TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

SAKATA LA MURO: KESI YA PANYA KAPEWA PAKA.
SAKATA la madai ya kuomba Rushwa ya shilingi Mil.10 linalomkabili mwandishi wa shirika la Habari la TBC, Jerry Muro linahitaji uchanganuzi wa Kina, na fikra yakinifu zitakazokidhi haja za watanzania wanaofuatilia swala hili, na kuondoa utata unaoonekana wazi.

Suala la Muro limejaa utata na halieleweki wazi si tu kwa wananchi wanafuatilia, bali hata yeye nadhani hajui kunachoendelea.

Utata huu unatokana na mambo makuu mawili. Kwanza ni mazingira ya kukamatwa kwa hicho kinachodaiwa “Rushwa” na pili ni wahusikakatika Kesi yake.

Mazingira ya Kesi tangu kukamatwa kwake hadi kufikishwa kituoni yanaibua maswali mengi kwa kila mwenye fikra hai. Murro alikamatwa Jumapili ya tarehe 31/01/2009 akiwa katika gari lake aina ya Cresta GX100 lenye namba za usajili T 545 BEH na kufikishwa katika kituo kikuu cha Polisi Mkoa wa Dar; kwa madai ya kuomba rushwa ya Sh. Million 10 kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo. Bw. Michael Wage.

Bw. Wage anadai kwamba aliombwa rushwa hiyo na Muro siku mbili kabla ya kukamatwa, walipokutana na Muro katika Hotel moja jijini Dar. Hivyo Muro alipofikishwa kituoni hapo alitakiwa kutoa maelezo kuhusu tukio la siku mbili zilizopita.

Haingii akilini mtu kuomba rushwa leo halafu eti akamatwe siku mbili baadae; Lazima Umma uelezwe kwanini hakukamatwa siku hiyo hiyo alipoomba rushwa? Au labda makachero wote wa Polisi walikuwa wameenda likizo hivyo ilibidi kusubiri hadi siku mbili baadaye watakaporudi kutoka huko walikokuwa wameenda kula “good time”.

Lakini pia ni kwanini Bw. Wage hakuripoti Sakata hilo TAKUKURU ambao kisheria ndio wanaoshughulikia rushwa? Angeenda TAKUKURU angepewa noti zilizojizolea umaarufu kama “Pesa za moto” ambazo zingetumika kama ushahidi mzuri wa kumtia Murro hatiani. Je, Wage hafamu kuwa TAKUKURU ndio wenye dhamana ya madai yote yanayohusu rushwa? Kama anafahamu hilo, alienda Polisi kufanya nini?

Kwanini alikimbilia Polisi badala ya TAKUKURU? Huko polisi alikuwa anamfuata nani? Lazima swali hili lijibiwe kwa ufasaha na uyakinifu.

Lakini cha kuchekesha ni kwamba alikamatwa bila ushahidi wowote uliohusu Rushwa. Si “noti za moto” za TAKUKURU wala sarafu za Polisi alizokutwa nazo Murro.

Badala yake Polisi waliibua madai ya kukutwa na pingu ambayo hayana uhusiano wowote na kesi ya msingi ya Rushwa.

Lakini hili la pingu nalo linahitaji mjadala mpana. Mjadala huu ni kutokana na mazingira ya kukutwa kwa Pingu hizo. Gazeti la Nipashe la Jumatatu February 1/2010 liliripoti kuwa Murro alipofikishwa Kituoni hapo alipelekwa sehemu ya juu (Ghorofani) ya kituo kwa ajili ya mahojiano. Wakati Murro akiwa kwenye mahojiano gari lake lilikuwa likilindwa na askari kanzu.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi, siku hiyo alipoombwa rushwa Wage alidai kuona Pingu ndani ya gari la Muro. Hivyo Muro alipokamatwa gari yake ikalazimika kupekuliwa. Lakini funguo zikapotea katika mazingira yaliyojaa utata hapohapo kituoni. Hivyo Muro kulazimika kupiga simu nyumbani kuomba funguo za akiba.

