Tafadhar soma hapa, mchango wako wa mawazo wahitajika.

BIF

Member
Aug 2, 2012
47
10
Ebana mi naomba mnipe mawazo juu ya ili swala la interview kufanyika kwa lugha ya kigeni(English) Wote tunajua fika Watanzania walio wengi icho kizungu ni cha kubabaisha babaisha na hii ni kutokana na mfumo wetu wa Elimu ulivyo, wengi wetu tumepitia kwenye izi shule za wakina "kayumba" na Sec vilevile tulikua tunaongoza kuvaa lile bango la Swahili speaker.Uwa nalitafakali hili alafu nashindwa pata jibu ina maana kigezo hasa cha kujua kua uyu mtu yupo sawa kwenye hii fani flan ni icho kizungu?.Twende kwenye ivi vyuo vyetu vikuu, wanafunzi walio wengi iicho kimombo hawakijui ipasavyo kama wabisha nenda kafanye Analysis chuo chochote kile utakuja kubaliana na mimi, sasa kama ni ivi kuna aja gani hasa ya kuwafanyia watu interview kwa lugha ya kigeni? na kama kuna ulazima basi huu mfumo tulionao sasa ubadilishwe watu wawe wanatumia kizungu toka vidudu(chekechea) na kuendelea sio mara shule ya msingi kiswahili tupu Sec kingereza.Kwa matazamo wangu wapo watu wazuri wenye sifa na uwezo wa kufanya makubwa katika Nchi hii lakini walishindwa shule (kufaulu)huko masekondari kwasababu ya Lugha, unajua swala la kuklemu si la mchezo nakumbuka wakati nipo "O level" mambo yalikua mazito mtu unashinda ukiimba definition ya History na masomo mengine, ebana huku ni kama kutesa wanafunzi wa kitanzania na ndo matokeo yake tunapata makanjanja kwenye kila kona kwasababu wengine waliibia ibia tu kwenye mitihani.Wengi wanashindwa majalibio kwasababu ya lugha kujieleza kwa kizungu shida tupu ila mwambie kwa kiswahili atajieleza mpaka kesho.Sijui wenzangu mnalionaje ili?
 
1. si elewi kabisa kuna sababu gani ya kuendelea kufundisha kiswahili mashuleni wakati mahitaji ni lugha ya english
2. kwa nini wanatutesa kupata kazi kwa kigezo cha kutojua ung'eng'e
3. napata shida kuamini kwamba yeyote anayejua ung'eng'e ndio mchakazi na anajua kazi
4. sie tunajifunza lugha yao kwa kukariri na kwa lazima je wao wanafanya hivyo
5. af tunatabia ya kusifia vya wenzetu na kukashifu vya kwetu mfano mzuri ni humu humu jf kama unabisha fanya hata leo hili zoezi andika kwa kiswahili ukosee maneno karibu yote hakuna mtu yeyote atayejitokeza akwambie umekosa sasa andika kwa kizungu af ukosee utapata majibu ya ajabu ivi kwa nini hatupendi vya kwetu?
 
1. si elewi kabisa kuna sababu gani ya kuendelea kufundisha kiswahili mashuleni wakati mahitaji ni lugha ya english
2. kwa nini wanatutesa kupata kazi kwa kigezo cha kutojua ung'eng'e
3. napata shida kuamini kwamba yeyote anayejua ung'eng'e ndio mchakazi na anajua kazi
4. sie tunajifunza lugha yao kwa kukariri na kwa lazima je wao wanafanya hivyo
5. af tunatabia ya kusifia vya wenzetu na kukashifu vya kwetu mfano mzuri ni humu humu jf kama unabisha fanya hata leo hili zoezi andika kwa kiswahili ukosee maneno karibu yote hakuna mtu yeyote atayejitokeza akwambie umekosa sasa andika kwa kizungu af ukosee utapata majibu ya ajabu ivi kwa nini hatupendi vya kwetu?

Ki English ni tatizo kubwa itabidi tuamue moja.
 
ndugu yang n kero ya weng bt hata 2meshaulizana sana imekuwa kzngmkuti yan nalo labda kwe kura za maon katba mpya
 
Mkuu unachosema ni ukweli mtupu. Wenzetu wenye lugha hawashindwi usail, wanashindwa kuelewana kwenye mshahara. Huu mfumo ni mbaya sana, cha msingi mimi na wewe tujifunge ili tuwasomeshe watoto wetu ili waweze kupambana na hili soko linaloongozwa na Lugha ya Kiingereza.
 
halafu kuna changamoto cku hizi wanatuweka kwenye soko la ajira la afrika mashariki wakati inajulikana fika kua nchi zote za afrika mashariki zko fiti kwenye lugha ukiondoa bongo.hawa jamaa watatuonea sana.
 
halafu kuna changamoto cku hizi wanatuweka kwenye soko la ajira la afrika mashariki wakati inajulikana fika kua nchi zote za afrika mashariki zko fiti kwenye lugha ukiondoa bongo.hawa jamaa watatuonea sana.

Unajua nini, hii Nchi kuna viongozi ambao awastahili kuwa viongozi kwa kua wao watoto wao wanasoma uko maulaya hawahangaiki na wananchi maskini,yani ni wabinafsi sana hawa viongozi wetu.Nilishawahi kumsikia Prof mmoja wa chuo kikuu cha Dsm akisema kuwa walishafanya mchakato wa kubadili silabasi za masomo yote ya Sec kuwa ktk kiswahili na walishaanza kutafasili baadhi ya masomo kua kwa kiswahili lkn uabaishaji wizara ya Elimu ndo unakwamisha haya pia nilishawahi kusoma hisoria ya mwalimu mmoja raia wa uingereza alisema yeye amejifunza kiswahili toka yupo kwao na alikipenda sana alipo pata nafasi ya kuja TZ akajifunza zaidi na sasa ni mwalimu wa Kiswahili na akasema ili mwanafunzi akuelewe vzr ni lazima umfundishe kwa lugha anayoilewa.Sasa mi naishangaa hi Nchi tutaendelea kuyumbayumba mpaka lini jamani.
 
Karibu wote mmenena sawasawa, nilishawahi kufanyiwa interview na Mkenya, uzuri alitumia lugha mbili kama nilivyoandika kwenye CV, yaani kiswahili na kiingereza. Sasa pale alipoona nashindwa kumuelewa katika kiingereza akanitelemshia kiswahili vizuri sana na nilimjibu vizuri sana kiasi kwamba tulielewana vizuri sana mpaka unafuu wa kwenye mawasiliano ulipendeza.

Tatizo sisi wengi wetu tumefundishwa kukariri kujua kiingereza tu kuliko kujua jinsi ya kufanya kazi, na jinsi ya kuwa mfanyakazi kamili na utakavyotoa mchango wako ukiwa kama mwajiriwa wa kampuni husika, kwa njia hiyo naamini kabisa mtu atakuwa mfanyakazi bora mwenye mchango mzuri kwake yeye binafsi, kwa ofisi anayofanyia kazi, taifa lake na duniani kwa ujumla.

Ni hayo tu!
 
Wewe jipange tu ukafanye interview kwa kiingereza maana ndo lugha ya wawekezaji na kama unavojua sasa hivi mpaka ardhi yetu tumewapa wageni so hata mkulima siku za usoni itatakiwa ajue kiingereza ili aweze kupata kibarua kwa mwekezaji wa kilimo cha mahindi
 
Back
Top Bottom