonekana kuwa mashabiki wa chama tawala.
Mratibu wa Temco, Dk. Benson Banna, yumo ndani ya Redet sasa kweli hapa haki itatendeka, hata kama wataona matokeo halisi hawawezi kusema ukweli wa mambo tunajua ndani ya Temco kuna mashabiki wa CCM, walisema
Wakurugenzi wa Temco ndio wamo pia kwenye Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (REDET) na kwamba walishatoa utafiti kuonesha wagombea urais, ubunge na udiwani wa CCM ndio wanaoongoza na hivyo inawapa shaka kama Temco inaweza kusema uhalisia wa hali ya uchaguzi ulivyokwenda.