Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,693
- 20,454
Kuna habari kwamba shirika la umeme nchini (TANESCO) limesimamisha kuunganishia wateja wake wapya huduma hiyo muhimu. Kwa mujibu wa vyanzo vya habari hii toka ndani ya shirika hilo, sababu kubwa inayotolewa na shirika hilo ni kukosekana kwa nyaya za kuunganisha kutoka kwenye mlingoti kwenda katika jengo (service line) na kwamba mteja wa mwisho kupata huduma hiyo katika mkoa wa Ilala (wa TANESCO) aliwekewa mwezi wa Mei 2010. Kama kuna ukweli wa habari hii, maana yake ni kwamba iwapo ataonekana mteja ameunganishiwa umeme hivi karibuni, basi huyo atakuwa ametoa rushwa au amepita njia za 'panya' na anatakiwa aripotiwe TAKUKURU ili wachunguze ni nani amemuwekea umeme na ametoa wapi nyaya wakati inajulikana kwamba nchi nzima hakuna nyaya na huduma ilishasimamishwa. Naona MD mpya amekuja na mikosi. Karibuni jamvini ...
NB: Naombeni msaada wa kisheria kwani nataka niwashitaki TANESCO kwa kukiuka mkataba wa kuniwekea umeme ndani ya siku 60 baada ya kufanya malipo halali.
NB: Naombeni msaada wa kisheria kwani nataka niwashitaki TANESCO kwa kukiuka mkataba wa kuniwekea umeme ndani ya siku 60 baada ya kufanya malipo halali.