Mohammed Dewji
New Member
- Nov 30, 2009
- 3
- 7
Mambo mengi yamesemwa kuhusu tatizo la umeme nchini Tanzania, mimi nitaanza kwa kugusia mambo machache yanayoonyesha matatizo ya umeme yalivyokuwa makubwa ndani ya bara letu la Afrika:
Lakini hili tatizo linaweza likakaa milele kwa nchi zetu za Afrika iwapo hatutaamka kwa kuangalia tatizo hili kama la miaka hamsini ijayo. Sisi tunazinduka pale umeme unapoanza kuwa wa mgao jijini Dar Es Salaam, je tunajiuliza vipi kule Kigoma mjini ambao wanapata adha ya mgao huo miaka nenda rudi.
Mimi ninafikiria tatizo la umeme nchini linaweza likapatiwa ufumbuzi iwapo tukiamua sasa kuwa nchi inabidi iangalie matumizi ya nishati ya umeme itakavyoongezeka miaka ijayo hivyo tujiandae kuongeza Megawati nyingi kwa ajili ya miaka ijayo na pia kuboresha usambazaji.
Unaweza ukachagua kampuni isiyokuwa sahihi kwenye mchakato mzima iwapo maamuzi yako yanakuwa yale ya haraka na yaliyofanyika kutokana na matatizo yanayowakabili watu wako kwa muda huo. Lakini iwapo ukiwa na muda wa kutosha ninaamini tunaweza tukaamua vizuri kwa ajili ya kusuluhisha matatizo ya umeme yanayotukabili.
Kitu kingine ambacho wataalam mbalimbali walioulizwa (consultantancy experts) jinsi ya kulitatua tatizo hilo walikuja na njia moja kuu.
Wakasema kuwa ili nchi za kusini mwa jangwa la Sahara ziweze kujinasua kwenye tatizo hilo inabidi zijenge vituo viwili au vitatu vikubwa vya kuzalishia umeme kwa pamoja, kuliko kila mtu kuanza kutengeneza kituo chake ambacho kitakuwa kidogo na gharama yake ya uzalishaji inaweza ikawa kubwa kuliko ile ya vituo vikubwa.
Maoni yangu ili Tanzania iweze kuondokana na tatizo hili la umeme inabidi viongozi wahusika wakae chini watafakari nini kifanyike ili sehemu nyingine za Tanzania umeme ufike wa kutosha kwa miaka mingi ijayo, tusiwe na fikra za kufikisha Megawati kadhaa kwa ajili ya sasa hivi, tuwe tunajiuliza vipi hapo baadaye tutafanyaje?
Hivyo tatizo la umeme la leo nchini Tanzania na nchi nyingi za Kiafrika linatokea kwa sababu hatuoni mbele, kama mfano wa Eskom ya Afrika Kusini ambao kama wangeweza kupanga vizuri basi leo mgao wa umeme kwao usingetokea, vivyo hivyo TANESCO inabidi waje na mipango thabiti ya kutupa umeme wa kutosha kwa miaka mingi ijayo.
Nashukuru kwa kusoma makala haya, ninajua kuna mengi sijagusia lakini mimi ninapendelea kuongelea jambo kwa kutoyarudia yaliyosemwa badala yake napenda kuongeza vitu vipya kwenye mjadala ili tuweze kujadiliana kwa kina.
MO
- Hatujawekeza ipasavyo kwa miaka 15 hadi 20 katika kitengo cha uzalishaji na usambazaji wa umeme, hayo maneno yalitamkwa na Lawrence Musaba, Meneja wa Southern African Power pool, muungano na mtandao wa nchi kumi na mbili kusini mwa Sahara.
- Kuanzia Nigeria, Ghana mpaka Luanda hela nyingi inatumika kuzalisha umeme kwa majenereta hali inayofanya uchumi wa nchi nyingi za Afrika kupungua ukuaji kwa asilimia mbili – ripoti ya Benki ya dunia.