Lakini kabla funguo za akiba hazijafika, zile zilizopotea zilipatikana na pingu hizo kukutwa ndani ya gari la Jerry; Je, nani alikuwa na funguo hizo?? Je, nikisema kwamba kuna askari alipoka fungua hizo na kwenda kuweka Pingu kwenye gari la Muro nitakuwa nimekosea?? Au nikisema wale makachero walioachwa kulinda gari wakati Muro akiwa kwenye mahojiano walitumia mbinu zao za “Kimafya” kutumbukiza Pingu katika gari la Muro nitakuwa navunja kifungu gani cha Sheria??

Lakini Wage, (mhasibu aliyesimamishwa kazi na waziri Mkuu kutokana na shutuma za ubadhirifu) akaibua hoja nyingine mufilisi. Eti alipokuwa kwenye gari ya Muro (wakati Muro akimuomba rushwa) alisahau miwani yake ambayo baada ya upekuzi ilikutwa kiti cha mbele wakati wa upekuzi.

Binafsi sidhani kama kukutwa kwa miwani kinahusika na sakata la msingi la Rushwa. Bali kwa kutumia ushahidi wa miwani kwa mbaaali kunaweza kutusadikisha (japo si sana) kuwa Wage alipanda gari ya Muro. Lakini je, kila anayepanda gari ya Muro anaombwa rushwa? Kama kila anayepanda gari ya Muro huombwa rushwa basi madai ya Wage yatakuwa na msingi; vinginevyo hizo ni fikra kurupushi tu.

Katika gari ya Muro kulikutwa vitu kadhaa, vikiwemo vifaa vyake vya kazi. Lakini pia ilikutwa miwani, boksi mbili za tissue na pingu za mkononi.
Viwili kati ya hivyo yaani miwani pamoja na tissue, Wge alidai ni mali zake na alizisahau aliposhuka. Kama amekiri kumiliki miwani na tissue na kwamba alivisahau aliposhuka, basi yawezekana hata hizo pingu yeye ndiye mmiliki wake na alizisahau tu, kama alivyosahau hivyo vingine. Kama aliweza kusahau miwani (anayoitumia kila siku), kwanini tushindwe kuamini kuwa hata hizo pigu alizisahau??.

Baada ya kuona namna MAZINGIRA ya Kesi yalivyojaa utata hebu tuangalie WAHUSIKA katika Kesi hii.

Michael Wage ambaye ndiye mlalamikaji mkuu katika Kesi hii ni “mhanga” katika “bomoabomoa” iliyofanywa na waziri mkuu mhe.Mizengo Pinda ambapo watendaji wa juu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo walisimamishwa kazi.

Lakini ikumbukwe kuwa hadi waziri mkuu kufikia hatua ya kuwasimamisha watendaji hao kazi inadaiwa Murro ndiye aliyefichua ufisadi uliokuwa umeighubika Halmashauri hiyo. Kwa tafsiri hiyo Muro ndiye “aliyewachomea utambi” watendaji hao, na kwa maana hiyo wana hasira nae. Hivyo nikisema Kesi hii ni ya kupikwa sidhani kama kimantiki itapingika.

Lakini hata jeshi la Polisi nao si marafiki sana wa Muro maana nao walishajeruhiwa na makucha yake.

Akiwa ITV Muro aliwahi kufichua rushwa iliyotolewa kwa trafiki katika maeneo ya barabara ya Dar – Moro. Habari hiyo ilirushwa na kituo cha televition cha ITV kupitia kipindi cha Ripoti maalum haikufurahiwa sana na Polisi maana Askari polisi 13 walisimamishwa kazi kwa tuhuma hizo za rushwa. Lakini pia hivi majuzi Murro alishiriki kuandaa kipindi cha Usiku wa Habari kilichorushwa na TBC -1 ambapo askari wa Usalama barabarani Mkoa wa Iringa walionekana wakipokea Rushwa.

Hili nalo liliongeza idadi ya maadui wa Muro na labda pia liliibua mbinu za namna ya kumzima. Ndio! Hatakiwi kuendelea kuumbua wakubwa kwa kile anachokiita “Habari za Uchunguzi”. Nani ana uhakika wa kupona kama akiachiwa aendelee kufichua? Yeah! Lazima azimwe maana fichua fichua yawezekana akafichua pasipofichulika.

