Taarifa za mikopo midogo midogo ya kibiashara!

Mimi nimekuwa na wazo ambalo linaweza kuwasaidia vijana kama wengi tukifanya hivyo. Mfano kama vijana kadhaa wanataka kuanzisha kamradi kao ka ufundi chuma, nanunua mtambo wa weding na vifaa vyake na nawakopesha kisha kila mwezi warudishe kidogo kidogo kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi mitatu na interest ya 8- 12%. Nitakuwa nimewasaidia sana kuliko masharti magumu ya bank. Wengi tukifanya hivyotutakuwa tumewasaidia sana vijana na papo pesa zetu kuweka kwenye mzunguko wa faida.
 
Mimi nimekuwa na wazo ambalo linaweza kuwasaidia vijana kama wengi tukifanya hivyo. Mfano kama vijana kadhaa wanataka kuanzisha kamradi kao ka ufundi chuma, nanunua mtambo wa weding na vifaa vyake na nawakopesha kisha kila mwezi warudishe kidogo kidogo kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi mitatu na interest ya 8- 12%. Nitakuwa nimewasaidia sana kuliko masharti magumu ya bank. Wengi tukifanya hivyotutakuwa tumewasaidia sana vijana na papo pesa zetu kuweka kwenye mzunguko wa faida.

Ni wazo zuri ila uwe mwanalifu uzijedhaniwa kuwa unatafuta ubunge au udiwani...Wakipata hisia kama hizo basi tena, utakuwa umetoa sadaka!!
 
Kwa wanasiana waendelee na siasa zao maana wengine tunapendelea kubaki na heshima zetu kuliko kutemeana mate majukwaani. Unamwona Mengi anavyobaki na heshima yake, angethubutu kuingiza mkono kwenye siasa kama akina Rostam yangemkuta yanayowakuta akina Rostam

Cha msingi mtindo nilioeleza ndio wengi wa mataifa makubwa hufanya, vinginevyo kuanzisha miradi wewe mwenyewe hutajiona unatuliza kichwa, bora uwe na miradi miwili hivi midogo na kuwekeza kwa wengine papo hapo unasaidia vijana na tatizo la ajira. Kwa wanaotaka faida kubwa hapa si penyewe, lakini kwa wanaoridhika na kidogo anachopata sioni kama ni tatizo.
 
Ni kweli interests ni kubwa sana katika mabenki lakini lazima ukubali kuwa mazingira yetu ya Tanzania ni risk kukopesha watu , mfano mdogo tuu , kuna mdau kasema marekani interest rate ndogo , huwezi linganisha mazingira ya ukopeshaji ya marekani na bongo hata siku moja , wananchi wana credit reference , unaweza kujua aliishi wapi , sasa we niambie bongo unampa mil 20 unsecured loan kesho unakuja kafunga duka , sawa insurance wanalipa benki manake mikopo ipo insured lakini ndio hivyo inabidi tukubali mazingira yetu ni magumu si kwetu tu waangaikaji hata kwa hao watoaji , lakini with time mambo yatabadilika , STANBIC bank najua wanatoa unsecured loan , kariakoo pale ,nafikiri mpaka mil 30
 

Mfumo wa mifuko ya mafao ya kustaafu Tanzania si mizuri kwa maana yakutoa pesa kwa mkupuo badala ya kuwalipa wastaafu kwa kiwango cha mwezi au miezi miwili hii itampa mstaafu uhakika wa kupata kidogo kila baada ya muda fulani. Hii ya kupokea kwa mkupuo pesa yote si wote wanaoweza kupanga bajeti na mikakati ya kurudufu pesa walizopata, na baada ya muda mfupi husihia maisha ya dhika isiyo kifani.

mi naona hata hiyo ya kumlipa mstaafu kwa mwezi mwezi pia haitomkomboa. Hela itaishia kwenye chakula na matumizi madogo madogo. Nashauri wapewe fungu lao lote then wapewe trainning ya namna wataanzisha japo biashara ndogo ndogo.
 
Hahahahahaha,

Hao watu wa maandazi ndio wanaibiwa sana...Hebu nenda kwenye hizi taasisi kama FINCA, PRIDE, BRACC n.k,

Nasikiwa watu wanalipa 50% na zaidi!!

Siwezi kumshauri mtu ajaribu PF!!

