Tanzania na siasa: Lugha ya kutumia Kiswahili au Kiingereza, Tatizo lipo wapi?

Kwanza nikupe heko mtoa mada. Mojawapo ya matatizo makubwa tuliyonayo Tanzania ni kutafuta njia rahisi kutatua matatizo magumu. Kiukweli wengi wetu lugha hizi zote mbili hatuzifahamu ipasavyo, yaani tunababia babia tu iwe kisw au kiing. Na matokeo yake ndio kuchanganya lugha kusiko na maana. Tutatue kwanza tatizo hili jamani. Kiingereza hatuwezi kukiepuka hata kidogo kama tunataka kasi ya maendeleo yetu iwe ya maana. na hatuwezi kufikia huko kama tunaridhika tu kukariri misamiati michache ya kiingereza na kuitupia tupia tu kwenye mazungumzo ili kuwatisha watu! Na kwa vile lugha zote hatuzijui kikamilifu, ndio maana tunatafuta nafuu katika kuondoa moja au sijui kufanya nini. Tufikirie vizuri, turekebishe mitaala yetu na hapo ndio tutakuwa kwenye mstari safi wa kutatua tatizo hili.

Na wewe pia unajaribu kutoa suluhisho kwa kuendelea kufanya makosa yale yale, kubadilisha mtaala kutasaidia nini? nani kakwambia tatizo ni mitaala? kwa taarifa yako miaka ambayo Watanzania tanajifunza kiingereza ni mingi sana hivyo kwa hali ya kawaida ilipaswa itoshe kabisa na zaidi, katika hali ya kawaida unaweza kujifunza lugha ya kigeni na kuweza kuitumia kwa ufasaha kabisa ndani ya miaka miwili tu, ushahidi upo wazi wapo Watanzania wengi ambao wanakwenda kusoma nje ya nchi na hawajawahi kusoma lugha za nchi wanazokwendwa hata siku moja, lakini ndani ya mwaka wanakuwa wanauwezo wakuitumia vyuoni na kusoma na kumaliza vizuri, wazee wetu wote waliosoma kama ni urusi au Uchina au Brazili. mimi rafiki yangu kaenda Japani na katumia mwaka mmoja kujifunza Kijapani sasa hivi ana shahada ya uhandisi ya Japani, hivyo tatizo la nchi yetu sio sijui kuanza kusomesha watoto kiingereza tangu chekechea kwani kiingereza tunaweza tukawafundisha kwa Kiswahili na bado tukatilia mkazo katika soma la kiingereza na bado wakaweza kukielewa, ndivyo nchi zote za watu wenye akili wanavyofanya, hata siku moja hawajaribu kujadili nafasi au umuhimu wa lugha yao katika nchi yao, bali wanabakiza ya kwao halafu hizo nyingine wunajifunza tu, miaka miwili inatosha kabisa!
 
Wapendwa, Tanzania shida yetu kubwa ni ubinafsi. Tumeua elimu yetu kwa kutowezesha mashule, waalimu, vyuo vya ngazi zote kwa garama ya kusomesha wachache ambao ni watoto wa viongozi. Hatutaweza kujisimamisha katika lugha yeyote kama tunategemea shule za kata ambazo hazina walimu, vifaa, na hata majengo yenye mwelekeo. Hatutaweza kujijenga katika lugha yeyote kama watoto kuanzia preschool hawapewi elimu inayohitajika. Angalieni primary schools zetu ambazo ni msingi wa lugha, elimu, sayansi, maisha nk. ziko katika hali gani?
Kwa kweli tutaendelea kuyumba hadi tutakapokubali kuwa tuna hali mbaya na kufanya mabadiliko ya uongozi wa nchi yetu bila kujionea aibu. Inauma sana kuona nchi inadorora katika afya, elimu, miundombinu n.k. Yaana hata raisi anatoka kwa tabasamu kuzindua mifereji iliyojengwa chini kabisa ya viwango akidanganya walalahoi eti ni barabara. Ni wapi duniani watu wanafyanya upuuzi kama huo leo hii? Tukubali ujinga wetu uliotupelekea kuiua elimu yetu kitaifa kwa kuwakubali viongozi wabovu namna hii. Tuache utani na tuikomboe nchi hii kwanza. Tukisharudisha elimu yetu katika msingi wake lugha itajileta yenyewe kama ilivyo mataifa mengine tunayoyajadili hapa.
 
