Taarifa za mikopo midogo midogo ya kibiashara!

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,599
Naomba wadau wa jukwaa hili tusaidiane kuweka taarifa muhimu za kibenki ili ziwasaidie wadau wanaohitaji mikopo midogo midogo na ile ya kati kwa ajili kuendesha biashara. Natamani tungekuwa na business directory ila sijui kama ipo ....(wenye taarifa watatusaidia).

Nimeweza kukusanya hizi taarifa na naomba wadau muongeze kile mnachokijua,

1. CRDB Bank Ltd...Mikopo midogo midogo (may be 1-20 mil), interest rate (with insurance) ni 20%, na lazima mtu awe na hati ya kiwanja au nyumba

2. FINCA .....Nimepata taarifa kuwa mtu akikopa 15mil anatakiwa kurudisha 1.7mil kwa mwezi ambayo inatupa interest ya 33.3%

3. NBM.....Kuna mtu kachukua loan ya 30mil ambayo atailipa kwa miaka 4; interest + other charges imefikia 12mil (40%)
........Nimepata taarifa za NMB kwamba small loans (100K-5mil) interest rates in 24% (2% per month)

4. TIB (Tanzania investment Bank)...Wanatoa mikopo ya kati na mikubwa...Nasikia wanaanzia USD 150K

5. SACCOS...SACCOS ambayo mie ni mwanachama inatoza 13% ila wanatoa pesa ndogo ndogo (1-10mil) na lazima ukae kwenye queue kwa karibu miezi 6!

7. NBC...Wanatoa mikopo kwa riba ya 20-24% ila iko based on overdraft. Unatakiwa kuwa na hati ya nyumba au dhamana nyingine. Kwa ujumla nimependa package yao ingawa riba bado iko juu sana!!

8. Exim wanatoa mikopo ya biashara kwa riba ya 19%. Unaweza kuchukua zote au kwa overdraft!!

9. Barclays bank wanatoa mikopo ya kati na mikubwa tu (>50mil). Interest yao ni 25%.

10. Stanbic wanatoa mikopo ya biashara pia...interest rates zao ni 21% na matakwa mengine ni kama kwa banks nyingine (hati ya nyumba, leseni ya biashara, audited accounts etc)!! Hawa nao wanatoa overdraft facilities!

11. Kenya Commercial Bank (KBC)....wana mikopo ya biashara kuwanzia 10mil na interest rates zao ni 19%. Masharti mengine ni kama banks nyingine na wanakubali overdraft..Ila sikuweza kupata details za interest rates per month kwenye overdraft!

12. Equity Bank....Inasemekana watakuwa na masharti nafuu ila bado hawajaanza kufanya biashara rasmi. Tutazidi kuwafuatilia!


Mwenye taarifa zaidi atuwekee hapa ili tuweza ku-update hii page ili iwasadie wale wanaohitaji mikopo ili wajikwamue!

Babu DC!!

Updates

Important information (TIB)

TIB wana mikopo ya investments zote zinazohusika na kilimo kwenye agricultural financing window ambayo ina masharti nafuu sn hd 1billion na riba yake ni 5% pa. Tena wana grace period kutegemea nature ya mradi au mazao husika. Security yake nayo sio km bank zingine kwani kuna watu wamepata ht kwa kuwa na Shamba lenye hati ya kimila tu.

Kuna financial leasing ambayo ni ya mitambo pia nayo inahitaji equity ya 40% kwa mradi mpya na 20% unaoendelea. Hii riba yake ni negotiable kati ya 8-15% na kuna grace period hii ni kwa miradi na investments aina zote na wanatoa hd 30billion Tshs.

Kama Una investments uliyoianalyze vizuri na ukiweza kuwaconvince hii ni better than any other bank in Tz.

quote_icon.png
By Mzuzu

TIB Wana dirisha maalum la kilimo ambalo linatumia pesa ya ruzuku ya serikali na riba yake ni 5% na kuna mikopo ya biashara nyingine zote ambazo riba yake ni negotiable kuanzia 8% hadi 15%

Equity Bank

nimeweza ku confirm location zao, Equity bank kwa dar wapo quality centre (pugu road) na nyingine posta wapo PSPF plaza karibu na ppf. Ni bank nzuri sana kwa mikopo ya wafanyabiashara wadogo na wakulima, niliongea muda mrefu sana na wafanyakazi wao na kweli niliwakubali.
Target yao ni watu wa kipato cha chini hata kama una biashara ya maandazi watakuthamini
 
Babu ahsante kwa taarifa ila hizo riba..... Mmmh!

