nuruyamnyonge
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 4,386
- 2,151
Jukumu la kuthibitisha bila shaka ni la mahakama. At least kama aliona haki haikutendeka angesema ataishawishi mahakama ili kesi isikilizwe upya. Kutoa watuhumiwa wa jinai gerezani ndo mamlaka yaliyopitiliza ya rais tunayoyalalamikia kila siku. Siku nyingine akimtoa Rostam gerezani (kama atafungwa) mtawezaje kulalamika?
Ngoja nikusaidie, Lowassa aliombwa na wananchi akipewa nchi amrudishe babu Seya, sasa wewe huoni hapo kuna tatizo? Alichokijibu Lowassa ni kwamba, atahitisha mafaili upya na kuona kama kuna haki ilikiukwa anarejeshewa hiyo haki. Kuna tatizo hapo.