Sasa si ndio tunaanza kuweka!.

Katika kutohoa, kanuni za msingi za lugha zibakishwe.

Kwa mfano. Kiswahili kina tabia na kanuni ya msingi kwamba kipo phonetic, neno linatamkwa kama linavyoandikwa (ndio maana kiswahili kina logic kubwa zaidi ya kiingereza katika matamshi). Huu ni msingi mzuri. Hatutaki kutohoa mambo tu bila kuuzingatia msingi huu. Na ndiyo maana nikasema "kwantam" inavutia zaidi kuliko "kwantum" kwa sababu "kwantam" inadumisha kanuni hii ya matamshi.

Vivyo hivyo, kuna matamshi mengine ya puani na kooni yaliyo kwa mfano kwenye kifaransa, hayapo kwenye Kiswahili. Na hata kama tunataka kutohoa maneno, tutohoe kwa kufuatisha kanuni za msingi za kiswahili zilizofanya "motocar" iwe "motokari" na si "motokar".
 
Quantum kwa mujibu wa kamusi ya TUKI ni "Kwanta". Quantum theory ni "nadharia ya kwanta".

Kingereza maneno yenye kuishia na ~um wingi wake huwa ~a, kama Datum kuwa Data, Quantum-> Quanta, sasa tukisema iwe "Kwanta" tutapata wapi wingi au umoja wake?Kama kweli hii ndio tafsiri yake ktk kamuzi,ni wazi hakuna umakini na well documented procedures ,naming schemes za kutumika kabla ya kutafsiri neno.

Kuna maneno ya kiswahili ambayo sidhani kama watu wanapenda kupeleka kwenye wingi kama "Jiko" ->"meko", watu wanapenda "majiko" au kutumia "jiko" ktk wingi na kuonyesha seheu nyingine za sentesi kuweka sifa ya wingi ,hata mimi pia sipendi wingi wake kama nisivyopenda tumia "datum" au "formulae" ktk "formula".Sijui taasisi ya kiswahili inafanya nini kwa hilo.Kuna majina ya viwango kama mwizi,jizi, je akiwa mdogo zaidi ya mwizi ataitwaje?

Nini maana ya neno "fantasy"?
 
Mfano.

Nimepewa deal la kutafsiri kitabu cha Brian Green cha Fizikia kwenda kwenye Kiswahili.

Kabla sijakubali, inabidi nijue jinsi ya kutafsiri misamiati.

Niambie neno "quantum" kiswahili chake ni nini?

Pole kwa kuwa siku zote naamini (kutokana na posts zako humu - hata kama tulishawahi kupeana za uso!) kuwa una maadili (which means hutanufaika na dili ulilopewa)
 
Kingereza maneno yenye kuishia na ~um wingi wake huwa ~a, kama Datum kuwa Data, Quantum-> Quanta, sasa tukisema iwe "Kwanta" tutapata wapi wingi au umoja wake?Kama kweli hii ndio tafsiri yake ktk kamuzi,ni wazi hakuna umakini na well documented procedures ,naming schemes za kutumika kabla ya kutafsiri neno.

Kuna maneno ya kiswahili ambayo sidhani kama watu wanapenda kupeleka kwenye wingi kama "Jiko" ->"meko", watu wanapenda "majiko" au kutumia "jiko" ktk wingi na kuonyesha seheu nyingine za sentesi kuweka sifa ya wingi ,hata mimi pia sipendi wingi wake kama nisivyopenda tumia "datum" au "formulae" ktk "formula".Sijui taasisi ya kiswahili inafanya nini kwa hilo.Kuna majina ya viwango kama mwizi,jizi, je akiwa mdogo zaidi ya mwizi ataitwaje?

