Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 9,232
- 6,363
Anahutubia kama msaliti wa chama chake, kwa kifupi, huyu Professor sasa ni official kuwa kafirisika kisiasa kama nduguye Zitto maana wananunuliwa na CCM huku wakidanganya wananchi kuwa wao ni wapinzani kumbe hamna kitu, ni magarasa tu kama wanaume wa Dar.Hili ni swali ambalo Wajuzi wa Protokali mnatakiwa mtueleze ili sisi wengine tuelewe.
Rais Samia , ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, yuko kwenye ziara ya kikazi huko Tabora, akizindua miradi mbalimbali na kutembelea Ofisi na Matawi ya CCM, sasa kwenye ziara hiyo ameambatana na Ndugu Haruna Lipumba, ambaye ni Mwenyekiti wa Chama kilichokufa cha CUF, na cha kushangaza zaidi Lipumba anapewa nafasi ya kuhutubia Wananchi, na kufanya Kampeni za Urais wa Samia 2025, ambaye hata Chama chake hakijampitisha.
Ikumbukwe kwamba hatuna shida yoyote kwa Haruna Lipumba kuhutubia, bali tunachouliza ni hiki. JE. KWENYE ZIARA HIYO LIPUMBA ANAHUTUBIA KAMA NANI?