Tanzania na tishio la migomo

Mhh Ndoto hii huenda ikatimia; mwenzio yuko Libya kwa shughuli ya kikazi- eti walimu; eti wanafunzi kugoma; eti EAC kuandaa kombora; eti TRL; eti richmond; eti EPA ya nini; eti Buzwagi; eti raslimali na migodi kutonufaisha waTZ; eti OIC; eti kadhi; yote upepo mwenzio yuko Libya!!!! anakula kuku; sasa je nini zaidi ya hapo kusema huyu si mwenzetu
 
Mhh Ndoto hii huenda ikatimia; mwenzio yuko Libya kwa shughuli ya kikazi- eti walimu; eti wanafunzi kugoma; eti EAC kuandaa kombora; eti TRL; eti richmond; eti EPA ya nini; eti Buzwagi; eti raslimali na migodi kutonufaisha waTZ; eti OIC; eti kadhi; yote upepo mwenzio yuko Libya!!!! anakula kuku; sasa je nini zaidi ya hapo kusema huyu si mwenzetu

Bwana Malunde kumbe ulikuwa bado hujajua kama JK si mwenzetu tuu??? nitajie waziri wake mmoja ambae mtoto wake anasoma mwembeni primarly school, nitajie ndugu wa karibu wa anaetiba hospitali ya amana...nitajie nduguyake wa karibu kama ni mwalimu??? kama wanapanda daladala... kamawanasoma vyuo wa tanzania....
 
Kufuatia taarifa kwamba DIT wamegoma (Tz daima), wakidai wale wanafunzi waliofukuzwa warudishe, ni kitendo cha kishujaa kufanywa na wanafunzi. Natamani mlipuko huu wa mgomo uambukize vyuo vingine, halafu sekondari na walimu wao, tutamalizia na wanafunzi wa shule ya msingi. Mgomo utaendelea kwa wafanyakazi wa mashirika fulani wakiunga mkono waalimu,TRL, NMB... Hatimaye mgomo uwe nchi nzima, ikiwezekana mpaka wafanyakazi wa ikulu wenyewe. Usalama wa taifa na polisi nao watagoma, hakuna FFU wa kuzuia migomo na maandamano. Manesi na madaktari wataendelea na kazi yao kama kawaida huku wakiunga mkono hatua itakayofanywa na wenzao katika idara na taasisi zote.

Tutaona watu wakielekea ikulu, tutaona rais aliye waangusha watanzania kwa kujiangusha mwenyewe akitoka ikulu. Tutashuhudia nchi inapita kipindi cha mpito. Tutaona mabadiliko ya amani , hakutakuwa na vifo wala watu kuzimia, ambayo yatakuwa simulizi na fundisho kwa vizazi vijavyo.

Kutakuwa na mjadala wa taifa kuhusu mabadiliko ya katiba, yatakayotoa fursa kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa kuwa kila chama kitapata nafasi serikalini kulingana na kura walizopata.

Tutaona Tanzania mpya, ambayo siku zote ni nzuri inayoharibiwa na watu wachache kwa uroho wao, kisa kwa sababu ya upole na uungwana wa watanzania. Tutaona nchi iliyobarikiwa kwa mali asili ikifaidi matunda ya uumbaji wake, kwa kila raia kufaidikia na matunda yake.Tutajua vizazi vijavyo jinsi vitakavyokuja kuisifu tanzania ya sasa kwa maamuzi haya mazito. Huku wenyewe tukifanya kazi kwa bidii kila siku pasi kuwa na chembe ya ufisadi.

Nguvu kidogo tu inahitajika sasa, kama hali ni hii migomo nchini kila mahali wataalamu mko wapi, JF je?

wakatabahu!

Naona kama inaelekea vile maana migomo imezidi.
 
Hivi yule 1st lady wetu si alikuwa teacher?
Au tuseme kwa vile anakula mikuku na misosi heavy amesahau matatizo ya walimu?
Kweli waTZ wasahaulifu sana huyu mama naye amekulia maisha magumu leo hii anashindwa hata kuwasaidia wenzie?Anashindwa kumbania pua mzee awasaidie walimu wenzie?
 
