Tanzania Socio-Economic news: Ziwa jipe la huko Kilimanjaro na uwepo wa madini ya uranium

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797


Saturday, July 20, 2013


http://www.letsgokenya.com/upload/images/lake-jipe-2.png
203258416.jpg



IMEELEZWA kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa madini ya uraniamu katika ziwa Jipe lililopo wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.



Kutokana na kuwepo kwa dalili za kuwepo kwa madini hayo katika ziwa hilo kwa sasa wataalamu wa kuchunguza madini wapo katika mchakato wa kufanya uchunguzi ili kubaini kiasi cha madini kilichopo katika ziwa hilo.


Hayo yamebainishwa na Meneja wa mipango na utafiti wa madini wa ofisi ya wakala wa ukaguzi wa madini nchini Julius Mushi, wakati wa mafunzo maalumu kwa vyombo vya usalama na wadau wa madini juu ya kudhibiti magendo ya utoroshaji wa madini kwenda nje, yaliyo fanyika wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.




 
Oh WOW... Sasa na HUKO KASKAZINI wana URANIUM??? This Country is Blessed; Lakini Wajinga Wachache wanaanza kutamani hizo Mali bila kujua jinsi ya kuendeleza Wananchi...
 
Utajiri wa Tanzania ni zaidi ya tunavyoufahamu!! Duh!! Tanzania kila mahali ni madini tu!!!
 
Kwa kweli nchi hii inahitaji mtu mwelewa, mwerevu na anaye jali utu wa wananchi wake
sio wale wanaosema pigeni tuu nasema wapigeni tuu sisi tumechoka na hakuna njia nyingine
 
IMEELEZWA kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa madini ya uraniamu katika ziwa Jipe lililopo wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.Kutokana na kuwepo kwa dalili za kuwepo kwa madini hayo katika ziwa hilo kwa sasa wataalamu wa kuchunguza madini wapo katika mchakato wa kufanya uchunguzi ili kubaini kiasi cha madini kilichopo katika ziwa hilo. Hayo yamebainishwa na Meneja wa mipango na utafiti wa madini wa ofisi ya wakala wa ukaguzi wa madini nchini Julius Mushi, wakati wa mafunzo maalumu kwa vyombo vya usalama na wadau wa madini juu ya kudhibiti magendo ya utoroshaji wa madini kwenda nje, yaliyo fanyika wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro. Hapo mafisadi wakaweke kambi kabisa kwa wananchi wa kipato cha chini hawatafaidika nayo kabisa mpaka pale mkombozi wa hii nchi atakapokuja
 
Hata misitu ya kilimanjaro kuna madini ya dhahabu sema tu hawajaanza utafiti kila sehemu ni mimali tu...lakini kwa serikali hii ni sawa na bure tu! Tutaambulia 1/4!
 
Aiseee Mushi! Sasa na hayo madini mtampa Obama au? Muda si mrefu Clinton atarudi Bongo ili kukamilisha makubaliano. Ardhi ya Kilimanjaro ni ndogo, hata wengine tukaamua kukimbia, kwa mbali naona watu wakihamishwa bila ya utu ili kupisha "Wawekezaji", Wawekezaji wataowanyanyasa, kama zama za ukoloni, kwa zaidi ya miaka 99.
Nchi kila mahali ni dili, muda si mrefu unaweza kusikia ya kwamba Ikulu inabidi kuhama ili kupisha wawekezaji wa madini.
 
Bado mwendawazimu mwingine anasema hajui kwa nini nchi yake ni maskini!!!

Kiongozi!

Kile kichwa kina piga chini kutwa 2X3 si ni lazima kikose uwezo wa kufahamu yanayo jiri nchini mwake!!!???? wewe si unaona siku hizi nyuma yake kuna jamaa watatu wametega kumdaka kwani mieleka ni kama dose vile.
 
IMEELEZWA kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa madini ya uraniamu katika ziwa Jipe lililopo wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.Kutokana na kuwepo kwa dalili za kuwepo kwa madini hayo katika ziwa hilo kwa sasa wataalamu wa kuchunguza madini wapo katika mchakato wa kufanya uchunguzi ili kubaini kiasi cha madini kilichopo katika ziwa hilo. Hayo yamebainishwa na Meneja wa mipango na utafiti wa madini wa ofisi ya wakala wa ukaguzi wa madini nchini Julius Mushi, wakati wa mafunzo maalumu kwa vyombo vya usalama na wadau wa madini juu ya kudhibiti magendo ya utoroshaji wa madini kwenda nje, yaliyo fanyika wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro. Hapo mafisadi wakaweke kambi kabisa kwa wananchi wa kipato cha chini hawatafaidika nayo kabisa mpaka pale mkombozi wa hii nchi atakapokuja

Hali ni mbaya, tufanyeje?
 
Ni vizuri kugundulika kwa hayo madini,lakini tujiulize wananchi wa hali ya chini wanafaidikaje na madini hayo?
 
Back
Top Bottom