Tauendelee kuuliza uliza...naamini tutapata wale ambao wana unafuu!!

Babu DC!!

babu unaidis sana PF ingawa na yenyewe ina faida zake.
 
Mimi nimekuwa na wazo ambalo linaweza kuwasaidia vijana kama wengi tukifanya hivyo. Mfano kama vijana kadhaa wanataka kuanzisha kamradi kao ka ufundi chuma, nanunua mtambo wa weding na vifaa vyake na nawakopesha kisha kila mwezi warudishe kidogo kidogo kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi mitatu na interest ya 8- 12%. Nitakuwa nimewasaidia sana kuliko masharti magumu ya bank. Wengi tukifanya hivyotutakuwa tumewasaidia sana vijana na papo pesa zetu kuweka kwenye mzunguko wa faida.

wazo zuri candid. Kwahiyo nitafute vijana wenzangu? Lol.
 
mi naona hata hiyo ya kumlipa mstaafu kwa mwezi mwezi pia haitomkomboa. Hela itaishia kwenye chakula na matumizi madogo madogo. Nashauri wapewe fungu lao lote then wapewe trainning ya namna wataanzisha japo biashara ndogo ndogo.

Amini usiamini, hii ya kupewa kwa mkupuo kwa wengi ni mbaya sana, kwani unavyoona we unaweza kurudufu pesa yako hadi utakapokufa si wote wenye uwezo na upeo huo. Hata kama watapewa mafunzo ni sawa na shule wanaokuja kufauulu ni mmoja au kushindwa wote. Mataifa yaliyoendelea yanatoa mafao hayo kwa utaratibu wa kupewa kila mwezi na hii hadi kifo kitakapomchukua, hii inamhakikishia kupata kila mwezi au kila baada ya miezi miwili.

Pato lake hilo ni msaada pia kupata mkopo kama anataka kuanzisha biashara kwa kuwa ni income ya uhakika ambayo itampa dhamana bank kupata mkopo wenye riba nafuu. Kumbuka mataifa makubwa wamefanya utafiti wa miaka mingi na wameishia kuwalipa kwa mzwei badala ya kwa mkupuo ktuokana na wengi kuishia kuwa homeless.
 
Ni kweli interests ni kubwa sana katika mabenki lakini lazima ukubali kuwa mazingira yetu ya Tanzania ni risk kukopesha watu , mfano mdogo tuu , kuna mdau kasema marekani interest rate ndogo , huwezi linganisha mazingira ya ukopeshaji ya marekani na bongo hata siku moja , wananchi wana credit reference , unaweza kujua aliishi wapi , sasa we niambie bongo unampa mil 20 unsecured loan kesho unakuja kafunga duka , sawa insurance wanalipa benki manake mikopo ipo insured lakini ndio hivyo inabidi tukubali mazingira yetu ni magumu si kwetu tu waangaikaji hata kwa hao watoaji , lakini with time mambo yatabadilika , STANBIC bank najua wanatoa unsecured loan , kariakoo pale ,nafikiri mpaka mil 30

Ahsante sana ndugu,

Nitawatembelea Stanbic bank J3 ili inione deals zao.

Suala la kutokopesheka kwa watanzania linatumika sana kama kisingizio...Ukifuatilia utakuta hata mtu anayefanya kazi mahali panapojulikana na mwenye hadhi ya kutosha hawezi kupewa hata mil5 bila kuweka dhamana kama nilivyosema kwa CRDB.

Yaani kama naweza kuweka pesa zangu kwao na wakati mwingine zinazidi 10mil ila wao hawawezi kunipa 5 mil, wanatumia kigezo gani??
 
mi naona hata hiyo ya kumlipa mstaafu kwa mwezi mwezi pia haitomkomboa. Hela itaishia kwenye chakula na matumizi madogo madogo. Nashauri wapewe fungu lao lote then wapewe trainning ya namna wataanzisha japo biashara ndogo ndogo.

Hata hiyo haiwezi kusaidia...siyo watu wote waweza kufanya biashara.

Ingekuwa bora tuanze kutoa customized services ili wale ambao wamekuwa na biashara toka wako kazini basi wapewe mtaji zaidi na mafunzo waendelee.

Ila wale wanaotamani kuanza biashara basi washauriwe kuchukua pesa kidogo kidogo na ili wafanye majaribio!
 
