Abunwasi
JF-Expert Member
- Jun 25, 2009
- 5,486
- 3,468
IGP Upoo???? ningekuwa mimi hali kama hii ikitokea ningekuwa nashika shingo ya RPC na hao mabosi wa mikoa kama wanataka kuendelea na nyadhifa zao ingebidi wawe wakali sana kwa wala rushwa, wazembe nk. Tatizo kwa sasa ninasikia {sina uhakika] ni kuwa kuna syndicate ambapo migao ya rushwa inapanda juu hadi kufikia kwa mabosi mikoani na kama unataka upelekwe sehemu nzuri [hasa kwa traffic] inabidi uwe na uso wa chuma ili uendelee .Ajali basi la SABENA huko Tabora laua 17, yajeruhi 78. Hivi Tz kuna basi linaweza chukua watu 95? askari kwa nini wasiwajibike? Source ITV
Mkitaka kuthibitisha kidogo tuu kuhusu haya jaribu kuangalia mali wanazomiliki huwezi kuamini kuwa wamepata kupitia vijishahara wanavyolalamikia. Kwa dar ndiyo usiseme jaribu kuangali hizi dala dala na teksi huwezi amini/