Tanzania inatambua Haki za MASHOGA

PMNBuko

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
967
154
Nasikitika kusema kuwa nchi yetu, licha ya kupinga tamko la Uingereza na Marekani juu ya Haki za Mashoga, tayari Tanzania iliridhia haki za Mashoga tangu 2009.

Kwa Mjibu wa Mkakati wa Taifa la Tanzania wa Kinga Dhidi ya VV/UKIMWI wa 2009 - 2012, Mkakati Na.9 (b): Kuongeza Uelewa na Kupunguza Mienendo Hatarishi Miongozi mwa Watu wenye uwezekano wa ongezeko la uambukizi wa VVU, unabainisha kuwa wanaume wanaolawitiana wana haki zifuatazo (soma ukurasa wa 35 - Huduma muhimu kwa wanaolawitiana) - nimetaja baadhi tu:

1. Kupata ulinzi wa kisheria na sera za msaada na uraghabishi.

2. -

3. Usambazaji wa vilainishi vya maji na kondomu.

4. , n.k.

Maoni yangu: Kwa kuwa Mkakati huu ni serikali ya Tanzania, na tayari unaridhia uwepo wa Mashoga na kwamba wanastahili kupewa haki za msingi pamoja na huduma muhimu kama vilainishi vya maji (kwa maana ya wakati wa kulawitiana), ina maana kwamba Serikali ya Tanzania kupitia kwa Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, hakukuwa na haja ya kulumbana na Mataifa ya Magharibi yanayoshinikiza nchi za Afrika kuheshimu haki za Mashoga kwani tayari tulishaheshimu haki zao tokea kuandikwa kwa mkakati huu mwaka 2009.

Kwa lugha nyingine, Serikali yetu iliridhia haki za mashoga mwaka huo wa 2009 kupitia mkakati huu. Siamini kama Membe hajasoma mkakati huu na kama ndiyo, tuna viongozi wavivu wa kusoma.

WanaJF hili mnalichukuliaje? Nawasilisha.
 
peleka MMU huu upuuzi

Mkuu usi-conclude bila kufanya utafiti. Soma Mkakati wa Taifa wa Kinga Dhidi ya UKIMWI 2009-2012. Unapatikana kwenye Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu/TACAIDS. Tena umesainiwa na Peniel M. Lyimo - Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Dkt. Fatma H. Mrisho, Mwenyekiti Mtendaji - TACAIDS.
 
Kwa kweli mimi baada ya kupitia Document hii ya serikali nimesikitika sana. Nimewadharau, siyo tu wale waliouandaa bali wale pia viongozi wasiojua kuwa kuna living document ya kisheria na kiserikali namna hiyo. Huu ni upuuzi wa viongozi tulionao.
 
Katika utawala udikteta unatakiwa hasa katika kutetea na kulinda utamaduni wa jamii serikali inatakiwa kupinga hilo.
 
Mkuu usi-conclude bila kufanya utafiti. Soma Mkakati wa Taifa wa Kinga Dhidi ya UKIMWI 2009-2012. Unapatikana kwenye Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu/TACAIDS. Tena umesainiwa na Peniel M. Lyimo - Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Dkt. Fatma H. Mrisho, Mwenyekiti Mtendaji - TACAIDS.

kwangu mimi chochote kinachohusu ushoga ni upuuzi na huwa sisomi habari za namna hii hata siku moja. Tunapo andika andika habari za ushoga ndio tunavyoyazoesha masikio ya watu na mwisho wa siku tutaanza kuzungumzia ushezi huu mbele ya watoto wetu. Kama tupo serious na kuukataa huu ufilauni basi tusiandike chochote kuhusu ushenzi huu hapa nyumbani iwe magazetini, mtandaoni, radio au tv.
Unajua hili swala linahusishwa sana kisiasa na ujuaji mwingi kwenye kutafuta umaarufu na hao wanaojifanya wapigania haki za binadamu wakati mioyoni mwao wanasema ee mungu niepushie isijetokea kwa wanangu.

