Ajali basi la SABENA huko Tabora laua 17, yajeruhi 78. Hivi Tz kuna basi linaweza chukua watu 95? askari kwa nini wasiwajibike? Source ITV
Ajali basi la SABENA huko Tabora laua 17, yajeruhi 78. Hivi Tz kuna basi linaweza chukua watu 95? askari kwa nini wasiwajibike? Source ITV
Du me najua basi nyingi max kama abiria 65 sasa hao 30 waliozidi walikaa vp humo ndani? Mkuu wa usalama barabara ni wa tbr ajiuzulu tu kwa manufaa ya umma!
zitungwe sheria ukikutwa umesimama ni viboko na kifungo hata ya siku moja na ukikutwa hujafunga mkanda viboko..
Mkuu trust me basi kama la sabena halina mikanda na ni mabasi mengi tu hayana mikanda na kama ipo basi ni viti vichache sana sasa unategemea mtu ufanye nn na kuna mabasi yanaongoza kwa kuua kwa kuzidisha abiria na kukimbia sana lakini hayafungiwi leseni na ajali zinazidi kila siku trafik nao ndo hivo tena watakula wapi??yani sjui ni nn kifanyike maana kila siku tunaangamia kwenye hizi ajali.halafu wa tanzania huwa hatutaki kujifunga mikanda mpaka ukimuona polisi sasa mimi huwa najiuliza hivi mikanda inamsaidia traffic au wewe abiria kama tunataka kupunguza vifo vinavyotokana na ajari, zitungwe sheria ukikutwa umesimama ni viboko na kifungo hata ya siku moja na ukikutwa hujafunga mkanda viboko..
Mkuu nakubaliana kabisa na wewe lakini bado mimi nitawalaumu watanzania kwasabau vitu ninavyo viongea siyo wa kuambiwa ni vyakujionea kutokana na shughuli zangu huwa na safari mara kwa mara.. kuna wakati mna fika kwenye mizani mnaambiwa mshuke mtangulie kwa miguu au mnakodishiwa hiace iwatangulize...mimi niseme kwasasa usafiri wa mikoani mabasi ni mengi sana kama basi hilo lina matatizo kwanini ulipande? ni kweli Tabora mbeya ni basi hilo tu? bado kwenye mabasi ambayo kuna mikanda abiria huwa hawajifungi ukumbuke safari hizo ni ndefu huku mmejazwa kama mizigo na kunapotokea na tatizo kuna sehemu ukifika unaulizwa na traffic kama kuna tatizo unasema hakuna tatizo wakati basi linakimbizwa speed mpaka 120...Mkuu trust me basi kama la sabena halina mikanda na ni mabasi mengi tu hayana mikanda na kama ipo basi ni viti vichache sana sasa unategemea mtu ufanye nn na kuna mabasi yanaongoza kwa kuua kwa kuzidisha abiria na kukimbia sana lakini hayafungiwi leseni na ajali zinazidi kila siku trafik nao ndo hivo tena watakula wapi??yani sjui ni nn kifanyike maana kila siku tunaangamia kwenye hizi ajali.
baadhi ya matrafic huwa wanapeleka % kwa wakubwa wao hivyo linapotokea tatizo kama hilo huwatetea...hivyo ni sisi abiri kuchukua hatua tunapoona tatizo mfano kuna mabasi seat moja hukatiwa watu zaidi ya mmoja mkishaingia kwenye gari mnaanza kugombana abiri kwa abiria badala udai nauli urudishiwe au kushitaki kwa wahusika maana napo kuhahirisha safari ni gharama saa zingine......Ingekuwa ikitokea ajali ya nmna hii, kabla ya kitu chochote Mkulu anamtimua mkuu wa trafiki wa mkoa na mule mwote basi lilimopita. labda watu wangeogopa na kuanza kuheshimu kazi zao. Si mnakumbuka lile basi la kutoka Tanga, sijui ni Zafanana vile, lilipita pale Muheza likiwa limejaza abiria hadi pomoni lakini baada ya 'mazungumzo' trafiki wakaliacha liendelee na safari na hatua mia tu mbele lote likasombwa na maji na ikawa kilio! Kama matrafiki waliohusika hawakutimuliwa pale, watatimuliwa wapi tena???