VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kama watanzania tulijiandaa kuhesabiwa jana tarehe 23 Agosti, 2022, mambo yamekuwa si mambo. Nilikuwa nyumbani kwangu Sombetini, Arusha tangu asubuhi hadi usiku nikawasubiri makarani wa sensa bila mafanikio, sikuhesabiwa.
Sitaki kusema mengi, sitaki kuonekana nachonga kwa mambo ya kitaifa kama haya ya sensa. Mambo ya sensa ni mambo ya kisasa, ni mambo muhimu kuliko ndimu kwenye maendeleo ya taifa letu. Lakini, kama kawaida yetu, siasa imeiingilia sensa yetu na kuitishia kuiharibu bila aibu.
Sensa yetu imegeuka uwanja wa kisasa wa siasa. Kwanza, siasa ilianza kwenye kuwapata makarani, CCM yetu ikateka mchakato na 'kuteua' makarani tuliowataka. Pili, matangazo yote ya sensa yalituma ujumbe mmoja wa wazi; sensa ingefanyika tarehe 23 Agosti, 2022.
Hawafiki watanzania mia waliojua kuwa sensa ingefanyika kwa siku saba. Nani alipaswa kutuambia mapema na kutuelewesha? Bila kutulewesha kuhusu hili hakutimiza wajibu wake, tumfanyaje? Pia, utitiri wa maswali ya sensa unasemwa kupunguza kasi ya zoezi la sensa.
Halafu, ni kama jana wamehesabiwa viongozi tu na 'wenye majina' huko mitaani. Asilimia kubwa ya wananchi wa kawaida hawakufikiwa na kuhesabiwa. Viongozi wanarindima mitandaoni kuonesha walivyohesabiwa. Ni sensa au siasa? La mwisho, malipo ya makarani yawe wazi; wanalipwa ngapi, lini na kwa namna gani? Kificho ni kitisho!
Sensa kwa maendeleo, sensa si upendeleo!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kwenda Dodoma)
Sitaki kusema mengi, sitaki kuonekana nachonga kwa mambo ya kitaifa kama haya ya sensa. Mambo ya sensa ni mambo ya kisasa, ni mambo muhimu kuliko ndimu kwenye maendeleo ya taifa letu. Lakini, kama kawaida yetu, siasa imeiingilia sensa yetu na kuitishia kuiharibu bila aibu.
Sensa yetu imegeuka uwanja wa kisasa wa siasa. Kwanza, siasa ilianza kwenye kuwapata makarani, CCM yetu ikateka mchakato na 'kuteua' makarani tuliowataka. Pili, matangazo yote ya sensa yalituma ujumbe mmoja wa wazi; sensa ingefanyika tarehe 23 Agosti, 2022.
Hawafiki watanzania mia waliojua kuwa sensa ingefanyika kwa siku saba. Nani alipaswa kutuambia mapema na kutuelewesha? Bila kutulewesha kuhusu hili hakutimiza wajibu wake, tumfanyaje? Pia, utitiri wa maswali ya sensa unasemwa kupunguza kasi ya zoezi la sensa.
Halafu, ni kama jana wamehesabiwa viongozi tu na 'wenye majina' huko mitaani. Asilimia kubwa ya wananchi wa kawaida hawakufikiwa na kuhesabiwa. Viongozi wanarindima mitandaoni kuonesha walivyohesabiwa. Ni sensa au siasa? La mwisho, malipo ya makarani yawe wazi; wanalipwa ngapi, lini na kwa namna gani? Kificho ni kitisho!
Sensa kwa maendeleo, sensa si upendeleo!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kwenda Dodoma)