Lakini jumatatu tarehe 1/February/2010 Kamanda wa Polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam; Selemani Kova aliongea na waandishi wa habari kuelezea tukio la kukamatwa kwa Muro. Pamoja na kuongea sana (kama kawaida yake) alinukuliwa na vyombo vya habari akisema “…..hapa namsaidia Wage kusema; maana haya alipaswa kuyasema yeye”.

Kauli hii inaibua utata kwa kila mwenye akili timamu. Wage ni nani hadi aajiri Jeshi la Polisi kumsemea? Kwa lipi hasa? Na kwa ujira wa shilingi ngapi?

Baadhi ya watu wenye fikra finyu walimsifu RPC Kova kutoa tamko bila kujua kuwa Kova alikuwa anajishtaki mwenyewe. Kwa kukiri kwamba anasema kwa niaba ya Wage; ina maana kuwa Wage ndiye aliyemtuma aseme. Swali. Tangu lini Kamanda Kova amefanyika kuwa Afisa habari/msemaji wa Wage??

Napotafakari kauli ya Kova (Kwamba alimsaidia Wage Kusema) naanza kupata majibu kwanini Wage hakwenda TAKUKURU na badala yake akakimbilia Polisi.

Kutokana na kauli hii uhusiano baina ya Kova na Michael Wage unapaswa uchunguzwe ili tujue msimamo wa RPC wetu. Ikiwezekana achague moja kama ataendelea kuwa RPC au ataacha kazi yake ya upolisi abakie na hiyo mpya ya kuwa Afisa habari wa Wage.

Kwa ujumla mlalamikaji katika Kesi hii Michael Wage pamoja na wanaoendesha kesi hii Jeshi la Polisi wamewahi kuwa “majeruhi” wa Muro kwa nyakati tofauti. Halafu eti leo ndio wanaongoza upande wa mashtaka katika Kesi ya yuleyule “mbaya wao”. Halafu tunategemea haki itendeke. Thubutu!! Hicho ni kichekesho. Tusishangae kuona Muro akipokwa HAKI yake waziwazi maana Kesi ya Panya kapelekewa Paka. Ni uzandiki.


Niachie ujumbe:
0715-187677;
0712-025958
 
sakata la muro: Kesi ya panya kapewa paka.

sakata la madai ya kuomba rushwa ya shilingi mil.10 linalomkabili mwandishi wa shirika la habari la tbc, jerry muro linahitaji uchanganuzi wa kina, na fikra yakinifu zitakazokidhi haja za watanzania wanaofuatilia swala hili, na kuondoa utata unaoonekana wazi.

Suala la muro limejaa utata na halieleweki wazi si tu kwa wananchi wanafuatilia, bali hata yeye nadhani hajui kunachoendelea.

Utata huu unatokana na mambo makuu mawili. Kwanza ni mazingiraya kukamatwa kwa hicho kinachodaiwa “rushwa” na pili ni wahusikakatika kesi yake.

mazingiraya kesi tangu kukamatwa kwake hadi kufikishwa kituoni yanaibua maswali mengi kwa kila mwenye fikra hai. Murro alikamatwa jumapili ya tarehe 31/01/2009 akiwa katika gari lake aina ya cresta gx100 lenye namba za usajili t 545 beh na kufikishwa katika kituo kikuu cha polisi mkoa wa dar; kwa madai ya kuomba rushwa ya sh. Million 10 kutoka kwa aliyekuwa mhasibu wa halmashauri ya wilaya ya bagamoyo. Bw. Michael wage.

Bw. Wage anadai kwamba aliombwa rushwa hiyo na muro siku mbili kabla ya kukamatwa, walipokutana na muro katika hotel moja jijini dar. Hivyo muro alipofikishwa kituoni hapo alitakiwa kutoa maelezo kuhusu tukio la siku mbili zilizopita.

