Tarehe 1/4 Siku ya Wajinga Duniani, uliwahi kudanganywa nini?

Mcheza Viduku

JF-Expert Member
Jun 24, 2020
1,049
2,535
Wandugu wapendwa wana Jf happy fulishi dei, Mama anaupiga mwingi.

Tuje kwenye mada sasa maana mi sipendagi mambo ya kusalimiana salimiana huwa inaleta ka unafiki.

Mara ya kwanza; miaka kadhaa iliyopita katika tarehe hii hii inayoitwa siku ya wajinga, nikapigiwa simu na jamaa yangu akanipa taarifa za kwamba wanahitajika mabondia kwa ajili ya kujiunga na jeshi (enzi hizo nilikuwa nafanya mazoezi ya ubondia na timu ya jeshi) natakiwa niwahi kambi ya jeshi pale nyegezi kona Mwanza kabla ya saa 4 asubuhi.

Kufupisha stori, niligandishwa pale hadi saa 6 mchana ndio nikastukia mchezo.

Mara ya pili; nilikuwa kwenye hali ngumu sana kiuchumi, saa 11 alfajiri jamaa yangu askari wa wanyamapori akanipigia simu ananiambia nisubiri hapo barabarani nakupitishia nyama ya porini njoo na mfuko mkubwa, niliganda pale hadi saa 4 asubuhi nilikuja kustuka baada ya kusikia watu wanaongelea siku hii.

Mara ya tatu; ilikuwa mwaka jana tu jamaa yangu aka-edit sms ya M pesa halafu akanitumia akaniambia nikaitoe kabla ya saa 4......unaambiwa hadi nilikorofishana na mawakala zaidi ya watatu.

Vipi kwako mwananzengo mwenzangu tangu huyu mjinga aliyebuni hii siku ushawahi kudanganywa mara ngapi na ulidanganywa kuhusu nini.
 
This is the day when my lovely 🌹 mama died. This day 2011 is still fresh in my mind.
Rest ease mama. You are always remembered till when we shall meet in the eternity.
Natamani ungekuwepo ningemalizia masomo yangu mama.
Hakika nimekukumbuka Sana maana natumia nguvu kubwa ili niishi but Asante kwa kutulea vyema. Lala salama.
 
Sijui hii Tamaduni kwamba kila mwaka 1/4 ni siku ya Wajinga, lakini nakumbukaga ili tukio.

Siku moja nimekaa zangu sielewi wala nini alafu WeekEnd nikasema ngoja niende Beach, Nikasema ngoja kwanza nimpigie simu Mtoto wa Mama Mkwe.

Me: Yo, Upo wapi Babe?
She: Nipo nyumbani.
Me: Nataka twende sehemu.
She: Hapana, naumwa Babe.
Me: Ooh unaumwa nini tena?
She: Aah sijajua bado nataka niende hospital.
Me: Ooh okay, Pole basi baadae nitakuja kukuona.
She: Sawa.

Tukaagana hivyo nikatoka zangu Ghetto nikapita maeneo nikachukua vitu vyangu nikajisogeza Beach.

Nikatafuta Place nikatulia nipo busy na mambo yangu kama 2 hrs, Nikasema ngoja nitembee kidogo nione Watu wanavyofurahi na Wapenzi zao.

Aiseeh kidogo namuona Msichana kama Mtoto wa Mama Mkwe alafu na Mwanangu wa Damu(Unayemuamini ndio anayekuua), nikasema "Hivi macho yangu nayaona kweli namfananisha"

Nikapata mshutuko kama 5 min hivi, nikajiambia tena sio wao aiseeh acha kuwa na mawenge na vitu vyako.

Basi kuhakikisha nikatafuta Pozi wasione alafu nikachukua simu nikapiga kwa Mtoto wa Mama Mkwe, Aiseeh naona kweli pale walipokaa Watu simu inatolewa, wanateta jambo alafu anapokea.

Me: Yo, Upo wapi?
She: Nipo hospital.
Me: Hospital mbona nasikia upepo sana.
She: Aaah, Unajua, Mimi, Sahivi, Ndio naenda nipo kwenye Bodaboda.
Me: Aah poa, hospital gani nije?
She: Aah usijali, Mama alisema anakuja kwahiyo tutaonana nyumbani maana nahisi ugonjwa sio Mkubwa.
Me: Sawa pole sana, Mungu akuponye Babe.

Basi hapo nina hasira kama zote, Nikawapiga picha kadhaa za kupiga Bomu langu uhakika.

Nikasema hapa nikienda Ghetto naweza kujinyonga ngoja niendelee kutembea sema nikae mbali nao, Basi nasogea mbele kidogo nakutana na Ex.

Oya kumbe mkiachana Watu wanazidi kuwa wazuri, basi tukasilimiana, akaniambia "Nipo mwenyewe tuu nilikuwa alone nimekuja kupunguza mawazo".

Nikamwambia twende sehemu nyingine tofauti na hapa (Kiporo hakitaki Moto mwingi) basi tukaondoka tukaenda Place tunapiga Story.