Hus,

Yaani hata sielewi kwa nini riba ni kubwa kiasi hicho...Ila taasisi nyingi zinatumiwa mwanya wa kutokuwepa comparative figures kati ya taasisis mbali mbali kuwaibia wananchi.

Bado nafuatilia ila kuna baadhi ya taasisi zinatoza hadi riba ya 50%

Babu DC
 
Interest ilivyokubwa inakatisha tamaa. Una uhakika gani wa uzalishaji iwapo bado biashara hujaianza na kujua mwelekeo wake?

Mkuu,

Huwezi kwenda kukopa pesa katika mazingira yetu ili kufinance biashara ya kufikirika!! Ndiyo maana taasisi nyingi zinataka kuona kama mwombaji ana biashara inayoendelea na inategeneza faida.

Tatizo ni kwamba hawa wenye fedha wanatumia ujinga wetu na pia kutokuwa na choices kutuibia.

Hata SACCOS nazo zina riba kubwa sanai!
 
Hus,

Yaani hata sielewi kwa nini riba ni kubwa kiasi hicho...Ila taasisi nyingi zinatumiwa mwanya wa kutokuwepa comparative figures kati ya taasisis mbali mbali kuwaibia wananchi.

Bado nafuatilia ila kuna baadhi ya taasisi zinatoza hadi riba ya 50%

Babu DC

kwa mwendo huo personal financing ndio best solution babu ingawa sijui tutadunduliza mpaka lini hadi kibubu kijae. Lol.
 
SACCOS nazo zinaweza kuwa ni sehemu nzuri ya kukopa ila bado wana riba kuwa pia.

SACCOS ya mahali ninapofanyakazi, ikikopesha 1mil kwa mwaka wanatoza interest ya 3% kwa mwezi na jumla ya marejesho ni 1.13mil (interest ni 13%). Najua kuna inflation kubwa kwa sasa ila hizi riba zimekuwa hivi hata kabla serikali haijachakachua uchumi!!
 
kwa mwendo huo personal financing ndio best solution babu ingawa sijui tutadunduliza mpaka lini hadi kibubu kijae. Lol.

Hus,

Personal financing ni suicide...Ndiyo maana watu wanatake risk na kuingia kwenye ufisadi...Tungekuwa na taasisi za fedha zinazotoza riba zinazolipika, watu wengine (tena wengi) wangekimbilia huko kuchukua pesa kihalali.

Tusaidiane ili tupate taasisi ambazo ni fair tutakope. Usithubutu hata siku moja kutegemea kipato chako kukuza mtaji....You will need more than 200 yrs to make it....Utafika huko??


Babu DC!!
 
Mkuu,

Huwezi kwenda kukopa pesa katika mazingira yetu ili kufinance biashara ya kufikirika!! Ndiyo maana taasisi nyingi zinataka kuona kama mwombaji ana biashara inayoendelea na inategeneza faida.

Tatizo ni kwamba hawa wenye fedha wanatumia ujinga wetu na pia kutokuwa na choices kutuibia.

Hata SACCOS nazo zina riba kubwa sanai!

Najua fika kama ulivyoeleza anayeanzisha biashara huwa amefanya tathmini ya kutosha na kujiridhisha kwamba atapata faida na biashara itasimama.

Hata hivyo si hakika kama mafanikio yatafikiwa kama business plan ilivyo, maana kuna mengi yanahitajika kuweka sawa ili biashara isimame na enzi hizi za ushindani wa kibiashara na ubora wa bidhaa na huduma. Na hadi biashara isimame kwa haraka ni miezi 6 na pengine huchukua hadi miaka miwili.

Kiwango cha riba bila uficho kiko juu mno na kabisa kwa nchi maskini kama Tanzania. Nashangaa nchi tajiri riba inazidi kuwa chini kila kuikicha wakati nchi maskini ndio wanapandisha riba kama hawatumii akili vile.

Mikopo mingi ya bongo ni kati ya mwaka mmoja na miaka mitano, lakini riba ni juu sana kana kwamba ni mkopo wa miaka zaidi ya 30. Riba ingekuwa walao 12% ingekuwa fair hata hivyo ni bado juu kutosha lakini hii mnayotaja inatisha. Utakachochuma unachumia bank tu usipokuwa mwangalifu hata mtaji utaishia kwao.
 
