Tanzania govt on Homosexuality: We can do without UK aid

Mh Membe leo amekutana na waandishi wa habari kutujulisha yaliyojiri kwenye mkutano wa Jumuiya ya Madola uliofanyika huko Australia hivi karibuni. Mh Membe ametoa tamko dhidi ya kauli iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Uingereza ya kutishia kusitisha misaada ya kiuchumi kwa nchi za Jumuiya ya Madola zinazopinga suala la mahusiano ya watu wa jinsia moja.

Mh Membe amesema Katiba ya nchi inatambua familia kwa maana ya mahusiano ya kijinsia kati ya mume na mke na si vinginevyo. Amesema pia jadi na utamaduni wa Watanzania unaruhusu uhusiano wa mwanaume na mwanamke tuu na si vinginevyo. Mh Membe amesema Tanzania haikubaliani kwa namna yoyote ile na kauli ya Cameron na kwamba tutakuwa tayari hata kujitoa kwenye Jumuiya ya Madola kama Uingereza itashinikiza Tanzania itambue mahusiano ya watu wa jinsia moja.
tujitoe tu kwenye hilo dudu CW. Kwani sisi bado tupo chini ya malkia?
 
naamini kauli ya membe ni kauli ya serikali.kama tuko serious tusiwaalike waingereza kwenye kilele cha sherehe za miaka 50 ya uhuru ili wasirudie kutoa kauli zao za kipuuzi!!ndio maana sinaga mzuka na ligi ya uingereza,naichukulia kama ligi ya mashoga.
 
Mnajua wazungu ni washenzi sana. Wanaweza kuleta vyakula ambavyo ukila unawashwa ile mbaya. Unadhani ni nini kitatumika kuukuna muwasho huo? Teh, teh teheee!
 
Wallah huyu Cameroon ni fedhuli mkubwa, Hakika leo Tanzania ikakakubali mashoga wawepo; kesho watasema mashoga wasipo fika asilimia 40 ya wanaume wote hawatoi fedha zao.
 
So, Tanzania joins Ghana and Uganda. Ghana's President John Atta Mills has also rejected the UK's threat to cut aid if he refuses to legalise homosexuality. Mr Atta Mills said the UK could not impose its values on Ghana and he would never legalise homosexuality.

Mr Atta Mills said Mr Cameron was entitled to his views, but he did not have the right to "direct to other sovereign nations as to what they should do". He said Ghana's "societal norms" were different from those in the UK. "I, as president, will never initiate or support any attempt to legalise homosexuality in Ghana," Mr Atta Mills said.

Uganda also rejected the threat, with an official accusing the UK of showing a "bullying mentality". On Monday, Ugandan presidential adviser John Nagenda said Mr Cameron was showing a "bullying mentality" and Ugandans would not tolerate being treated like "children".

http://www.bbc.co.uk/news/world-africa-15558769
 
Mh Membe leo amekutana na waandishi wa habari kutujulisha yaliyojiri kwenye mkutano wa Jumuiya ya Madola uliofanyika huko Australia hivi karibuni. Mh Membe ametoa tamko dhidi ya kauli iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Uingereza ya kutishia kusitisha misaada ya kiuchumi kwa nchi za Jumuiya ya Madola zinazopinga suala la mahusiano ya watu wa jinsia moja.

Mh Membe amesema Katiba ya nchi inatambua familia kwa maana ya mahusiano ya kijinsia kati ya mume na mke na si vinginevyo. Amesema pia jadi na utamaduni wa Watanzania unaruhusu uhusiano wa mwanaume na mwanamke tuu na si vinginevyo. Mh Membe amesema Tanzania haikubaliani kwa namna yoyote ile na kauli ya Cameron na kwamba tutakuwa tayari hata kujitoa kwenye Jumuiya ya Madola kama Uingereza itashinikiza Tanzania itambue mahusiano ya watu wa jinsia moja.

Kumbe viongozi wetu yana wapata mengi nyuma ya pazia .! Nakumbuka Mkulu alipoambiwa apunguze Matrip ya huko ughaibuni hasa mamtoni, alidai waTz twaweza kufa njaa. Sasa sijui huwa anapewa masharti gani huko?? Na sijui huwa anakubali au anakataa?? Mmmh wakubwa wana mambo.,
 
Kwanini tusianza na sisi kususia kununua vitu vyao, kupanda ndege zao, kusikiliza radio zao, kushiriki vikao vyao tuseme mashoga ndio wanao jishughulisha na hivyo vitu nasisi kama africa hatutaki. Jumuiya ya madola ya nini gadaffi kapigwa nini kimesemwa?? hopeless tujitoe humo
 
Cameron kanifurahisha sana manake labda sasa tutatia akili na kuanza kuzifanyisha kazi akili zetu na kubuni mbinu na mikakati mipya ya kujikwamua kiuchumi.

Na pia huenda hiyo ndo ilikuwa nia ya Cameron. Kwamba hawa watu inabidi uwatishe kwa jambo ambalo wanajifanya hawalipendi kabisa ili waache utegemezi wao.

