TANZIA: Dr. Ferdinand Masau wa Tanzania Heart Institue afariki dunia

Dr. Masau alikuwa hatibu bure watanzania walilipa ada mbalimbali za tiba; kosa la mfanyibiashara la kutokuwa na mipango ya kibiashara inalaumiwa vipi serikali? Mkataba upo wazi hapakuwa na kipengele kinachomzuia mwenye jengo kunadi vifaa vya mpangaji iwapo atashindwa atalipa pango; Dr. Masau alitakiwa akope benki alipe deni lake huo ndio utaratibu wa kibiashara; haya mangine yote mnayopoteza muda wenu kuandika ni uzushi na udaku tu
chama wakati mwingine tunapojadili masuala mazito ya kitaifa kama hili unatakiwa kuacha kuongea mambo ya kibwegebwege hapa.

Hospitali za serikali tunatibiwa kwa kulipia na hakuna huduma ya bure, hata zile huduma za bure zilizotangazwa kuwa zitakuwa bure kwa wazee na watoto wa umri wa chini ya miaka mitano hazipatikani bure.

Na hakuna mtu aliyesema kwamba alitakiwa atibu bure. Kinachoangaliwa hapa ni ule unafuu wa kupata tiba ama upasuaji wa magonjwa ya moyo hapa hapa nchini kwa gharama nafuu ukilinganisha na kama mtu angepelekwa India ambako wananchi wengi walikuwa hawawezi kwenda na hivyo wagonjwa wengi wa moyo wakaishia kufariki kwa sababu ya ufukara wao.

Lakini kuwepo kwa THI kulisaidia sana hata watu masikini waliweza kusafiri kutoka kona yoyote ya nchi ya Tanzania na kufika Dsm pale THI na kupata matibabu kwa gharama nafuu. Hapa JF tu wapo watu wanaoshuhudia namna ndugu zao walivyopata kutibiwa na hadi kupona pale THI na wanakiri kuwa kama sivyo basi ndugu zao wangeshaaga dunia siku nyingi.

Huo upuuzi wenu mnaofanya huko ccm na serikalini kila mtu kutaka share au 10% katika kila shughuli yoyote inayoanzishwa nchini uuache huko huko unapokuwa unajadili mambo makubwa kama haya. Kwakuwa mlizoea kujichotea mamilioni kwa kupeleka wagonjwa India ndio maana mkamuona Dr. Masau kuwa kitisho kwenu kwakuwa alikuwa amewanyima ulaji na hivyo mkaamua kumfanyia mizengwe. Watu wa ajabu sana nyie sijui ubinadamu wenu una tofauti gani na manyani.
 
Last edited by a moderator:
Mimi kinachonisikitisha jamani hivi kwanini mmoja wetu asiseme jamani kuna hili suala la mtu Mtanzania mwenztu anapata shida hii na hii how can we help kwa umoja wetu, sasa kulalama wakati mtu kafa sio vizuri nashauri kama kuna matatizo tuwe tunayatoa na kuyashughulikia...nwy RIP Dr Massau...
 
Kama ni kweli Dr Masau kafariki then its a shame for this country, SHAME ON YOU TANZANIA!
Sasa Tanzania inakosa gani hapo jamani ... kwani kufa ni option? na Kwani magonjwa yote yanatibika jamani? he was a good doctor lakini mda wake wa kutangulia umefika na kila nafsi itaonja mauti kwa imani za kikristo ndivyo maandiko yanavyosema... Doctor alikuwa jirani yangu hapa victoria na ameugua mda mrefu sana na alikuwa hawezi hta kwenda kazini hapa mwishoni, na miezi michache tu hapa na kuamia kwenye nyumba yake... sio kitu cha ghafla ameugua mda. sio kila jambo kulaumu Nchi km desturi vile.

RIP Doctor Masau... you were a good man indeed.
 
Mzalendo wa kweli kwa nchi yake aliyependa kuwatumikia wananchi wenzake hasa makini lakini akakwamishwa na mfumo wa wala rushwa serikalini! Siku moja Mwenyezi Mungu atainua jina lako ktk historia ya nchi hii. Upumzike kwa Amani Dr. Masau.
 
waziri wa afya yuko wapi kuwalinda watu kama hawa???? Kwann watanzania kama hawa wasiendelezwe na kupewa fursa ya kusaidia watanzania maskini???? Kwa kweli inauma sana
 
Watu wema wanaondoka na wema wao,lakini wema unapoondoka,ni nini huchukua nafasi yake?nawahurumia watz wanaokubali kuonewa na kuuacha wema ukiondoka taratibu lakini kwa hakika.R.I.P daktari mwema.
 
Acheni kumtetea huyu Dr kama mfanyabiashara alitakiwa awe na mipango thabiti.

Huwezi kukopa halafu utegemee msamaha! kama alitaka kusaidia watanzania na angekuwa na nia angeomba msaada kutoka kwenye NGO's halafu angetoa huduma bure au kwa bei nafuu.
 
Hakika ni pengo hasa kwa wapambanaji. Alikuwa mpambanaji kupitia taaluma yake ya udaktari wa magonjwa ya moyo kuhakikisha anachangia kubadilisha Tanzania inakuwa mahala bora. Licha ya jitihada zake kukabiliana na changamoto nyingi hakurudi nyuma. Alizidi kusonga mbele (hapa ni funzo wa watu wa sekta ya Afya kuendelea na mapambano ya kuleta mabadaliko; sambamba na sekta nyingine).

Tanzania Heart Institute itaendelea kuwa ishara angavu ya jitihada katikati ya matatizo. Ishara angavu ya jitihada katikati ya urasimu. Ishara angavu ya dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko.

Mungu amlaze mahala pema peponi!
 
Nilishuhudia alipokuwa anahamishwa kutoka kwenye ofisi zake na kusitisha huduma kwa sababu za kisiasa na mkuu wa nchi kuacha kuingilia kati kunusuru TUNU hii ya taifa na badala yake kuwaachia mbwa wake wamrarue watakavyo kwa maslahi yao wakishirikiana na wanaojiita madaktari bingwa wa MNH,kipindi fulani niliona ameanza kujenga kituo chake huko pembeni mwa mji na niliwaona wazungu wenye uchungu na watz wakikagua kwa ajili ya kuleta vifaa vya matibabu,sijui nini hatima ya kituo hicho???????
Je,siku ya mazishi yake wataongea nini,au wanastahili kupigwa mawe???????inaumaa sana kwa jambo hili la kumaliza wazalendo wa taifa hili??????????????????
 
Dr Ferdinand Masau umekufa kimwili lakini kroho uko pamoja nasi. Nina hakika siku moja Taasisi ya magonjwa ya moyo itapewa jina lako kama Tribute, hakika siku ya ukombozi halisi wa mtanzania inakuja.
 
DK Dau wa NSSF, madaktari wa taasisi ya moyo muhimbili na watendaji wa wizara ya afya ndio wameusika kwa asilimia kubwa kusababisha kifo cha dk Masau pumuzika kwa amani ya Bwana dk Masau dk dau na wezake wakija kwenye msiba wapigwe mawe.
 
Sasa Tanzania inakosa gani hapo jamani ... kwani kufa ni option? na Kwani magonjwa yote yanatibika jamani? he was a good doctor lakini mda wake wa kutangulia umefika na kila nafsi itaonja mauti kwa imani za kikristo ndivyo maandiko yanavyosema... Doctor alikuwa jirani yangu hapa victoria na ameugua mda mrefu sana na alikuwa hawezi hta kwenda kazini hapa mwishoni, na miezi michache tu hapa na kuamia kwenye nyumba yake... sio kitu cha ghafla ameugua mda. sio kila jambo kulaumu Nchi km desturi vile.

RIP Doctor Masau... you were a good man indeed.

Hivyo unataka kutueleza kwamba dau wa nssf na wale mafisadi wa Muhimbili hawausika wapigwe mawe.
 
Back
Top Bottom