SACCOS nazo zinaweza kuwa ni sehemu nzuri ya kukopa ila bado wana riba kuwa pia.

SACCOS ya mahali ninapofanyakazi, ikikopesha 1mil kwa mwaka wanatoza interest ya 3% kwa mwezi na jumla ya marejesho ni 1.13mil (interest ni 13%). Najua kuna inflation kubwa kwa sasa ila hizi riba zimekuwa hivi hata kabla serikali haijachakachua uchumi!!


Hii ya SACCOS ni afadhali kidogo kuliko mabenki, mfanyabiashara anaweza kuendesha biashara na atakapomaliza atabakiwa na mtaji wa kuendeshea biashara yake, lakini ya mabenk ni ya kumfilisi mfanyabiashara.
 
Najua fika kama ulivyoeleza anayeanzisha biashara huwa amefanya tathmini ya kutosha na kujiridhisha kwamba atapata faida na biashara itasimama.

Hata hivyo si hakika kama mafanikio yatafikiwa kama business plan ilivyo, maana kuna mengi yanahitajika kuweka sawa ili biashara isimame na enzi hizi za ushindani wa kibiashara na ubora wa bidhaa na huduma. Na hadi biashara isimame kwa haraka ni miezi 6 na pengine huchukua hadi miaka miwili.

Kiwango cha riba bila uficho kiko juu mno na kabisa kwa nchi maskini kama Tanzania. Nashangaa nchi tajiri riba inazidi kuwa chini kila kuikicha wakati nchi maskini ndio wanapandisha riba kama hawatumii akili vile.

Mikopo mingi ya bongo ni kati ya mwaka mmoja na miaka mitano, lakini riba ni juu sana kana kwamba ni mkopo wa miaka zaidi ya 30. Riba ingekuwa walao 12% ingekuwa fair hata hivyo ni bado juu kutosha lakini hii mnayotaja inatisha. Utakachochuma unachumia bank tu usipokuwa mwangalifu hata mtaji utaishia kwao.

Ahsante sana ndugu,

Hapa ninaongelea biashara ambayo tayari inaendelea. Katika mazingira yetu, ni hatari kukopa ili kuanzisha biashara. Hiyo miezi 6 unayoongelea ni kidogo sana....Kuna biashara tulianzisha, ilituchukua karibia miezi 5 kupata vibali vyote na ziadi ya miezi 7 kupata sehemu ya kufanyia biashara. Ndiyo maana wastaafu wengi waliojaribu kuingia kwenye biashara baada ya kustaafu wameishia kufa kwa BP!!
 
Hii ya SACCOS ni afadhali kidogo kuliko mabenki, mfanyabiashara anaweza kuendesha biashara na atakapomaliza atabakiwa na mtaji wa kuendeshea biashara yake, lakini ya mabenk ni ya kumfilisi mfanyabiashara.

Ni kweli kabisa ila inategemeaa michango ya wanachama (ambao wana mishahara midogo na wengi ni kima cha chini cha mshahara, KCC) kwa hiyo uwezo wake wa kukopesha ni mdogo sana!!

Tatizo la riba kubwa na upatikanaji wa pesa ni motivation muhimu sana ya ufisadi. Ndiyo maana Sumaye aliamua kujichukulia 50mil kutoka NSSF!!
 
Hus,

Personal financing ni suicide...Ndiyo maana watu wanatake risk na kuingia kwenye ufisadi...Tungekuwa na taasisi za fedha zinazotoza riba zinazolipika, watu wengine (tena wengi) wangekimbilia huko kuchukua pesa kihalali.

Tusaidiane ili tupate taasisi ambazo ni fair tutakope. Usithubutu hata siku moja kutegemea kipato chako kukuza mtaji....You will need more than 200 yrs to make it....Utafika huko??


Babu DC!!

kweli babu, unaweza ukajikuta unazeeka bado unasave tu na pesa lenyewe linavyoshuka thamani utashangaa upo palepale. Ila Kwa sisi tunaokuza mitaji ya maandazi PF inatufaa sana. Au sio babu?
 
Asante babu kwa taarifa. Niliwahi ambiwa kuwa riba kwa unsecured loan ni kubwa sababu ya risk, hakuna mfumo wa kuwabana defaulters. Ila hayo Masharti ya CRDB si secure loan hiyo? Kwanini riba bado kubwa sana?
 
kweli babu, unaweza ukajikuta unazeeka bado unasave tu na pesa lenyewe linavyoshuka thamani utashangaa upo palepale. Ila Kwa sisi tunaokuza mitaji ya maandazi PF inatufaa sana. Au sio babu?

