Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Luku
Hatimaye Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), limeanza kuingiza mita za Luku ambazo jana zilianza kusambazwa katika mikoa mbalimbali.
Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Adrian Sererin, aliliambia NIPASHE jana kuwa hadi sasa mita 11, 500 zimeishaingizwa nchini.
Aidha, alisema Mita zingine 75, 000 zinatarajia kuingizwa nchini ili kuhakikisha kwamba wateja wao wanafungiwa kwa nchi nzima.
Kuanzia mwanzoni mwa mwaka huu, Tanesco lilikuwa linakabiliwa na uhaba wa ,ita na vifaa vingine ambavyo vinahitajika kwa ajili ya kuwaunganishia wateja umeme.
Hivi sasa hatuna tena uhaba wa mita na tumeishaingiza mita za kutosha na jana (juzi) tulianza kuzisambaza mikoani ili zianze kufungwa kwa wateja, alisema.
Alifafanua kuwa Tanesco inatarajia kufunga mita mpya kwa wateja wote na kuondoa zile za zamani na kwamba zoezi hilo linatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi ujao.
Hizi Mita zote za sasa zitabadilishwa na kuweka mpya kwa nchi nzima na hivi tunavyoongea tayari zimeanza kusambazwa mikoani, alisema Zaidi ya wateja 6000 walioomba kuwekewa umeme katika maeneo mbalimbali wameshindwa kupata huduma hiyo kutokana na Tanesco kutokuwa na mita kwa kipindi kirefu.
CHANZO: NIPASHE