Akaanza kunipa Mikasa yake ya mapenzi aiseeh ni huzuni, ila nikamwambia bora wewe Mimi yamenikuta leo hii tuu.

Basi vitu vikatuzidia tukaondoka zetu Ghetto, naamka asubuhi sielewi elewi Mtoto anacheka Cheka.

Navuta simu naona missed call nyingi kumbe nilituma zile Picha wakiwa wote kwa She na Mwanangu.

Basi nikawapiga Block, alafu nikasema Ugomvi wetu huu hauishi kwa uSnitch wenu, na nikaamua ngoja nitulie tuu hata na huyu kidogo hana mambo mengi.

NB: KUWENI MAKINI NA MAPENZI.
Aisee!!
 
This is the day when my lovely mama died. This day 2011 is still fresh in my mind.
Rest ease mama. You are always remembered till when we shall meet in the eternity.
Natamani ungekuwepo ningemalizia masomo yangu mama.
Hakika nimekukumbuka Sana maana natumia nguvu kubwa ili niishi but Asante kwa kutulea vyema. Lala salama.
Pole sana mkuu kumbe kwenye upweke huu wa kupoteza mama umenizidi mwaka mmoja
 
Sijui hii Tamaduni kwamba kila mwaka 1/4 ni siku ya Wajinga, lakini nakumbukaga ili tukio.

Siku moja nimekaa zangu sielewi wala nini alafu WeekEnd nikasema ngoja niende Beach, Nikasema ngoja kwanza nimpigie simu Mtoto wa Mama Mkwe.

Me: Yo, Upo wapi Babe?
She: Nipo nyumbani.
Me: Nataka twende sehemu.
She: Hapana, naumwa Babe.
Me: Ooh unaumwa nini tena?
She: Aah sijajua bado nataka niende hospital.
Me: Ooh okay, Pole basi baadae nitakuja kukuona.
She: Sawa.

Tukaagana hivyo nikatoka zangu Ghetto nikapita maeneo nikachukua vitu vyangu nikajisogeza Beach.

Nikatafuta Place nikatulia nipo busy na mambo yangu kama 2 hrs, Nikasema ngoja nitembee kidogo nione Watu wanavyofurahi na Wapenzi zao.

Aiseeh kidogo namuona Msichana kama Mtoto wa Mama Mkwe alafu na Mwanangu wa Damu(Unayemuamini ndio anayekuua), nikasema "Hivi macho yangu nayaona kweli namfananisha"

Nikapata mshutuko kama 5 min hivi, nikajiambia tena sio wao aiseeh acha kuwa na mawenge na vitu vyako.

Basi kuhakikisha nikatafuta Pozi wasione alafu nikachukua simu nikapiga kwa Mtoto wa Mama Mkwe, Aiseeh naona kweli pale walipokaa Watu simu inatolewa, wanateta jambo alafu anapokea.

Me: Yo, Upo wapi?
She: Nipo hospital.
Me: Hospital mbona nasikia upepo sana.
She: Aaah, Unajua, Mimi, Sahivi, Ndio naenda nipo kwenye Bodaboda.
Me: Aah poa, hospital gani nije?
She: Aah usijali, Mama alisema anakuja kwahiyo tutaonana nyumbani maana nahisi ugonjwa sio Mkubwa.
Me: Sawa pole sana, Mungu akuponye Babe.

Basi hapo nina hasira kama zote, Nikawapiga picha kadhaa za kupiga Bomu langu uhakika.

Nikasema hapa nikienda Ghetto naweza kujinyonga ngoja niendelee kutembea sema nikae mbali nao, Basi nasogea mbele kidogo nakutana na Ex.

Oya kumbe mkiachana Watu wanazidi kuwa wazuri, basi tukasilimiana, akaniambia "Nipo mwenyewe tuu nilikuwa alone nimekuja kupunguza mawazo".

Nikamwambia twende sehemu nyingine tofauti na hapa (Kiporo hakitaki Moto mwingi) basi tukaondoka tukaenda Place tunapiga Story.

Akaanza kunipa Mikasa yake ya mapenzi aiseeh ni huzuni, ila nikamwambia bora wewe Mimi yamenikuta leo hii tuu.

Basi vitu vikatuzidia tukaondoka zetu Ghetto, naamka asubuhi sielewi elewi Mtoto anacheka Cheka.

Navuta simu naona missed call nyingi kumbe nilituma zile Picha wakiwa wote kwa She na Mwanangu.

Basi nikawapiga Block, alafu nikasema Ugomvi wetu huu hauishi kwa uSnitch wenu, na nikaamua ngoja nitulie tuu hata na huyu kidogo hana mambo mengi.

NB: KUWENI MAKINI NA MAPENZI.
Duh.....msemo niliokariri ni "kiporo hakipashwi kwa moto mwingi"
 
😀😃
 

Attachments

  • 1680356240480.jpg
    1680356240480.jpg
    71.1 KB · Views: 4
Back
Top Bottom