miaka ya 90 na 2000 mwanzoni ushoga ilikuwa ni kitu cha ajabu sana lakini baada ya shigongo kuanza na magazeti yake leo hii unaona alipolipeleka taifa. Huyu ni wa kulaumiwa sana kwa aliyoyafanya, yeye alikuwa anajifanya anakemea uovu akiwa na lengo la kufanya biashara ya magazeti yake tena kwa kuzipa habari hizi front page
 
kwangu mimi chochote kinachohusu ushoga ni upuuzi na huwa sisomi habari za namna hii hata siku moja. Tunapo andika andika habari za ushoga ndio tunavyoyazoesha masikio ya watu na mwisho wa siku tutaanza kuzungumzia ushezi huu mbele ya watoto wetu. Kama tupo serious na kuukataa huu ufilauni basi tusiandike chochote kuhusu ushenzi huu hapa nyumbani iwe magazetini, mtandaoni, radio au tv.
Unajua hili swala linahusishwa sana kisiasa na ujuaji mwingi kwenye kutafuta umaarufu na hao wanaojifanya wapigania haki za binadamu wakati mioyoni mwao wanasema ee mungu niepushie isijetokea kwa wanangu.

miaka ya 90 na 2000 mwanzoni ushoga ilikuwa ni kitu cha ajabu sana lakini baada ya shigongo kuanza na magazeti yake leo hii unaona alipolipeleka taifa. Huyu ni wa kulaumiwa sana kwa aliyoyafanya, yeye alikuwa anajifanya anakemea uovu akiwa na lengo la kufanya biashara ya magazeti yake tena kwa kuzipa habari hizi front page

Narubongo, nakubaliana na maoni yako. Lakini hoja iliyoko hapa ni kwamba tayari Mkakati wa Taifa unatambua haki za Mashoga. Kwa hiyo, la msingi siyo kuziba masikio maana hata ukiziba masikio bila kushiriki udhibiti, haitasaidia. Maadam document hiyo ipo, tunatakiwa kuishikia bango serikali irekebishe document hii maana tayari ipo na inatambua haki za mashoga.

Pili ni kwamba iweje Membe aseme serikali haitambua haki hizo wakati Mkakati huu umeandaliwa na serikali????? Hapa ndipo tunaweza kuanzia...
 
Huduma nyingine ambazo mkakati huo unazitaja ni pamoja na ... serikali kuweka mipango ya kutoa rufaa ya tiba na matunzo kwa walioathiriwa na vitendo vya kulawitiana.

Moja ya sentensi za mkakati zinasema: Kutokana na kwamba utafiti wa Makwagile na wenzake (2001) na Hoffman na wenzake (2004) kuonesha kuwa vitendo vya kulawitiana vipo nchini na kwamba wanaume wanaolawitiana wanafanya pia ngono na wanawake, ni lazima kwa mkakati wa kinga dhidi ya VVU kutathmini zaidi ukubwa wa desturi hizi na kupendekeza mikakati inayofaa. Mikakati hiyo haina budi kujumuisha kutoa kipaumbele kwa mazingira ya HAKI ZA BINADAMU..."
 
Katika utawala udikteta unatakiwa hasa katika kutetea na kulinda utamaduni wa jamii serikali inatakiwa kupinga hilo.

Mkuu, serikali haiwezi kupinga kitu ilichokiandaa yenyewe.... Wamekaa chini wakaandaa mkakati unaotambua haki za mashoga nchini tena kwa kulipana posho zetu. Iweje ipinge jambo la ushoga??? Huo si ni ujuha, kama Membe anavyofanya??
 
Mkakati huu unatamka wazi kuwa haki za binadamu ni pamoja na kukomesha unyanyapaa kwa watu wanaolawitiana. Ndio maana kuna maelekezo ya sera kwa serikali kutoa huduma kwa mashoga kama vile vilainishi vya maji na Kondomu.

Wana JF naomba mlipe uzito unaostahili suala hili ikiwa ni pamoja na kupendekeza hatua za kuchukuliwa ili document hii irejewe (iwe-reviewed) na ikiwezekana itolewe taarifa kwa umma juu ya mkanganyiko huu.

Naomba kuwasilisha tena... Karibu
 
Back
Top Bottom