Tafsiri ya Mwongozo wa Spika kuhusu hoja ya Kumwondoa Waziri Mkuu

so, Zito anaweza kufanya nini baada ya uamuzi huu wa spika?
 
Nimemwangalia anavoongea tu anaonekana mtu aliyehamanika, hana maana yule mama,watu wa Njombe wasirudie kosa hili tena 2015 kuteletea wabunge wa sampuli hii
 
Kiranja: Huu ni sehemu ya ushahidi mkubwa kuwa Spika wa Bunge huwa hafuati kanuni katika kufanya maamuzi yake , na hivyo anapaswa na yeye kufanyiwa kazi kwa mujibu wa kanuni za bunge kifungu cha 134 ambacho hakihitaji hata saini za wabunge ila ni mbunge mmoja kuwasilisha taarifa hiyo na hatimaye atapigiwa kura na theluthi mbili ya wabunge.

Nafikiri, kuna haja sasa kwa wananchi wetu kila mmoja akawa anawaelewesha kuhusiana na kanuni na sheria mbalimbali ili pindi wanapopotosha basi wakutane na wananchi ambao wanaelewa
Kiranja, asante sana kwa mnyumbulisho wako uliosimama wima. Mimi nipo hapo nilipo paonyesha

Ukigundua kuwa nyoka amejificha nyuma ya jiwe, basi anza kuondoa jiwe kwanza ili ukabiliane naye vizuri.
Mama Makinda ni 'adui' mkubwa wa maendeleo na taifa hili. Anajitahidi kulinda ubadharifu ulioshindwa kulindwa na CAG na kamati zote. Huyu kwa lugha za fasihi kwingineko anaweza kuitwa 'puppet'.

Kuna umhimu wa kumshughulikia haraka sana kwa manufaa ya nchi.
Ningeomba wabunge waaze naye kwanza kabla ya kufikiria hoja za mawaziri au PM.

Umasikini wa nchi inayoporwa kila kukicha hautaisha akina Makinda wakiwa wamevaa majoho.
Huyu ni Spika wa kiwango kisichoandikika katika historia ya bunge letu.
Mtu anyetetea uhalifu hatuwezi kumtenga na uhalifu.

Ashughulikiwe kwanza
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom