Exaud J. Makyao
JF-Expert Member
- Nov 30, 2008
- 1,518
- 22
Shamrashamra za SIKU KUU ZA Christmas na mwaka mpya zimeanza.
TAHADHARI INAHITAJIKA,
1. Vibaka sasa wamejiweka tayari kuwakwapua watu simu zao za
mikonomni na vitu vinginevyo.
2. Matapeli nao wakijua kuwa watu wanahitaji pesa za matumizi,
wametunga mbinu nyingi kuwahadaa watu kwa kisingizio cha
kuwajaza mapesa.
3. Madereva wengi wasiorasmi sasa wanaendesha vyombo vya
usafiri kwa lengo la kupata pesa za chapchap.Hawa ni rahisi
kusababisha ajal.
4. Kumbi zinazoitwa za Starehe zinaandaliwa kufanya
maonyesho kama walivyofanya kule Tabora na kusababisha vifo
lukuki vya watoto.Wanastarehe hao husema ''KUTAKUWA NA
DISCO LA KUFA MTU '' na kweli watu hufa eidha kwa
kuambukizwa virusi au kwa tukio kama lile la Tabora.
Je hizi ni kumbi za starehe au ni kumbi za vifo?
NASHAURI,
1. Watu tuwe makini kwa kila tukifanyacho.
2. Vyombo vya usalama viwe makini katika wajibu wao.
3. Waumini tumwombe Mungu atuepushe na athari mbaya zozote.
4. Sikukuu zitumiwe kwa kusudi halisi na siyo makusudi bandia.
5. Watoto walindwe wasiingie katika uharibifu unaoitwa starehe.
EXAUD JOHN MAKIYAO
+255784347001
makyaoexaud@yahoo.com
TAHADHARI INAHITAJIKA,
1. Vibaka sasa wamejiweka tayari kuwakwapua watu simu zao za
mikonomni na vitu vinginevyo.
2. Matapeli nao wakijua kuwa watu wanahitaji pesa za matumizi,
wametunga mbinu nyingi kuwahadaa watu kwa kisingizio cha
kuwajaza mapesa.
3. Madereva wengi wasiorasmi sasa wanaendesha vyombo vya
usafiri kwa lengo la kupata pesa za chapchap.Hawa ni rahisi
kusababisha ajal.
4. Kumbi zinazoitwa za Starehe zinaandaliwa kufanya
maonyesho kama walivyofanya kule Tabora na kusababisha vifo
lukuki vya watoto.Wanastarehe hao husema ''KUTAKUWA NA
DISCO LA KUFA MTU '' na kweli watu hufa eidha kwa
kuambukizwa virusi au kwa tukio kama lile la Tabora.
Je hizi ni kumbi za starehe au ni kumbi za vifo?
NASHAURI,
1. Watu tuwe makini kwa kila tukifanyacho.
2. Vyombo vya usalama viwe makini katika wajibu wao.
3. Waumini tumwombe Mungu atuepushe na athari mbaya zozote.
4. Sikukuu zitumiwe kwa kusudi halisi na siyo makusudi bandia.
5. Watoto walindwe wasiingie katika uharibifu unaoitwa starehe.
EXAUD JOHN MAKIYAO
+255784347001
makyaoexaud@yahoo.com