Nini maana ya neno "fantasy"?

Karibu sana katika ulimwengu wa isimu. Cha muhimu kukumbuka ni kwamba kanuni za isimu/lugha zinaenda zinatofautiana. Mfano, neno 'hospital' uwingi wake ni 'hospitals'. Sasa 'hospital' kwa Kiswahili ni 'hospitali'. Uwingi wa 'hospitali' ni nini?
 
Karibu sana katika ulimwengu wa isimu. Cha muhimu kukumbuka ni kwamba kanuni za isimu/lugha zinaenda zinatofautiana. Mfano, neno 'hospital' uwingi wake ni 'hospitals'. Sasa 'hospital' kwa Kiswahili ni 'hospitali'. Uwingi wa 'hospitali' ni nini?

Ahsante sana kwa ufafanuzi.neno kama hospital pia kuna shida, watu wana shida ya kutumia "hospitali" kama wingi ikisaidia na prefix za maneno mengine zenye wingi kwani wengi tuu wanaonekana kuwa huwa confortabale na neno "mahospitali"
 
Ahsante sana kwa ufafanuzi.neno kama hospital pia kuna shida, watu wana shida ya kutumia "hospitali" kama wingi ikisaidia na prefix za maneno mengine zenye wingi kwani wengi tuu wanaonekana kuwa huwa confortabale na neno "mahospitali"

Wingi wa hospitali ni hospitali.

Hospitali hii, hospitali hizi.
 
Hapa ndo tatizo letu linapoanzia, kwa nini tutafsiri vitatabu vya watu wengine? Kama tunataka vitabu vilivyoandikwa kiswahili kwa nini tusitunge vya kwetu? Nimesoma Ujerumani, hakuna kitabu cha kiingereza kinachotafsiriwa, wanatumia vitabu vyao walivyoandika wenyewe kwa Kijerumani, vitabu vilivyoandikwa kwa kiingereza vinatumika mashuleni vikiwa hivyo hivyo, labrary za vyuo vikuu huko zina vitabu vingi tu viliyoandikwa kwa lugha ya Kiingereza na vinatumika vikiwa hivyohivyo.

Point yangu hapa ni kumsapoti mleta maada, watu wamekariri kwamba nchi zilizoendelea hazithamini Kiingereza, HIYO NI NOTION YA UONGO. Huwa wanakikomalia hasa kuhakikisha mtoto anayemaliza shule anajuwa kuongea Kiingereza, mtoto aliyemaliza sekondari Ujerumani anaongea kingereza vizuri huwezi kabisa kulinganisha na anayemaliza sekondari Tanzania.

Mfano tu ni kwamba wajerumani pamoja na kuwa wanapenda lugha yao, lakini TV yao ya DW ina channel inayotangaza duniani kwa kiingereza. Academic journals nyingi ziaandikwa kwa English, zikiwemo nyingi zinazoandikwa na kumilikiwa na wajerumani, au hata mataifa mengine ambayo lugha zao za asili si Kiingereza.

Tutaendelea kukaa na kujifariji na umaimuna wetu eti tukipotezee kingereza, lakini hiyo haitabadilisha umuhimu wa English katika kuleta maendeleo kwenye dunia ya leo. Ni wajinga kama sisi tu tunaoweza kudhani tutaendelea kama tutakipotezea kiingereza.


Mzee Kipara!
kwa kweli huwa nawashangaa watu na wengine ni maproff wa vyuo vikuu wanakazana eti kiswahili kiwe lugha ya kufundishia waaki argue kwamba wajerumani, wajapani, warusi wachina nk wanatymia lugha zao na ndio maana watoto wanaelewa vizuri lakini wanasahau kwamba hao watu wana wataalam wao katika nyanja zoote za sayansi tangu zamani, na wavumbuvi ni wao wenyewe sisi ni siasa tu kila mahali, mfano mdogo tu wanyarwanda juzi tu walikuwa ma franco-phone wamechange kwenda anglo-phone watatupita kama tumesimama!