Amini usiamini, hii ya kupewa kwa mkupuo kwa wengi ni mbaya sana, kwani unavyoona we unaweza kurudufu pesa yako hadi utakapokufa si wote wenye uwezo na upeo huo. Hata kama watapewa mafunzo ni sawa na shule wanaokuja kufauulu ni mmoja au kushindwa wote. Mataifa yaliyoendelea yanatoa mafao hayo kwa utaratibu wa kupewa kila mwezi na hii hadi kifo kitakapomchukua, hii inamhakikishia kupata kila mwezi au kila baada ya miezi miwili.

Pato lake hilo ni msaada pia kupata mkopo kama anataka kuanzisha biashara kwa kuwa ni income ya uhakika ambayo itampa dhamana bank kupata mkopo wenye riba nafuu. Kumbuka mataifa makubwa wamefanya utafiti wa miaka mingi na wameishia kuwalipa kwa mzwei badala ya kwa mkupuo ktuokana na wengi kuishia kuwa homeless.

Nakubaliana na wewe kabisa,
 
Ni kweli interests ni kubwa sana katika mabenki lakini lazima ukubali kuwa mazingira yetu ya Tanzania ni risk kukopesha watu , mfano mdogo tuu , kuna mdau kasema marekani interest rate ndogo , huwezi linganisha mazingira ya ukopeshaji ya marekani na bongo hata siku moja , wananchi wana credit reference , unaweza kujua aliishi wapi , sasa we niambie bongo unampa mil 20 unsecured loan kesho unakuja kafunga duka , sawa insurance wanalipa benki manake mikopo ipo insured lakini ndio hivyo inabidi tukubali mazingira yetu ni magumu si kwetu tu waangaikaji hata kwa hao watoaji , lakini with time mambo yatabadilika , STANBIC bank najua wanatoa unsecured loan , kariakoo pale ,nafikiri mpaka mil 30

Nakubaliana nawe kwa hoja hiyo, hata hivyo mikopo ya bank sioni kama kuna risk kubwa wakati reheani inayowekwa kwa walio wengi ni mali isiyohamishika kama nyumba amazo hati za kumiliki wanazishikilia, sasa hapa risk iko wapi? Uchumi wa mataifa makubwa ni wa ushindani mkubwa mno kuliko kuliko mataifa maskini, hivo si vizuri kufananisha nao katika utoaji wa mikopo kwa baadhi ya miwango na utekelezaji.
 
TIB wana mikopo ya investments zote zinazohusika na kilimo kwenye agricultural financing window ambayo ina masharti nafuu sn hd 1billion na riba yake ni 5% pa. Tena wana grace period kutegemea nature ya mradi au mazao husika. Security yake nayo sio km bank zingine kwani kuna watu wamepata ht kwa kuwa na Shamba lenye hati ya kimila tu.

Kuna financial leasing ambayo ni ya mitambo pia nayo inahitaji equity ya 40% kwa mradi mpya na 20% unaoendelea. Hii riba yake ni negotiable kati ya 8-15% na kuna grace period hii ni kwa miradi na investments aina zote na wanatoa hd 30billion Tshs.

Kama Una investments uliyoianalyze vizuri na ukiweza kuwaconvince hii ni better than any other bank in Tz.
 
TIB wana mikopo ya investments zote zinazohusika na kilimo kwenye agricultural financing window ambayo ina masharti nafuu sn hd 1billion na riba yake ni 5% pa. Tena wana grace period kutegemea nature ya mradi au mazao husika. Security yake nayo sio km bank zingine kwani kuna watu wamepata ht kwa kuwa na Shamba lenye hati ya kimila tu.

Kuna financial leasing ambayo ni ya mitambo pia nayo inahitaji equity ya 40% kwa mradi mpya na 20% unaoendelea. Hii riba yake ni negotiable kati ya 8-15% na kuna grace period hii ni kwa miradi na investments aina zote na wanatoa hd 30billion Tshs.

Kama Una investments uliyoianalyze vizuri na ukiweza kuwaconvince hii ni better than any other bank in Tz.

Hiyo TIB ni kwa investors wakubwa ambao ardhi wanayomiliki ni assert kubwa isiyohamishika jambo ambalo waanzaji na wafanyabiashara wadogo si wa kiwango chao. Ndio maana unataja mabilioni.

