Taarifa ya daktari wa rais

Cha msingi dakitari kasema mhe. hana matatizo makubwa yeyote ya kiafya ukiondoa hilo la kuwa na damu nyingi. Nashukuru kwa huduma wanazoendelea kuzitoa kwa mkuu wa nchi yetu. Hata hivyo, inabidi wamaanishe hivyo, kwamba hana matatizo makubwa zaidi ya la damu kuwa nyingi. Vinginevyo, watanzania tutakuja kuumbuka kama mengine yatatokea kwa sababu tu ya usiri uliokuwa umekumbatiwa. Isiwe suala la longolongo na usanii mkifikiri eti kuumwa ni suala geni kwa rais. Ninachoamini ni mwanadamu kama binadamu wengine. Hivyo, kuumwa si kitu kigeni. Isipokuwa kama kundi fulani ikatokea likawa na mtazamo tofauti na huu wa rais kuwa miongoni mwa wanadamu, basi ni hatari!! Namuombea tu kwa Mwenyezi Mungu azidi kumuongezea siku zake za kuishi.
 
Mhh hapa kuna tatizo, kuna haja gani ya kucheki presidaa kama ana VVU kila baada ya miezi sita????

tuangalie na upande wa pili wa shilingi, tumeambiwa rais ana takiwa kudonate damu kila baada ya miezi 6. Kwa mtu yeyote yule, kabla ya kudonate blood kuna vipimo ambavyo lazima viangaliwe na moja yapo ya hivyo ni vipimo vya VVU...
 
tuangalie na upande wa pili wa shilingi, tumeambiwa rais ana takiwa kudonate damu kila baada ya miezi 6. Kwa mtu yeyote yule, kabla ya kudonate blood kuna vipimo ambavyo lazima viangaliwe na moja yapo ya hivyo ni vipimo vya VVU...

Kama ana donate damu kila mwezi sita maana yake amepewa clean certificate ya VVU
 
tuangalie na upande wa pili wa shilingi, tumeambiwa rais ana takiwa kudonate damu kila baada ya miezi 6. Kwa mtu yeyote yule, kabla ya kudonate blood kuna vipimo ambavyo lazima viangaliwe na moja yapo ya hivyo ni vipimo vya VVU...
Nadhani hufahamu utaratibu,unapodonate blood, wanachukua damu bila kuandika jina au kuweka alama yoyote zaidi ya blood type, na damu inachekiwa separate sio pale. Hivyo ni vigumu kujua kama ana VVU kwa kudonate blood.
Pia kama Mh haja-engage in risky behaviour hamna haja ya kupima kila miezi sita VVU, kwa hiyo kwa kukiri kuwa wanampima kila miezi sita ina maana kuwa rais wetu ni mhuni, na hajikingi, which shows that he is inconsiderate and reckless. Definitely a very important point that should disqualify him from being president.

Na kwa wale wapambe wasije na mfano wa Bill Clinton, kwa sababu IQ ya Jk haimfikii hata kwa 10% Bill, so spare me the comparison.
 
Nadhani hufahamu utaratibu,unapodonate blood, wanachukua damu bila kuandika jina au kuweka alama yoyote zaidi ya blood type, na damu inachekiwa separate sio pale. Hivyo ni vigumu kujua kama ana VVU kwa kudonate blood.
Pia kama Mh haja-engage in risky behaviour hamna haja ya kupima kila miezi sita VVU, kwa hiyo kwa kukiri kuwa wanampima kila miezi sita ina maana kuwa rais wetu ni mhuni, na hajikingi, which shows that he is inconsiderate and reckless. Definitely a very important point that should disqualify him from being president.

Na kwa wale wapambe wasije na mfano wa Bill Clinton, kwa sababu IQ ya Jk haimfikii hata kwa 10% Bill, so spare me the comparison.

Mkuu umemaliza kila kitu.
 
Watanzania tu wepesi mno kusahau."Moderators na Mwanachama mmoja mmoja itunzeni Report hii ya Dr.Mfisi" Ukweli wa Jambo hili utajulikana tu...Na ikiwa Rais ni mgonjwa ni lazima watu wawajibike kwa kusema UONGO.
Wanaweza kuja kuibadilisha lugha baadae mkuu kwa kusema...at that time, and after taking all the measurements....hatukuona kama kulikuwa na tatizo zaidi ya uchovu...then wataconect na lolote litakaloibuka wakati huo....siasa na PR ndogo tu, watu wanachoropoka kwenye scandal...
Lakini my guts tells me...Muheshimiwa ni mgonjwa....
 
Nadhani hufahamu utaratibu,unapodonate blood, wanachukua damu bila kuandika jina au kuweka alama yoyote zaidi ya blood type, na damu inachekiwa separate sio pale. Hivyo ni vigumu kujua kama ana VVU kwa kudonate blood.
Pia kama Mh haja-engage in risky behaviour hamna haja ya kupima kila miezi sita VVU, kwa hiyo kwa kukiri kuwa wanampima kila miezi sita ina maana kuwa rais wetu ni mhuni, na hajikingi, which shows that he is inconsiderate and reckless. Definitely a very important point that should disqualify him from being president.

Na kwa wale wapambe wasije na mfano wa Bill Clinton, kwa sababu IQ ya Jk haimfikii hata kwa 10% Bill, so spare me the comparison.

Nimekupata mkuu…ni kweli sifahamu utaratibu huo hapo juu

Process ninayoijua ni kwamba mtoa damu anajulikana na damu aliyotoa ikionekana haifai kwa donation kwa mfano HIV positive :

  • Anakuwa notified confidentially na ku shauriwa kumuona councellor
  • Haruhusiwi tena kutolewa damu kwa ajili ya blood donation (permanently deffered)
  • Anawekwa kwenye confidential registry ya wasioruhusiwa kudonate blood
 
Pia kama Mh haja-engage in risky behaviour hamna haja ya kupima kila miezi sita VVU, kwa hiyo kwa kukiri kuwa wanampima kila miezi sita ina maana kuwa rais wetu ni mhuni, na hajikingi, which shows that he is inconsiderate and reckless. Definitely a very important point that should disqualify him from being president.

.

