Tafadhali naomba ushauri wako

Edson Carrington

JF-Expert Member
Oct 30, 2022
216
634
Habari wakuu

Mimi ni mwanafunzi wa chuo, mwaka wa pili hapa Dar es salaam na ninasomea shahada ya teknolojia ya habari( information Technology) na pia ni loan beneficiary ( mnufaika wa mkopo).

Ninaishi na mzazi wangu mmoja wa kike yaani mama yangu na mdogo wangu, japokuwa kwa sasa nipo mbali nao kidogo kutokana na masomo yangu hivyo nimeamia sehemu nyingine.

Mazingira ya kiuchumi sio mazuri sana nyumbani, kwani mama hana kazi na pia mdogo wangu mdogo anasoma ( darasa la nne), hivyo basi baadhi ya vitu kama msosi, kodi na pesa za hapa na pale zinakuwa changamoto nyumbani.

Sasa mara nyingi huwa boom langu naligawa kwa familia na pia mimi mwenyewe huwa linatakiwa kunikidhi kitu ambacho inakuwa ni changamoto kwani pesa haitoshi.

Sasa kwa huu mwaka wa pili nahitaji baadhi ya vitu mimi kama mwanafunzi kama laptop kwani ni muhimu kwa masomo yangu ya IT na pia kununua simu maana hii simu ninayoitumia imeingia ubovu wa kujizima.

Lakini Changamoto inakuja nafikiria kuhusu hali ya nyumbani ngumu natamani hata nifungue angalau kaduka cha kujiingizia kipato kisaidie nyumbani lakini bado inakuwa changamoto nikifkiria mahitaji yangu binafsi.

Naumia kichwa sana maana nyumbani wahitaji msaada na inaniuma nikipigiwa simu wakiniambia wana njaa lakini pia na mimi nina mahitaji yangu ya muhimu kwa hiyo nashindwa hata kufanya maamuzi.

Tafadhali kwa mwenye ushauri au aliewahi kupitia changamoto kama yangu na akachomoka naomba msaada ndugu zangu kwani naona kama ni mtihani.

Asante.
 
Pole kijana hata sisi Enzi hizo tulijisomesha huku tunahudumia home. Kama mama sio mlemavu, nashauri muulize aina ya biashara anaweza fanya ili kujikimu.. Maana kutoa hela kila siku alafu huingizi ndio shidaaa, biashara za wamama sziko nyingi, kama ya vitafunwa.. Mama lishe nk. Angalia ktk boom lako kiasi gani unaweza toa kama mtaji alafu umwambie apange nini cha kufanya kwa mtaji husika ili nawe usonge mbele kimaisha na masomo. Bila hivyo ujiandae maisha kukushinda... 😁
 
Pole kijana hata sisi Enzi hizo tulijisomesha huku tunahudumia home. Kama mama sio mlemavu, nashauri muulize aina ya biashara anaweza fanya ili kujikimu.. Maana kutoa hela kila siku alafu huingizi ndio shidaaa, biashara za wamama sziko nyingi, kama ya vitafunwa.. Mama lishe nk. Angalia ktk boom lako kiasi gani unaweza toa kama mtaji alafu umwambie apange nini cha kufanya kwa mtaji husika ili nawe usonge mbele kimaisha na masomo. Bila hivyo ujiandae maisha kukushinda...
Shukrani mkuu
 
Pole sana kwa unayoyapitia kijana naamini ni suala la mda tu kila kitu kitakua sawa... naomba nikushauri ila unisamehe kama nitakua na maneno magumu ya kumuumiza
Iko hivi, wewe hapo na kwa umri wako na mazingira yako uliyoeleza hapa, jukumu la kulea familia sio lako ( I mean umejibebesha mzigo)... em fanya assumptions usingekua na boom ina maana nyumbani wasingekua wanakula??
Kwa mimi ninavyoona huu ni wakati wako wa ku focus zaidi kwenye masomo yako na kupambania ndoto zako kwanza kwa hicho kipato chako kidogo ulichonacho., cause I don't think kama unaweza ukatimiza malengo na ndoto zako ukiwa umejibebesha mzigo hivyo wa majukumu ambayo naweza kusema hayakuhusu..kwanza unaweza ukapata sonona na ukafeli hata huko chuoni.
Cha kufanya ni hiki, kaa chini na mzazi wako umuelekeze kwa upole kabisa, kama anataka muendelee kua na maisha magumu basi aendelee kukuomba hizo hela, lakini kama anataka mfanikiwe basi akuache kwanza yeye atafute namna nyingine anayoweza akapata hivyo vihela vya kula na mahitaji mengine madogomadogo... wewe kwenye hiyo hela ya boom fanya ujitimizie mahitaji yako ya msingi na nyingine kama utaweza kusave ukapata hata kimtaji ufanye hata vibiashara ukiwa hapo chuoni....
Nachomaanisha ni kwamba jisaidie kwanza wewe mwenyewe ndipo usaidie na ndugu zako
 
pole sana, back then nimewahi kupitia situation kama yako ingawa mimi mdogo wangu tu ndo alikua tegemezi kwangu [mimi ndo baba na mama kwake hadi kesho]

Chakukushauri..
Sijajua upo chuo gani ila as long as ni Dar then ni advantageous kwako, vaa uhalisia wa uanaume, kaa tuliza akili tafuta kitu cha kuweza kukuingizia kipato apoapo chuo kuna pesa za kutosha hasa kwa hao watoto wa mama (wakishua).
Wafanyie individual assignments, research, wafulie, uza bites kama bablish, cookies, ubuyu, karanga n.k. muda wa kujisomea darasani na kwenye vimbweta, nunua printer ndogo uwe unaprint kazi usiku muda stationery zimefungwa utakula pesa nyingi za zimamoto.