Haingii akilini mtu kuomba rushwa leo halafu eti akamatwe siku mbili baadae; lazima umma uelezwe kwanini hakukamatwa siku hiyo hiyo alipoomba rushwa? Au labda makachero wote wa polisi walikuwa wameenda likizo hivyo ilibidi kusubiri hadi siku mbili baadaye watakaporudi kutoka huko walikokuwa wameenda kula “good time”.

lakini pia ni kwanini bw. Wage hakuripoti sakata hilo takukuru ambao kisheria ndio wanaoshughulikia rushwa? Angeenda takukuru angepewa noti zilizojizolea umaarufu kama “pesa za moto” ambazo zingetumika kama ushahidi mzuri wa kumtia murro hatiani. Je, wage hafamu kuwa takukuru ndio wenye dhamana ya madai yote yanayohusu rushwa? kama anafahamu hilo, alienda polisi kufanya nini?

kwanini alikimbilia polisi badala ya takukuru? Huko polisi alikuwa anamfuata nani? Lazima swali hili lijibiwe kwa ufasaha na uyakinifu.

Lakini cha kuchekesha ni kwamba alikamatwa bila ushahidi wowote uliohusu rushwa. Si “noti za moto” za takukuru wala sarafu za polisi alizokutwa nazo murro.

Badala yake polisi waliibua madai ya kukutwa na pingu ambayo hayana uhusiano wowote na kesi ya msingi ya rushwa.

Lakini hili la pingu nalo linahitaji mjadala mpana. Mjadala huu ni kutokana na mazingira ya kukutwa kwa pingu hizo. Gazeti la nipashe la jumatatu february 1/2010 liliripoti kuwa murro alipofikishwa kituoni hapo alipelekwa sehemu ya juu (ghorofani) ya kituo kwa ajili ya mahojiano. Wakati murro akiwa kwenye mahojiano gari lake lilikuwa likilindwa na askari kanzu.

Kwa mujibu wa taarifa za polisi, siku hiyo alipoombwa rushwa wage alidai kuona pingu ndani ya gari la muro. Hivyo muro alipokamatwa gari yake ikalazimika kupekuliwa. Lakini funguo zikapotea katika mazingira yaliyojaa utata hapohapo kituoni. Hivyo muro kulazimika kupiga simu nyumbani kuomba funguo za akiba.

Lakini kabla funguo za akiba hazijafika, zile zilizopotea zilipatikana na pingu hizo kukutwa ndani ya gari la jerry; je, nani alikuwa na funguo hizo?? Je, nikisema kwamba kuna askari alipoka fungua hizo na kwenda kuweka pingu kwenye gari la muro nitakuwa nimekosea?? Au nikisema wale makachero walioachwa kulinda gari wakati muro akiwa kwenye mahojiano walitumia mbinu zao za “kimafya” kutumbukiza pingu katika gari la muro nitakuwa navunja kifungu gani cha sheria??

Lakini wage, (mhasibu aliyesimamishwa kazi na waziri mkuu kutokana na shutuma za ubadhirifu) akaibua hoja nyingine mufilisi. Eti alipokuwa kwenye gari ya muro (wakati muro akimuomba rushwa) alisahau miwani yake ambayo baada ya upekuzi ilikutwa kiti cha mbele wakati wa upekuzi.

Binafsi sidhani kama kukutwa kwa miwani kinahusika na sakata la msingi la rushwa. bali kwa kutumia ushahidi wa miwani kwa mbaaali kunaweza kutusadikisha (japo si sana) kuwa wage alipanda gari ya muro. Lakini je, kila anayepanda gari ya muro anaombwa rushwa? kama kila anayepanda gari ya muro huombwa rushwa basi madai ya wage yatakuwa na msingi; vinginevyo hizo ni fikra kurupushi tu.

Katika gari ya muro kulikutwa vitu kadhaa, vikiwemo vifaa vyake vya kazi. Lakini pia ilikutwa miwani, boksi mbili za tissue na pingu za mkononi.
Viwili kati ya hivyo yaani miwani pamoja na tissue, wge alidai ni mali zake na alizisahau aliposhuka. kama amekiri kumiliki miwani na tissue na kwamba alivisahau aliposhuka, basi yawezekana hata hizo pingu yeye ndiye mmiliki wake na alizisahau tu, kama alivyosahau hivyo vingine. Kama aliweza kusahau miwani (anayoitumia kila siku), kwanini tushindwe kuamini kuwa hata hizo pigu alizisahau??.

Baada ya kuona namna mazingira ya kesi yalivyojaa utata hebu tuangalie wahusika katika kesi hii.

Michael wage ambaye ndiye mlalamikaji mkuu katika kesi hii ni “mhanga” katika “bomoabomoa” iliyofanywa na waziri mkuu mhe.mizengo pinda ambapo watendaji wa juu wa halmashauri ya wilaya ya bagamoyo walisimamishwa kazi.

Lakini ikumbukwe kuwa hadi waziri mkuu kufikia hatua ya kuwasimamisha watendaji hao kazi inadaiwa murro ndiye aliyefichua ufisadi uliokuwa umeighubika halmashauri hiyo. Kwa tafsiri hiyo muro ndiye “aliyewachomea utambi” watendaji hao, na kwa maana hiyo wana hasira nae. Hivyo nikisema kesi hii ni ya kupikwa sidhani kama kimantiki itapingika.

Lakini hata jeshi la polisi nao si marafiki sana wa muro maana nao walishajeruhiwa na makucha yake.

Akiwa itv muro aliwahi kufichua rushwa iliyotolewa kwa trafiki katika maeneo ya barabara ya dar – moro. Habari hiyo ilirushwa na kituo cha televition cha itv kupitia kipindi cha ripoti maalum haikufurahiwa sana na polisi maana askari polisi 13 walisimamishwa kazi kwa tuhuma hizo za rushwa. Lakini pia hivi majuzi murro alishiriki kuandaa kipindi cha usiku wa habari kilichorushwa na tbc -1 ambapo askari wa usalama barabarani mkoa wa iringa walionekana wakipokea rushwa.

Hili nalo liliongeza idadi ya maadui wa muro na labda pia liliibua mbinu za namna ya kumzima. Ndio! Hatakiwi kuendelea kuumbua wakubwa kwa kile anachokiita “habari za uchunguzi”. nani ana uhakika wa kupona kama akiachiwa aendelee kufichua? Yeah! Lazima azimwe maana fichua fichua yawezekana akafichua pasipofichulika.

Lakini jumatatu tarehe 1/february/2010 kamanda wa polisi wa kanda maalumu ya dar es salaam; selemani kova aliongea na waandishi wa habari kuelezea tukio la kukamatwa kwa muro. Pamoja na kuongea sana (kama kawaida yake) alinukuliwa na vyombo vya habari akisema “…..hapa namsaidia wage kusema; maana haya alipaswa kuyasema yeye”.

kauli hii inaibua utata kwa kila mwenye akili timamu. Wage ni nani hadi aajiri jeshi la polisi kumsemea? Kwa lipi hasa? Na kwa ujira wa shilingi ngapi?

Baadhi ya watu wenye fikra finyu walimsifu rpc kova kutoa tamko bila kujua kuwa kova alikuwa anajishtaki mwenyewe. Kwa kukiri kwamba anasema kwa niaba ya wage; ina maana kuwa wage ndiye aliyemtuma aseme. swali. tangu lini kamanda kova amefanyika kuwa afisa habari/msemaji wa wage??

Napotafakari kauli ya kova (kwamba alimsaidia wage kusema) naanza kupata majibu kwanini wage hakwenda takukuru na badala yake akakimbilia polisi.

Kutokana na kauli hii uhusiano baina ya kova na michael wage unapaswa uchunguzwe ili tujue msimamo wa rpc wetu. Ikiwezekana achague moja kama ataendelea kuwa rpc au ataacha kazi yake ya upolisi abakie na hiyo mpya ya kuwa afisa habari wa wage.