Taifa hili bado sana, kama wale wanaoweza kutumia komputa (chini ya 1%) wenye uwezo wa kuaccess I-net (>0.5%) hawajui VVU inaambukizwaje basi tuandike maamivu. Kwa taarifa yako mtu anayepima na harudi tena ni yule aliyeambukizwa tayari, tukisha confirm kuwa una VVU basi huhitaji kuendelea kupima tena. wewe mwenzangu na mimi kama umepima na ukaonekana upo Negative basi haimaanishi upo salama, tunachomaanisha ni kuwa hatujakuona na maambukizi muda huo wa kupima kwa hiyo unashauriwa kupima tena kwa sababu UKIMWI unaambukizwa kwa njia nyingi ndugu yangu sio ngono peke yake. Duu kazi kweli kweli yaani mpaka unapata hasira unaposoma michango mingine. Simpendi JK lakini siwezi kuanza kunyambulisha hoja kizembe namna hii eti basi atakuwa MUHUNI!! Khaa!!! Swali la msingi? Umewahi KUINGIA VCT?

Ni Mtizamo tu
 
From the way the administration has been operating....Covering up for each other and not being truthful in Critical issues....I Seriously doubt the Doctor's report.
 
Kila binadamu ni mgonjwa-mbona mchonga sana kwa baba chodo.nae pia ni binadamu-uchovu,lakini yuko fit as per press release.
 
Kila binadamu ni mgonjwa-mbona mchonga sana kwa baba chodo.nae pia ni binadamu-uchovu,lakini yuko fit as per press release.


Mayogela,

Kama umesoma michango ya wachangiaji wote waliotangulia na bado unatoa hayo maneno basi wewe ndiye una matatizo. Hakuna anayesema kuwa Mh rais ni chuma cha pua kwa hiyo haiwezekani hata siku moja akawa mgonjwa. Ndiyo maana hakuna mtu anashangaa au kuhoji kwa nini rais anao madaktari (tunaowalipa kwa kodi zetu) ili kuangalia afya yake muda wote. Kinachojadiliwa hapa ni kuwa hao madaktari wameshindwa kazi na wanaanza kudandia siasa. Taarifa yao ni ya kisiasa na kwa upande wa utaalamu wameshindwa kazi. Kwa sababu wameshindwa kuthibiti afya ya rais hadi anapatwa na matukio ya aibu ya kuanguka mbele ya kadamnasi. Hilo siyo suala dogo na watu makini hawawezi kumeza ripoti ya madaktari kama ilivyotolewa. Labda kama wewe ulikuwa (au ni) mtu wa madesa (tena yale ya kunakili kila kitu hadi jina)! Hii ripoti haijitoshelezi na ina maswali mengi kuliko majibu. Hebu rudi nyuma usome hii thread!
 
Rais Kikwete akianguka tena daktari atasema nini?