Wasomi wetu wote wangelitambua hili na kukiri publicly implications za Migomo kama Mkandi alivyo fanya, ingesaidia sana kudeliver message hii kwa mheshimiwa na pia kuwapa warning CCM, waliojaza uozo wakila aina kwenye serikali yao.

Watz si mbumbu tena japo kuwa (serikali) wanajitahidi kuwafanya wawe hivyo kwa kuwanyima elimu wototo wetu na vijana wetu, kwa sera za kibabe kama ilivyo sera ya uchangiaji ya Higher Learning Institutions!
 
Nafikiri kwa mara nyingine wasomi wataanza kurudisha heshima yao waliyoipoteza siku nyingi. Nafikiri kipindi cha utawala wa awamu ya pili au karibu na hapo ndipo wasomi walianza kupuuzwa sana

nakumbuka kipindi cha utawala wa baba wa taifa mabo yote ya kimsingi yaliyokuwa na impact kubwa kwa maisha ya watanzania na mabo ya kisera alikuwa either anaenda kuyatangazia UDSM au kuwahusisha kiasi kikubwa wasomi kwenye majadiliano kabla ya kupeleka kwa wananchi. Na UDSM ilikuwa source kubwa ya viongozi na wanamapiduzi barani Africa.

Siku hizi hata wanafunzi wanaoweza kuanalyse mambo pale Mlimani hawapo (corect me, ni mtazamo wangu)!! Kumbuka siku Mtikila anawahutubia wanachuo pale Nkhuruma hall discussion zilizokuwepo. Wanafunzi walikuwa moto na wanajua outer world hata waliweza kujadili mambo ukaona tofauti na mtu asiye na elimu ya chuo.

Naamini hili vuguvugu huenda litakuwa chachu ya kurudisha status ya elimu yetu. Baada ya kueleweka kuhusu mikopo then tuendelee na mjadala wa kitaifa kuweza kurekebisha mitaala yetu iweze kuzalisha responsible people wenye maadili pia, ikiwa ni pamoja na kuweka direction mpya ya nini tunaamini na kutaka elimu yetu itupe. Hatimaye tuwe na Taifa linaloheshimika tena sio kwa kuwa liliasisiwa na JKN (RIP) bali lenye norms zinazotutamblisha popote tuendako

Nawakilisha
 
Kufuatia taarifa kwamba DIT wamegoma (Tz daima), wakidai wale wanafunzi waliofukuzwa warudishe, ni kitendo cha kishujaa kufanywa na wanafunzi. Natamani mlipuko huu wa mgomo uambukize vyuo vingine, halafu sekondari na walimu wao, tutamalizia na wanafunzi wa shule ya msingi. Mgomo utaendelea kwa wafanyakazi wa mashirika fulani wakiunga mkono waalimu,TRL, NMB... Hatimaye mgomo uwe nchi nzima, ikiwezekana mpaka wafanyakazi wa ikulu wenyewe. Usalama wa taifa na polisi nao watagoma, hakuna FFU wa kuzuia migomo na maandamano. Manesi na madaktari wataendelea na kazi yao kama kawaida huku wakiunga mkono hatua itakayofanywa na wenzao katika idara na taasisi zote.

Tutaona watu wakielekea ikulu, tutaona rais aliye waangusha watanzania kwa kujiangusha mwenyewe akitoka ikulu. Tutashuhudia nchi inapita kipindi cha mpito. Tutaona mabadiliko ya amani , hakutakuwa na vifo wala watu kuzimia, ambayo yatakuwa simulizi na fundisho kwa vizazi vijavyo.

Kutakuwa na mjadala wa taifa kuhusu mabadiliko ya katiba, yatakayotoa fursa kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa kuwa kila chama kitapata nafasi serikalini kulingana na kura walizopata.

Tutaona Tanzania mpya, ambayo siku zote ni nzuri inayoharibiwa na watu wachache kwa uroho wao, kisa kwa sababu ya upole na uungwana wa watanzania. Tutaona nchi iliyobarikiwa kwa mali asili ikifaidi matunda ya uumbaji wake, kwa kila raia kufaidikia na matunda yake.Tutajua vizazi vijavyo jinsi vitakavyokuja kuisifu tanzania ya sasa kwa maamuzi haya mazito. Huku wenyewe tukifanya kazi kwa bidii kila siku pasi kuwa na chembe ya ufisadi.