- Ukiitoa nchi ya Afrika Kusini kwenye mambo hayo, nchi zote zilizobaki za kusini mwa jangwa la Sahara lenye watu milioni 700, linapata umeme sawa na wananchi wa Poland ambao ni milioni 38 tu.
- Eskom, kampuni ya umeme ya Afrika Kusini mwaka 1998 iliambiwa mwaka 2007 itaanza kupata tatizo la mgao wa umeme nchini iwapo isipopanga jinsi ya kuongeza uzalishaji wa nishati, lakini kutokana na matatizo ya fedha na mipango kampuni haikufanyia kazi yale mapendekezo ya wataalamu kwenye ripoti ya mwaka 1998, na kuanzia mwaka 2006 Afrika Kusini imeanza kupata misuko suko ya mgao wa umeme pia.
- Nigeria, nchi yenye watu wengi kuliko wote Afrika na yenye utajiri wa mafuta ina vituo 79 vya kuzalisha umeme lakini ni vituo 19 vinavyofanya kazi na hivyo kusababisha hasara ya dola za kimarekani bilioni moja kwa mwaka kiuchumi.
Lakini hili tatizo linaweza likakaa milele kwa nchi zetu za Afrika iwapo hatutaamka kwa kuangalia tatizo hili kama la miaka hamsini ijayo. Sisi tunazinduka pale umeme unapoanza kuwa wa mgao jijini Dar Es Salaam, je tunajiuliza vipi kule Kigoma mjini ambao wanapata adha ya mgao huo miaka nenda rudi.
Mimi ninafikiria tatizo la umeme nchini linaweza likapatiwa ufumbuzi iwapo tukiamua sasa kuwa nchi inabidi iangalie matumizi ya nishati ya umeme itakavyoongezeka miaka ijayo hivyo tujiandae kuongeza Megawati nyingi kwa ajili ya miaka ijayo na pia kuboresha usambazaji.
Unaweza ukachagua kampuni isiyokuwa sahihi kwenye mchakato mzima iwapo maamuzi yako yanakuwa yale ya haraka na yaliyofanyika kutokana na matatizo yanayowakabili watu wako kwa muda huo. Lakini iwapo ukiwa na muda wa kutosha ninaamini tunaweza tukaamua vizuri kwa ajili ya kusuluhisha matatizo ya umeme yanayotukabili.
Kitu kingine ambacho wataalam mbalimbali walioulizwa (consultantancy experts) jinsi ya kulitatua tatizo hilo walikuja na njia moja kuu.
Wakasema kuwa ili nchi za kusini mwa jangwa la Sahara ziweze kujinasua kwenye tatizo hilo inabidi zijenge vituo viwili au vitatu vikubwa vya kuzalishia umeme kwa pamoja, kuliko kila mtu kuanza kutengeneza kituo chake ambacho kitakuwa kidogo na gharama yake ya uzalishaji inaweza ikawa kubwa kuliko ile ya vituo vikubwa.
Maoni yangu ili Tanzania iweze kuondokana na tatizo hili la umeme inabidi viongozi wahusika wakae chini watafakari nini kifanyike ili sehemu nyingine za Tanzania umeme ufike wa kutosha kwa miaka mingi ijayo, tusiwe na fikra za kufikisha Megawati kadhaa kwa ajili ya sasa hivi, tuwe tunajiuliza vipi hapo baadaye tutafanyaje?
Hivyo tatizo la umeme la leo nchini Tanzania na nchi nyingi za Kiafrika linatokea kwa sababu hatuoni mbele, kama mfano wa Eskom ya Afrika Kusini ambao kama wangeweza kupanga vizuri basi leo mgao wa umeme kwao usingetokea, vivyo hivyo TANESCO inabidi waje na mipango thabiti ya kutupa umeme wa kutosha kwa miaka mingi ijayo.
Nashukuru kwa kusoma makala haya, ninajua kuna mengi sijagusia lakini mimi ninapendelea kuongelea jambo kwa kutoyarudia yaliyosemwa badala yake napenda kuongeza vitu vipya kwenye mjadala ili tuweze kujadiliana kwa kina.
MO