Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,149
Ntimizi awania uenyekiti UWT Tabora
Lucas Raphael, Tabora
Daily News; Friday,November 28, 2008 @20:01
Mbunge wa Igalula, Tatu Ntimizi amejitokeza kuwania uenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora. Licha ya Mbunge huyo, pia yumo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Mwasiti Ngesi, Mwalimu Lucy Kayanda na mfanyabiashara Maimuna Mohamed.
Akizungumza na gazeti hili, Katibu wa UWT wa Mkoa, Martha Kanakamfumu alisema watu hao wanne ndio pekee waliojitokeza kuwania nafasi hiyo. Alisema kazi ya kuwachuja wagombea hao inaendelea na itafanyika chini ya Kamati ya Siasa ya Mkoa.
Alisema vikao vyote vya jumuiya hiyo vitafanyika kwa mujibu wa kanuni na taratibu za UWT kwani kwa sasa ni vikao vya ndani ndio vinaendelea. Alisema uchaguzi wa jumuiya hiyo mkoa unatarajia kufanyika Desemba 6, mwaka huu katika ukumbi wa mkutano wa Kituo cha Wanafunzi mkoani hapa.
Uteuzi wa wagombea kwa jumuiya hiyo wamelazimika kurudia kutokana na mgombea mmoja kati ya wawili waliokuwa wameomba kukosa sifa. Hivyo kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), kilichoketi mwanzoni mwa mwezi huu mjini Dodoma, kiliamuru nafasi hiyo itangazwe upya. Wagombea hao ni Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Urambo, Martha Susu na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Mwasiti Ngesi.
Lucas Raphael, Tabora
Daily News; Friday,November 28, 2008 @20:01
Mbunge wa Igalula, Tatu Ntimizi amejitokeza kuwania uenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora. Licha ya Mbunge huyo, pia yumo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Mwasiti Ngesi, Mwalimu Lucy Kayanda na mfanyabiashara Maimuna Mohamed.
Akizungumza na gazeti hili, Katibu wa UWT wa Mkoa, Martha Kanakamfumu alisema watu hao wanne ndio pekee waliojitokeza kuwania nafasi hiyo. Alisema kazi ya kuwachuja wagombea hao inaendelea na itafanyika chini ya Kamati ya Siasa ya Mkoa.
Alisema vikao vyote vya jumuiya hiyo vitafanyika kwa mujibu wa kanuni na taratibu za UWT kwani kwa sasa ni vikao vya ndani ndio vinaendelea. Alisema uchaguzi wa jumuiya hiyo mkoa unatarajia kufanyika Desemba 6, mwaka huu katika ukumbi wa mkutano wa Kituo cha Wanafunzi mkoani hapa.
Uteuzi wa wagombea kwa jumuiya hiyo wamelazimika kurudia kutokana na mgombea mmoja kati ya wawili waliokuwa wameomba kukosa sifa. Hivyo kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), kilichoketi mwanzoni mwa mwezi huu mjini Dodoma, kiliamuru nafasi hiyo itangazwe upya. Wagombea hao ni Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Urambo, Martha Susu na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Mwasiti Ngesi.