Kwa ujumla mlalamikaji katika kesi hii michael wage pamoja na wanaoendesha kesi hii jeshi la polisi wamewahi kuwa “majeruhi” wa muro kwa nyakati tofauti. Halafu eti leo ndio wanaongoza upande wa mashtaka katika kesi ya yuleyule “mbaya wao”. halafu tunategemea haki itendeke. Thubutu!! Hicho ni kichekesho. Tusishangae kuona muro akipokwa haki yake waziwazi maana kesi ya panya kapelekewa paka. Ni uzandiki.




niachie ujumbe:






0715-187677;



0712-025958

hamna lolote... Hamna utata... Nakuachia ujumbe... Wacha longolongo... Dogo tapeli huyu... Kama ilivyo kawaida ya waandishi wa habari wengi tanzania alitaka kuvuta kitu kidogo.. Wacha sheria ichukue mkondo wake.. Usitete wahalifu..
 
Maggid;

Hard Facts:
1. Jerry ameonekana kwenye camera ya hotel akiwa na huyo mhasibu na wale matapeli wa Dar wanaojulikana.

2. Jerry alikutwa na pingu aliyothibitisha kuwa ni yake. pingu na mwandishi wa habari wapi na wapi?

3. Kwenye Camera ya Jerry kulikuwa na picha ya ghorofa za huyu mhasibu wa bagamoyo9Nyumba anazojenga Morogoro)

4. Jerry hakutaka kushuka kwenye gari bali alitaka kukutana na jamaa kwenye gari badala ya sehemu public.

5. Jerry anadai Kamanda Kova (kamishna wa polisi) ni mtu mdogo sana hapa Tanzania.

Madai:

1. Ni tabia ya Jerry kula rushwa
2. Jerry siku hiyo aliwazunguka wenzie.
3. Wale jamaa waliokamatwa na kuonekana na jerry ni matapeli makubwa.


Machache tu hayo

FP


FairPlayer... ubarikiwe kwa kutoshabikia upande wowote na kuanika ukweli..
 
Haja aende kuku akienda bata ohoo ameharisha....where are you guys mliokuwa mnasema ongezeko la thread zinazomuhusu Jerry Muro zinakera? Ningepost mimi hii ingekuwa balaaa! Lakini wengine walaaaa zinaachwa tu.....Nikiweka mimi oooh zinawachefua! Oooh mara ziunganishwe sijui wapi huko! Haya!
 
Haja aende kuku akienda bata ohoo ameharisha....where are you guys mliokuwa mnasema ongezeko la thread zinazomuhusu Jerry Muro zinakera? Ningepost mimi hii ingekuwa balaaa! Lakini wengine walaaaa zinaachwa tu.....Nikiweka mimi oooh zinawachefua! Oooh mara ziunganishwe sijui wapi huko! Haya!

Pape dont take it too personal and emotional jamani!!!!!!!!!!!!! hii kitu tumekoment ikapotea nashangaa imerudi hapa upya without the comment we made!!!!!!!!!!!
 
Pape dont take it too personal and emotional jamani!!!!!!!!!!!!! hii kitu tumekoment ikapotea nashangaa imerudi hapa upya without the comment we made!!!!!!!!!!!
sawa, ama kweli wa mbili ni wa mbili havai moja hata siku moja!
 
Nina Swali: Kwa nini Jerry Muro alikuwa anatembea na Bastola?

Tanzania hivi sasa unaweza kuomba kununua bastola kwa ajili ya usalama wako, Ukipata kibali unanunua na unatembea nayo as you wish.

Polisi wanaleta mazezeta wao kama wana ushahidi kwamba huyu bwana ana kosa wamshitaki hakuna sababu ya malumbano yasiyokuwa na tija. Kama hawaezi kumshitaki wafyate mkia.
 
I said, "But suppose there isn't anything to find?"

And the Boss said, "There is always something."

And he said, "Man is conceived in sin and born in corruption and he passeth from the stink of the didie to the stench of the shroud. There is always something."
Two miles more, and he said, "And make it stick."

All The King's Men

Robert Penn Warren
 
Aise nimecheka sana na hii issue. Kwa kweli Tanzania bado sana katika mambo ya haki na sheria, polisi pamoja na mtuhumiwa kwa nini wanaongelea hii kesi kabla ya kwenda mahakamani? Hii sio sahihi kabisa, nimeona kamanda wa polisi (I presume) ati anaonyesha pingu hadharani na kuuliza maswali je huu ndio utendaji wa kazi wa polisi? Je, hizo pingu alizoonyesha ndio za mtuhumiwa? Je, anaweza ku-prove kwamba hazijabadilishwa kwa kutumia technology ya finger printing?