Nguvu kidogo tu inahitajika sasa, kama hali ni hii migomo nchini kila mahali wataalamu mko wapi, JF je?

wakatabahu!

Slaa, Zito, Mbowe, Mrema, Mnyika,n.k mko wapi?
Hii ni nafasi adimu kupatikana, Tanzania sasa kuna popular democracy asimame mtu aimbe aina ya wimbo wa ''yes we can'' kama Kikwete alivyoimba nguvu mpya.....kasi mpya....., .SERIKALI IKO MIKONONI MWETU SASA.

Nguvu kidogo inahitajika, kama silaha ya moto kila kitu kimewekwa inahitaji mtu tu ku -trigger!

Njua kuna operation sangara, bado hubirini hali ya sasa tangazeni maandamano, msiogope kukamatwa jamani nyie tegemeo letu
 
Hivi yule 1st lady wetu si alikuwa teacher?
Au tuseme kwa vile anakula mikuku na misosi heavy amesahau matatizo ya walimu?
Kweli waTZ wasahaulifu sana huyu mama naye amekulia maisha magumu leo hii anashindwa hata kuwasaidia wenzie?Anashindwa kumbania pua mzee awasaidie walimu wenzie?

Ni kweli First Lady alikuwa teacher lakini naamini mikuku alianza kuila muda mrefu kabla hajaingia kwenye lile jumba jeupe. JK alianza ufisadi kimya kimya muda mrefu, angalia mikataba aliyosaini alipokuwa na dhamana hiyo Wizara ya madini na kwingineko.

Hivyo naamini misosi mikali mikali ilikuwa haikosi nyumbani kwake. Adha wanazopata walimu siamini kama ilikuwa inamgusa direct First Lady. Kama mshahara ulikuwa unachelewa Baba alikuwa ana-cover na kuhakikisha watoto wanasoma bila upungufu wa fedha.

Labda mtu kama Mama Sitta anaweza kuwa na experience kidogo maana aliwahi kukikalia kiti anachokalia sasa Bw. Mukoba. Cha ajabu ukishalishwa peremende za serikalini basi unasahau shubiri za uraiani
.
 
Sasa moto wa mgomo huu inabidi usambae kwa kuuwaunga mkono waalimu,wanafunzi,wazazi nao waingie kudai haki ya watoto wao kufundishwa,najua miongoni mwao wapo polisi,wansheria nao wagome ili kuunga mkono harakati za kudai haki nk. Viongozi wa upinzani tumieni uwezo wenu kuhamasisha haya,tunahitaji mabadiliko mapema sana iwezekanayo.Mapinduzi Daima.


Serikali inayotumia mabavu kuzima sauti za wanaodai haki ni ya kulaaniwa kwa nguvu zote. Watanzania huwa tunakua na mshikamano katika shida na raha,huu ndio muda unaohitaji mshikamano zaidi kulinusuru taifa letu na kizazi kijacho. Vuguvugu la ukombozi,na ndoto za mababu zetu kukataa kwa nguvu kutawaliwa na kukandamizwa,vuguvugu la kudai uhuru wa Tanganyika na jinsi babu zetu walivyopigania uhuru hawakumaanisha kwamba sisi leo hii tuwe katika hali hii.

Kwa hali iliyopo sasa inamaanisha kwamba babu zetu walipigania kubadilisha rangi ya ngozi za watawala tu,i mean kutoka mkoloni mweupe kwenda mkoloni mweusi.Hapana,sidhani kama hivi ndivyo alivyopigania Mwl. JK Nyerere (RIP) na mashujaa wetu wengine.Tushikamane,tuhamasishane tufue ndoto za ukombozi ambazo ni ndioto za mashujaa wetu
 
Be careful what you wish for, you may receive it.

Kikwete akitoka kuna mkakati gani wa kuhakikisha tunapiga hatua madhubuti mbele?

Kwa hali yoyote Kikwete ana kikomo cha mihula mwaka 2015, baada ya hapo kuna mkakati gani? Tutaenda na sera au ndio tutabaki na siasa za kufuata watu? Tunahakikishaje hatutompata Kikwete mwingine?
 
