BADILI TABIA
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 32,772
- 23,164
ndo maana wanawake hawatoi lifti, heri uonekane una roho mbaya kuliko kulizwa
Huyo naye alikuwa boya kweli.
Watu sio wastaarabu kabisa...lift upewe na bado uibe...kweli ni somo kwetu sote
Sasa kama Wababa wanafanyiwa hivi, wamama itakuwaje? hii ni moja ya sababu wanawake wengi hawatoi lift kwa yeyote njiani, potelea mbali acha tuonekane tuna roho mbaya tumechoka kuibiwa mapochi na vipodozi vyetu kila siku!
Huyo naye alikuwa boya kweli.
huyo ni f.a.l.la haswa!
inakuwaje uwape lift watu usio wajua halafu wajimilikishe uenyeji kwenye gari yako,kisha we unajifanya huna habari nao!?!au jana yake ulipitia shell?
Ni gari gani hiyo? Mpaka wanapitisha mkono uingie kwenye buti? Huyo dereva au robot?
Noma sana aisee...Mkuu, Hao jamaa hawakua na shida ya kupata lifti, lengo Lao ilikua na kuiba mali yeyote kwny gari.
Hii kitu mbaya sana, yaani unaingia kwenye gari la mtu kwa kusudi la kudokoa, kuiba au kufanya madude yako mengine unayoyajua mwenyewe,...., hii kitu mbaya sana and I hate it to the bottom of my heart. Halafu naomba siku moja nije nifanikiwe kukamata mtu kama hii, siku hiyo itanitambua hiyo mtu!Wadau.. Mfanyakazi mwenzangu, ameibiwa LAPTOP baada ya kuwapa lift watu watatu, mmoja akiwa ni mwanafunzi FAKE. Alikuwa anatoka maeneo ya MAJOHE asubuhi kuelekea maeneo ya Gongolamboto halafu kibaruani. Alipofika Relini, Watu wawili na mwanafunzi FAKE wakaomba lift. Jamaa alipoona na mwanafunzi yupo. akasimama na kuwapa lift.
Wale watu, walilaza kiti cha nyuma na kupata ACCESS kwenye buti ambako alikuwa ameweka Laptop. Wakaitoa kwenye BAG lake, na kuupitisha chini ya kiti cha abiria aliyeko upande wa kushoto wa gari mbele, (Mwanafunzi fake) kwani alipoingia garini, aliweka madaftari yake chini. Hivyo basi, alipofika Pugu Sec, akatelemka, na kuchukua madaftari (Counters) yake na kuunganisha na laptop ya jamaa.
Jamaa alikuja kushtuka baada ya kufika kibaruani na kuona hana laptop na alijua kaibiwa kwani zile shughuli aliziona zikifanyika, lakini hakuhisi kama ni wizi ulikuwa unaendelea. Wale wezi wawili wakatelemkia Gongo la Mboto..
Hivyo hata nyuma ya BUTI la gari sio salama tena. Dawa ni kutompa mtu yeyote lift.
hivi happiness win ndio Miss Tanzania 2013 from Dodoma?
Gari hujakabidhiwa ushakula kiapo hutupi lift kwenda Chako ni Chako?
Mi huwa napita sana Kinyerezi mwisho au Goba na huwa naota lift kwa wanafuzi sana tu, lakini kabla sijatoa lifti nahakikisha kila kitu nimeweka vizuri na kama siku hiyo gari yangu iko na vitu vingi sitoi lift.Usafiri ni wa shida sana jamani tusaidiane na Mungua atatulinda. Naumia sana especially ninapoona STK/STG zinakatisha na mtu mmoja hata hazitoi lift gari za serikali madereva na ma boss wao wanaroho mbaya sana jamani.
Wale watu, walilaza kiti cha nyuma na kupata ACCESS kwenye buti ambako alikuwa ameweka Laptop. Wakaitoa kwenye BAG lake, na kuupitisha chini ya kiti cha abiria aliyeko upande wa kushoto wa gari mbele, (Mwanafunzi fake) kwani alipoingia garini, aliweka madaftari yake chini. Hivyo basi, alipofika Pugu Sec, akatelemka, na kuchukua madaftari (Counters) yake na kuunganisha na laptop ya jamaa.