Nafikiri wana haja ya kufuatilia case files kama zile za FBI files nk. Sina hamu kabisa ndio sababu mafisadi wanapeta Tanzania. Too many loop holes.
 
Tuache vyombo vya dola vifanye kazi ....mtuhumiwa ni mtuhumiwa tu

Vyombo vya dola vinapokosa kuaminiwa kwa uadilifu hivyo si vyombo vya dola tena ni vyombo vya uhalifu na hatuwezi kaa kimya wanatuharibia nchi yetu kwa kuwa tu wao ni custodian wa SMG ambazo zimenunuliwa kwa kodi yetu.

Trust is the best weapon for any state organ than SMG and bombs. Watu wasipokuwa na imani na wewe unakosa legitimacy ya kuwepo kwako. Otherwise upo kidictator so jeshi la polisi limeoza haliaminiki tena na ndiyo maana wanafanya kila njia ikiwemo kutengeneza CCTV ambazo hazipo ili kuonesha wao wapo sahihi kitu ambacho kinazidi kuwashushia credibility yao.

On this the Public is on the side of Jerry Murro halina ubishi. Ndiyo maana nasema sasa umefika wakati wa kuwa na watu intelligent kwenye nafasi kama za kina Kova ambao hata neno electronics linamshinda na kutamka "ELEKITIRONIKI"
 
Just Curious, Do Tanzanian laws and courts allow and admit pictures and video recording as substantial evidence in any case? what about voice recording?

If there is no such law or such things are not admissible in court, how can Kova state that he has video evidence?

Does the Video evidence have voice recording to colaborate the conspiracy?

Is the CCTV in question a police property or who is the owner and who actually recorded the meeeting?

Why did Jerry Muro rush to plea his case online and to the mass and not open a defamation case against the Police in our courts?

If it is true that Jerry met these 2 guys, who are alleged to be high calibre crooks, what can Jerry Muro tell Tanzanians about such meeting?
 
Just Curious, Do Tanzanian laws and courts allow and admit pictures and video recording as substantial evidence in any case? what about voice recording?

If there is no such law or such things are not admissible in court, how can Kova state that he has video evidence?

Does the Video evidence have voice recording to colaborate the conspiracy?

Is the CCTV in question a police property or who is the owner and who actually recorded the meeeting?

Why did Jerry Muro rush to plea his case online and to the mass and not open a defamation case against the Police in our courts?

If it is true that Jerry met these 2 guys, who are alleged to be high calibre crooks, what can Jerry Muro tell Tanzanians about such meeting?

Maswali yako muhimu sana Rev, na ukiiangalia hii picture impartially hata kama huwezi kupata majibu mahsusi, utaweza kuona yafuatayo.At least I do.

I will cut this story short Rev (or I will at least try).

1.Jerry Muro was engaging in some very unorthodox, most probably criminal type of extortion or similarly shady deals.

2. The police is delighted in nailing him and it is also using some very unorthodox and possibly criminal shady means of prosecuting him. First of all he has a big mouth and lack humility, intelligence and decorum. The "Kova ni mtu mdogo sana" comment just adds insult to the injury of his police incriminating photos. Ukimuangalia Kova vizuri utaona he is barely containing his vendetta.

3. The Tanzanian people are fvcked up once again. They thought there was a mesiah here, just a dragon breathing fire.

4. The law is an ass, legally if Jerry can get good lawyers there is no case here.

5. Kama alivyosema Mr. Warren katika "All The Kings Men", nobody is clean in this world, you just have to set a mark on what degree of dirt is acceptable. Kama alivyosema AZ katika "Royal Salute" "You got those that touch a little. Then there's those that rape " sasa it is up to you kama utasema kuiba reams za karatasi kazini ndiyo ku touch a little au hata Jerry na unorthodox extortions zake bado ni "ku touch a little" na anaweza kusamehewa kutokana na kazi aliyofanya.

Kwangu mimi Jerry si Revolutionary enough, ana tamaa mbele mauti nyuma.

Lakini at the same time hiyo haimaanishi polisi wam clobber up bila kufuata taratibu.
 
