Gamba la Nyoka
JF-Expert Member
- May 1, 2007
- 7,022
- 9,285
Hongera sana ndugu bethlehemu kwa kusimamia Ukweli, Kama alivyosema mh Zitto, Uwongo hupanda Lifti ukafika mapema, Lakini Ukweli huja kwa ngazi, na kufika baadae ukatwaa nafasi yake. Sisi kama Jamii huru iliyoazimia kujenga Taifa la kidemokrasia, ni haki yetu kuukataa uwongo kama ilivyo wajibu wetu kuukubali ukweli, Itakuwa ni makosa kuuenzi uwongo kwa sababu unatupa faraja ya Muda tu.
Ukiangalia kwa anayotuhumiwa mheshimiwa Zitto, ni tuhuma tu, hakuna Uthibitisho wowote wa tuhuma hizo. kama ni Waraka, hakuna ushahidi unaomtia hatiani kuhusika nao. Kama ni kukihujumu Chama, Mwenyewe Mh Zitto ameomba achunguzwe, na ripoti iletwe chamani ionyeshe amekihujumu vipi.
Kinachomponza Zitto ni Umahiri Wake, Charisma yake, Upeo wake. MIONGONI MWA VIONGOZI WA CHADEMA WANAOMCHUKIA, SABABU KUU NI HUSDA ZAO, WIVU WAO NA HOFU YA UENYEKITI KAMA ULIVYOSEMA.
Ukiangalia kwa anayotuhumiwa mheshimiwa Zitto, ni tuhuma tu, hakuna Uthibitisho wowote wa tuhuma hizo. kama ni Waraka, hakuna ushahidi unaomtia hatiani kuhusika nao. Kama ni kukihujumu Chama, Mwenyewe Mh Zitto ameomba achunguzwe, na ripoti iletwe chamani ionyeshe amekihujumu vipi.
Kinachomponza Zitto ni Umahiri Wake, Charisma yake, Upeo wake. MIONGONI MWA VIONGOZI WA CHADEMA WANAOMCHUKIA, SABABU KUU NI HUSDA ZAO, WIVU WAO NA HOFU YA UENYEKITI KAMA ULIVYOSEMA.