Tatizo la umeme nchini linahitaji ufumbuzi wa muda mrefu na sio muda mfupi

Kama huna cha kuchangia bora ukae kimya na sio kuja kuharibu thread hapa. Hoja hapa ni kupata uvumbuzi wa kudumu wa tatizo la umeme. Hii ni pamoja na kuongeza uzalishaji wa sasa na kutafuta vyanzo vingine vya umeme.

usilete u-CCM hapa hiyo Kilimo Kwanza ni usanii na jamaa ana point huyu Presida hana seriousness yaani hamna tangible plan kutekeleta Kilimo Kwanza declaration! sasa jiulize Kambarage mwenyewe aliyeanzisha Azimio la Arusha aligonga ukuta na u-seriousness wake je huyu Vasco Da Gama atafanya nini kama ata huo ukuta hataufikia yaani atateleza kabla! Humu ndani yeyote anachambwa kama hutaki kula kona hata Rais tunamkaribisha ajiunge tumpe vidonge vyake! eboo hatutaki utani!!
 
Mzee Mwanakijiji.

Mradi huo wa Stiegler Gorge ni bomu. Gharama yake kimazingira itazidi faida ya huo umeme. ........

Engineers (FM nadhani ni mmoja wao) huwa tunaamini kwamba always tunaweza kuja na sustainable solution which meets the present needs without compromising the environment or future generations. Kuna faida gani kuacha maji yatiririke tuu hadi baharini kisa species fulani za samaki, vyura etc. zitaangamia. Watu wa environment tunawajua sana - huwa wanapinga kila kitu - nuclear, hydro, fossil enegy. Technologies za kuzalisha substantial solar/wind energy bado sana na ni ghali.

Tusisahau vilevile kwamba kuna faida zingine kiuchumi zaidi ya umeme kwa kuwa na miradi kama hii. Itakomesha mafuriko, itaendeleza shughuli za uvuvi na hata utunzaji wa maji kwa ajiki ya kilimo cha kuwagilia, etc. Chukua mfano wa Hoover Dam/mto Colorado ilivyosaidia ustawi wa Maeneo ya Las Vegas NV & Central Valley (California). Unaambiwa hakuna hata tone na maji ya mto Colorado yanayofika Atlantic ocean. Haya tuna mifano yetu ya Mtera & Nyumba ya Mungu na faida zake kibao.
 
Mkuu, wewe ndiye uliyemuingiza Idriss humu. Hamna cha rhetoric whatever. Usitake kukwepa responsibility kama anavyotaka kufanya huyo unayemtetea.

Tatizo sio kuwa matengenezo yalikuwemo kwenye bajeti au la. Tatizo ni item kama ya maua ya plastiki iliingiaje kwenye hiyo bajeti. Tatizo ni kuwa katika wakati huu mgumu, kiongozi makini anaweza kupeleka maombi kama hayo kwa bodi yake? Kupitishwa na bodi si hoja. Bodi zetu mara nyingi zinategemea fadhila za menejimenti au unadhani vibahasha vinatoka wizarani au bungeni?

Wakati mwingine tunahitaji kubomoa kabla ya kujenga. Hapa hakuna anayemchukia Dr. Idriss kama mtu bali tuna kila haki ya kupinga kuwa anastahili kuendelea kama ilivyo kwako kumtetea kuwa anafaa.

Amandla.......

Utabomoa msingi wa nyumba ili ujenge nyumba nzuri mzee? Pia unajua akija CEO mpya ana malengo gani? na kwanini umemtoa CEO wazamani what was the performance criteria?
 
Akija CEO mpya mnaweza kurudi back to square one halafu mkaanza tena malalamiko eti shirika haliendi mbele sasa ipi bora shirika lisimame ndipo tubadilishe au tulirudishe nyuma msilete argument zisizo na kichwa wala miguu hapa.
 
Wabunge ndio hupitisha mipango ya muda mfupi na ya muda mrefu ya serikali na ni wao huitengenea fedha. Na pale ambapo hakuna sheria ya kusababisha jambo fulani kufanyika wabunge wana uwezo (kama kundi -chama, au kama mtu mmoja mmoja) kuleta mswada wa sheria wa kusababisha jambo hilo kutendeka au kutotendeka.

Suala la tatizo la nishati siyo geni kwa TAnzania na kwa eneo letu la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara. Kwa upande wetu Tanzania tatizo hili ni dalili tu ya tatizo lenyewe tulilonalo ambalo ni mipango mibovu ya wanasiasa wetu. Tanzania haina sababu hata chembe ya kuwa upungufu wa nishati ya umeme.

Leo hii kuweza kuyarejesha mabwawa yetu yote ya kuzalishia umeme kwenye full capacity inakadiriwa kutumia karibu dola bilioni 2! Lakini tukifanya hivyo zaidi tutakachopata ni kama Megawatts 1000 hivi (kama sikosei). Lakini wakati huo huo tukitamua kujenga bwawa moja kubwa la Stielger's Gorge itatugharimu karibu dola bilioni 2 vile vile lakini tunaweza kupata Megawatts zaidi 2900!

Wanasiasa wetu hawajui wachague nini! suluhisho lao ni kuingiza majenereta ya umeme na kutoa tenda zaidi ya majenereta. Wako tayari shilingi milioni nyingi kila siku na ukiwauliza hadi leo (kuanzia 1995) serikali imetumia kiasi gani katika kulipia mafuta na IPPs, jibu lake litawafanya muinamishe kichwa kwa aibu!


Sasa, Mhe. Dewji,

a. una mpango gani wa kuleta mswada Bungeni wa kusababisha ujenzi wa Stielger's gorge au kutengea fedha mradi huo mkubwa ilii hatimaye tuondokane na tatizo la umeme?

b. Una msimamo gani kuhusu kampuni ya Dowans ambayo iliingia nchini kitapeli na hadi leo tunahangaika na majenereta yao. Je, kwa maoni yako serikali itaifishe mitambo hiyo na kuwachukulia hatua wahusika wote?

c. Unafikiri Kamati yenu Teule ya Bunge ilifanya kazi yake vizuri katika suala la Richmond na hivyo kazi yake iheshimiwe na wabunge wote au unaamini ilikuwa imewaonea watu mbalimbali?

mpango wao ndio huo!

Wao ndo kina nani? Maana kwenye earlier post umesema hawajui (wanasiasa) wachague nini! Sasa itakuwaje mpango wao kama hawajui kama wauchague huo? Au by wao you mean Tanesco. Then does the issue become Tanesco vs Serikali? Who directs the other? Politicians vs Experts...labda ndo maana tuko kwenye giza mpaka leo!!
 
Fundi na Mo nashukuru kwa michango yenu/post na wachangiaji wengine walio toa Point endelevu,
Sasa Fundi mimi ningependa kuulizia Hii EIA ya Three Gorges kule China ilikuwaje Vs kujenga Nuklia Power Station maana wenzetu wana weza?
Pili Mo wewe ukiwa kama mbunge wa Singida, na kwa kuwa serikali kwa hivi sasa wamejikita zaidi katika kuwekeza kwenye Miradi midogo midogo ya MW 100 nk
je umefanya nini kushauri wadau binafsi kama wewe, au halmashauri ya Mji wa kauza Shares ilikupata mtaji wa kufungua katanesco kadogo hapo Singida, na mkiona Mtaji unao hitajika ni mkubwa, basi mnaweza omba mitaji toka nje ya Singida, na kutoka kwenye institution zingine kama world bank, na watu wa moja moja hapa Bongo na Nje?
Ili mradi shares ziwe zinauzwa pale DSE
 
Fundi na Mo nashukuru kwa michango yenu/post na wachangiaji wengine walio toa Point endelevu,
Sasa Fundi mimi ningependa kuulizia Hii EIA ya Three Gorges kule China ilikuwaje Vs kujenga Nuklia Power Station maana wenzetu wana weza?
Pili Mo wewe ukiwa kama mbunge wa Singida, na kwa kuwa serikali kwa hivi sasa wamejikita zaidi katika kuwekeza kwenye Miradi midogo midogo ya MW 100 nk
je umefanya nini kushauri wadau binafsi kama wewe, au halmashauri ya Mji wa kauza Shares ilikupata mtaji wa kufungua katanesco kadogo hapo Singida, na mkiona Mtaji unao hitajika ni mkubwa, basi mnaweza omba mitaji toka nje ya Singida, na kutoka kwenye institution zingine kama world bank, na watu wa moja moja hapa Bongo na Nje?
Ili mradi shares ziwe zinauzwa pale DSE

EIA ya Stiegler Gorge ilifanywa na Norwegians wakati wa Rubada. Wachina walionywa kuhusu mradi wao, hawakusikia. matokeo ni hizo earthquakes kila kukicha!

Amandla.......
 
Salaam JF,

Kuna msemo hapa wa Waafrika Ndivyo Walivyo. Mtoa mada ametoa takwimu moja nzuri sana. Mojawapo ni kuonyesha kuwa ukiondoa South Afrika ambayo nayo ina matatizo ya umeme, nchi zilizobaki zina matatizo makubwa ya nguvu za umeme. Na vilevile ameonyesha kuwa Poland inazalisha umeme kwa kiwango kikubwa kuliko nchi za kiafrika combined.

Hili suala sio la kisiasa. Japokuwa wanasiasa ndio waliochika ufunguo wa kutatua matatizo haya na mengine yaliokuwepo ya kijamii.

Mtamlaumu Kikwete, Idrisa, Nyani Ngabu mnavyotaka lakini ufumbuzi wa matatizo ya umeme unahitaji collective efforts. Miongoni mwa collective efforts ninazopendekeza:

1./ Vyanzo vya umeme wa maji sasa hivi havitabiliki. Hivyo ni lazima tujifunze kukabiliana na matatizo ya hali ya hewa.

2./ Ongezeko la watu nalo linasababisha upungufu wa upatikanaji wa umeme. Nchi nyingi za Ulaya zina ongezeko ambalo ni asilimia -1% au 1%. Hivyo kwa miundo mbinu ya miaka 20 iliyopita nchi za Ulaya zinaweza kupata umeme bila matatizo. Hiyo tuchague kukabiliana na ongezeko la watu au kuwa na sera zenye kwenda sambamba na ongezeko la watu.

3./Hakuna nchi inayofaidika na umeme bila kuwa na watu waliosoma sayansi na mathematics vizuri. Sasa hivi tunavuna mipango mibovu ya elimu tuka tumepata uhuru. Elimu ya darasa la saba haitoshi.

4./ Watanzania tuache biashara za uchuuzi na ulanguzi na kujiingiza kwenye biashara za innovations. Ingawaje serikali nyingi zinadhamini uzalishaji wa umeme, ni sekta binafsi iliyogundua. Nikola Tesla, Thomas Alva Edison walifanya uvumbuzi katika sekta binafsi.

5./ Vilevile ziwepo sera za maendeleo ya jamii ambazo zitazingatia miji iliyopangwa na sio kujengwa ovyovyo kama uyoga. Miji iliyopangwa inasaidia usambazaji na ukusanyaji wa mapato ambayo yataendeleza sekta ya umeme.

6./ Ushirikiano na nchi zingine katika maeneo yetu unaweza kutatua matatizo ya umeme kwa haraka. Kama kuna uwezekano wa kuanzisha shirika la nyuklia la nchi za Afrika mashariki na kati. Inakuwa bora zaidi. Na vile vile nchi ku-share mgao wa umeme. Kama Kagera inaweza kupata umeme kutoka Uganda, basi wasisubiri umeme wa Kidatu.

7. Na mapendekezo mengime ..........
 
Salaam JF,

Kuna msemo hapa wa Waafrika Ndivyo Walivyo. Mtoa mada ametoa takwimu moja nzuri sana. Mojawapo ni kuonyesha kuwa ukiondoa South Afrika ambayo nayo ina matatizo ya umeme, nchi zilizobaki zina matatizo makubwa ya nguvu za umeme. Na vilevile ameonyesha kuwa Poland inazalisha umeme kwa kiwango kikubwa kuliko nchi za kiafrika combined.

Hili suala sio la kisiasa. Japokuwa wanasiasa ndio waliochika ufunguo wa kutatua matatizo haya na mengine yaliokuwepo ya kijamii.

Mtamlaumu Kikwete, Idrisa, Nyani Ngabu mnavyotaka lakini ufumbuzi wa matatizo ya umeme unahitaji collective efforts. Miongoni mwa collective efforts ninazopendekeza:

1./ Vyanzo vya umeme wa maji sasa hivi havitabiliki. Hivyo ni lazima tujifunze kukabiliana na matatizo ya hali ya hewa.

2./ Ongezeko la watu nalo linasababisha upungufu wa upatikanaji wa umeme. Nchi nyingi za Ulaya zina ongezeko ambalo ni asilimia -1% au 1%. Hivyo kwa miundo mbinu ya miaka 20 iliyopita nchi za Ulaya zinaweza kupata umeme bila matatizo. Hiyo tuchague kukabiliana na ongezeko la watu au kuwa na sera zenye kwenda sambamba na ongezeko la watu.

3./Hakuna nchi inayofaidika na umeme bila kuwa na watu waliosoma sayansi na mathematics vizuri. Sasa hivi tunavuna mipango mibovu ya elimu tuka tumepata uhuru. Elimu ya darasa la saba haitoshi.

4./ Watanzania tuache biashara za uchuuzi na ulanguzi na kujiingiza kwenye biashara za innovations. Ingawaje serikali nyingi zinadhamini uzalishaji wa umeme, ni sekta binafsi iliyogundua. Nikola Tesla, Thomas Alva Edison walifanya uvumbuzi katika sekta binafsi.

5./ Vilevile ziwepo sera za maendeleo ya jamii ambazo zitazingatia miji iliyopangwa na sio kujengwa ovyovyo kama uyoga. Miji iliyopangwa inasaidia usambazaji na ukusanyaji wa mapato ambayo yataendeleza sekta ya umeme.

6./ Ushirikiano na nchi zingine katika maeneo yetu unaweza kutatua matatizo ya umeme kwa haraka. Kama kuna uwezekano wa kuanzisha shirika la nyuklia la nchi za Afrika mashariki na kati. Inakuwa bora zaidi. Na vile vile nchi ku-share mgao wa umeme. Kama Kagera inaweza kupata umeme kutoka Uganda, basi wasisubiri umeme wa Kidatu.

7. Na mapendekezo mengime ..........

Mawazo yako ni sawa...lakini...whats next? Utandaji vipi? Wewe binafsi unaishia hapa JF na keyboard au unafanya nini cha ziada? Tunahitaji kuwa na impact kubwa zaidi ama sivyo hatutakuwa tofauti na hao wanasiasa.
 
Mawazo yako ni sawa...lakini...whats next? Utandaji vipi? Wewe binafsi unaishia hapa JF na keyboard au unafanya nini cha ziada? Tunahitaji kuwa na impact kubwa zaidi ama sivyo hatutakuwa tofauti na hao wanasiasa.

Mjue mtu kabla ya kumlaumu. Kwa muda mrefu sijachangia hapa JF. Na cha ziada nilichofanya ni kuwa One man family.
 
Mjue mtu kabla ya kumlaumu. Kwa muda mrefu sijachangia hapa JF. Na cha ziada nilichofanya ni kuwa One man family.
Pole kama ulikumbwa na maswaiba Bin Maryam, it's been a while, welcome back. Hiyo habari ya Poland kuzalisha umeme zaidi ya Afrika combined inahuzunisha sana....

Afrika bara zima na utajiri wote huo?Binafsi naamini tunahitaji viongozi wenye mawazo mapya,viongozi wenye mawazo kama Rev Kishoka na wengi tu humu JF, tunaweza kuona kuna pengo kubwa sana,hakuna kiongozi wa kutuvusha kwenye kipindi cha mpito ambapo Afrika ni lazima inegehitaji mwelekeo mpya,viongozi wapya wenye mawazo mapya na ya tofauti yenye kuendana na wakati tuliopo, viongozi tulio nao ni wale wale wenye mawazo yale yale.

Kubwa na baya zaidi ni tatizo la kuomba omba na wakati utajiri wa rasilimali unatolewa kwa mlango wa nyuma kwa maslahi binafsi,na nishati tulizo nazo hakuna anayejisumbua kila siku ni kufikiri wapi kiguu na njia kuomba na kutalii tuu!

Hakuna kufikiri kuhusu mustakabali wa wananchi na mwelekeo wa Taifa kwa ujumla, mabadiliko ni lazima, mabadiliko yatakayopelekea mwamko kwa wananchi ambao nao hawajui kuwa kuna rasilimali za kutosha kutuondoa kwene umasikini, na wao pia wameadapt kuridhika na umasikini na kuomba omba....

Mpaka tutakapoweza kuwatumia wale viongozi wenye ability ya kuona hilo pengo na kufikiri pamoja na kutenda kinyume na reflection ya wananchi hence revolution....Ndio maana umeona mara nyingi kumekuwa na madikteta Afrika, maana hata Nyani Ngabu ana ubavu wa kusema ndivyo tulivyo, imagine mtu kama huyo awe Rais.

Naamini bado tunaweza kupata viongozi ambao si madikteta lakini wenye kuweza kuchochea mabadiliko ya kijamii na kiuchumi Afrika Tanzania ikiwemo.
 
Last edited by a moderator:
Bin Maryam uko sahihi kwa kiasi kikubwa katika maelezo hapo juu!

Kimsingi mimi (na taasisi yangu) nimeanza na miradi midogo midogo ya umeme kwa ajili ya kusambaza umeme vijijini (micro hydro electricity). Lengo ni kusaidia wakulima kuongeza kipato kwa kufanya agroprocessing pale pale walipo kwa kutumia umeme huu.

Umeme wa gridi haufiki maeneo ya vijijini kutokana na gharama kubwa za kuusafirisha, hivyo inakuwa ni hasara kwa Tanesco! Umeme huu mdogo ni rafiki wa mazingira. Hata Tanesco wana mitambo ya namna hii, kama ule wa Uwemba Njombe, Tosamaganga na Mbalizi.

Polepole tutafika.
 
Kama tunashindwa kutunza miradi tuliokuwa nayo mnafikiria vipi ujenzi wa mipya hali matatizo yetu ni Utunzaji?..Hapo ndipo sijaelewa kabisa!
 
Bin Maryam uko sahihi kwa kiasi kikubwa katika maelezo hapo juu!
Kimsingi mimi (na taasisi yangu) nimeanza na miradi midogo midogo ya umeme kwa ajili ya kusambaza umeme vijijini (micro hydro electricity). Lengo ni kusaidia wakulima kuongeza kipato kwa kufanya agroprocessing pale pale walipo kwa kutumia umeme huu.
Umeme wa gridi haufiki maeneo ya vijijini kutokana na gharama kubwa za kuusafirisha, hivyo inakuwa ni hasara kwa Tanesco! Umeme huu mdogo ni rafiki wa mazingira. Hata Tanesco wana mitambo ya namna hii, kama ule wa Uwemba Njombe, Tosamaganga na Mbalizi.
Polepole tutafika.

Haya ndiyo maneno. Hii ndiyo miradi niliyokuwa nikizungumzia siyo hiyo ya Stiegler Gorge. Miradi hiyo itawafaidia makonsaltant na wala 10%! Mwananchi wa kawaida ataishia kulipia gharama ya madeni tutakayoingia na kupandishiwa bei ya luku kila kukicha.

Ni lazima tubadilishe mwelekeo.

Amandla........
 
Haya ndiyo maneno. Hii ndiyo miradi niliyokuwa nikizungumzia siyo hiyo ya Stiegler Gorge. Miradi hiyo itawafaidia makonsaltant na wala 10%! Mwananchi wa kawaida ataishia kulipia gharama ya madeni tutakayoingia na kupandishiwa bei ya luku kila kukicha.

Ni lazima tubadilishe mwelekeo.

Amandla........
Na ndio maana na mimi nasisitizia wadau wakila sehemu. iwe wabunge, wafanya baishara, halmashauri etc etc wajikite katika kuhamasishana katika kutatua tatizo la umeme sehemu zao, kwa hii ndio itaongeza vipato na kuchochea maendeleo sehemu zao. na pia kuongeza ushindani wa kibiashara na hata kukuza soko letu la mitaji.
 
Mkuu August na hayo uliyoyaleta kuhusu 3 gorges Dam ingetufanya tufikirie mara mbili kuhusu mradi kama wa Stiegler's Gorge. Lakini mbele ya 10% ya $ bilioni mbili.........

Amandla.......
 
Engineers (FM nadhani ni mmoja wao) huwa tunaamini kwamba always tunaweza kuja na sustainable solution which meets the present needs without compromising the environment or future generations. Kuna faida gani kuacha maji yatiririke tuu hadi baharini kisa species fulani za samaki, vyura etc. zitaangamia. Watu wa environment tunawajua sana - huwa wanapinga kila kitu - nuclear, hydro, fossil enegy. Technologies za kuzalisha substantial solar/wind energy bado sana na ni ghali.

