Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imeionya Jumuiya ya Nchi za Ulaya (EU) na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania kutoiingilia kabisa mambo yake ya ndani na pia imeuponda utafiti wa kisiasa kuhusu mbio za urais wa Zanzibar mwaka 2010 uliofanywa na kampuni ya the Steadman Group kwa kuuita ni wa kitapeli.
Onyo hilo kwa EU na kupondwa kwa utafiti ulioonyesha kubashiri kukubalika kwa wagombea wa urais huku Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad na Waziri Kiongozi wa awamu ya tano Dk Mohamed Gharib Bilal wakikabana koo, limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi Hamza Hassan Juma katika mkutano wake na waandishi wa habari ofisini kwake Vuga Mjini hapa jana.
Juma alisema Zanzibar ina mamlaka yake kamili ya kikatiba na kisheria na hivyo haiongozwi kwa shinikizo la mtu au jumuiya yeyote kutoka nje au ndani ya nchi.
Alisema kampuni ya Steadman Group juni 18 mwaka huu iliiomba ofisi ya Waziri Kiongozi ifanye utafiti juu ya masuala ya kiutamaduni na kiuchumi lakini kwa makusudi wamekiuka taratibu na kufanya utafiti wa kisiasa kinyume na ombi lao la msingi.
SMZ haiongozwi kwa kumuogopa mtu au kwa shinikizo lolote,ina katiba yakae,sheria zinayosimamia masuala mbalimbali na upana mkubwa wa maendeleo ya demokrasia Alisema
Waziri huyo wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi alisisitiza kuwa SMZ ina utawala wake kamili ikiwemo pia na sheria inayosimamia uchaguzi ambayo iliyopitishwa na BLW kama chombo cha kutungia sheria.
hatuongozwi na EU wala AU,sisi ni nchi yenye kuheshimu sheria zake na kufuata utawala bora,demokrasia na kuheshimu haki za binadamu,EU wanatakiwa wafanye utafiti wa kutosha huko Pemba kabla ya kutoa shutumaAlionya
Alieleza kuwa mazingira mazima ya zoezi la uandikishaji katika daftari la kudumu la wapiga kura huko Pemba yanakwamishwa na wanasiasa wa vyanma vya upinzani wanaowachochea wafuasi wao wavunje na kukiuka sheria jambo ambalo alidai kamwe halitavumiliwa na vyombo vya serikali.
Hata hivyo amemtupia lawama nyingi Katibu Mkuu wa chama cha Wananchi CUF Maalim Seif na kumtaja kama ni mtu mmojawapo anayefanya mikutano ya hadhara ya uchochezi ili kuhatarisha amani katika kisiwa cha Pemba.
serikali haitamtazama na kumvumilia mtu yeyote ambaye ataamua kuvunja na kukiuka sheria,vitambulisho vya ukaazi vinatajwa katika sheria ya uchaguzi hivyo kila anayetaka kuandikishwa ni lazima awe na sifa ya ukaazi wa miaka mitatu mfululizoAlifafanua
Kuhusu utafiti uliofanywa na Steadman Group aliubeza na kusema ni utafiti uliojaa utapeli ambao ulikiuka maudhui yaliotajwa na wahusika wakati wakiomba kibali cha kuendesha zoezi hilo la utafiti katika visiwa vya Pemba na Unguja.
Waziri Juma alisema juni 18 mwaka huu kampuni hiyo iliwasilisha barua ikiomba kufanya utafiti juu ya masuala ya hali ya kiuchumi na kiutamaduni na siyo kutafuta kura ya maoni kuhusu mbio za urais mwaka 2010 na kuupotosha umma.
SMZ inaitaka kampuni hiyo kuomba radhi kupitia vyombo vya habari kuhusu upotoshaji wa habari uliofanyika kwamba Seif Sharif Hmad ndiye anaeyekubalika kwa nafasi ya urasi wa Zanzibar
Alisema kwa kukiuka mantiki ya ombi lao la awali katika kuendesha kwao utafiti walioukusudia ni wazi kampuni hiyo itakuwa imeidanganya serikali,ofisi ya waziri Kiongozi na kuupotosha umma.
