Tausi kuorodheshwa ndege waharibifu India

Primier

Member
Dec 16, 2015
86
14
150416141446_peacock_640x360_ap_nocredit.jpg
Image copyright AP
Image caption Tausi
Jimbo moja nchini India limependekeza kumuorodhesha tausi miongoni mwa ndege waharibifu ,kulingana na vyombo vya habari.


Waziri wa kilimo katika eneo la Goa Ramesh Tawadkar amesema kuwa tausi wanaharibu mimea na huenda wakakatwa midomo.

Tumbili,Ngiri pia watakatwa mdomo katika mpango huo.Upungufu wa misito katika eneo la Goa umepunguza kuwepo kwa maneo ya kujificha wanyama pori ambao sasa wanakimbiliana katika makaazi ya binaadamu.


Bwana Tawadkar amesema kuwa kamati imebuniwa kuona athari za ndege hao pamoja na wanyama wengine.

''Baadhi ya wakulima wamesema kuwa tausi uharibu mimea katika mashamba yaliopo katika maeneo ya milima,''alikiambia chombo cha habari cha India.

141123121550_thar_pakistan_640x360_afp_nocredit.jpg
Image copyright AFP
Image caption Tausi India
Wanyama hao kwa sasa wanalindwa kwa mujibu wa sheria za mwaka 1972 za wanyama pori nchini India.

Waziri huyo amesema kuwa anajua kuhusu hadhi ya ndege huyo,lakini akasisitiza kwamba serikai itafuata utaratibu ambapo ndege huyo huenda akaorodheshwa miongoni mwa wanyama waharibifu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom