KIGENE
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,552
- 813
Babu mmoja alikuwa na wake wawili wa kwanza alikuwa azai wa pili alikuwa na watoto. Huyo mke wa pili na watoto wake kila kukicha walikuwa hawaishi kumnyanyasa mke mgumba kwa vijembe vya hapa na pale Pamoja na kutokuwa na mtoto lakini babu alitokea kumpenda sana. Siku moja akamwambia kwamba kwa vile mke mwenza na wanae wanamwandama sana na akifa lazima watamtolea nje akamwambia ikitokea nikatangulia mbele ya haki urithi wako nimeuficha juu darini kwa hiyo nikifa nikunje vizuri halafu panda darini uchukue urithi wako halafu piga mayowe kuwataarifu majira. Siku ya siku babu akaanguka chini nakujigaragaza akaonekana anakata roho yule mgumba hakujali kumweka sawa babu wakati anaaga dunia akawa kwenye harakati za kupanda darini kuchukua uridhi aliohaidiwa na babu kila anachojaribu kutumia kufika darini kinakuwa kifupi akaamua kusogeza maiti ya babu nakuweka kinu juu yake hili aweze kupanda darini. Babu akazinduka na kumuliza hivi mke wangu hivyo ndivyo tulivyohaidiana nimejifanya nimekufa nione akili zako zikoje uenda hata mwenyezi Mungu aliona una huruma ndio maana akakufanya hivyo mke hapohapo akazimiaaj