amka2.gif

NAANDIKA kwa uangalifu mkubwa kwa sababu mada yenyewe ni nyeti, kuhusu mjadala uliotawala wiki hii juu ya afya ya Rais Jakaya Kikwete, hata baada ya ofisi yake kujitetea na daktari wake kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari. Wananchi wamekataa kunyamaza. Kwa nini?
Ni vigumu kuwanyamazisha watu, na si vema kuwanyamazisha, wanapojadili suala gumu na zito kama hili. Na hapa si tu kwamba wanajadili, bali wanamjali rais wao; na wanaipenda nchi yao.
Na katika hili hatugombani na rais hata kidogo. Tunamfariji. Rais ni mgonjwa kwa daktari wake; ni kiongozi kwa wananchi wake. Ingawa ugonjwa wa rais ndiyo ajira ya daktari wake, naamini kwamba sote, na daktari akiwamo, tunaguswa sana na msukosuko wa kiafya unaomgusa rais kwa namna yoyote ile.
Na inapofika mahali ofisi ya kiongozi mkuu wa nchi ikatoa idhini kwamba daktari wake azungumze hadharani kuhusu afya ya mgonjwa wake, ujue kuna tatizo kubwa. Lakini kubwa ninaloliona hapa ni kwamba kisaikolojia rais amefedheheshwa na matukio ya kuzidiwa na kudondoka hadharani pamoja na lile la kuishiwa nguvu hivi karibuni jijini Mwanza, na njia mojawapo ya kuyakabili na kupunguza porojo juu ya afya yake ni kufanya hiki walichofanya wiki hii.
Binadamu yeyote mwenye akili timamu na moyo wa utu, atamuonea huruma rais wetu, atamtakia mema na hata kumwombea apone (hata kama wanatuambia hana tatizo). Ndivyo tunavyofanya sasa. Lakini kuna jambo la ziada.
Tuna ugomvi na wasaidizi wa rais. Hatuwezi kuwaacha wamdhalilishe na kumfedhehesha kiongozi mkuu wa nchi, halafu wakatoa taarifa za kujisafisha. Wakitaka kutoa maelezo rasmi wajiandae vizuri zaidi.
Katika blogu yangu ya Kiingereza (www.ngurumo.wordpress.com) nimelijadili suala hili kwa kifupi, nikisisitiza kwamba kiongozi wa nchi hapaswi kuzidiwa na kuanguka hadharani; na nikatoa mifano ya wachache waliovunja kanuni hii, Rais Kikwete akiwamo.
Nimedokeza pia kwamba kuzidiwa kwa Rais Kikwete Jumapili iliyopita akiwa anahutubia umati wa waamini wa Kanisa la African Inland (AIC), Mwanza, lilikuwa tukio la tatu ninalokumbuka kumpata hadharani ndani ya miaka 12.
Alipokuwa waziri wa mambo ya nje ya ushirikiano wa kimataifa, aliwahi kuzidiwa ghafla mwaka 1997 katika uwanja wa ndege wa Brussels, Ubelgiji, akiwa njiani kuelekea Cuba. Ilibidi alazwe kwa saa nane kabla ya kuruhusiwa kuendelea na safari.
Tunakumbuka pia kilichomtokea mwaka 2005, siku moja kabla ya uchaguzi mkuu; alipozidiwa ghafla na kudondoka kutoka jukwaani, akakatiza hotuba yake katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam. Viongozi waandamizi waliokuwapo, wanausalama, wanahabari na wananchi waliokuwa uwanjani na hata waliokuwa wanafuatilia katika redio na runinga, walipatwa na mshtuko mkubwa.
Baada ya ‘mgonjwa’ kupewa huduma hospitalini, aliweza kuzungumza na vyombo vya habari akiwa nyumbani kwake, akasema alianguka kwa sababu ya uchovu wa kampeni, na kwa kuwa siku hiyo alikuwa amefunga. Naamini tukio hilo lilimpatia pia ‘kura za huruma.’
Sijui tukio jingine la kuanguka kwake hadharani au faragha, lakini hili la Mwanza la juzi, lilikuwa la tatu. Kwa serikali iliyo makini, na kwa wahudumu wanaotaka tuwaamini kwamba wanatimiza wajibu wao katika kumhudumia kiongozi mkuu wa nchi, tukio la Mwanza lilipaswa kuepukwa.
Wanaofanya kazi kwa karibu na rais wamekuwa wakisimulia jinsi ambavyo katika miezi yake ya awali ya utawala wake, alikuwa akipatwa na hisia mbaya kila alipokumbuka anguko la jangwani.
Fedheha ya kuanguka hadharani ilimnyima imani ya kujiamini mbele ya umma, kiasi kwamba alikuwa akizungumzia mara kwa mara kwa utani ili kuliondoa kwenye hisia chafu.
Miaka minne baadaye, linapomtokea tukio jingine linalofanana na hili katika mazingira ya jukwaani mbele ya umma, linamtonesha vidonda na kumdhuru kisaikolojia. Kujiamini kunatoweka tena.
Hawezi kusema hadharani, lakini sasa hivi rais anapaswa asaidiwe kuondokana na hofu ya kusimama hadharani.
Baada ya yote yaliyotokea, haitoshi kauli ya dakatri wa rais kwamba “tumejifunza, na tunaahidi kuwa waangalifu zaidi” inaeleza kwamba anatambua kosa lake na wenzake, lakini haitoshi.
Wanapaswa wafanye jambo la ziada la kumuimarisha rais mwenyewe kimwili na kisaikolojia. Bila hivyo, ataanguka tena, na tutaambiwa “hana tatizo la kiafya.”
Haitoshi kabisa kusema kwamba rais hana tatizo lolote la kiafya, bali uchovu pekee ndio umesababisha matukio yote hayo.
Tunavyojua, kwa kawaida, watawala na wanajeshi hawaanguki hovyo hovyo - tena hadharani. Si kawaida, ni aibu, na haitarajiwi kwa watawala na wanajeshi kuzidiwa na kuanguka hadharani.
Inakuwaje Amiri Jeshi Mkuu, mtawala na mwanajeshi kitaaluma azidiwe na kudondoka mara kadhaa, halafu wasaidizi wake wanacheka cheka na kusema hakuna tatizo? Wanamdanganya yeye au wanatudanganya sisi?
Si tu rais ni mwanajeshi, bali anatunzwa kama mtoto - anakula vizuri, anapimwa afya kila mara, analala pazuri, anasafiri kwa raha katika daraja la juu kwenye ndege, anafunguliwa hata mlango wa gari, anapangiwa ratiba ya kazi, anapangiwa hata muda wa kulala.
Ndiyo, anafanya kazi zinazoweza kumchosha akili lakini hayuko peke yake.
Rais wetu si dhaifu kama wananchi wake ambao wengi wanalalala au kushinda njaa; wanapata mlo mara moja moja (na wenyewe haujakamilika virutubisho); wanafanya kazi nzito na ngumu zinazokula nguvu ya mwili na akili; wana pato duni sana (chini ya shilingi 1000 kwa siku); wanakabiliwa na magonjwa hatari na hawana huduma ya matibabu inayoeleweka na inayoaminika; wanaishi katika mazingira hatari; wanakabiliwa na magonjwa sugu kwa miaka mingi; wanatembea kwa miguu au baiskeli, bajaji au wanasafiri kwa malori na mabasi mabovu; hata kwa wanaosafiri kwa ndege, wanatumia madaraja ya chini yanayochosha; wanalala kwa saa 2 au tatu kila siku; wanasumbuliwa na umaskini wa kutisha kiasi kwamba kila wanapolala hawana tumaini kama wataiona kesho.
Watanzania hawa hawazimii, hawaishiwi nguvu wala hawaanguki, aanguke rais mwenye afya isiyotetereka (kama tulivyoelezwa) na mwenye matunzo ya viwango vya juu? Hapa ndipo kuna swali kuu ambalo daktari wa rais, Dk. Peter Mfisi, hajalijibu.
Na ingawa tunajua kuwa afya ya mgonjwa ni siri yake na daktari wake, kwa kuwa Dk. Mfisi amepewa ruhusa na mteja wake (rais) kutangaza taarifa hiyo, alipaswa kujua kwamba ripoti yake ingeibua maswali mengine yaliyofichika.
Kwanza, wapo wanaosema amekwenda mbali kuliko alikopaswa; kwamba ingetosha tu yeye kutoa tamko kwamba rais anaumwa nini, au kwamba haumwi bali amezidiwa kutokana na uchovu tu.
Kauli hiyo pekee kutoka kwa daktari wa rais ingekuwa na uzito wa kutosha, na labda ingeibua maswali machache zaidi.
Pili, uungwana wa kawaida unatulazimisha kukubaliana na daktari, maana sisi hatuna taarifa za ziada. Lakini kwa kuwa daktari na mteja wake wamewasiliana na sisi kwa kutumia taarifa ya kisiasa kupitia vyombo vya habari; wala hakuna mwanahabari au mwana taaluma mwingine aliyeonyeshwa faili la afya ya rais, wananchi wana haki ya kuendelea kujadili suala hili na kuhoji maswali zaidi, hata yanayoudhi. Tusiwachukie. Tuwavumilie.
Hili la kuchoka na kuzidiwa si kosa binafsi la rais, bali ni la wasaidizi wake, ingawa naye ana uamuzi wa kufanya au kuacha jambo lolote analopangiwa. Washauri wa rais katika fani mbalimbali lazima walinde heshima yao kwa kuzingatia kwamba wao ni wataalamu wa maeneo husika.
Rais anapaswa awasikilize wao wanapomshauri kwa kuwa ndio wataalamu aliowateua au aliokabidhiwa. Ni makosa makubwa rais kudhani kwamba wataalamu waliomzunguka ni matarishi wa kumbebea mafaili na kuimba vibwagizo vyake kwa madhumuni ya kisiasa.
Yeye mwenyewe amekiri kwamba walimshauri akawagomea. Tungetarajia mambo mawili: kwanza, wataalamu hao wangelinda heshima ya taaluma zao kwa kujiuzulu kazi, kwa sababu hawana sababu ya kufanya kazi ya kumshauri kiongozi asiyeshaurika. Hawana kazi ya kufanya Ikulu.
Pili, baada ya tukio la Mwanza, rais alipaswa awawajibishe, kwamba wameshindwa kummudu na kumlindia afya na heshima mbele ya umma. Bahati mbaya, kama ilivyo kawaida yake, badala ya kuwawajibisha kwa kumfedhehesha, amewatetea! Wamepata bahati ile ile wanayofaidi mafisadi wanaocheka vizuri na wakubwa - kulindwa. Matarajio yetu ni kwamba wasaidizi wamejifunza, lakini wajue bado wananchi wanahoji: Kama rais ni mzima kiasi tulichoelezwa, mbona anazidiwa na kuanguka? Kama ni uchovu tu, na kama wanasema wamejifunza, watatuambia nini iwapo rais atazidiwa tena hadharani kwa mara ya nne?
 