Be careful what you wish for, you may receive it.

Kikwete akitoka kuna mkakati gani wa kuhakikisha tunapiga hatua madhubuti mbele?

Kwa hali yoyote Kikwete ana kikomo cha mihula mwaka 2015, baada ya hapo kuna mkakati gani? Tutaenda na sera au ndio tutabaki na siasa za kufuata watu? Tunahakikishaje hatutompata Kikwete mwingine?

Thats right! Kikwete anaweza kuondoka easily tu lakini je nani ameandaliwa kuchukua nafasi yake? Kwa sasa waroho wote wapo gado wakitia ubani jamaa aondoke na majority ya hao hawafai bora ya JK. Kwenye msukosuko huu tusipokuwa waangalifu tutaishia kumtoa lesser devil na kuingiza bigger one
 
Naamini miongoni mwa walimu hawa kuna wanachama wa vyama mbalimbali, lakini bado hatujasikia lolote kutoka Kwa Mrema, Mbatia n.k Jamani hizi ni haki kwa wafanyakazi wote nchini wanaodai haki yao. Najua kuwa ni walimu pekee ambao wameonyesha kutunishiana misuli dhidi ya serikali. Viongozi mbalimbali nchini mnatakiwa kusimama kidete kusaidia hawa watu wapate haki zao.
Hili si suala la kiitikadi bali suala la haki kwa kila mwenye madai. SISIEMU ilishatoa tamko kwa serikali yake kupitia kwa Chiligati kuwa ianze kuwashughulikia viongozi wa CWT, na tumeshaanza kuona baadhi yao wakianza kushughulikiwa huko Dodoma. Kwa maana hiyo SISIEMU ilishaonyesha ni upande upi imeegemea. Tuhamasishe huu mgomo nchi nzima, vyuo vikuu vimefungwa, walimu wamegoma, wanafunzi msingi 7 wameandamana kwa wingi kudai haki yao ya kufundishwa. Kuna kila njia ya kuibana serikali kuwalipa walimu na hata kuwalipia wanafunzi vyuo vikuu ada zao kama tutakuwa na mshikamano.

Pamoja na mateso hayo tusisahau yatakapokuja masanduku ya kura. This time SISIEMU has to go. Si kweli kwamba pesa haipo, bali MAFISADI wameachiwa kuendesha biashara zao watakavyo. Pesa zetu wamekalia bado. Wanakula vinono huku walimu wanapata shida huku wanafunzi wakitaabika bila kupata elimu bora.
Umefika wakati wa mageuzi sasa. Muda wa kuchekeana na kukenuliana meno umekwisha.
 
Be careful what you wish for, you may receive it.

Kikwete akitoka kuna mkakati gani wa kuhakikisha tunapiga hatua madhubuti mbele?

Kwa hali yoyote Kikwete ana kikomo cha mihula mwaka 2015, baada ya hapo kuna mkakati gani? Tutaenda na sera au ndio tutabaki na siasa za kufuata watu? Tunahakikishaje hatutompata Kikwete mwingine?

Thats right! Kikwete anaweza kuondoka easily tu lakini je nani ameandaliwa kuchukua nafasi yake? Kwa sasa waroho wote wapo gado wakitia ubani jamaa aondoke na majority ya hao hawafai bora ya JK. Kwenye msukosuko huu tusipokuwa waangalifu tutaishia kumtoa lesser devil na kuingiza bigger one

Hi there, I understand your concern, ni wale tu wenye macho kama nyie ndio wanaotakiwa kwa sasa, ila kwa maoni yenu bado mmetuacha gizani.

Kumbukeni nyie ni sehemu ya mkakati huu, kama ni timu uwanjani nyie mnatakiwa kuwa wamaliziaji.

Ok mna maoni gani tutampataje huyo mwingine? shaurini lakini mkakati wetu wa kumuondoa Kikwete hupo palepale now!!!!!!!!

Kuwa nani atakuka kama Punditi utahsindwa kutupa jibu, tutyamjua uda huohuo.HATUTAMUACHA KIKWETE MADARAKANI ETI KWA SABABU YA KUKOSA WA KUMRITTH!
 