Tunachojadili hapa ni hawa wawekezaji wadogo na wajasirimali wadogo wanaotaka kujiajiri kwa kiwango chao inaniwia vigumu kunishawishi kwamba huku TIB kuweza kuwa kimbilio lao.
 
Hiyo TIB ni kwa investors wakubwa ambao ardhi wanayomiliki ni assert kubwa isiyohamishika jambo ambalo waanzaji na wafanyabiashara wadogo si wa kiwango chao. Ndio maana unataja mabilioni.

Tunachojadili hapa ni hawa wawekezaji wadogo na wajasirimali wadogo wanaotaka kujiajiri kwa kiwango chao inaniwia vigumu kunishawishi kwamba huku TIB kuweza kuwa kimbilio lao.

Mkuu nimeongelea masharti na maximum amount ya mkopo, ina maana unaweza kupata chini ya hapo, nimeona watu waliopata 20m na wengine wamechukua trekta moja tu la 16m so anayetaka akawaone ajifunze or just ignore it coz hapa umeuliza sources na tumechangia uzoefu. Sorry km imekwenda kinyume na matarajio
 
TIB wana mikopo ya investments zote zinazohusika na kilimo kwenye agricultural financing window ambayo ina masharti nafuu sn hd 1billion na riba yake ni 5% pa. Tena wana grace period kutegemea nature ya mradi au mazao husika. Security yake nayo sio km bank zingine kwani kuna watu wamepata ht kwa kuwa na Shamba lenye hati ya kimila tu.

Kuna financial leasing ambayo ni ya mitambo pia nayo inahitaji equity ya 40% kwa mradi mpya na 20% unaoendelea. Hii riba yake ni negotiable kati ya 8-15% na kuna grace period hii ni kwa miradi na investments aina zote na wanatoa hd 30billion Tshs.

Kama Una investments uliyoianalyze vizuri na ukiweza kuwaconvince hii ni better than any other bank in Tz.

This is very useful,

Umetoa taarifa muhimu sana....Kwa idhini yako, nitaiweka kwenye post ya kwanza kabisa ili kila anayetembelea thread hii aione!

Mkuu nimeongelea masharti na maximum amount ya mkopo, ina maana unaweza kupata chini ya hapo, nimeona watu waliopata 20m na wengine wamechukua trekta moja tu la 16m so anayetaka akawaone ajifunze or just ignore it coz hapa umeuliza sources na tumechangia uzoefu. Sorry km imekwenda kinyume na matarajio

Usiwe na shanka ndugu,

Taarifa uliyotoa ni muhimu sana na ndiyo vitu tulivyokuwa tunatafuta!

Babu DC!!
 
Mkuu nimeongelea masharti na maximum amount ya mkopo, ina maana unaweza kupata chini ya hapo, nimeona watu waliopata 20m na wengine wamechukua trekta moja tu la 16m so anayetaka akawaone ajifunze or just ignore it coz hapa umeuliza sources na tumechangia uzoefu. Sorry km imekwenda kinyume na matarajio

Nimefurahi kusikia kama kiwango chao cha mikopo kinashuka hadi kuwagusa wa kiwango cha chini, sikuwa na maana ya kubeza ukweli ulioleta, ila nilitoa kauli hiyo kutokana na tamko lako la kiwango cha juu cha ukopeshaji nikaona kwa kiwango hicho kinawagusa mapapa zaidi na kuwaacha dagaa wakigaagaa bila mafsnikio.

Je hao hutoa mikopo kwa shughuli za kilimo tu au wako open kwa mikopo ya shughuli nyingine zisizohusisha kilimo?
 
Nimefurahi kusikia kama kiwango chao cha mikopo kinashuka hadi kuwagusa wa kiwango cha chini, sikuwa na maana ya kubeza ukweli ulioleta, ila nilitoa kauli hiyo kutokana na tamko lako la kiwango cha juu cha ukopeshaji nikaona kwa kiwango hicho kinawagusa mapapa zaidi na kuwaacha dagaa wakigaagaa bila mafsnikio.

Je hao hutoa mikopo kwa shughuli za kilimo tu au wako open kwa mikopo ya shughuli nyingine zisizohusisha kilimo?

Nasikia wanagusa na sehemu nyingine kama estate business, viwanda n.k!
 
Back
Top Bottom