Rais Kikwete akianguka tena daktari atasema nini?



amka2.gif

NAANDIKA kwa uangalifu mkubwa kwa sababu mada yenyewe ni nyeti, kuhusu mjadala uliotawala wiki hii juu ya afya ya Rais Jakaya Kikwete, hata baada ya ofisi yake kujitetea na daktari wake kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari. Wananchi wamekataa kunyamaza. Kwa nini?
Ni vigumu kuwanyamazisha watu, na si vema kuwanyamazisha, wanapojadili suala gumu na zito kama hili. Na hapa si tu kwamba wanajadili, bali wanamjali rais wao; na wanaipenda nchi yao.
Na katika hili hatugombani na rais hata kidogo. Tunamfariji. Rais ni mgonjwa kwa daktari wake; ni kiongozi kwa wananchi wake. Ingawa ugonjwa wa rais ndiyo ajira ya daktari wake, naamini kwamba sote, na daktari akiwamo, tunaguswa sana na msukosuko wa kiafya unaomgusa rais kwa namna yoyote ile.
Na inapofika mahali ofisi ya kiongozi mkuu wa nchi ikatoa idhini kwamba daktari wake azungumze hadharani kuhusu afya ya mgonjwa wake, ujue kuna tatizo kubwa. Lakini kubwa ninaloliona hapa ni kwamba kisaikolojia rais amefedheheshwa na matukio ya kuzidiwa na kudondoka hadharani pamoja na lile la kuishiwa nguvu hivi karibuni jijini Mwanza, na njia mojawapo ya kuyakabili na kupunguza porojo juu ya afya yake ni kufanya hiki walichofanya wiki hii.
Binadamu yeyote mwenye akili timamu na moyo wa utu, atamuonea huruma rais wetu, atamtakia mema na hata kumwombea apone (hata kama wanatuambia hana tatizo). Ndivyo tunavyofanya sasa. Lakini kuna jambo la ziada.
Tuna ugomvi na wasaidizi wa rais. Hatuwezi kuwaacha wamdhalilishe na kumfedhehesha kiongozi mkuu wa nchi, halafu wakatoa taarifa za kujisafisha. Wakitaka kutoa maelezo rasmi wajiandae vizuri zaidi.
Katika blogu yangu ya Kiingereza (www.ngurumo.wordpress.com) nimelijadili suala hili kwa kifupi, nikisisitiza kwamba kiongozi wa nchi hapaswi kuzidiwa na kuanguka hadharani; na nikatoa mifano ya wachache waliovunja kanuni hii, Rais Kikwete akiwamo.
Nimedokeza pia kwamba kuzidiwa kwa Rais Kikwete Jumapili iliyopita akiwa anahutubia umati wa waamini wa Kanisa la African Inland (AIC), Mwanza, lilikuwa tukio la tatu ninalokumbuka kumpata hadharani ndani ya miaka 12.
Alipokuwa waziri wa mambo ya nje ya ushirikiano wa kimataifa, aliwahi kuzidiwa ghafla mwaka 1997 katika uwanja wa ndege wa Brussels, Ubelgiji, akiwa njiani kuelekea Cuba. Ilibidi alazwe kwa saa nane kabla ya kuruhusiwa kuendelea na safari.
Tunakumbuka pia kilichomtokea mwaka 2005, siku moja kabla ya uchaguzi mkuu; alipozidiwa ghafla na kudondoka kutoka jukwaani, akakatiza hotuba yake katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam. Viongozi waandamizi waliokuwapo, wanausalama, wanahabari na wananchi waliokuwa uwanjani na hata waliokuwa wanafuatilia katika redio na runinga, walipatwa na mshtuko mkubwa.
Baada ya ‘mgonjwa’ kupewa huduma hospitalini, aliweza kuzungumza na vyombo vya habari akiwa nyumbani kwake, akasema alianguka kwa sababu ya uchovu wa kampeni, na kwa kuwa siku hiyo alikuwa amefunga. Naamini tukio hilo lilimpatia pia ‘kura za huruma.’
Sijui tukio jingine la kuanguka kwake hadharani au faragha, lakini hili la Mwanza la juzi, lilikuwa la tatu. Kwa serikali iliyo makini, na kwa wahudumu wanaotaka tuwaamini kwamba wanatimiza wajibu wao katika kumhudumia kiongozi mkuu wa nchi, tukio la Mwanza lilipaswa kuepukwa.
Wanaofanya kazi kwa karibu na rais wamekuwa wakisimulia jinsi ambavyo katika miezi yake ya awali ya utawala wake, alikuwa akipatwa na hisia mbaya kila alipokumbuka anguko la jangwani.
Fedheha ya kuanguka hadharani ilimnyima imani ya kujiamini mbele ya umma, kiasi kwamba alikuwa akizungumzia mara kwa mara kwa utani ili kuliondoa kwenye hisia chafu.
Miaka minne baadaye, linapomtokea tukio jingine linalofanana na hili katika mazingira ya jukwaani mbele ya umma, linamtonesha vidonda na kumdhuru kisaikolojia. Kujiamini kunatoweka tena.
Hawezi kusema hadharani, lakini sasa hivi rais anapaswa asaidiwe kuondokana na hofu ya kusimama hadharani.
Baada ya yote yaliyotokea, haitoshi kauli ya dakatri wa rais kwamba “tumejifunza, na tunaahidi kuwa waangalifu zaidi” inaeleza kwamba anatambua kosa lake na wenzake, lakini haitoshi.
Wanapaswa wafanye jambo la ziada la kumuimarisha rais mwenyewe kimwili na kisaikolojia. Bila hivyo, ataanguka tena, na tutaambiwa “hana tatizo la kiafya.”
Haitoshi kabisa kusema kwamba rais hana tatizo lolote la kiafya, bali uchovu pekee ndio umesababisha matukio yote hayo.
