Taarifa kwa umma kwa wasafiri wanaokwenda Hong Kong

Vipi inawezekana nao wakija huko kwetu wawekewe vikwazo? au sisi hatuna mamlaka hiyo.
Sisi viwanja vyetu vikubwa JNIA na KIA vinaendeshwa na wageni, KIA kasimama Mwarabu, na JNIA kasimama SwissPort japo mwarabu naye anapanyemelea.
 
Naona ubalozi wa Tz unaongea kwa kufichaficha mambo, shida kubwa ya Watanzania walio wengi zaidi ni kutaka mafanikio ya haraka haraka kwa njia za mkato, hivyo wanajikuta wanalazimika Kufanya Mambo ya uhalifu ya Kusafirisha na Kufanya Biashara ya Madawa ya Kulevya. Hapa Tz, wanalindwa na utawala uliopo, wakumbuke huko nje hakuna CCM ya kuweza kuwalinda. Balozi zote za Tz huko nje zitoe ilani kwa mamlaka za nchi husika kuwashughulikia ipasavyo Watanzania wote wanaojihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya ili kusafisha jina la nchi huko ugenini.

Jina la Tanzania limechafuka kimataifa kwa sababu ya watu wachache washenzi, ni vyema hao watu wakanyongwa hukohuko ili kuwatia adabu watu wengine waliobaki wenye nia ya kufanya hiyo biashara ya madawa ya kulevya.

Watanzania wamezidi ktk kufanya uhalifu wa kujihusisha na madawa ya kulevya, Passport ya Tanzania imekuwa haifai tena huko duniani kwa sababu ya hao watu wa madawa ya kulevya.

Ndio maana Mimi binafsi nilipokuwa nje ya Tz, sikutaka kabisa kujihusiha kwa namna yoyote ile na Watanzania, sikutaka ku-socialise na Mtz yoyote yule, nilikaa nao mbali sana. Kila sehemu walikopita Watanzania wameacha legacy mbaya ya kujihusisha na uhalifu mbalimbali ikiwamo na hii biashara ya madawa ya kulevya, Watanzania wote sasa hivi tumekuwa hatuaminiki kutokana na ushenzi huu wa watu wachache wanafanya biashara ya madawa ya kulevya. Wanyongwe huko huko China endapo kama Watakamatwa huko, wasiwarudiahe Tanzania.

Najua China ya Visiwani, yaani Hong Kong hakuna sheria ya kunyonga watu wanaojihusiha na madawa ya kulevya, Mimi nazishauri Mamlaka za China Visiwani (Hong Kong), wanapowakamata Watanzania wenye madawa ya kulevya waende wakawafungulie mashtaka katika China Bara (Mainland China), yaani Beijing, miji mingine ya China Bara na kwingineko kwenye sheria ya kunyonga wahalifu wa madawa ya kulevya ili kuwapukutisha na kuwapunguza idadi yao kwa haraka ili vitendo hivyo vikome na hatimaye kulisafisha tena jina la Tanzania kimataifa.

Watanzania wachache wanaojihusiha na uhalifu wa madawa ya kulevya huko nje wanawakoseha fursa Watanzania wengine wenye nia safi ya kutaka kwenda kutafuta fursa za maisha na kufanya shughuli halali huko nje.
Ndio maana JPM alisema wanyongwe tu na balozi zisihusishwe na kujihusisha na powders.
 
Back
Top Bottom