MFUMO WA SIASA---Tanzania ni sehemu ndogo sana ila ina serikali kubwa sana,ni fedha nyingi sana zinatumika kuwalipa Mawaziri,naibu mawaziri na makatibu.kwa mtazamo wangu tunatakiwa tuwe na wizara zisizozidi tano .wizara ya ulinzi,wizara ya mambo ya nnje,wizara ya mambo ya ndani,wizara ya maendeleo na wizara ya elimu,hizi wizara pamoja na statehouse ndio iwe serikali kuu,na mawazili wao wawe wanachaguliwa na Raisi na wawe wanapitiswa na bunge,baada ya kufanyiwa na kuchunguzwa kama wana uwezo wa kuongoza na bunge,kwa kufanya hivi tutapunguza galama nyingi sana,pili kuwe na wakuu wa mikoa ambao wanachaguliwa na wananchi.hawa wawe wanasimamia ukusanyaji wa kodi katika mikoa yao,na mipango ya maendeleo ya mikoa yao,madiwani wakuu wa wilaya wawe wanafanya kazi na mkuu wa mkoa kupanga kila kitu cha mkoa husika.pili kila mkoa uwe na wabunge wawili tu .