Naombea Obama na Sarkozy nao wafuate nyayo za Cameron. Tena wasitishie. Ni wasitishe kabisa hiyo misaada.
 
Safi kabisa mh membe,CDM ni marafiki wa Conservative anakotoka Cameron,msimamo wa Chadema ni upi kwa hili la ushoga kwani mashoga zao Conservative wanatetea ushoga!
 
Nasikia ZNZ wao walishatangaza mvua 25 kwa kulawitiana. Sasa sisi tunasubiri mpaka Cameron aseme ndiyo na sisi tunaanza kuropoka msimamo wetu bila hata kufikiria kua akina aunt Mood kibao pale Magomeni na Kinondoni lakini hatujawafanya kitu!!!

All in all alitakiwa azungumzie kulekule ambako vyombo kibao vya kimataifa vingetoa msimamo wao wazi badala ya kuja kuzungumzia huku kwenye magazeti ya udaku!!
 
Enzi za utawala wa Ben.nkapa nilifurahia sana, sababu statement hii ya Cameroun ingetokea kipindi hicho ze.nkapa asingepoteza muda kama anavyofanya ******, jamaa angemchana live Cameroun.Ndiyo maana enzi za Ben.nkapa aliwaweka pembeni JK na Sumaye baada ya kugundua were not vigilant.Haaaaaaa we miss u ben.nkapa.
 
aisee naomba ufafanuzi, hivi wanachosema ni kwamba wanataka watubandue watanzania kwa misaada na fadhila tulizokula????
 
Japokuwa Membe ametoa tamko kwa kuchelewa nampongeza kwa kuweka wazi msimamo wa taifa la Tanzania.

Hawa wazungu wanapaswa kutambua kuwa mataifa ya Africa ni huru na yashajikomboa kutoka katika ukoloni wa wazungu. Kwa hiyo tupo huru kufanya nao biashara kwa manufaa ya wote katika mjadala wa wazi bila shinikizo la yeyote. Waheshimu mila zetu na taratibu zetu kama wanavyotaka nasi tuwaheshimu.

Hatuamini katika misaada kama vile ambavyo tunavyoamini katika kazi. Kazi ndio msingi wa maisha na wala sii vimisaada ukizingatia kwamba misaada ni mahsusi kwa jamii ya walemavu ambapo hilo ni tatizo la kudumu kwao.
 
Hawa jamaa hali yao kiuchumi si nzuri wanachotafuta ni namna ya kupunguza matumizi.

Hivyo waliipotoa sharti lile walijua fika kuwa kwa Jinsi Miafrika Tulivyo na vitendo hivyo hatutakubaliana na sharti lao hivyo itawapa wao unafuu na kuwaondolea lawama kwa kushindwa sisi wenyewe masharti.

Recently wameanza ku sense li commonwealthy lenyewe ni zigo tu kwake wani nchi kama USA, China nk hazina cha common wealty wala nini na kila uchao wanaimarika while England goes down and down while the fire flames go hire.

My take kwa viongozi wetu:
Na nyie mmezidi kudoea na kuomboleza hv mnadhani kwa hizi rasilimali zetu kama mngekuwa na uzalendo wa kweli tungeshindwa kujiendesha bila misaada yao?

Lile sharti halikuhitaji mrudi nyumbani mjadiliane halafu ndiyo mkatae ilitakiwa kuwakatalia there there... Halafu nyumbani mnakuja kujadiliana namna ya ku-fix gape na kama nchi tusonge mbele. Lakini namna mlivyoutoa huo msimamo ni kama vile mnapima eti tuone kama tukikataa watatunyima kweli?

Hatuna muda zaidi ya tulio nao mtuambie sasa tunajiandaa vp na maisha mapya hatuna sifa ya kufaa njaa sisi , we are wealthy enough.
 
Mtu anapokushawishi uukubali ushoga amekudharau kweli, hili serikali ikishindwa kulisimamia kwa njaa zao itabidi tusiangaliane usoni.

Aisee! Kuishi kwingi ni kuona mengi, ndio tumefikia huku tena. Kwa hili watusamehe, tutakuja letewa wachumba wakiume na watoto wetu wa kiume eti, 'Dady huyu ndo my hubby' aggggrrh!!!!!!!!!!!!!!
 
Mwenye macho na aone na mwenye masikio na asikie: Marekani kuna watu wanaihagaikia sana hiyo dollar, inakuwaje wanasema wanatoa msaada kwa wananchi wa nchi zinazoendelea wakati wa kwao bado wanashida? Akili mukichwa! Hiyo siyo misaada ila ni biashara bubu kwetu.
 
Mzee Yusufu Makamba ndiye aliyemkimbiza Matonya Dar. ina maana wazungu ndio wanatufukuza kwa ule usemi "AKUFUKUZAYE HAKUAMBII TOKA" wao wanajua nchi nyingi za kiafrika zitapinga na ndio urafiki utakapoishia hapo.Nalitafuta sana tamko la Zimbabwe mwenye nalo alibwage hapa.Na log off
Tumezidi kuwa kuomba omba na rasilimali tunazo kibao, ngoja tukomeshwe.
 
Back
Top Bottom