Nilishaongea hapa kwamba mabadiliko ya kitaasisi (katiba, kukua kwa utawala wa sheria, utamaduni wa ufuatiliaji kwa watu wote etc) ni muhimu kuliko mabadiliko ya watawala. Kama anakuja rais mwingine akakuta katiba ya sasa ambayo inamfanya rais kuwa mungu mtu fulani, ukweli utabaki kuwa kama hatatumia vibaya nguvu hizo atakuwa anatufanyia hisani tu.

Dawa ya kuondokana na uwezekano wa kukutwa na urais wa Kikwete mwingine ni kuwa na taasisi zenye misingi madhubuti katika utawala wa sheria. Najua hili linaweza kuwa ni lengo la muda mrefu na kwa muda mfupi tunaweza kutaka kumuondoa Kikwete tu, lakini vile vile tuangalie Kikwete anaendesha mambo yake katika mfumo na utamaduni gani, tukiweza kuuondoa huu mfumo wa "top down" na utamaduni wa kuogopana tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana.
 
WENYEVITI wa vijiji na vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya Tandahimba wamegoma kuanzia Novemba 10 mwaka huu wakidai malimbikizo ya posho za miaka miwili.

Katika risala yao ya utii kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Francis Miti iliyosomwa na Katibu wao, Ahmed Khalifa viongozi hao wa vijiji walisema hawatafanya kazi hizo mpaka halmashauri hiyo itakapowalipa madai yao ya kuanzia Juni, 2006.


"Kwa kipindi hiki cha miezi 28 kuanzia Juni, 2006 hadi Oktoba mwaka huu wenyeviti wa vijiji wote wa kata hizo tatu (za Tarafa ya Mahuta, Mkundi na Chingungwe), tulikuwa tunaidai Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Sh5,880,000."


"Na wenyeviti wa vitongoji ilikuwa halmashauri ya wilaya iwalipe Sh 9,380,000. Madai haya ni kwa wenyeviti wa vijiji 21 na wenyeviti wa vitongoji 67 wa kata hizo tatu," ilisema risala ya wenyeviti hao na kuongeza: "Na hali hii ni kwa Kata zote 22 za wilaya."


Madai hayo yanatokana na malimbikizo ya posho ya mwezi ya Sh 10,000 wanazostahili kulipwa wenyeviti wa vijiji na Sh5,000 kwa wenyeviti wa vitongoji.


Wenyeviti hao wanamshutumu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo, Gedra Msuya kwa kushindwa kuwatekelezea madai yao ambayo walisema kwamba ni madogo kulinganisha na malipo ya wilaya jirani ya Newala.


Viongozi hao wanadai kwamba Msuya amekataa kuwalipa posho zao na hata ruzuku ya asilimia 50 ya pato la vijiji ili halmashauri zao zijiendeshe.


Wanasema kwamba licha ya kukataa kufanya yote hayo ameshindwa pia kufikisha hoja zao katika baraza kuu la madiwani kama ilivyo sheria.


Akizungumzia madai hayo, Mkurugenzi Mtendaji huyo alikiri kuwa wenyeviti hao wanaidai ofisi yake na ameahidi kwamba suala lao linashughulikiwa.


"Ni kweli taarifa hizo zimenifikia na jana tulifanya kikao na madiwani wote wa Wilaya ya Tandahimba kujadili suala hilo," alisema Msuya.


Hata hivyo, alijitetea kwamba huenda malipo yao yamekwama mahali akidai kwamba amekuwa akiwalipa kwa kutumia utaratibu wa kuandika hawala moja... "Nadhani tatizo liko kwenye akaunti zao hasa kutokana na umbali kwani benki yetu iko Newala."


Msuya alisema kwamba baada ya kukutana na madiwani hao ameunda tume kufuatilia suala hilo.

Huenda wenyeviti waliona mbali kabla yako...
 
Kuunda tume ndiyo jibu, halafu tume ikifikia muda wake wa kutoa ripoti (kama ilipewa muda, kama haikupewa til kingdom come tena) kutaundwa tume nyingine kuhakiki ripoti ya tume.Mwishowe uchunguzi wa madai ya shilingi milioni 6 utachukua shilingi milioni mia sita.
 
Back
Top Bottom