Tunavyojua, kwa kawaida, watawala na wanajeshi hawaanguki hovyo hovyo - tena hadharani. Si kawaida, ni aibu, na haitarajiwi kwa watawala na wanajeshi kuzidiwa na kuanguka hadharani.
Inakuwaje Amiri Jeshi Mkuu, mtawala na mwanajeshi kitaaluma azidiwe na kudondoka mara kadhaa, halafu wasaidizi wake wanacheka cheka na kusema hakuna tatizo? Wanamdanganya yeye au wanatudanganya sisi?
Si tu rais ni mwanajeshi, bali anatunzwa kama mtoto - anakula vizuri, anapimwa afya kila mara, analala pazuri, anasafiri kwa raha katika daraja la juu kwenye ndege, anafunguliwa hata mlango wa gari, anapangiwa ratiba ya kazi, anapangiwa hata muda wa kulala.
Ndiyo, anafanya kazi zinazoweza kumchosha akili lakini hayuko peke yake.
Rais wetu si dhaifu kama wananchi wake ambao wengi wanalalala au kushinda njaa; wanapata mlo mara moja moja (na wenyewe haujakamilika virutubisho); wanafanya kazi nzito na ngumu zinazokula nguvu ya mwili na akili; wana pato duni sana (chini ya shilingi 1000 kwa siku); wanakabiliwa na magonjwa hatari na hawana huduma ya matibabu inayoeleweka na inayoaminika; wanaishi katika mazingira hatari; wanakabiliwa na magonjwa sugu kwa miaka mingi; wanatembea kwa miguu au baiskeli, bajaji au wanasafiri kwa malori na mabasi mabovu; hata kwa wanaosafiri kwa ndege, wanatumia madaraja ya chini yanayochosha; wanalala kwa saa 2 au tatu kila siku; wanasumbuliwa na umaskini wa kutisha kiasi kwamba kila wanapolala hawana tumaini kama wataiona kesho.
Watanzania hawa hawazimii, hawaishiwi nguvu wala hawaanguki, aanguke rais mwenye afya isiyotetereka (kama tulivyoelezwa) na mwenye matunzo ya viwango vya juu? Hapa ndipo kuna swali kuu ambalo daktari wa rais, Dk. Peter Mfisi, hajalijibu.
Na ingawa tunajua kuwa afya ya mgonjwa ni siri yake na daktari wake, kwa kuwa Dk. Mfisi amepewa ruhusa na mteja wake (rais) kutangaza taarifa hiyo, alipaswa kujua kwamba ripoti yake ingeibua maswali mengine yaliyofichika.
Kwanza, wapo wanaosema amekwenda mbali kuliko alikopaswa; kwamba ingetosha tu yeye kutoa tamko kwamba rais anaumwa nini, au kwamba haumwi bali amezidiwa kutokana na uchovu tu.
Kauli hiyo pekee kutoka kwa daktari wa rais ingekuwa na uzito wa kutosha, na labda ingeibua maswali machache zaidi.
Pili, uungwana wa kawaida unatulazimisha kukubaliana na daktari, maana sisi hatuna taarifa za ziada. Lakini kwa kuwa daktari na mteja wake wamewasiliana na sisi kwa kutumia taarifa ya kisiasa kupitia vyombo vya habari; wala hakuna mwanahabari au mwana taaluma mwingine aliyeonyeshwa faili la afya ya rais, wananchi wana haki ya kuendelea kujadili suala hili na kuhoji maswali zaidi, hata yanayoudhi. Tusiwachukie. Tuwavumilie.
Hili la kuchoka na kuzidiwa si kosa binafsi la rais, bali ni la wasaidizi wake, ingawa naye ana uamuzi wa kufanya au kuacha jambo lolote analopangiwa. Washauri wa rais katika fani mbalimbali lazima walinde heshima yao kwa kuzingatia kwamba wao ni wataalamu wa maeneo husika.
Rais anapaswa awasikilize wao wanapomshauri kwa kuwa ndio wataalamu aliowateua au aliokabidhiwa. Ni makosa makubwa rais kudhani kwamba wataalamu waliomzunguka ni matarishi wa kumbebea mafaili na kuimba vibwagizo vyake kwa madhumuni ya kisiasa.
Yeye mwenyewe amekiri kwamba walimshauri akawagomea. Tungetarajia mambo mawili: kwanza, wataalamu hao wangelinda heshima ya taaluma zao kwa kujiuzulu kazi, kwa sababu hawana sababu ya kufanya kazi ya kumshauri kiongozi asiyeshaurika. Hawana kazi ya kufanya Ikulu.
Pili, baada ya tukio la Mwanza, rais alipaswa awawajibishe, kwamba wameshindwa kummudu na kumlindia afya na heshima mbele ya umma. Bahati mbaya, kama ilivyo kawaida yake, badala ya kuwawajibisha kwa kumfedhehesha, amewatetea! Wamepata bahati ile ile wanayofaidi mafisadi wanaocheka vizuri na wakubwa - kulindwa. Matarajio yetu ni kwamba wasaidizi wamejifunza, lakini wajue bado wananchi wanahoji: Kama rais ni mzima kiasi tulichoelezwa, mbona anazidiwa na kuanguka? Kama ni uchovu tu, na kama wanasema wamejifunza, watatuambia nini iwapo rais atazidiwa tena hadharani kwa mara ya nne?

Pdidy,

Mbona huweki chanzo, kuwa hii ni makala ya Ngurumo aliyoitoea kwenye Tanzania Daima Jumapili?
 
Pdidy,

Mbona huweki chanzo, kuwa hii ni makala ya Ngurumo aliyoitoea kwenye Tanzania Daima Jumapili?

Mkuu,

Naona umeweka chanzo kwa kutumia swali .... mhhh
Je, inajalisha nani ameandika habari hii kuhusu afya ya raisi?
 
