Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya ligi kuu Tanzania (TPL), kuendelea tena leo Jumamosi, Novemba 3, 2018 kwa michezo kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti nchini ambapo mechi kali na ya kusisimua itakayovuta hisia za wadau wa soka ni uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga, kwa wenyeji JKT Tanzania walio na nafasi ya sita kwenye msimamo (TPL) kupapatuana vilivyo na mabingwa wa nchi Simba SC.
Je..JKT Tanzania wataweza kuzuia makali ya Simba Sports Club? Usikose Ukaambiwa. Kumbuka mechi ni saa 10:00 jioni na itakuwa mubashara Azam Sports 2.
Kikosi kinachoanza leo kwa upande wa Simba SC;
Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohamed Hussein, Erasto Nyoni, Pascal Wawa, Jonas Mkude, James Kotei, Hassan Dilunga, John Bocco Meddie Kagere, Emmanuel Okwi.
Subs;
Deogratias Munish, Juuko Murshid, Said Ndemla, Cleoutus Chama, Shiza Kichuya, Mzamiru Yassin, Adam Salamba
Naaaaaaaam mpira umeanza uwanja wa Mkwakwani
JKT Tanzania 0-0 Simba SC
01' Hasan Dilunga anapiga shuti kali lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick.
07' JKT wanakwenda sasa...Hassan Matelema anapiga shuti kali na Aishi anapangua na kukuta Kotei na kuokoa hatari ile
Ilikuwa hatari mno
11' Gooooooooooaaal Gooooooaaal..Mfumba Jicho MK 14 Meddie Kagere anawatangulia Simba bao la kwanza
JKT Tanzania 0-1 Simba SC
15' mashambulizi makali kwa pande zote..JKT wakitaka kukomboa kadhalika Simba wakitaka kuongeza
22' mchezaji Aziz Gilla anapiga shuti kali lakini mpira unagonga mwamba katika lango la Simba SC.
30' Kelvin anaonyeshwa kadi ya njano kwa mchezo mbaya kumchezea Tshabalala
JKT Tanzania 0-2 Simba SC
37' Gooooooooooaaal goooooaal MK 14 Mfumba Jicho Meddie Kagere anaandika bao la pili baada ya kumalizia shuti la Okwi lililogonga mwamba
JKT Tanzania 0-2 Simba SC
45+2' Kuelekea kuwa mapumziko uwanja wa Mkwakwani
Naaaaaaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wako mbele ya mabao mawili bila majibu dhidi ya JKT Tanzania
45' Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga JKT Tanzania Vs Simba SC
48' Goo laaaaaaa MK14 anakosa bao la wazi, ilitokea piga nikupige lango la JKT Tanzania na mpira kuokolewa na mabeki
57' Ali Shiboli anaingia upande wa JKT Tanzania na Mussa anakwenda kwenye benchi
60' Aishi Manula anapata matibabu baada ya kuchezewa vibaya
69' Meddie Kagere anaonyeshwa kadi ya njano
JKT Tanzania 0-2 Simba SC
69' Mabadilko upande wa Simba, anakwenda kwenye benchi Dilunga na anaingia Kichuya
72' JKT Tanzania wanafanya mabadilko, anatoka Kilemile anaingia Bilali
Mpira unachezwa kwa kutegeana hasa kipindi hiki cha lala salama, rafu za hapa na pale
82' Meddie Kagere anakwenda kwenye benchi anaingia Mzamiru upande wa Simba
Wanakwenda JKT, lakini mpira unaokolewa na mabeki wa Simba
89' Ali Shiboli aliyeingia kipindi cha pili anaonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumpiga mwamuzi wa kati
90+3 Wakati wowote mpira unamalizika
Naaaaaaaam mpira umekwisha hapa uwanja wa Mkwakwani ambapo Simba wameibuka na ushindi wa mabao mawili bila majibu bila majibu
Mabao ya MK 14, Meddie Kagere Mfumba Jicho kunako dakika ya 11' 37 za mchezo huu wa TPL
Timu mzima ya JF imekuletea mtanange huu
Asanteni sana....Ghazwat
Je..JKT Tanzania wataweza kuzuia makali ya Simba Sports Club? Usikose Ukaambiwa. Kumbuka mechi ni saa 10:00 jioni na itakuwa mubashara Azam Sports 2.
Kikosi kinachoanza leo kwa upande wa Simba SC;
Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohamed Hussein, Erasto Nyoni, Pascal Wawa, Jonas Mkude, James Kotei, Hassan Dilunga, John Bocco Meddie Kagere, Emmanuel Okwi.
Subs;
Deogratias Munish, Juuko Murshid, Said Ndemla, Cleoutus Chama, Shiza Kichuya, Mzamiru Yassin, Adam Salamba
Naaaaaaaam mpira umeanza uwanja wa Mkwakwani
JKT Tanzania 0-0 Simba SC
01' Hasan Dilunga anapiga shuti kali lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick.
07' JKT wanakwenda sasa...Hassan Matelema anapiga shuti kali na Aishi anapangua na kukuta Kotei na kuokoa hatari ile
Ilikuwa hatari mno
11' Gooooooooooaaal Gooooooaaal..Mfumba Jicho MK 14 Meddie Kagere anawatangulia Simba bao la kwanza
JKT Tanzania 0-1 Simba SC
15' mashambulizi makali kwa pande zote..JKT wakitaka kukomboa kadhalika Simba wakitaka kuongeza
22' mchezaji Aziz Gilla anapiga shuti kali lakini mpira unagonga mwamba katika lango la Simba SC.
30' Kelvin anaonyeshwa kadi ya njano kwa mchezo mbaya kumchezea Tshabalala
JKT Tanzania 0-2 Simba SC
37' Gooooooooooaaal goooooaal MK 14 Mfumba Jicho Meddie Kagere anaandika bao la pili baada ya kumalizia shuti la Okwi lililogonga mwamba
JKT Tanzania 0-2 Simba SC
45+2' Kuelekea kuwa mapumziko uwanja wa Mkwakwani
Naaaaaaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wako mbele ya mabao mawili bila majibu dhidi ya JKT Tanzania
45' Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga JKT Tanzania Vs Simba SC
48' Goo laaaaaaa MK14 anakosa bao la wazi, ilitokea piga nikupige lango la JKT Tanzania na mpira kuokolewa na mabeki
57' Ali Shiboli anaingia upande wa JKT Tanzania na Mussa anakwenda kwenye benchi
60' Aishi Manula anapata matibabu baada ya kuchezewa vibaya
69' Meddie Kagere anaonyeshwa kadi ya njano
JKT Tanzania 0-2 Simba SC
69' Mabadilko upande wa Simba, anakwenda kwenye benchi Dilunga na anaingia Kichuya
72' JKT Tanzania wanafanya mabadilko, anatoka Kilemile anaingia Bilali
Mpira unachezwa kwa kutegeana hasa kipindi hiki cha lala salama, rafu za hapa na pale
82' Meddie Kagere anakwenda kwenye benchi anaingia Mzamiru upande wa Simba
Wanakwenda JKT, lakini mpira unaokolewa na mabeki wa Simba
89' Ali Shiboli aliyeingia kipindi cha pili anaonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumpiga mwamuzi wa kati
90+3 Wakati wowote mpira unamalizika
Naaaaaaaam mpira umekwisha hapa uwanja wa Mkwakwani ambapo Simba wameibuka na ushindi wa mabao mawili bila majibu bila majibu
Mabao ya MK 14, Meddie Kagere Mfumba Jicho kunako dakika ya 11' 37 za mchezo huu wa TPL
Timu mzima ya JF imekuletea mtanange huu
Asanteni sana....Ghazwat