kama lugha ni tija tuangalie nchi kama Ethiopia wana lugha yao , tena yenye herufi zake! mbona wapo hoi? sisi tunapiga domo eti kiswahili kiswahili! yaani watz tuna mambo wengine utawasikia eti yaani miaka 50 ya uhuru nchi bado masikini, ina uhusiano gani? kama uhuru ni issue Ureno ilikua wakoloni tangu enzi za vasco da gama, lakini leo wanakopa angola iliyopata uhuru juzi! we do not think! kila kwetu ni siasa htutanda mbali!

kimsingi naungana nawe pamoja na mtoa mada and thanks for a very constructive thread!
 
Kiswahili hakina Q, as far as I know.

Wewe mkorofi na huna mpango wa kuandika kitabu chochote kwa kiswahili. Waarabu hawana X, P, V nk na bado wa kiburi cha kutumia lugha yao.

Alexandria mji ulipo Misri wanaita Ishkandaria.

Quantum imeanza miaka kama 300 iliyopita. Je wachina, wajapan, wakorea walitafuta misamiati kwa njia gani kuelezea hiyo concept miaka 100 iliyopita walipoanza kujifunza?
 

Mzee Kipara!
kwa kweli huwa nawashangaa watu na wengine ni maproff wa vyuo vikuu wanakazana eti kiswahili kiwe lugha ya kufundishia waaki argue kwamba wajerumani, wajapani, warusi wachina nk wanatymia lugha zao na ndio maana watoto wanaelewa vizuri lakini wanasahau kwamba hao watu wana wataalam wao katika nyanja zoote za sayansi tangu zamani, na wavumbuvi ni wao wenyewe sisi ni siasa tu kila mahali, mfano mdogo tu wanyarwanda juzi tu walikuwa ma franco-phone wamechange kwenda anglo-phone watatupita kama tumesimama!

kama lugha ni tija tuangalie nchi kama Ethiopia wana lugha yao , tena yenye herufi zake! mbona wapo hoi? sisi tunapiga domo eti kiswahili kiswahili! yaani watz tuna mambo wengine utawasikia eti yaani miaka 50 ya uhuru nchi bado masikini, ina uhusiano gani? kama uhuru ni issue Ureno ilikua wakoloni tangu enzi za vasco da gama, lakini leo wanakopa angola iliyopata uhuru juzi! we do not think! kila kwetu ni siasa htutanda mbali!

kimsingi naungana nawe pamoja na mtoa mada and thanks for a very constructive thread!


Unasema Maprofesa. Kumbuka hao ndio wataalam wenyewe.
 
nimesoma baadhi ya michango nahisi kuna kitu tuna kikosa hapa, wanazuoni wengi wanao tetea hili swala hata ukiwauliza leo hawasemi kingereza kifutwe kabisa, ila wanataka tupite kwenye njia nchi nyingine zinazopitia mfano kuna watu wametoa mifano ya ujerumani, na sisi hapa wanataka kingereza kifundishwe kwa ufasaha ila angalau mwanafunzi anapo maliza kidato cha nne awe na uwezo wa kuongea kiswahili na kingereza kwa ufasaha. Ila leo tunatumia kingereza kama lugha ya kufundishia na kuna wanafunzi wanamaliza hata chuo kikuu na hawawezi kukitumia kingereza wala kiswahili kwa ufasaha, tunachokitaka nikua kiingereza kifutwe kama lugha ya kufundishia ila kibaki kama somo na walimu waandaliwe ili wawe na utaalamu wa kikifundisha kiingereza kwa ufasaha mkubwa
 
Wewe mkorofi na huna mpango wa kuandika kitabu chochote kwa kiswahili. Waarabu hawana X, P, V nk na bado wa kiburi cha kutumia lugha yao.

Alexandria mji ulipo Misri wanaita Ishkandaria.

Quantum imeanza miaka kama 300 iliyopita. Je wachina, wajapan, wakorea walitafuta misamiati kwa njia gani kuelezea hiyo concept miaka 100 iliyopita walipoanza kujifunza?

