Samawia
JF-Expert Member
- Dec 6, 2017
- 594
- 458
Inawezekana vipi sms ikajituma kwa mtu kupitia simu yako pasipo wewe kuandika hiyo sms?
Iko hivi baada ya kuhisi nasalitiwa na Nanii ikabidi nichukue simu yake kwa ajili ya kufanya uchunguzi,nimekaa na simu siku mbili nikisubiri kupigiwa au kutumiwa ujumbe,usiku nimetulia simu ikiwa pembeni sms imeingia na namba ni ileile ninayoichunguza
Wakati nafungua simu nisome sms iliyoingia nimeona kuna sms nyingine ambayo sijaiandika mimi ila imejituma kwa huyo mtu,kwahiyo huyo mtu katuma sms akijibu ile sms iliyojituma kwake.
Nimejiuliza maswali kibao nimekosa majibu, nimewaza inawezekana mwenye simu kamwambia mtu wake kwamba simu yake inachunguzwa halafu mtu wake kafanya utundu ionekane mimi nimetuma sms kwake,baada ya kujiuliza hayo na kukosa majibu nimeona nije kwenu huenda mkawa na mnajua lolote.
Nipeni elimu tafadhali.
Iko hivi baada ya kuhisi nasalitiwa na Nanii ikabidi nichukue simu yake kwa ajili ya kufanya uchunguzi,nimekaa na simu siku mbili nikisubiri kupigiwa au kutumiwa ujumbe,usiku nimetulia simu ikiwa pembeni sms imeingia na namba ni ileile ninayoichunguza
Wakati nafungua simu nisome sms iliyoingia nimeona kuna sms nyingine ambayo sijaiandika mimi ila imejituma kwa huyo mtu,kwahiyo huyo mtu katuma sms akijibu ile sms iliyojituma kwake.
Nimejiuliza maswali kibao nimekosa majibu, nimewaza inawezekana mwenye simu kamwambia mtu wake kwamba simu yake inachunguzwa halafu mtu wake kafanya utundu ionekane mimi nimetuma sms kwake,baada ya kujiuliza hayo na kukosa majibu nimeona nije kwenu huenda mkawa na mnajua lolote.
Nipeni elimu tafadhali.