Mfumo wa mifuko ya mafao ya kustaafu Tanzania si mizuri kwa maana yakutoa pesa kwa mkupuo badala ya kuwalipa wastaafu kwa kiwango cha mwezi au miezi miwili hii itampa mstaafu uhakika wa kupata kidogo kila baada ya muda fulani. Hii ya kupokea kwa mkupuo pesa yote si wote wanaoweza kupanga bajeti na mikakati ya kurudufu pesa walizopata, na baada ya muda mfupi husihia maisha ya dhika isiyo kifani.
 
kweli babu, unaweza ukajikuta unazeeka bado unasave tu na pesa lenyewe linavyoshuka thamani utashangaa upo palepale. Ila Kwa sisi tunaokuza mitaji ya maandazi PF inatufaa sana. Au sio babu?

Hahahahahaha,

Hao watu wa maandazi ndio wanaibiwa sana...Hebu nenda kwenye hizi taasisi kama FINCA, PRIDE, BRACC n.k,

Nasikiwa watu wanalipa 50% na zaidi!!

Siwezi kumshauri mtu ajaribu PF!!

Tauendelee kuuliza uliza...naamini tutapata wale ambao wana unafuu!!

Babu DC!!
 
Asante babu kwa taarifa. Niliwahi ambiwa kuwa riba kwa unsecured loan ni kubwa sababu ya risk, hakuna mfumo wa kuwabana defaulters. Ila hayo Masharti ya CRDB si secure loan hiyo? Kwanini riba bado kubwa sana?

Ahsante sana ndugu,

Katika pita pita yangu, sijasikia hata sehemu moja wanakotoa unsecured loan....Kama unawajua tujuvye ili tuwatembelee.

Hiyo riba za CRDB sijui kwa nini ni kubwa wakati wana masharti mazito sana...Kwani pamoja na hati ya mali, lazima uwe na account nao ambayo inaonesha kuwa umekuwa ukiingiza na kutoa pesa!
 
Asante babu kwa taarifa. Niliwahi ambiwa kuwa riba kwa unsecured loan ni kubwa sababu ya risk, hakuna mfumo wa kuwabana defaulters. Ila hayo Masharti ya CRDB si secure loan hiyo? Kwanini riba bado kubwa sana?

Nilitembelea nchini Marekani karibuni nchi ambayo miaka michache nilikuwa nakula vitabu vyao. Kwa udadisi tu niliamua kwenda bank kuulizia wanafanyeje ukopeshaji wa pesa. Niliambiwa mkopo wa secured money ni free under one year period. Zaidi ya mwaka wanaanza charge kidogo za riba lakini haizidi 3%. Lakini bank za bongo ni mtindo mmoja tu kana kwamba unawekeza rehani ya nyumba.

NIliporudi kuwaeleza maofisa wa bank fulani (jina kapuni) waliniambia wao wakati mwingine wakakopa pesa huko majuu ndio maana riba huwa juu sana ili kufidia kotekote. Hoja hii haijaniingia vizuri katika mikopo ya mabeni kwa mabenki kimabara.
 
Nilitembelea nchini Marekani karibuni nchi ambayo miaka michache nilikuwa nakula vitabu vyao. Kwa udadisi tu niliamua kwenda bank kuulizia wanafanyeje ukopeshaji wa pesa. Niliambiwa mkopo wa secured money ni free under one year period. Zaidi ya mwaka wanaanza charge kidogo za riba lakini haizidi 3%. Lakini bank za bongo ni mtindo mmoja tu kana kwamba unawekeza rehani ya nyumba.

NIliporudi kuwaeleza maofisa wa bank fulani (jina kapuni) waliniambia wao wakati mwingine wakakopa pesa huko majuu ndio maana riba huwa juu sana ili kufidia kotekote. Hoja hii haijaniingia vizuri katika mikopo ya mabeni kwa mabenki kimabara.

Ahsante sana mkuu kwa taarifa,

Hata majirani zetu Kenya wako juu sana katika kutoa mikopo.

Hapa Tanzania, maafisa mikopo wamekaa benki na kula kiyoyozi wakisubiri watu tunaohangaika tuwafuate.

Ndiyo maana nadhani kwamba benki zetu zinaatamia pesa wakisubiri kupata vifaranga!!
 
Back
Top Bottom