Sijasema nina mpango wa kuandika kitabu, rudia kusoma vizuri.

Sijasema kwamba kama hatuna Q kwenye Kiswahili tusitumie lugha yetu, hiyo habari ya waarabu ni moot, non sequitur.

Kusema kwamba quantum "imeanza" miaka 300 iliyopita is laughable.

Sijui Wachina, Wajapan, Wakorea walitafuta misamiati kwa njia gani. Najua waingerez walitohoa kutoka kilatini bila ya kuharibu misingi fulani ya kutohoa ambayo imekuwapo tangu wafaransa walivyotohoa kwa Warumi, Warumi walivyotohoa kwa Wagiriki na Wagiriki walivyotohoa kwa Wamisri na Waarabu.

Kwamba kutohoa si jambo geni hakukatai kwamba kutohoa bila kuua misingi ya matamshi ya lugha nako si jambo geni.
 
nimesoma baadhi ya michango nahisi kuna kitu tuna kikosa hapa, wanazuoni wengi wanao tetea hili swala hata ukiwauliza leo hawasemi kingereza kifutwe kabisa, ila wanataka tupite kwenye njia nchi nyingine zinazopitia mfano kuna watu wametoa mifano ya ujerumani, na sisi hapa wanataka kingereza kifundishwe kwa ufasaha ila angalau mwanafunzi anapo maliza kidato cha nne awe na uwezo wa kuongea kiswahili na kingereza kwa ufasaha. Ila leo tunatumia kingereza kama lugha ya kufundishia na kuna wanafunzi wanamaliza hata chuo kikuu na hawawezi kukitumia kingereza wala kiswahili kwa ufasaha, tunachokitaka nikua kiingereza kifutwe kama lugha ya kufundishia ila kibaki kama somo na walimu waandaliwe ili wawe na utaalamu wa kikifundisha kiingereza kwa ufasaha mkubwa

Tunakazania lugha wakati huenda matatizo yetu ni diet na hata ukifundisha lugha gani kwa mtu mwenye njaa haelewi.

Au tatizo letu ni kutothamini usomi kiujumla, vijana wanaona wasomi wenye integrity zao wanakuwa frustrated wakati wauza madawa ya kulevya wanatanua na kuongoza nchi.

Nchi yetu ina matatizo ya msingi kuliko lugha. Ile kazi ya kujenga nchi walioifanya kina Nyerere tumeona "imeshaisha" wakati kikweli ndo kwanza ilikuwa inaanza.

Matokeo yake tunajikuta hatujui sayansi, hesabu, kiingereza, kiswahili.

I don't put much stock in the IQ concept, but as a short hand, naona kama kuna matatizo deeper zaidi ya lugha with us collectively as a nation.

Lugha ni sehemu ndogo tu ya utamaduni, tukitazama sana ustadi wa lugha bila ya kuangalia chemchemi ya lugha inatokea wapi kwenye utamaduni tutakuwa tunacheza makida makida.

Tuking'ang'ania utamaduni wa "vazi la taifa kwa kamati ziso tamati" basi mawazo ya kuendeleza lugha tutawaachia TUKI bila valangati.

Tukiangalia habari ya lugha bila kujua kwamba lugha inastawi na uchumi, na kwamba bila ya kuwa na printing presses zinazochapa vitabu vya Kiswahili, tusitegemee the yellow sheets of the Shigongos of this world ndio yataendeleza lugha. Na kama kuna printing presses bila ya watu kuwa na purchasing power, the culture of reading and the leisure time to do so, tutakuwa tuna descend kwenye idiocracy ya "tunakwendaga" kuwa formal Swahili.

Sisi, kama Watanzania collectively, si maskini na wajinga kwa sababu hatujui lugha.

Sisi hatujui lugha kwa sababu ni maskini na wajinga.

Tibu umaskini na ujinga mambo ya lugha yatajitengeneza yenyewe.
 
Back
Top Bottom