Binafsi nilikua dalali ila kwa mwanafunzi hii sikushauri japo kuna pesa nyingi sana kwenye kudalalisha simu, laptops, vyumba vya kupangisha na vitu vingine vya ndani kama vitanda, majiko ya gesi n.k ila kulala lockup ni suala la kugusa tu unless una connection na maaskari wa kituo husika.

Usijistress wala usioverthink kuhusu maisha utaondoka kwenye msitari, Kadri unavoyachukulia maisha siriaz sana nayenyewe yanakua more than serious, unaweza ukawehuka.

Ila kama wewe ni likes za kina John Kisomo then ushauri wangu fanya kama hujauona ⚠️

Amua sasa, the rest will be history ☝️
 
Pole sana kwa unayoyapitia kijana naamini ni suala la mda tu kila kitu kitakua sawa... naomba nikushauri ila unisamehe kama nitakua na maneno magumu ya kumuumiza
Iko hivi, wewe hapo na kwa umri wako na mazingira yako uliyoeleza hapa, jukumu la kulea familia sio lako ( I mean umejibebesha mzigo)... em fanya assumptions usingekua na boom ina maana nyumbani wasingekua wanakula??
Kwa mimi ninavyoona huu ni wakati wako wa ku focus zaidi kwenye masomo yako na kupambania ndoto zako kwanza kwa hicho kipato chako kidogo ulichonacho., cause I don't think kama unaweza ukatimiza malengo na ndoto zako ukiwa umejibebesha mzigo hivyo wa majukumu ambayo naweza kusema hayakuhusu..kwanza unaweza ukapata sonona na ukafeli hata huko chuoni.
Cha kufanya ni hiki, kaa chini na mzazi wako umuelekeze kwa upole kabisa, kama anataka muendelee kua na maisha magumu basi aendelee kukuomba hizo hela, lakini kama anataka mfanikiwe basi akuache kwanza yeye atafute namna nyingine anayoweza akapata hivyo vihela vya kula na mahitaji mengine madogomadogo... wewe kwenye hiyo hela ya boom fanya ujitimizie mahitaji yako ya msingi na nyingine kama utaweza kusave ukapata hata kimtaji ufanye hata vibiashara ukiwa hapo chuoni....
Nachomaanisha ni kwamba jisaidie kwanza wewe mwenyewe ndipo usaidie na ndugu zako
Bless sana kaka, nashukuru sana
 
pole sana, back then nimewahi kupitia situation kama yako ingawa mimi mdogo wangu tu ndo alikua tegemezi kwangu [mimi ndo baba na mama kwake hadi kesho]

Chakukushauri..
Sijajua upo chuo gani ila as long as ni Dar then ni advantageous kwako, vaa uhalisia wa uanaume, kaa tuliza akili tafuta kitu cha kuweza kukuingizia kipato apoapo chuo kuna pesa za kutosha hasa kwa hao watoto wa mama (wakishua).
Wafanyie individual assignments, research, wafulie, uza bites kama bablish, cookies, ubuyu, karanga n.k. muda wa kujisomea darasani na kwenye vimbweta, nunua printer ndogo uwe unaprint kazi usiku muda stationery zimefungwa utakula pesa nyingi za zimamoto.

Binafsi nilikua dalali ila kwa mwanafunzi hii sikushauri japo kuna pesa nyingi sana kwenye kudalalisha simu, laptops, vyumba vya kupangisha na vitu vingine vya ndani kama vitanda, majiko ya gesi n.k ila kulala lockup ni suala la kugusa tu unless una connection na maaskari wa kituo husika.

Usijistress wala usioverthink utaondoka kwenye msitari, Kadri unavoyachukulia maisha siriaz sana nayenyewe yanakua more than serious, unaweza ukawehuka.

Ila kama wewe ni likes za kina John Kisomo then ushauri wangu fanya kama hujauona

Amua sasa, the rest will be history
Blessed sana Our King, mdogo wako nimekuelewa na ntafanyia kazi
 
Mama inabidi ajifunze biashara ndogo ndogo! Mpatie hata 60,000/= afungue hata biashara ya mboga mboga,Na nikuulize kabla ya boom mliishi vipi?
 