Rais Kikwete hajapumzika http://www.majira.co.tz/index.php?v...mzika&format=pdf&option=com_content&Itemid=57 http://www.majira.co.tz/index.php?v...nt&print=1&page=&option=com_content&Itemid=57 http://www.majira.co.tz/index.php?o...6aWthJm9wdGlvbj1jb21fY29udGVudCZJdGVtaWQ9NTc= Wednesday, 25 November 2009 07:56 *Wasomi wasema ushauri wa daktari umepuuzwa
*Wadai si rahisi kuona tija za safari zake


Na Tumaini Makene

Majira

LICHA ya ushauri wa daktari na Ofisi Binafsi ya Rais Jakaya Kikwete kuwa kiongozi huyo apumzike baada ya kuishiwa nguvu na kukatisha hotuba mjini Mwanza, safari zake za ndani na nje ya nchi anazoendelea kufanya zimezua upya mjadala huku akidaiwa hajapumzika..

Mjadala huo umeibuka wakati Rais Kikwete akiwa nje ya nchi kwa ziara ndefu itakayomchukua takribani siku 10 za kukutana na viongozi wa nchi na kufanya mikutano kadhaa katika nchi tatu tofauti.

Safari ya sasa ya Rais Kikwete ambayo itamfikisha katika nchi za Jamaica (siku 3), Trinidadi na Tobago (siku 3) na Cuba (4) itakuwa ni mwendelezo wa ratiba ndefu ya kusafiri ndani na nje ya nchi kuanzia katikati ya Oktoba, siku 53 baada ya kuishiwa nguvu huko katika Uwanja wa Kirumba, Mwanza, wakati wa maadhimisho ya miaka 100 ya kanisa la Africa Inland Church (AIC).

Masuala mawili ambayo kwa sasa yameibua mjadala huo wa mara kwa mara ni kuhusiana na hali ya afya yake kama ilivyofafanuliwa na kaktari wake, Dkt. Peter Mfisi Oktoba 7, mwaka huu pamoja na tija zinazotokana na safari za nje ya nchi ambazo zinatumia gharama kubwa.

Baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili kuhusu iwapo Ikulu imefanyia kazi taarifa yake kuwa Ofisi Binafsi ya Rais (OB) ingepitia upya ratiba ya mkuu huyo wa nchi na ushauri wa madaktari wake wa kumtaka apumzike, wameonesha wasiwasi juu ya utekelezaji wa suala hilo katika kulinda afya ya rais.

Wamehoji pia kauli yake baada ya kupata nafuu kuwa alipata msukosuko wa kiafya kutokana na kazi nyingi na safari ndefu na ahadi yake kuwa angeacha ubishi na kuanza kuwasikiliza washauri wake wanaotaka apumzike.

Siku chache baada ya tukio la kuishiwa nguvu Oktoba 4, Rais Kikwete alianza safari ya kikazi Mkoa wa Mara (Okt 13-14) alipofanya shughuli ya kuzima mwenge na kukagua miradi mbalimbali.

Oktoba 17 alikuwa kwenye harambee ya kiwanda cha Tangawizi iliyoandaliwa na Mbunge wa Same Mashariki, Bi. Anna Kilango na baadaye kufanya ziara siku sita katika mikoa ya Iringa na Mbeya kuanzia Oktoba 26. Rais pia aliongoza na kutoa mada kwenye kongamano la wadau wa maendeleo Novemba 5 na 6, kabla hajaondoka kwenda Misri (Nov 10), akarejea nchini na baadaye kwenda Italia (Nov 15-19) ambako alihutubia mkutano wa chakula.

Novemba 20 rais alipokea Kombe la Dunia katika Uwanja wa Taifa na siku iliyofuata akawa mkoani Arusha katika maadhimisho ya miaka 10 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Siku mbilia baadaye Rais aliondoka kwenda safari ya Jamaica, Trinida na Tobago na kumalizia Cuba inayoendelea sasa.

Mwanazuoni Profesa Mwesiga Baregu alilieleza Majira kuwa rais ni binadamu wa kawaida, hivyo kama ameshauriwa na wataalamu kupunguza ratiba ngumu ni bora afanye kazi za karibu ambazo si lazima asafiri umbali mrefu.

"Hivi karibuni tulisikia maelezo ya daktari wake kuhusu afya yake, tukaambiwa kuwa anapaswa kupata wasaa wa kupumzika, tulitarajia itakuwa hivyo na badala yake angeweza kufanya kazi za karibu. Rais ni binadamu wa kawaida, asijioneshe kuwa ni mzima kama hali hairuhusu awe hivyo, ingembidi apumzike," alisema Prof. Baregu.

Prof. Baregu ambaye ni mtaalamu wa Sayansi ya Siasa na Ushirikiano wa Kimataifa, alisema ni ngumu kuona moja kwa moja tija zitokanazo na safari za rais kwa sababu hakuna taarifa za ziara hizo.

Alisema ni muhimu wananchi wakapewa taarifa za ziara za rais wao ikibidi kabla ya kuondoka na baada ya kurudi ili waweze kutoa tathmini iwapo zinawiana na kile 'kinachowekezwa' katika ziara hizo.

"Wakati mwingine unaweza kufikiri Rais Kikwete ni Waziri wa Mambo ya Nje, kila baada ya siku chache unamsikia yuko nje. Akirudi nyumbani atakwenda vijiji viwili vitatu kama vile kiinimacho halafu tena huyoo ameondoka. Na ninaambiwa msafara wake haupungui watu ishirini.

"Tumefikia mahali nchi hii rais anapaswa kufanya kama Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa akiwatembelea watu anapiga kambi kijijini na kujua kwa undani shida zao. Si kila wakati kwenda nje kunaweza kuwa na tija kwa maslahi ya taifa," alisema Prof. Baregu.

Aliongeza kuwa si vibaya Ofisi ya Rais ikawaambia wananchi kinachompeleka nchi fulani ni kitu gani hasa. Kwa sababu gharama anazotumia ni za walipa kodi. Alisema kama ilivyo kwa Waziri wa Mambo ya Nje anavyopaswa kutoa taarifa kwa rais anaporudi kutoka ziara, rais naye anapaswa kufanya hivyo kwa wananchi ambao ndio waajiri wake.

"Tumewahi kupata ripoti ya ziara za rais nje ya nchi mara moja nafikiri, tunaambiwa ameenda kuomba, lakini hatujui kama kilichoombwa kilipatikana na vimeishia wapi. Pia ni vyema tukafanya uchambuzi wa nchi tunazohusiana nazo kama ni sahihi kwa sisi kuweza kuendelea."

Kwa upande Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahimu Lipumba ambaye aliwahi kuchambua ziara hizo na kueleza kuwa hazina manufaa, alisema Rais Kikwete ana hulka ya kupenda safari na kumfananisha na Vasco Da Gama, Mreno wa zamani aliyekuwa maarufu kwa kusafiri na mvumbuzi wa nchi kadhaa.

Prof. Lipumba alisema kwa kusafiri mara kwa mara Rais Kikwete anakwepa majukumu na kuwa hataki bugudha ya kukaa nchini na kufanya mipango ya kuendeleza nchi, ikiwemo kutatua masuala kadhaa ambayo yamekuwa yakiyumbisha serikali yake na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Hivi karibuni tumesikia ripoti moja ikionesha kuwa katika taasisi zinazoongoza kwa kulipana 'allowances' (posho) Ikulu iko juu ya zote, sasa mojawapo ya njia za posho hizo ni hizo safari ambazo kwa kweli tija yake ni ndogo ukilinganisha na gharama tunazoingia.

"Kuna kazi zingine alipaswa kutumia wasaidizi wake, mawaziri au wawakilishi wetu huko nje ya nchi, yeye yuko safarini muda wote, huku mambo yanasambaratika, Waziri wake wa Utawala Bora anamshutumu mtu kwa kuuza dawa za kulevya," alisema.

Prof. Lipumba ambaye ni mchumi alisema safari za rais haziwezi kusaidia nchi kupunguziwa au kusamehewa madeni kwani hiyo inatokana na mipango ya nchi kupitia wizara zao za fedha na kuongeza kuwa, anapaswa kubaki nyumbani kusaidia kutoa maamuzi magumu hasa juu ya vita dhidi ya ufisadi.

"Ufisadi unaongezeka na hii ni moja ya vigezo ambavyo wafadhili wanatumia kutuongezea au kutupunguzia misaada, sio safari za rais. Kama safari hizo zitakuwa hazijengi kama hazisaidii vita dhidi ya rushwa na ufisadi mwingine. Kwanza lazima ieleweke kuwa negotiations (mazungumzo) ya namna hiyo hayafanywi na rais bali watendaji wa serikali," alisema.

 
Mambo ya Vasco Dagama na safari zake za uvumbuzi si tu zinanitia kichefuchefu bali siwezi kuziandikia tena maana JK hashauriki!
 
Tatizo anatumia pesa zetu sisi walipa kodi! Tufanyaje aache au kupunguza safari hizo?
 
Napenda kugusia kwa ufupi hoja zilizotolewa na mwandishi hapa chini yenye kichwa: RAIS HAJAPUMZIKA TANGU APATE KASHESHE LA KUISHIWA NGUVU HUKO MWANZA...." kwamba Ushauri una sura tatu:
1. Unampa mshauriwa mawazo mbadala juu ya suala husika
2. Unamwongezea hazina ya mawazo mshauriwa.
3. Haumlazimishi mshauriwa kuzingatia au kutokuzingatia ushauri uliotolewa
juu ya suala husika au jingine lolote.

Kwa sababu dhamana ya kufanya uamuzi na kuwajibika kwa maamuzi
afanyayo mshauriwa juu ya jambo lolote yamebebwa na mshauriwa na si mwenye kutoa ushauri! Kuhusu masuala ya kiafya- ni haki ya msingi ya kibinadamu kukubali au kukataa ushauri au matibabu yaliyopendekezwa na daktari anayekutibukwa sababu yeyote ile ambayo muhusika/mshauriwa ataona "haijakaa vizuri/hakubaliani nayo na hawajibiki kutoa sababu za kukataa ushauri huo kwa mwenye kumshauri au mtu mwingine yeyote.!!!!

Hebu tusome mawazo haya hapa chini:

Rais Kikwete hajapumzika Wednesday, 25 November 2009 07:56 *Wasomi wasema ushauri wa daktari umepuuzwa
*Wadai si rahisi kuona tija za safari zake


Na Tumaini Makene


LICHA ya ushauri wa daktari na Ofisi Binafsi ya Rais Jakaya Kikwete kuwa kiongozi huyo apumzike baada ya kuishiwa nguvu na kukatisha hotuba mjini Mwanza, safari zake za ndani na nje ya nchi anazoendelea kufanya zimezua upya mjadala huku akidaiwa hajapumzika..

Mjadala huo umeibuka wakati Rais Kikwete akiwa nje ya nchi kwa ziara ndefu itakayomchukua takribani siku 10 za kukutana na viongozi wa nchi na kufanya mikutano kadhaa katika nchi tatu tofauti.

Safari ya sasa ya Rais Kikwete ambayo itamfikisha katika nchi za Jamaica (siku 3), Trinidadi na Tobago (siku 3) na Cuba (4) itakuwa ni mwendelezo wa ratiba ndefu ya kusafiri ndani na nje ya nchi kuanzia katikati ya Oktoba, siku 53 baada ya kuishiwa nguvu huko katika Uwanja wa Kirumba, Mwanza, wakati wa maadhimisho ya miaka 100 ya kanisa la Africa Inland Church (AIC).

Masuala mawili ambayo kwa sasa yameibua mjadala huo wa mara kwa mara ni kuhusiana na hali ya afya yake kama ilivyofafanuliwa na kaktari wake, Dkt. Peter Mfisi Oktoba 7, mwaka huu pamoja na tija zinazotokana na safari za nje ya nchi ambazo zinatumia gharama kubwa.

Baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili kuhusu iwapo Ikulu imefanyia kazi taarifa yake kuwa Ofisi Binafsi ya Rais (OB) ingepitia upya ratiba ya mkuu huyo wa nchi na ushauri wa madaktari wake wa kumtaka apumzike, wameonesha wasiwasi juu ya utekelezaji wa suala hilo katika kulinda afya ya rais.

Wamehoji pia kauli yake baada ya kupata nafuu kuwa alipata msukosuko wa kiafya kutokana na kazi nyingi na safari ndefu na ahadi yake kuwa angeacha ubishi na kuanza kuwasikiliza washauri wake wanaotaka apumzike.

Siku chache baada ya tukio la kuishiwa nguvu Oktoba 4, Rais Kikwete alianza safari ya kikazi Mkoa wa Mara (Okt 13-14) alipofanya shughuli ya kuzima mwenge na kukagua miradi mbalimbali.