Aidha nakala ya barua ya kampuni ya Steadman ya juni 18 mwaka huu iliyotumwa kwenda kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Kiongozi Zanzibar inaoyesha kuomba kufanya utafiti juu ya masuala ya uchumi na utamaduni ili kupata maoni ya watu na kuweza kufahamu sekta zipi wangependelea serikali ya Tanzania kuboresha.
Alipotakiwa ataje athari zilizomepatikana kutokana na matokeo ya utafiti huo alisema zimeutikisa mfumo wa siasa za zanzibar na pia kuwapotezea mwelekeo na matarajio watu wenye kui ya kuwania urais kwa kufanya utabiri wa kitapeli.
hata Naibu Katibu Mkuu wa CUF Juma Duni Haji pengine alikwa na nia ya kuwania urais ili ashindane na Seif inawezekana amekatishwa tamaa,lakini pia si msingi wa ombi la kampuni husika bali kilichofanyika ni hadaa na utapeliAliongeza
Katika hatua nyingine Waziri Juma alibainisha kuwa SMZ kamwe haitamkamata Maalim Seif Sharif Hamad na kumuweka kolokoloni licha ya kufanya kwake uchochezi wa makusudi ambao ni kosa la jinai.
Alisema Maalim Seif anachochea wafuasi wake ili wavunje sheria na kusema atazidi kufanya hivyo bila kuchoka kwa kutegemea akamatwe ili apate umaarufu wa kisiasa jambo ambao SMZ kamwe halitafanya.
hatuna mpango wa kumkamata Maalim Seif na kumfikisha kortini,yule atamalizika kidogo kidogo mpaka wananchi watampuuza,ni jamaa yetu,mwenzetu,analipwa maslahi yake na SMZ hakuna wa kumkamata na kufanya hivyo ni kumjengaAlisisitiza.
SOURCE: ZANZIBAR YETU WEB BLOG.
Onyo hilo kwa EU na kupondwa kwa utafiti ulioonyesha kubashiri kukubalika kwa wagombea wa urais huku Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad na Waziri Kiongozi wa awamu ya tano Dk Mohamed Gharib Bilal wakikabana koo, limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi Hamza Hassan Juma katika mkutano wake na waandishi wa habari ofisini kwake Vuga Mjini hapa jana.
Juma alisema Zanzibar ina mamlaka yake kamili ya kikatiba na kisheria na hivyo haiongozwi kwa shinikizo la mtu au jumuiya yeyote kutoka nje au ndani ya nchi.
Alisema kampuni ya Steadman Group juni 18 mwaka huu iliiomba ofisi ya Waziri Kiongozi ifanye utafiti juu ya masuala ya kiutamaduni na kiuchumi lakini kwa makusudi wamekiuka taratibu na kufanya utafiti wa kisiasa kinyume na ombi lao la msingi.
SMZ haiongozwi kwa kumuogopa mtu au kwa shinikizo lolote,ina katiba yakae,sheria zinayosimamia masuala mbalimbali na upana mkubwa wa maendeleo ya demokrasia Alisema
Waziri huyo wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi alisisitiza kuwa SMZ ina utawala wake kamili ikiwemo pia na sheria inayosimamia uchaguzi ambayo iliyopitishwa na BLW kama chombo cha kutungia sheria.
hatuongozwi na EU wala AU,sisi ni nchi yenye kuheshimu sheria zake na kufuata utawala bora,demokrasia na kuheshimu haki za binadamu,EU wanatakiwa wafanye utafiti wa kutosha huko Pemba kabla ya kutoa shutumaAlionya
Alieleza kuwa mazingira mazima ya zoezi la uandikishaji katika daftari la kudumu la wapiga kura huko Pemba yanakwamishwa na wanasiasa wa vyanma vya upinzani wanaowachochea wafuasi wao wavunje na kukiuka sheria jambo ambalo alidai kamwe halitavumiliwa na vyombo vya serikali.
Hata hivyo amemtupia lawama nyingi Katibu Mkuu wa chama cha Wananchi CUF Maalim Seif na kumtaja kama ni mtu mmojawapo anayefanya mikutano ya hadhara ya uchochezi ili kuhatarisha amani katika kisiwa cha Pemba.
serikali haitamtazama na kumvumilia mtu yeyote ambaye ataamua kuvunja na kukiuka sheria,vitambulisho vya ukaazi vinatajwa katika sheria ya uchaguzi hivyo kila anayetaka kuandikishwa ni lazima awe na sifa ya ukaazi wa miaka mitatu mfululizoAlifafanua
Kuhusu utafiti uliofanywa na Steadman Group aliubeza na kusema ni utafiti uliojaa utapeli ambao ulikiuka maudhui yaliotajwa na wahusika wakati wakiomba kibali cha kuendesha zoezi hilo la utafiti katika visiwa vya Pemba na Unguja.
Waziri Juma alisema juni 18 mwaka huu kampuni hiyo iliwasilisha barua ikiomba kufanya utafiti juu ya masuala ya hali ya kiuchumi na kiutamaduni na siyo kutafuta kura ya maoni kuhusu mbio za urais mwaka 2010 na kuupotosha umma.
SMZ inaitaka kampuni hiyo kuomba radhi kupitia vyombo vya habari kuhusu upotoshaji wa habari uliofanyika kwamba Seif Sharif Hmad ndiye anaeyekubalika kwa nafasi ya urasi wa Zanzibar
Alisema kwa kukiuka mantiki ya ombi lao la awali katika kuendesha kwao utafiti walioukusudia ni wazi kampuni hiyo itakuwa imeidanganya serikali,ofisi ya waziri Kiongozi na kuupotosha umma.
Aidha nakala ya barua ya kampuni ya Steadman ya juni 18 mwaka huu iliyotumwa kwenda kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Kiongozi Zanzibar inaoyesha kuomba kufanya utafiti juu ya masuala ya uchumi na utamaduni ili kupata maoni ya watu na kuweza kufahamu sekta zipi wangependelea serikali ya Tanzania kuboresha.
Alipotakiwa ataje athari zilizomepatikana kutokana na matokeo ya utafiti huo alisema zimeutikisa mfumo wa siasa za zanzibar na pia kuwapotezea mwelekeo na matarajio watu wenye kui ya kuwania urais kwa kufanya utabiri wa kitapeli.
hata Naibu Katibu Mkuu wa CUF Juma Duni Haji pengine alikwa na nia ya kuwania urais ili ashindane na Seif inawezekana amekatishwa tamaa,lakini pia si msingi wa ombi la kampuni husika bali kilichofanyika ni hadaa na utapeliAliongeza
Katika hatua nyingine Waziri Juma alibainisha kuwa SMZ kamwe haitamkamata Maalim Seif Sharif Hamad na kumuweka kolokoloni licha ya kufanya kwake uchochezi wa makusudi ambao ni kosa la jinai.
Alisema Maalim Seif anachochea wafuasi wake ili wavunje sheria na kusema atazidi kufanya hivyo bila kuchoka kwa kutegemea akamatwe ili apate umaarufu wa kisiasa jambo ambao SMZ kamwe halitafanya.
hatuna mpango wa kumkamata Maalim Seif na kumfikisha kortini,yule atamalizika kidogo kidogo mpaka wananchi watampuuza,ni jamaa yetu,mwenzetu,analipwa maslahi yake na SMZ hakuna wa kumkamata na kufanya hivyo ni kumjengaAlisisitiza.
SOURCE: ZANZIBAR YETU WEB BLOG.