Ungetuelezea back ground ya nyuma sawa upo na mama na mdogo wako na hali ya maisha nyumbani si nzuri swali hali hii ya maisha nyumbani mama na mdogo wako imejitokeza tu baada ya jambo furani kwenye familia kutokea yani pengine kuna mtu au kitu mlikitegemea hakipo tena hivyo mzigo umekuangukia wewe kwa sasa au mama alipoteza ajira au mtaji au maradhi yamemkuta nk

Kwanini nasema hivi ikiwa tangu wewe unasoma mama aliishi maisha ya kuomba omba tu hakujishughulisha na jambo lolote la kumuingizia kipato watu hawa kufanya shughuli ya kipato huwa ngumu sana hawamini katika kukaa na kupata buku na kutumia mia tano na kutunza mia tano wakati anaweza akaomba akapata elfu tano akaitumia ikaisha kesho akaomba tena, maana kuomba omba huwa ni kama ugonjwa hivyo angalia hilo kwanza

Tunaishi na jamii zetu kuna familia zipo eneo zuri la biashara mfano warabu wengi mijini hawataki kufanya kazi wao nikuomba tu kwa ndugu zao uko uarabuni au hapa haoa bongo kwa mwarabu mwezie anayejituma yani ni kuomba omba tu some times wanaishi maisha magumu kisa tu wanayemtegemea awape pesa ajatuma, mtu anatumiwa gari mpaka pesa ya mafuta anaomba uarabuni ni mazoea shule hawataki kwa sababu wana uhakika wa kula, kuvaa kwa kuomba omba sometimes wanashindia chai tu pesa hawana ila siku zikitumwa hayo mapishi yake acha


Nini nachotaka kusema kama mama ajazoea jishugulisha huo mtaji unaoshauliwa umpe utapotea utamlaumu maana hawa waomba pesa bwana ukimpa pesa nyingi siku hiyo ndio sherehe sasa ya kunumua samaki mkubwa, kama mkristo anaenda kaanga kiti moto nk

Pole sana ila ni mapito tu wengi wamepita hayo mapito sasa imebaki story, kinachoumizaga sana unakomaa hivi na mzazi ile time umejipata sasa unaitaji mzazi ale bata, hawa wazazi wetu wanakuwaga hawapo sijui kuna siri ipi mungu kaiweka
 
Ni. Kweli unawapenda Sana ndugu zako ni Jambo jema Sana .

Ila Mwambie Mama na Mdogo wako wajaribu kuwaza Biashara au kilimo Kama wapo kijijini ili ukimpa hata 100k iwe kianzio au start up katika kupambana na changamoto za Maisha.


Boom now ni 600k unaweza mpatia Mama 100k ili aweze kuanza kukitafuta katika Maisha .


Ila kubwa la muhimu mtegemee Sana Mungu kuwa mtu wa ibada Sana maana hapo katika Mungu ndipo lilipo tegemeo letu Usiache kusali Usiku na mchana hakikisha unamwabia na Mama abadilike awe Mtu wa ibada Sana kanisani awe anajulikana kukaa mbali na Mungu kutaichelesha Familia yenu.
 
Blessed sana Our King, mdogo wako nimekuelewa na ntafanyia kazi
cha kuongezea, unaweza kutafuta leseni then tafuta bajaji au pikipiki [day worker au ya mkataba] uwe unapiga kazi usiku kulingana na mazingira yako ya uanafunzi. Paki maeneo ya kumbi za starehe kama ni pikipiki and make sure unawapa namba zako za simu, kwa bajaji vizia abiria wanaoenda stendi ya magufuli kukikucha hukosi 30k.

Mwisho kabisa mtangulize MUNGU, don't underestimate the power of prayers, yeye ndo kila kitu.

Goodluck 🤝
 
Mama inabidi ajifunze biashara ndogo ndogo! Mpatie hata 60,000/= afungue hata biashara ya mboga mboga,Na nikuulize kabla ya boom mliishi vipi?
Kabla ya kujiunga na chuo, nilikuwa najishughulisha na shughuli ya kuuza mikate ambayo kidogo ilikuwa kama msaada pale nyumbani.
Pindi nilipojiunga na chuo kwa mwaka wa kwanza kiukweli nilihitaji kusoma sana na kujikita zaidi na masomo hivyo ikapelekea kuacha biashara hiyo na kufanya michakato ya kitabu chuoni, na hapo ndo shida ilipoanzia.
Maisha yetu hatukuwahi kuishi na baba, kwani yupo lakini hana kitu na pia hana msaada na sisi.
 
Kabla ya kujiunga na chuo, nilikuwa najishughulisha na shughuli ya kuuza mikate ambayo kidogo ilikuwa kama msaada pale nyumbani.
Pindi nilipojiunga na chuo kwa mwaka wa kwanza kiukweli nilihitaji kusoma sana na kujikita zaidi na masomo hivyo ikapelekea kuacha biashara hiyo na kufanya michakato ya kitabu chuoni, na hapo ndo shida ilipoanzia.
Maisha yetu hatukuwahi kuishi na baba, kwani yupo lakini hana kitu na pia hana msaada na sisi.

Hio shughuli ya kuuza mikate, mama yako hawezi kuifanya?

Yano bado hujaeleweka, nini kinachomfanya mama yako asifanye kaze akutegemee wewe mtoto?
 
Back
Top Bottom