Oktoba 17 alikuwa kwenye harambee ya kiwanda cha Tangawizi iliyoandaliwa na Mbunge wa Same Mashariki, Bi. Anna Kilango na baadaye kufanya ziara siku sita katika mikoa ya Iringa na Mbeya kuanzia Oktoba 26. Rais pia aliongoza na kutoa mada kwenye kongamano la wadau wa maendeleo Novemba 5 na 6, kabla hajaondoka kwenda Misri (Nov 10), akarejea nchini na baadaye kwenda Italia (Nov 15-19) ambako alihutubia mkutano wa chakula.

Novemba 20 rais alipokea Kombe la Dunia katika Uwanja wa Taifa na siku iliyofuata akawa mkoani Arusha katika maadhimisho ya miaka 10 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Siku mbilia baadaye Rais aliondoka kwenda safari ya Jamaica, Trinida na Tobago na kumalizia Cuba inayoendelea sasa.

Mwanazuoni Profesa Mwesiga Baregu alilieleza Majira kuwa rais ni binadamu wa kawaida, hivyo kama ameshauriwa na wataalamu kupunguza ratiba ngumu ni bora afanye kazi za karibu ambazo si lazima asafiri umbali mrefu.

"Hivi karibuni tulisikia maelezo ya daktari wake kuhusu afya yake, tukaambiwa kuwa anapaswa kupata wasaa wa kupumzika, tulitarajia itakuwa hivyo na badala yake angeweza kufanya kazi za karibu. Rais ni binadamu wa kawaida, asijioneshe kuwa ni mzima kama hali hairuhusu awe hivyo, ingembidi apumzike," alisema Prof. Baregu.

Prof. Baregu ambaye ni mtaalamu wa Sayansi ya Siasa na Ushirikiano wa Kimataifa, alisema ni ngumu kuona moja kwa moja tija zitokanazo na safari za rais kwa sababu hakuna taarifa za ziara hizo.

Alisema ni muhimu wananchi wakapewa taarifa za ziara za rais wao ikibidi kabla ya kuondoka na baada ya kurudi ili waweze kutoa tathmini iwapo zinawiana na kile 'kinachowekezwa' katika ziara hizo.

"Wakati mwingine unaweza kufikiri Rais Kikwete ni Waziri wa Mambo ya Nje, kila baada ya siku chache unamsikia yuko nje. Akirudi nyumbani atakwenda vijiji viwili vitatu kama vile kiinimacho halafu tena huyoo ameondoka. Na ninaambiwa msafara wake haupungui watu ishirini.

"Tumefikia mahali nchi hii rais anapaswa kufanya kama Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa akiwatembelea watu anapiga kambi kijijini na kujua kwa undani shida zao. Si kila wakati kwenda nje kunaweza kuwa na tija kwa maslahi ya taifa," alisema Prof. Baregu.Cuba na

Aliongeza kuwa si vibaya Ofisi ya Rais ikawaambia wananchi kinachompeleka nchi fulani ni kitu gani hasa. Kwa sababu gharama anazotumia ni za walipa kodi. Alisema kama ilivyo kwa Waziri wa Mambo ya Nje anavyopaswa kutoa taarifa kwa rais anaporudi kutoka ziara, rais naye anapaswa kufanya hivyo kwa wananchi ambao ndio waajiri wake.

"Tumewahi kupata ripoti ya ziara za rais nje ya nchi mara moja nafikiri, tunaambiwa ameenda kuomba, lakini hatujui kama kilichoombwa kilipatikana na vimeishia wapi. Pia ni vyema tukafanya uchambuzi wa nchi tunazohusiana nazo kama ni sahihi kwa sisi kuweza kuendelea."

Kwa upande Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahimu Lipumba ambaye aliwahi kuchambua ziara hizo na kueleza kuwa hazina manufaa, alisema Rais Kikwete ana hulka ya kupenda safari na kumfananisha na Vasco Da Gama, Mreno wa zamani aliyekuwa maarufu kwa kusafiri na mvumbuzi wa nchi kadhaa.

Prof. Lipumba alisema kwa kusafiri mara kwa mara Rais Kikwete anakwepa majukumu na kuwa hataki bugudha ya kukaa nchini na kufanya mipango ya kuendeleza nchi, ikiwemo kutatua masuala kadhaa ambayo yamekuwa yakiyumbisha serikali yake na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Hivi karibuni tumesikia ripoti moja ikionesha kuwa katika taasisi zinazoongoza kwa kulipana 'allowances' (posho) Ikulu iko juu ya zote, sasa mojawapo ya njia za posho hizo ni hizo safari ambazo kwa kweli tija yake ni ndogo ukilinganisha na gharama tunazoingia.

"Kuna kazi zingine alipaswa kutumia wasaidizi wake, mawaziri au wawakilishi wetu huko nje ya nchi, yeye yuko safarini muda wote, huku mambo yanasambaratika, Waziri wake wa Utawala Bora anamshutumu mtu kwa kuuza dawa za kulevya," alisema.

Prof. Lipumba ambaye ni mchumi alisema safari za rais haziwezi kusaidia nchi kupunguziwa au kusamehewa madeni kwani hiyo inatokana na mipango ya nchi kupitia wizara zao za fedha na kuongeza kuwa, anapaswa kubaki nyumbani kusaidia kutoa maamuzi magumu hasa juu ya vita dhidi ya ufisadi.

"Ufisadi unaongezeka na hii ni moja ya vigezo ambavyo wafadhili wanatumia kutuongezea au kutupunguzia misaada, sio safari za rais. Kama safari hizo zitakuwa hazijengi kama hazisaidii vita dhidi ya rushwa na ufisadi mwingine. Kwanza lazima ieleweke kuwa negotiations (mazungumzo) ya namna hiyo hayafanywi na rais bali watendaji wa serikali," alisema.
 
Hivi sikusoma mahali fulani kuwa amekwenda mapumzikoni ngorongoro? labda walimshauri mapumziko ya siku chache kama alizotumia. Sijui kama uelewa wetu wa mapumziko na wake yeye unafanana. May be ukimuona ukamuuliza atajibu "nimepumzika sana sasa nimeona nifanye kazi kabla ya mapumziko mengine ya christmas"....sijui tulitaka apumzikaje na yeye sijui tafsiri yake ya kupumzika ikoje! huenda akienda nje anapumzika pia kuliko akiwa hapa! anyway sijui

We do not see things as they are: we see things as we are
NANYI MTAIFAHAMU HIYO KWELI NAYO KWELI ITAWAWEKA HURU
 
Back
Top Bottom