Tusisahau vilevile kwamba kuna faida zingine kiuchumi zaidi ya umeme kwa kuwa na miradi kama hii. Itakomesha mafuriko, itaendeleza shughuli za uvuvi na hata utunzaji wa maji kwa ajiki ya kilimo cha kuwagilia, etc. Chukua mfano wa Hoover Dam/mto Colorado ilivyosaidia ustawi wa Maeneo ya Las Vegas NV & Central Valley (California). Unaambiwa hakuna hata tone na maji ya mto Colorado yanayofika Atlantic ocean. Haya tuna mifano yetu ya Mtera & Nyumba ya Mungu na faida zake kibao.

Kama kwa FM unamaanisha Fundi Mchundo umekosea. Mimi sio engineer bali ni technician (Fundi Mchundo).

Majibu kuhusu hii miradi ( ongezea na Aswan Dam la Misri) utayapata kwenye bandiko la August. Big dams are a disaster in the making. Inaelekea utafurahi kusikia hakuna hata tone la maji ya Rufiji linafika Bahari ya Hindi! Are you for real?

Amandla......
 
Sawa wakuu nakubaliana na nyie but tujiulizage saa zengine hii miradi midogo midogo inawezekanika?. Position ya wananchi ikoje miradi ya umeme inataka careful planning maana ni infrastructural project ambazo Net Terminal value ni negative but inamarginal rate of development kubwa ambayo itasaidia jamii je hii miradi tunayoishauri are they feasible???

Pili tunaposhauri miradi kama hii tukae tukijuliza wale wawekezaje kutoka nje tunawavutia na kitu gani kama hatuna umeme wa kuaminika, zile banks zinazotaka kuja kuwekeza tanzania zinauhakika gani zitakuja kukutana na dilema ya umeme bongo. This means tunakitu gani cha kuwaguarantee kuwa umeme uliopo dar au mwanza ni reliable au tutapunguza matumizi ya umeme katika gridi ya taifa???

Mie kimtazamo wangu nadhani umeme vijijini ni wazo zuri but nadhani in short-term and temporary solution however nadhani pawepo either mashirika binafsi ya umeme yenye kuleta ushindani wa kibiashara nchini. hii itasaidia kwanza kupunguza gharama za umeme na pia kuleta ufanisi katika usambazaji wa umeme.

Pili tutafute njiambadala wa umeme. Sishauri Dam project kwani nadhani waliopita wameshalitolea tahadhari but nadhani ni ushauri mzuri kama nuclear ni expensive kwanini basi tusiombe mkopo World Bank?? kwavile tanzania tuna reserve kubwa za uranium tutumie hio opportunity kuzalisha umeme wa nguvu za atomic tukawa tunauza nchi nyenginezo given kuna shortage ya umeme barani afrika.

Ikiwa Nuclear energy ni expensive tuanze na coal basi mradi wa Kiwira ufufuliwe maana ni cheap na emerging markets kama india na china walianza huko huko basi nasie tufate huo mkondo ijapokuwa mkutano wa Copenhagen utakuja kutumaliza kama viongozi wetu hawakuwa makini katika makubaliano yao.
 
Bin Maryam uko sahihi kwa kiasi kikubwa katika maelezo hapo juu!
Kimsingi mimi (na taasisi yangu) nimeanza na miradi midogo midogo ya umeme kwa ajili ya kusambaza umeme vijijini (micro hydro electricity). Lengo ni kusaidia wakulima kuongeza kipato kwa kufanya agroprocessing pale pale walipo kwa kutumia umeme huu.
Umeme wa gridi haufiki maeneo ya vijijini kutokana na gharama kubwa za kuusafirisha, hivyo inakuwa ni hasara kwa Tanesco! Umeme huu mdogo ni rafiki wa mazingira. Hata Tanesco wana mitambo ya namna hii, kama ule wa Uwemba Njombe, Tosamaganga na Mbalizi.
Polepole tutafika.

Sawa kabisa. Miradi kama hii ni mizuri kwa mitambo midogomidogo na kuondoa vibatari huko vijiini. Lakini pia vilevile tunaitaji miradi ya aina ya Stiegler Gorge kuzalisha umeme wa kutosha kuendesha mitambo mikubwa kwenye viwanda vya cementi, vyuma, bia, migodini, n.k. ambayo ndiyo engine ya uchumi wa nchi.
 
Back
Top Bottom