Maggid;

Hard Facts:
1. Jerry ameonekana kwenye camera ya hotel akiwa na huyo mhasibu na wale matapeli wa Dar wanaojulikana.

2. Jerry alikutwa na pingu aliyothibitisha kuwa ni yake. pingu na mwandishi wa habari wapi na wapi?

3. Kwenye Camera ya Jerry kulikuwa na picha ya ghorofa za huyu mhasibu wa bagamoyo9Nyumba anazojenga Morogoro)

4. Jerry hakutaka kushuka kwenye gari bali alitaka kukutana na jamaa kwenye gari badala ya sehemu public.

5. Jerry anadai Kamanda Kova (kamishna wa polisi) ni mtu mdogo sana hapa Tanzania.

Madai:

1. Ni tabia ya Jerry kula rushwa
2. Jerry siku hiyo aliwazunguka wenzie.
3. Wale jamaa waliokamatwa na kuonekana na jerry ni matapeli makubwa.


Machache tu hayo

FP
hapa fp naona hujacheza fairly, kwa sababu kutokana na kazi zake huyo mwandishi kukutana na hao watu wawe matapeli/si matapeli ni jambo la kawaida ili aweze kufanikisha kazi yake ya kuwa nasa wala rushwa.
mfano leo hii wewe bila kujua/kwa kujua ufuatwe na na dada poa , na kile kipindi unaongea sema anakuomba nauli/lifti mtu akupige picha aseme huyo dada ni nyumba ndogo au ndio zako itkuwa ni kweli? wakati huyo dada ametumwa kwako kwa kazi maalum, moja upigwe picha nae pili ikiwezekana aenda hatu moja zaidi na wewe.
haya mengine kama zake au aliwazinguka wenzake si wezi ongelea.
 
Kuonekana na Tapeli siyo kosa jamani; vinginevyo kuna watu wangetiwa pingu kuanzia Ikulu kwa kupiga picha na mafisadi!
 
Najiuliza huyo raia mwema aliyetoa taarifa zilizowezesha kukamatwa hao matapeli sugu alikuwa ametapeliwa nini? Naona polisi watakuwa wanaendeleza sinema yao tu, hao jamaa walikuwa wanawafahamu siku nyingi (Kwa maelezo ya Kova) hivyo itakuwa waliwauliza tu wapo wapi muda huu, wakaenda kuwakamata ili kufanya finishing ya hii cinema wanayoendelea kuicheza!
 
Kwa kweli mimi namshangaa sana huyu mtu anaitwa Kamanda KOVA anapenda sana publicity kuliko kazi yake kama afande nahisi anamuonea wivu JM kwa kazi yake. tangu siku nyingi namfuatilia KOVA sio mtendaji hata kidogo na hii inadhihirishwa na alivyo ona alivyojinenepea hivi kweli POLISI unakuwa na tumbo kama mjamzito wapi umeona polisi wa vile?.

Mtu mwenye kufikiria majibu ya kero za watanzania hawezi kunenepa ovyo. Huyu kamanda achunguzwe inawezekana wale vijana wake anaowatuma JM anawakwamisha kwa namna moja au nyingine hivyo makusanyo yake kamanda yanapungua ndio maana kamzulia jambo hili. Polisi ya bongo imeoza inanuka inahitaji kusafishwa.

Namshangaa Kova hao jamaa anaowaita matapeli sugu ni mahakama gani iliyowahukumu? manake nijuavyo mimi KOVA sio mahakama, kawahukumu jamaa hao kabla ya mahakama anajua anachokifanya kweli? Namshauri kamanda aache sihasa na porojo zake za kwenye media, watanzania tuna kero nyingi hasa katika swala zima la usalama wa raia, twamtaka afanye kazi.

Namkumbuka Kamanda mmoja anaitwa TOSI niliwahi kumuona akipiga kazi kupambana na majangiri kwenye pori la kimisi, na bukombe-ngara akiwa Kagera RPC na njia zilipitika yuko wapi jamani? sijawahi kumuona akipiga porojo runingani, watanzania tufanye kazi jamani
 
Back
Top Bottom